KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, January 28, 2013

YANGA, PRISONS ZAINGIZA MIL 101/-



MCHEZO wa Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Yanga na Prisons uliochezwa juzi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, umeingiza sh. 101,016,000.

Katika mchezo huo, jumla ya watazamaji 17,946 walikata tiketi kushuhudia pambano hilo kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000.

Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura, alisema jana kuwa, watazamaji 16,158 walikata tiketi za sh. 5,000 wakati idadi ndogo ya washabiki ilikuwa ni 98 waliokata tiketi za sh. 20,000.

Wambura alisema kutokana na mapato hayo, kila klabu imepata mgawo wa sh. 24,314,752.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 15,409,220.34.

Alisema asilimia 15 iliyokwenda kwenye uwanja baada ya kuondoa VAT ni sh. 12,363,433.45 na mgawo mwingine wa mapato hayo ni gharama za tiketi sh. 3,183,890.

Alisema gharama za mchezo ni sh. 7,413,060.07, Kamati ya Ligi sh. 7,418,060.07, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 3,709,030.03 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 2,884,801.14.

No comments:

Post a Comment