KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, January 22, 2013

75 WAPITISHWA USAJILI WA DIRISHA DOGO

WACHEZAJI 75 wameidhinishwa kuzichezea timu mbalimbali katika mzunguko wa pili wa michuano ya soka ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara utakaoanza kutimua vumbi Jumamosi.

Katika usajili huo, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limemuidhinisha kipa Shaaban Kado, aliyekuwa akichezea Mtibwa Sugar ya Morogoro kujiunga na Coastal Union ya Tanga.

Ofisa Habari wa (TFF), Boniface Wambura alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji iliyokutana Januari 19 mwaka huu, ilipitia maombi ya usajili wa dirisha dogo kwa klabu zote za za Ligi Kuu.

Wambura alisema licha ya kuwaidhinisha wachezaji hao, kamati hiyo imekataa kumuidhinisha Martin Mlolere, aliyeombewa usajili na Mgambo Shooting kutoka Majimaji baada ya taratibu za uhamisho wake kutokamilika, hivyo ataendelea kuichezea Majimaji.

Aliwataja wachezaji walioidhinishwa katika usajili huo, klabu zao zikiwa kwenye mabano kuwa ni Humphrey Mieno, Brian Umony, Jockins Atudo, David Mwantika, Abdallah Seif, Malika Ndeule na Uhuru Selemani -kwa mkopo(Azam).

Wengine ni Juma Mdindi, Njaidi Mohamed na Mahmoud Mbulu (Ruvu Shooting), Mohamed Kayi na Emmanuel Gabriel (Tanzania Prisons), Nurdin Selemani, Shaibu Nayopa, Hamidu Hassan, Paul Malipesa, Josephat Moses, Muharami Mnyangamala, Majaliwa Mbaga na Alphonce Peter (Oljoro JKT).

Wachezaji wengine ni Shukuru Kassim, Chacha Marwa, Salum Machaku, Mzamiru Said, Victor Bundala, Delta Thomas, Edward Mzeru na Tizzo Chomba (Polisi Morogoro), Edmund Kashamila na Julius Mrope (Kagera Sugar). Pia wamo Rajab Mohamed, Zakayo Joseph, Baraka Anthony na Mussa Chambo (Mtibwa Sugar), Zahoro Pazi (kwa mkopo), Emmanuel Linjechele, Kisimba Luambano na Nashon Naftali (JKT Ruvu), Moaka Shabani, Ismail Mkaima na Damas Milanzi (Mgambo Shooting), Donald Obimma, Exavery Muhollery, Mohamed Hussein na Ulugbe Odia (Toto Africans).

Wengine ni Obadi Mungusa, Juma Seif, Yusuf Mgwao, Ibrahim Job- kwa mkopo, Shamte Ally- kwa mkopo, Buya Jamwaka, Takang Valentine, Nurdin Mussa, Salvatory Jackson, Mohamed Athuman, Athuman Kajembe na Jarufu Kizombi (African Lyon), Mussa Mudde na Abel Dhaila (Simba), Rashid Simba, Zuberi Hamisi, Shaongwe Ramadhan, Castory Mumbara, Tinashe Machemedze na Shabani Kado (Coastal Union).

No comments:

Post a Comment