KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, April 29, 2011

HAWA NDIO WASHIRIKI WA BIG BROTHER 2011

BHOKE (26) TANZANIA

CONFIDENCE (37) GHANA



HANNI (22) ETHIOPIA


HERMENIO (32) MSUMBIJI



JOSSY (28) NAMIBIA




LOMWE (27) MALAWI



LUCLAY (28) AFRIKA KUSINI


MILLICENT (28) KENYA




MUMBA (24) ZAMBIA




SHARON (25) UGANDA



VIMBAI (24) ZIMBABWE


VINA (26) NIGERIA



WEZA (26) ANGOLA



ZEUS (24) BOTSWANA



























Thursday, April 28, 2011

Filamu za 'Inye' zapigwa marufuku


SERIKALI imepiga marufuku kuonyeshwa hadharani na kwenye vyombo vya usafiri filamu tano zilizokaguliwa na kubainika kuwa zinakiuka maadili ya kitanzania.
Filamu zilizopigwa marufuku ni Mtoto wa Mama, Inye, Inye Plus, Inye Ndembendembe na Inye Gwedegwede.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Bodi ya Filamu na Michezo ya Kuigiza jana ilisema kuwa, filamu ya Shoga imeruhusiwa kuonyeshwa hadharani baada ya waandaaji kuifanyia marekebisho.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kati ya Februari na Machi mwaka huu, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kupitia Bodi ya Filamu na Michezo ya Kuigiza, ilifanya ukaguzi wa filamu 45, kati ya hizo zilizoruhusiwa kuonyeshwa ni 40 na zilizozuiwa kutokana na kutozingatia maadili ya Kitanzania ni tano.
“Sababu za kukataliwa ni pamoja na filamu hizo kutokuwa na maudhui na maadili ya Kitanzania, kwa kuwa zinaonyesha vitendo vya ushoga pia zinadhalilisha wanawake, hasa wanene kwa kugeuza miondoko yao, ambayo inaamsha hisia za kingono,”ilisema taarifa hiyo. “Filamu ya Mtoto wa Mama ni ya daraja ‘R’, yaani hairuhusiwi kuonyeshwa mahali popote na wakati wowote nchini Tanzania kwani inaonyesha vijana wa kiume wanaovaa na kuishi maisha ya kike (mashoga),”iliongeza.
“Filamu za Inye, Inye Plus, Inye Ndembendembe na Inye Gwedegwede zipo katika daraja hilo hilo kwani zinahusu vichekesho vinavyozingatia sana maumbile ya miili ya wanawake na miondoko yao, ambayo inaamsha hisia za kingono,” ilisema taarifa hiyo.
Bodi hiyo ya filamu imewataka watunzi na watengenezaji wa filamu kutotengeneza filamu bila kuwa na kibali cha waziri mwenye dhamana ya masuala yanayohusu filamu na michezo ya kuigiza na kutoonyeha filamu yeyote bila kukaguliwa na kupewa daraja. Wakati huo huo, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo imeridhia marekebisho yaliyofanywa katika filamu ya Shoga Yangu, ambayo hapo awali ilikuwa ikiitwa Shoga.
Taarifa ya wizara hiyo ilisema jana kuwa, marekebisho hayo yaliwasilishwa Aprili 8, 2011 na filamu hiyo imepewa daraja‘A’ 18.
“Filamu hiyo sasa inafaa kuangaliwa na watu wazima kuanzia miaka 18 na kuendelea. Marekebisho yaliyoelekezwa kufanyika katika filamu hiyo yalikuwa ni pamoja na kipande cha bafuni kinachoonyesha mashoga wakiwa wanaoga, kilitakiwa kuondolewa, maneno makali yanayotamkwa kiuhalisia yalitakiwa kutafutiwa maneno mbadala pia jina la filamu (Shoga) lilitakiwa kubadilishwa kwa kuwa halikuwa linaendana na maadili ya Kitanzania,” ilisema taarifa hiyo. Wizara imemtaka mtengenezaji wa filamu hiyo kutotumia tangazo lililotumika kuitangaza filamu hiyo hapo awali kwani haliendani na maudhui yaliyomo katika filamu baada ya marekebisho.
Awali, filamu ya Shoga ilipigwa marufuku kuonyeshwa hadharani, kufuatia kuandaliwa katika mazingira yanayokiuka maadili ya Mtanzania.

Kanumba kucheza filamu na Ramsey Nouah



MWIGIZAJI nyota wa filamu nchini, Steven Kanumba amesema anatarajia kumtumia mcheza sinema, Ramsey Nouah kutoka Nigeria katika filamu yake mpya itakayojulikana kwa jina la Devil Kingdom.
Kanumba amesema kupitia tovuti yake juzi kuwa, ameamua kumtumia Ramsey, kufuatia kura zilizopigwa na mashabiki wake.
Mwigizaji huyo mwenye mvuto alisema, alitoa nafasi kwa mashabiki wake kumchagua mmoja wa wacheza sinema watatu kutoka Nigeria, ili afanye naye kazi nchini.
Mbali na Ramsey, wacheza sinema wengine aliowapendekeza ni Desmond Elliot na Van Vicker.
Katika kura hizo, ambazo hakutaja idadi yake, Kanumba alisema nyingi zilimchagua Ramsey na kupendekeza filamu hiyo iwe katika lugha mchanganyiko (kiswahili na kiingereza).
Kanumba alisema filamu anayotarajia kuicheza na Ramsey inahusu masuala ya jamii fulani, ambayo haiamini Mungu bali shetani na wamefanikiwa kuiteka dunia kwa nguvu za giza, pesa na umaarufu.
Mbali na kuiteka dunia kwa njia hizo, Kanumba alisema jamii hiyo pia inawasiliana kwa kutumia ishara maalumu na inafanya ibada kwa utaratibu iliojiwekea.
Kanumba alisema uamuzi wa kuwashirikisha wasanii kutoka nje katika baadhi ya filamu zake, umelenga kupanua soko lake kimataifa. Alisema filamu hiyo itatayarishwa kupitia kampuni yake ya Kanumba Great Film.
Kwa mujibu wa Kanumba, tayari Ramsey ameshawasili nchini kwa ajili ya kupiga picha za filamu hiyo, ambayo ipo kwenye hatua za mwisho.
Akizungumza na waandishi wa habari juzi mjini Dar es Salaam, Ramsey alisema amefurahi kushirikishwa kwenye filamu hiyo na anaamini ushiriki wake utakuwa chachu.

SHAMTE ALLY: Nipo tayari kucheza Yanga au Simba


WAKATI kipindi cha usajili kinatarajiwa kuanza rasmi mwezi ujao, kumekuwepo na habari nyingi kuhusu uhamisho wa wachezaji kutoka timu moja kwenda nyingine, akiwemo mshambuliaji Ally Shamte wa Yanga. Katika makala hii ya Mwandishi Wetu mchezaji huyo anaelezea kuhusu usahihi wa taarifa hizo na mikakati yake kisoka.

SWALI: Pole kwa kuumwa kwa kipindi kirefu na kusababisha ukaa nje ya dimba kwa muda mrefu.
JIBU: Asante sana.
SWALI: Kuna taarifa kwamba Yanga ina mpango wa kutaka kukuacha kwenye usajili wake msimu ujao, je kuna ukweli wowote kuhusu taarifa hizi?
JIBU: Ukweli ni kwamba mimi sina taarifa yoyote kuhusu kuachwa na klabu yangu ya Yanga. Kama jambo hilo lipo, inawezekana nitapatiwa taarifa hivi karibuni.
Lakini kama wamefanya hivyo, watakuwa wamenitendea jambo baya kwa sababu hawajui uwezo wangu kwa sasa upo vipi.
Licha ya jambo hilo, hata Kocha Sam Timbe hajawahi kuona uwezo wangu, sasa sijui wametumia vigezo gani kunitema. Kama kweli wamefanya hivyo, watanisikitisha sana. Lakini mimi sina taarifa yoyote.
SWALI: Mara ya mwisho kukutana na viongozi wa klabu ya Yanga ilikuwa lini na walikueleza jambo gani kuhusu hatma na mustakabali wako?
JIBU: Nilikutana na viongozi wangu kabla ya mchezo wa mwisho wa ligi kuu dhidi ya Toto African. Wakati huo timu ilikuwa inajiandaa na safari ya kwenda mkoani Mwanza.
Nategemea ndani ya wiki moja nitawasiliana nao ili kujua ukweli wa habari hizi na nini kinachofuata.
SWALI: Umewahi kukutana na kiongozi yeyote wa klabu ya Simba kwa siku za hivi karibuni?
JIBU: Wamekuja kuzungumza na mimi, lakini niliwaeleza kwamba nasubiri kujua hatma yangu ndani ya Yanga. Viongozi hao wamenipa muda ili niwape majibu.
Lakini nipo tayari kujiunga na timu hiyo endapo watanipa dau la nguvu ili niweze kucheza kwa vile mimi maisha yangu yanategemea soka na sio kitu kingine.
SWALI: Unajisikiaje kutokana na kushindwa kuichezea Yanga kwa muda mrefu?
JIBU: Najisikia vibaya sana kwani nilikuwa nimepanga malengo makubwa ndani ya msimu huu uliomalizika hivi karibuni, ikiwemo kucheza kwa kiwango cha hali ya juu.
Mbali na hayo, nilipanga kuhakikisha narejea katika kikosi cha kwanza cha Yanga huku nikisaka nafasi ya kuitwa kuichezea Taifa Stars.
Pia nilikuwa nawaza kusaka mbinu ya kupata timu ya kuchezea nje ya nchi ili niweze kuongeza kipato changu kwa vile maisha ya kucheza mpira ni mafupi sana.
SWALI: Una jambo gani ambalo ungependa kuwaeleza wachezaji wenzako wa Tanzania?
JIBU: Ninayo mambo mengi ya kuwaeleza wachezaji wenzangu pamoja na viongozi wa soka. Hivi sasa kumezuka tabia moja mbaya sana ndani ya klabu kubwa, hasa Simba na Yanga.
Wapo baadhi ya viongozi, ambao iwapo watatofautiana na mchezaji fulani, wanaanza kumjengea hoja au vitendo vya ajabu ili ashindwe a kutimiza majukumu yake.
Tabia hii ni mbaya sana. Napenda kuwaasa wachezaji wenzangu wajitume kwa nguvu zao zote na kujiweka pembeni na migogoro kwa vile inaweza kusababisha maafa kwao na familia zao kwa ujumla.
Nimewasikia baadhi ya wachezaji, ambao wapo Simba wanalalamika kuhusu kuwepo baadhi ya viongozi, ambao wanaendekeza chuki na wakati mwingine kutaka wachezaji fulani wasipangwe, kisa wana ugomvi na kiongozi fulani.
SWALI: Wewe binafsi unafikiri nini kifanyike ili kuondokana na tabia hiyo?
JIBU: Nawaomba viongozi hao wabadilike na kuwaacha wachezaji wapate nafasi ya kuzitumikia klabu zao na kuongeza ushindani wa kuwania namba katika kikosi cha kwanza.
Pia wale ambao, wanakaa benchi ni vyema wakaongeza jitihada ili kuongeza ushindani wa kuwania namba. Kwa kufanya hivyo wanaweza kujiongezea kipato chao.
SWALI: Kitu gani hadi sasa ambacho kinakukera katika michuano ya ligi kuu iliyomalizikia hivi karibuni?
JIBU: Nachukizwa na baadhi ya waamuzi kushindwa kutafsiri vyema sheria 17 za soka ili mshindi aweze kupatikana kwa haki.
Wapo baadhi ya waamuzi, ambao ni chanzo cha timu nyingi kufanya vibaya kutokana na tabia zao za kutaka kuzibeba timu, ambazo hazina uwezo na kusababisha zishindwe kufanya vizuri katika mashindano ya kimataifa. Mbali na hayo, ninachukizwa na tabia ya wachezaji kuhujumu timu kama kigezo cha kutaka maslahi au kudai haki.
Hili ni jambo baya kwa vile zipo taratibu husika, ambazo zinapaswa kufuatwa na wachezaji katika kudai haki zao na zikapatikana. Hivyo ni vyema wachezaji watekeleze majukumu yao uwanjani bila kuziathiri timu zao.
Kuna jambo lingine, ambalo limekuwa likinikera sana, lakini sina ushahidi nalo. Lakini kama kweli lipo, ni vyema wanaofanya hivyo wakaacha mara moja ili kujenga heshima ya mchezo huo.
SWALI:Una maoni gani kuhusu timu ya Taifa Stars?
JIBU: Kwa kweli naona hali inazidi kuwa ngumu hata kwa Kocha wa Taifa Stars, Jan Poulsen ambaye hadi sasa hana kikosi cha kwanza.
Kila kukicha utakuta anajaribu wachezaji mbalimbali ili kusaka kikosi cha kwanza kutokana na uwezo wa wachezaji kupanda na kushuka. Nina imani kwamba soka ina mambo mawili ya msingi, kujituma na kusikiliza mafunzo ya kocha ili malengo ya ushindi yaweze kutimia.
SWALI: Una maoni gani kuhusu timu za Simba na Yanga ambazo mwakani zitawakilisha nchi katika mashindano ya kimataifa?
JIBU: Nawaomba viongozi wa benchi la ufundi wa timu hizo kuwa makini sana katika kipindi hiki cha usajili ili kuwapata wachezaji wenye uwezo wa kuzisaidia timu zao.
Hakuna jambo jingine kwa mchezaji kama kuweka historia ya kuwa mchezaji fulani aliweza kuchangia matokeo mazuri katika michuano ya Afrika na timu hizo ziweze kupata matokeo mazuri kwa kujiandaa na kucheza michezo mingi ya majaribio ndani na nje ya nchi.
Vilevile nawaomba wachezaji wa Yanga na Simba tuzingatie mafunzo ya walimu wetu ili tuweze kuwa katika kiwango cha hali ya juu.

INI EDO: Sichezi tena filamu zisizo na kiwango




LAGOS, Nigeria
MWIGIZAJI nyota wa filamu nchini Nigeria, Ini Edo amekiri kuwa amechoka kufanya kitu kile kile katika sinema anazoigiza na kwamba ameweka msimamo wa kutofanyakazi, ambazo hazimvutii.
Ini, mzaliwa wa Jimbo la Akwa Ibom nchini Nigeria, alisema wiki hii kuwa, miongoni mwa mambo yasiyomvutia katika fani hiyo hivi sasa ni maelezo yasiyo na mvuto katika baadhi ya sinema.
Mwanadada huyo, ambaye hivi karibuni aliteuliwa kuwa balozi wa Umoja wa Mataifa wa mazingira alisema anasikia faraja kubwa kupewa heshima hiyo kwa vile ni nafasi nzuri kwake kutoa mchango wake kwa jamii na watoto wanaoishi katika mazingira magumu.
Alisema kutokana na wadhifa wake huo, moja ya majukumu yake makubwa ni kuwasaidia watoto wa aina hiyo ili kuwaokoa katika maisha hatarishi.
“Kama tutawapa watoto hawa nafasi sahihi, kuwaunga mkono na kuwapa moyo, lazima watabadilika,”alisema mcheza sinema huyo wa Nollywood, aliyecheza filamu lukuki.
“Hakuwaumba kuishi walivyo. Hakutaka waishi mitaani, chini ya madaraja ama kufa wakiwa na umri mdogo. Mazingira yetu ndiyo yaliyosababisha waishi hivyo.
“Wajibu wangu nikiwa balozi wa Umoja wa Mataifa ni kuwasaidia kulingana na uwezo wangu na kuwasaidia watu hawana kuondokana na maisha hayo. Naelewa haitakuwa kazi nyepesi, lakini hilo ni jukumu langu.
“Mbali na kucheza filamu na kuwafurahisha watu kupitia kwenye video, tunapaswa kujifunza kuwapa misaada na kugusa maisha yao,”alisema nyota huyo wa Nollywood.
Ini alisema hakuwahi kutumia mbinu zozote ili kutaka apewe wadhifa huo na kuongeza kuwa, alipigiwa simu kuelezwa kuhusu uteuzi huo wakati akiwa kazini.
Mwanadada huyo mwenye sura na umbo lenye mvuto alisema si rahisi kwa mtu yeyote kutumia mbinu ili apate uteuzi huo na kwamba haamini iwapo wapo watu wa aina hiyo.
Ini alisema viongozi wa Umoja wa Mataifa wanatambua wazi kuwa, kwa kuwatumia wasanii wa aina yake, ni rahisi kuwafanya watu washiriki katika kazi za kusaidia jamii, hasa watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu.
“Uteuzi huu ulikuja moja kwa moja kutoka Umoja wa Mataifa na tulifanya mkutano na waandishi wa habari nchini Kenya. Ramsey Nouah na mwigizaji mmoja kutoka India nao pia waliteuliwa kuwa mabalozi wa umoja huo,”alisema.
Ini alikiri kuwa, tangu alipofunga ndoa mwaka jana, hajashiriki kucheza filamu nyingi kwa vile amechoka kufanya vitu vinavyofanana. Alisema baadhi ya filamu za Kinigeria hivi sasa hazina mvuto kutokana na kutokuwa na mambo mapya. “Inasikitisha kusikia watu wakizilinganisha filamu zetu na za nchi jirani. Tunaweza kufanya vizuri zaidi, hiyo ndiyo sababu iliyonifanya niamue kucheza filamu zenye kiwango cha juu pekee. Kama filamu haina kiwango, sichezi,”alisema.
“Watu wamechoka kutazama kazi zisizokuwa na mvutu, ambazo baadhi ya watu wanazitengeneza na mbaya zaidi baadhi yetu sura zetu zinaonekana,”aliongeza.
Akifafanua, Ini alisema uamuzi wake huo hauna maana kwamba hatashiriki kucheza filamu zinazotengenezwa Asaba na Enugu, bali filamu yoyote, ambayo haitakuwa na mvuto bila kujali wapi itachezwa.
“Kazi mbaya haihusiani na mazingira ya eneo litakalotumika kutengeneza filamu. Unaweza kwenda kupiga picha za sinema Marekani wakati filamu nzuri inaweza kutengenezwa Zamfara. Kama nitapata maelezo mazuri ya sinema kutoka Asaba ama Enugu, nitakwenda na kama nitapata hadithi mbaya kutoka Marekani, siwezi kwenda,”alisema.
Ini alisema wakati umefika kwa wacheza sinema nchini Nigeria kuwa na msimamo ili fani hiyo iweze kupiga hatua zaidi kimaendeleo na kusisitiza kuwa, kazi mbaya zisipewe nafasi.
Mwanadada hiyo alisema watayarishaji wengi wa sinema waliopo Asaba na Enugu ni rafiki zake na wanamwelewa kuhusu msimamo wake huo. Alisema baadhi ya wakati amekuwa akiwarejeshea pesa zao baada ya kusoma maelezo ya sinema na kutoridhishwa nayo.
“Hili si suala binafsi, ni msimamo wa kikazi kwangu. Nimeamua kucheza filamu zenye kiwango pekee. Nataka kufanyakazi zitakazonifanya nione fahari wakati wote,”alisema.
Kwa sasa, Ini anashiriki kuandaa filamu mpya ya ‘I’ll take my chances’, akishirikiana na mtayarishaji maarufu Emem Isong. Alisema wametumia fedha nyingi kuandaa filamu hiyo, ikiwa ni pamoja na wapiga picha kutoka nje ya nchi.
Ini alitamba kuwa, filamu hiyo ndiyo pekee bora aliyoshiriki kuitunga na kuicheza na amewataka mashabiki kuisubiri kwa hamu kubwa kwa sababi itakuwa ya aina yake. Alisema filamu hiyo itaingizwa sokoni kabla ya mwisho wa mwaka huu.
Mwanadada huyo mwenye tabasamu la bashasha alisema anafurahia maisha yake ya ndoa kwa sababu yeye na mumewe wanaelewana vyema. Alisema kazi yake haiwezi kuyaathiri maisha hayo.
“Tunazo baadhi ya changamoto, lakini tumekuwa tukiyatatua baadhi ya matatizo yanayojitokeza na kusonga mbele na maisha. Namfurahia mtu wangu huyu na ndoa yangu,”alisema.
Ini alikanusha madai kuwa, amekuwa hana uhusiano mzuri na wacheza filamu wenzake, Oge Okoye, Uche Jombo na Mercy Johnson. Alisema hana ugomvi wowote na wasanii hao.
“Sina ugomvi na watu hawa. Mimi ni mtu wa amani. Mwaka huu sitarajii kurudi nyuma, nasonga mbele. Baadhi ya watu hawa ni rafiki zangu, wengine ni watu wangu wa karibu,”alisisitiza.
Licha ya kuolewa, Ini amekiri kuwa baadhi ya wanaume wamekuwa wakimsumbua kwa kumtaka kimapenzi, lakini alisisitiza kuwa, hawezi kuwapa nafasi kwa vile anayafurahia maisha yake ya ndoa.
“Pete ya ndoa haiwazuii wanaume kukufuatafuata, nadhani ndiyo inayowavutia zaidi. Wanadhani utakuwa tayari kufanya nao mapenzi na huwezi kuwasumbua kama wanavyofanya wanawake, ambao hawajaolewa,”alisema.
“Naifurahia ndoa yangu, sihitaji bega la mwanaume yeyote. Na nahitaji kusema hivi kwa wanawake wengine; furaha katika maisha inakuja kutoka kwa penzi la mwanaume umpendaye. Kama utaifanyiakazi ndoa yako na kumuomba Mungu, atakusaidia,”alisisitiza.

Vijana wa Uganda kutua nchini leo





TIMU ya soka ya Taifa ya Uganda ya vijana wa chini ya miaka 23, The Cobs inatarajiwa kuwasili nchini leo jioni.
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura alisema jana kuwa, timu hiyo itawasili uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere saa 10.30 jioni kwa ndege ya Uganda Air.
Wambura alisema msafara wa timu hiyo utaongozwa na Ofisa wa Shirikisho la Vyama vya Soka vya Uganda (FUFA), Sam Lwere.
Kwa mujibu wa Wambura, wachezaji na viongozi wa timu hiyo wamepangiwa kukaa kwenye hoteli ya Durban, iliyopo barabara ya Uhuru, Dar es Salaam.
The Cobs inatarajiwa kurudiana na timu ya Taifa ya vijana wa umri huo ya Tanzania, Vijana Stars, Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika pambano la marudiano la michuano ya Michezo ya Afrika.
Katika mechi ya awali, iliyochezwa wiki mbili zilizopita mjini Kampala, The Cobs iliichapa Vijana Stars mabao 2-1.
Ili Vijana Stars isonge mbele katika michuano hiyo, italazimika kuishinda The Cobs bao 1-0.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 1,000 kwa viti vya kijani, bluu na rangi ya chungwa. Kwa upande wa VIP C na B, kiingilio kitakuwa sh. 5,000 na sh. 10,000 kwa VIP A. Tiketi kwa ajili ya mchezo huo zinatarajiwa kuanza kuuzwa keshokatika vituo vya Premier Betting (Kariakoo- mtaa wa Sukuma, Buguruni Sokoni, Manzese Midizini, JM Mall na Tandale kwa Mtogole), Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Steers (mtaa wa Ohio na Samora), Big Bon Msimbazi (Kariakoo) na Uwanja wa Uhuru.

Jahazi yapakua albamu mpya

KIONGOZI wa kundi la muziki wa taarab la Jahazi, Mzee Yusuf (katikati) akiimba sanjari na waimbaji wengine wa kundi hilo wakati wa uzinduzi wa albamu yao mpya uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye ukumbi wa hoteli ya Travertine, Magomeni, Dar es Salaam. Katika onyesho hilo, waimbaji Leila Rashid na Isha Mashauzi hawakuwepo kufuatia kusimamishwa kazi kwa makosa ya utovu wa nidhamu.


Rage awatangazia vita mafisadi Simba



MWENYEKITI wa klabu ya Simba, Ismail Aden Rage amekuwa mbogo baada ya kudai kwamba, kamwe hawezi kuacha baadhi ya watu wakinufaika na klabu hiyo.
Rage amesema ni makosa makubwa kwa watu hao kuitumia Simba kwa manufaa yao huku wachezaji, ambao ndio wavuja jasho wakiishi maisha duni na kupata mapato madogo.
Mwenyekiti huyo wa Simba alielezea msimamo wake huo juzi mjini Dar es Salaam, alipokuwa akizungumza na Burudani kuhusu mikakati yake ya kuiwezesha klabu hiyo ijitegemee.
Alisema katika kutekeleza azma yake hiyo, ameamua kuwashirikisha viongozi wenzake ili kupambana na watu hao na kuitokomeza kabisa tabia hiyo.
Rage alisema lengo la kufanya hivyo ni kuhakikisha mapato yote ya klabu yanaingia sehemu husika na wachezaji wanapata malipo yao halali kulingana na mikataba yao.
"Simba ni klabu kubwa, inazo mali nyingi, yakiwemo majengo na viwanja, lakini nimebaini kwamba wapo baadhi ya watu wananufaika navyo huku klabu ikiendelea kukabiliwa na hali mbaya,"alisema kiongozi huyo ambaye ni Mbunge wa Tabora Mjini.
Alisema kwa sasa bado wanaendelea kupitia mikataba yote ya wapangaji katika majengo ya klabu hiyo ili kujua uhalali wa malipo yao na mengine.
Kiongozi huyo wa juu wa Simba alisema, wakati umefika kwa watu hao kuacha mara moja tabia ya kuitumia klabu hiyo kama mtaji na kusisitiza kuwa hayupo tayari kuwafumbia macho.
"Mimi nilikuwa mchezaji hapa Simba, naona jinsi wachezaji wanavyoumia kwa ajili ya kuitetea klabu wakati kuna baadhi ya watu wanakula fedha za klabu kiulaini, nitaanza na watu hao, "alisema.

Bado nasaka timu Ulaya-Cannavaro


BEKI kisiki wa klabu ya Yanga, Nadir Haroub 'Canavaro' amesema bado anaendelea na mikakati ya kwenda kucheza soka ya kulipwa barani Ulaya.
Akizungumza mjini Dar es Salaam juzi, Cannavaro alisema hajafuta mpango wake huo kwa sababu moja ya malengo yake ni kujiendeleza zaidi kisoka.
Cannavaro ameelezea msimamo wake huo, kufuatia kuwepo na taarifa kwamba, klabu ya Azam inafanya mipango ya kumsajili kwa ajili ya msimu ujao.
Licha ya kuwepo kwa mipango hiyo, uongozi wa Yanga ulikaririwa hivi karibuni ukisema kuwa, hauna mpango wa kumuuza mchezaji huyo kwa klabu ya Azam.
"Napenda kwenda kucheza soka nje ya nchi ili kuongeza kipato na kujiandaa kwa maisha yangu ya baadaye baada ya kustaafu soka, lakini nitaendelea kuwepo Yanga hadi mpango huo utakapotimia,"alisema beki huyo.
Kwa mujibu wa Cannavaro, amekuwa akifanyakazi ya kusaka timu nje kwa kushirikiana na baadhi ya mawakala wa hapa nchini na wa nje.
Cannavaro aliwahi kwenda kufanya majaribio katika klabu ya Vancouver Whitecaps ya Canada akiwa na Nizar Khalfan mwaka juzi, lakini alikwama kupata namba kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo.
Nizar ndiye pekee aliyeweza kuvuka visiki vya majaribio katika klabu hiyo na hadi sasa ni mmoja wa wachezaji wanaotegemewa kwenye kikosi cha kwanza.
“Mipango yangu yote inafanyika kwa uwazi mkubwa, siwezi kuuficha uongozi wa Yanga. Mambo yatakapokuwa tayari, nitatoa taarifa kwa uongozi,”alisema.

Azam: Yanga ivunje benki kumrejesha Ngasa



UONGOZI wa klabu ya Azam umesema, hakuna klabu ya ligi kuu yenye uwezo wa kumsajili mshambuliaji Mrisho Ngasa kwa ajili ya msimu ujao wa ligi.
Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Nassoro Idrisa alisema mjini Dar es Salaam juzi kuwa, timu inayotaka kumsajili mshambuliaji huyo, inapaswa kuwa imejiandaa vilivyo.
Nassoro alisema Ngasa ana mkataba wa kuichezea Yanga kwa miaka miwili, hivyo iwapo kuna klabu inamuhitaji, inapaswa kulipa gharama za kuvunja mkataba huo.
Alisema hadi sasa hakuna kiongozi wa klabu yoyote, aliyewasiliana nao kwa ajili ya kumsajili mchezaji huyo zaidi ya kupata taarifa hizo kupitia kwenye vyombo vya habari.
“Tunasikia tu kwamba Yanga inataka kumrejesha Ngasa kwao, sisi hatuna pingamizi, lakini wanapaswa kuelewa kwamba gharama za kuvunja mkataba wake ni kubwa, ni mara mbili ya mkataba alionao na Azam,”alisema.
Ngasa alisajiliwa na Azam msimu uliopita akitokea Yanga. Usajili wa mshambuliaji huyo uliigharimu Azam sh. milioni 50.
Kumekuwepo na tetesi kwamba, uongozi wa Yanga unataka kumrejesha mchezaji huyo Jangwani baada ya yeye mwenyewe kuonyesha yupo tayari kufanya hivyo.
Alipoulizwa kuhusu taarifa hizo, Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Yanga, Seif Mohamed alikiri kuwa, bado hawajakutana na uongozi wa Azam kwa ajili ya usajili wa mchezaji huyo.
Hata hivyo, Seif alisema upo uwezekano wa klabu yake kumrejesha Ngasa, lakini itategemea uamuzi wa wanachama na benchi la ufundi.
“Azam wanasema wanahitaji pesa nyingi, mbona wao walipokuja kwetu, tulikaa na kuzungumza, hivyo hata nasi tunaweza kukutana nao na gharama za uhamisho wake zisiwe kubwa,”alisema.
Wakati huo huo, uongozi wa Azam umesema utatangaza kikosi chao kipya Juni 10 mwaka huu baada ya kukamilisha taratibu za usajili wa wachezaji wapya.
Katibu Mkuu wa Azam, Nassoro Idrisa alisema juzi kuwa, kikosi hicho kitaanza mazoezi siku hiyo hiyo kwenye uwanja wao uliopo Mbande, Temeke, Dar es Salaam.
Nassoro alisema hadi juzi walikuwa wameshafanikiwa kumsajili kipa wa zamani wa Yanga, Obren Curkovic na bado wanaendelea na kazi ya kuziba baadhi ya mapengo ya wachezaji watakaoachwa.

JKT yamwekea ngumu Kazimoto



KLABU ya Simba iko katika hati hati ya kumpata kiungo Mwinyi Kazimoto wa JKT Ruvu baada ya kigogo wa timu hiyo kuwa mbogo.
Mwenyekiti wa JKT Ruvu, timu inayomilikiwa na Jeshi la Kujenga Taifa nchini, Charles Mruge juzi alikaririwa na Radio Uhuru akisema ni vigumu kwa Kazimoto kwenda Simba.
Kiongozi huyo alisema, mchezaji wake hawezi kuchezea Simba kwa sababu ni mwajiriwa wa jeshi hilo na anapaswa kufuata taratibu za kuacha kazi kwanza kabla ya kutangaza anahama timu.
“Kazimoto ni mwajiriwa wa jeshi, sijui kwa nini Simba wanatangaza wamemsajili wakati wanafahamu hawezi kuchezea timu za uraia,” alisema mwenyekiti huyo.
Alisema juzi alikuwa Zanzibar kikazi na alitarajia kurejea Dar es Salaam, ambapo amepanga kuzungumza na Kazimoto binafsi kujua msimamo wake kabla ya kutoa taarifa yoyote kuhusu sakata hilo.
“Sina taarifa za kutoka Simba kuhusu huyu mchezaji ila nimesoma katika magazeti kuwa anakwenda Simba, kwa sasa siwezi kuzungumza zaidi mpaka nikutane na mchezaji mwenyewe,” alisema Mruge.
Kazimoto inaaminika ni miongoni mwa viungo bora nchini, ambaye klabu ya Simba imemtupia ndoano, ambapo ili ifanikiwe kumpata, inalazimika kumtoa kwenye ajira.
Hata hivyo, mara kadhaa wachezaji wanaocheza katika timu za jeshi wamekuwa na wakati mgumu kuhama kipindi cha usajili kinapofika, ambapo baadhi ya wanasoka waliowahi kupata kasheshe ni Primus Kasonzo na Heri Morris, ambao walikuwa katika timu ya Tanzania Prisons ya Mbeya.

Kado azitosa Simba na Yanga



KIPA wa timu ya taifa ya vijana, Shaabani Kado amesema hajafanya mawasiliano yoyote na viongozi wa klabu za Simba na Yanga kwa ajili ya kumsajili msimu ujao.
Akizungumza mjini Dar es Salaam jana, Kado alisema bado yeye ni mchezaji halali wa Mtibwa Sugar na ataendelea kuichezea msimu ujao.
Kado alisema amekuwa akisikia taarifa hizo kupitia kwenye vyombo vya habari, lakini binafsi hana mpango huo.
"Mimi sijawahi kukutana na viongozi wa klabu hizo kuzungumzia mpango wa kujiunga na timu zao, nitaendelea kuwepo Mtibwa Sugar msimu ujao,"alisema mlinda mlango huyo.
Wakati kipa huyo anatoa tamko hilo, klabu ya Simba ndiyo iliyoonyesha nia kubwa ya kutaka kumnasa Kado kutokana na kuwepo habari kwamba wana mpango wa kumtema Juma Kaseja.
Kutemwa kwa Kaseja na mshambuliaji Mussa Hassan ‘Mgosi’, kumeigawa klabu hiyo, ambapo kamati yake ya utendaji iliyokutana wiki iliyopita ilishindwa kutoa uamuzi.
Alipoulizwa jana, Mratibu wa Mtibwa Sugar, Jamal Bayser alisema hana taarifa za kutakiwa kipa huyo na klabu hizo mbili, ingawa ameeleza kuwa amesoma habari hizo kupitia magazetini.

Isha Mashauzi, Leila Rashid wapigwa stop Jahazi

Leila Rashid



Isha Mashauzi

WAIMBAJI tegemeo wa kundi la muziki wa taarab la Jahazi, Isha Ramadhani ‘Mashauzi’ na Leila Rashid wanadaiwa kusimamishwa kazi katika kundi hilo.
Habari za uhakika kutoka ndani ya kundi hilo zimeeleza kuwa, waimbaji hao wawili wamesimasishwa kazi kutokana na sababu mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kujiona mastaa.
Chanzo hicho kilisema, kwa muda mrefu Isha na Leila wamekuwa wakileta mapozi wakati wa maonyesho ya kundi hilo, hali iliyoufanya uongozi uamue kuwasimamisha kwa muda.
"Ulifika wakati waimbaji hawa wakawa wanaonekana mzigo katika kundi ndio sababu wamesimamishwa kwa sababu wapo waimbaji wengi wenye vipaji,” kilisema chanzo hicho.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, uamuzi wa kuwasimamisha Isha na Leila umelenga kutoa funzo kwa wasanii wengine wa kundi hilo wenye tabia kama hizo.
Chanzo hicho kilizidi kupasha kuwa, mara nyingi Isha alikuwa akichelewa kufika mazoezini na kwenye maonyesho na kila alipoonywa, alionyesha dharau.
Hata katika uzinduzi wa albamu ya saba ya kundi hilo uliofanyika Jumapili iliyopita katika ukumbi wa Travertine, Magomeni, Dar es Salaam, waimbaji hao wawili hawakuonekana ukumbini.
Kukosekana kwa waimbaji hao mahiri kulizusha hisia tofauti miongoni mwa mashabiki waliojitokeza katika uzinduzi huo, ambapo wengi walipongeza uamuzi uliofanywa wa kuwasimamisha kazi.
"Ni bora walivyosimamishwa, walikuwa wanalifanya kundi hili kama la kwao,” alisema mmoja wa mashabiki waliohudhuria onyesho hilo.
“Isha mwenyewe alikuwa akifika kwenye maonyesho kwa muda anaotaka, hii ni dharau kubwa kwa uongozi," aliongeza shabiki mwingine.
Uzinduzi wa albamu hiyo ulifana vilivyo kutokana na waimbaji chipukizi waliojiunga na kundi hilo hivi karibuni kuonyesha umahiri wa hali ya juu. Waimbaji hao ni Mohammed Chipolopolo na Fatuma Kasim.

Okwi, Owino waitesa Simba




UONGOZI wa klabu ya Simba umeshtukia mpango wa timu ya Azam FC kutaka kuwanasa baadhi ya nyota wake, akiwemo Emmanuel Okwi, kufuatia hivi karibuni kumnasa beki Joseph Owino.
Habari zilizothibitishwa na kiongozi mmoja wa juu wa Simba zimeeleza kuwa, wamesikitishwa na kitendo cha viongozi wa Azam kuteta na baadhi ya wachezaji wao, ambao bado wana mikataba.
Alisema kitendo kinachofanywa na viongozi wa Azam ni kibaya na wao wana uwezo wa kukifanya, lakini wanaheshimu sheria za usajili zinavyosema.
Kiongozi huyo, ambaye hakupenda jina lake litajwe gazetini alisema, wameshapata taarifa kwamba Azam imeshamsajili kiungo wao, Abdulhalim Humud bila kuzungumza na uongozi wa Simba.
Simba imekumbwa na hofu kuhusu Okwi baada ya kuwepo taarifa kwamba anatakiwa kwenda kufanya majaribio ya kucheza soka ya kulipwa kwa klabu ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini.
Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa Simba, taarifa hizo ni za uzushi kwa vile wamebaini hizo ni mbinu zinazofanywa na wapinzani wao kutaka kumsajili mshambuliaji huyo kutoka Uganda. Okwi pia anawindwa kwa udi na uvumba na Yanga.
Hivi karibuni, Azam ilitangaza rasmi kumsajili kipa wa zamani wa Yanga, Obren Cirkovic. Pia kulikuwa na habari kwamba, klabu hiyo inataka kuwasajili kipa Juma Kaseja na mshambuliaji Mussa Hassan ‘Mgosi’ wa Simba.
Hata hivyo, mipango ya Azam kuwasajili Kaseja na Mgosi ilikwama baada ya kuwepo na taarifa kwamba, bado wana mikataba na Simba. Lakini kuna habari kuwa, huenda wachezaji hao wakatemwa na Simba msimu ujao.
"Haiwezekani timu ikutane na mchezaji bila ya kufanya mazungumzo na klabu yake husika ili iweze kupata ridhaa ya kufanya hivyo,kwa kweli hili ni jambo baya,"alionya kiongozi huyo wa Simba.
Aliongeza kuwa, wakati klabu yake ilipokuwa ikifanya mipango ya kumsajili Salum Machaku kutoka Mtibwa Sugar, iliwasiliana kwanza na viongozi wake na kupata ruhusa.
"Hawa Azam ni watu wa ajabu, sisi tunaweza fujo, ambazo wanazifanya,lakini tunaheshimu sheria, vinginevyo tuna uwezo wa kusajili wachezaji wote tunaowahitaji kutoka timu yao,” alisema.
Baadhi ya vyombo vya habari viliripoti hivi karibuni kuwa, Azam imefanikiwa kumnasa Owino, ambaye alikuwa majeruhi kwa muda mrefu.
Mchezaji huyo aliondoka Simba baada ya kuumia katika michuano ya kombe la Chalenji na kumfanya afanyiwe upasuaji wa goti nchini India. Kuna habari kuwa, matibabu hayo yaligharamiwa na uongozi wa Azam.
Mwenyekiti wa Azam, Said Mohamed alipotakiwa kuzungumzia jambo hilo, alisema wana kikao kuhusu mambo mbalimbali, ikiwemo usajili wa wachezaji na kumtaka mwandishi wa habari hizi ampigie simu baadae.
Wakati hayo yakiendelea, Simba inatarajiwa kukamilisha mpango wa kumnasa beki Patrick Mafisango, ambaye alijiunga na Azam mwanzoni mwa msimu uliopita akitokea APR ya Rwanda.
Mafisango, ambaye alizaliwa Machi 7,1987 nchini Rwanda, imeelezwa kwamba anatarajiwa kuziba pengo la Owino. Pia kuna habari kuwa, Simba inataka kumrejesha kiungo wake, Ramadhani Chombo, aliyejiunga na Azam msimu uliopita.

Kaseja, Nsajigwa kuwania tuzo mwanamichezo bora


Kaseja Nsajigwa


WACHEZAJI Juma Kaseja wa Simba, Shadrack Nsajigwa wa Yanga na Mrisho Ngasa wa Azam ni miongoni mwa watakaowania tuzo za mwanamichezo bora wa mwaka 2010 zitakazotolewa na Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA).
Sherehe za utoaji wa tuzo hizo zimepangwa kufanyika Mei 6 mwaka huu kwenye hoteli ya Movenpick jijini Dar es Salaam.
Akitangaza majina hayo jana, Katibu Mkuu wa TASWA, Amir Mhando alisema jumla ya tuzo 18 zitatolewa kwa wanamichezo wa michezo tofauti.
Mhando alisema wanamichezo hao kwa upande wa wanaume na wanawake, watapigiwa kura na jopo maalumu la waandishi wa habari kwa ajili ya kuteua mchezaji bora wa mwaka.
Aliwataja wanamichezo hao kwa upande wa soka ya wanaume kuwa ni Kaseja,Nsajigwa, Ngasa na Khamis Mcha (Zanzibar Ocean View). Kwa wanawake ni Asha Rashid, Mwanahamisi Omary na Fatuma Omary.
Riadha wanaume ni Samson Ramadhan, Marco Joseph na John Bazil wakati wanawake ni Zakia Mrisho, Mary Naali na Magdalena Mushi. Wachezaji wa mpira wa wavu wanaume ni Kevin Peter (Magereza), Mbwana Ally (Mzinga Morogoro) na Ibrahim Christopher ( Nyuki Zanzibar) na wanawake ni Hellen Richard Mwegoha (Magereza), Yasinta Remmy na Zainabu Thabit (Jeshi Stars). Kwa upande wa netiboli ni Lilian Sylidion (Filbert Bayi), Mwanaid Hassan na Sekela Dominick (JKT Mbweni) wakati katika mchezo wa karate wanaume ni Sempai Steven Bella na Semapai Ayub Seleman.
Walioteuliwa kuwania tuzo kwa mchezo wa kikapu wanaume ni George Otto Tarimo (Savio-Dsm), Lusajo Samwel Mwakipunda na Gilbert Batungi (Oilers-DSM) na kwa wanawake ni Faraja Malaki- (Jeshi Stars-DSM), Zakhia Kondo (Lady Lioness-DSM) na Doritha Mbunda (JKT Stars).
Katika mchezo wa ngumi za kulipwa ni Karama Nyilawila, Mbwana Matumla na Francis Cheka wakati ngumi za ridhaa ni Revocatus Shomari, Selemani Kidunda na Said Dume.
Mchezo wa gofu kwa wanawake ni Hawa Wanyeche, Madina Iddi na Vailet Peter wakati wanaume ni Frank Roman, Adam Abbas na Isaac Anania. Kwa upande wa baiskeli wanaume ni Hamis Clement, Richard Laizer na Said Jumanne na wanawake ni Sophia Anderson, Martha Anthony na Ndashimba Kulia.
Kriketi wanaume ni Kassim Nassor, Seif Khalifa na Benson Mwita na kwa wanawake ni Hawa Salum, Mariam Said na Sophia Hemed. Mpira wa mikono wanaume ni Kazadi Monga (Magereza), Hemed Saleh na Abineri Kusena (JKT) na wanawake ni Happiness Mahinya (JKT), Teresia Kifukwe (Magereza), Zena Mohammed (JKT).
Tuzo nyingine ni ya wanamichezo wa Tanzania wanaocheza nje, ambayo itawaniwa na Hasheem Thabeet (kikapu),Henry Joseph na Nizar Khalfan (soka) na Rogers Mtagwa (ngumi) wakati wachezaji wa nje wanaocheza Tanzania ni Emmanuel Okwi (Simba), Yaw Berko (Yanga) na Kanda Kabongo (kickboxing).
Wanaowania tuzo ya mwanamichezo chipukizi kwa upande wa riadha ni John Bazil na Magdalena Cristian, Lilian Sylidion (netiboli), Vailet Peter (gofu) na mchezo wa judo ni Khamis Azan Hussein, Abeid Omar Dola na Masoud Amour Kombo wote kutoka Zanzibar

Kigogo Lyon amaliza sakata la Samatta

HATIMAYE sakata la mchezaji Mbwana Samatta huenda likafikia ukingoni baada ya aliyekuwa Mkurugenzi wa African Lyon, Jamal Kisongo kusema kuwa yeye ndiye aliyemhamisha mchezaji huyo kwenda Simba.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Kisongo alisema haoni sababu ya uongozi wa African Lyon kumng'ang'ania mchezaji huyo wakati alihamishwa kihalali.
Kisongo alisema wakati akiwa kiongozi katika klabu hiyo, alimshauri Samatta kukubali kuhamia Simba kwa ajili ya kuendeleza kipaji chake.
Alisema alisimamia hatua kwa hatua uhamisho wa mchezaji huyo na kuhakikisha anahamia Simba huku sheria na kanuni halali zikitumika katika uhamisho huo.
Alisema Samatta alikubali na akapelekewa fomu akiwa katika kambi ya timu ya taifa ya vijana na kumalizana na Simba huku African Lyon chini ya aliyekuwa Katibu Mkuu wake, Jeshi Zakaria akitia ubani kubariki kuondoka kwa mchezaji huyo.
Alisema baada ya Samatta kuondoka, African Lyon iliuzwa kwa wamiliki wa sasa wakati huo mchezaji huyo akiwa akiwa tayari amehama na kusema anashangaa kuona viongozi hao wanadai ni mchezaji wao wakati si kweli.
Alisema kutokana na hali hiyo, haoni sababu za viongozi wa sasa kuendeleza sakata hilo jambo ambalo litamchanganya mchezaji huyo na kushindwa kucheza.
Alisema kama African Lyon inataka fedha kidogo ni bora wakaongea na Simba na kumuacha mchezaji huyo akakuze kipaji chake pamoja na kwenda kujitafutia riziki yake.
Alisema hata kama Samatta ataichezea klabu hiyo, hakuna mtu yeyote atakayekuwa na mamlaka naye zaidi ya wakala wake, familia yake na klabu ya TP Mazembe.
Sakata la Samatta lilianza kuchukua kasi baada ya uongozi wa klabu ya Simba kutangaza kumuuza kwa klabu ya TP Mazembe kwa zaidi ya sh. milioni 150.
Baada ya hapo, wamiliki wa sasa wa klabu ya African Lyon waliibuka na kudai fedha za mauzo ya mchezaji huyo wanatakiwa wapewe wao kwa kuwa ni mchezaji wao halali.
Hata hivyo, sakata hilo bado halijapatiwa ufumbuzi hadi sasa kwa kuwa kila kukicha kumekuwa kukiibuka madai na malumbano tofauti.

Tuesday, April 26, 2011

UMELIONA KUNDI LA JAROWE?





Kutoka kushoto ni JACKLINE PENTZEL, WEMA SEPETU pamoja na ROSE NDAUKA kwa pamoja wanaunda kundi linaloitwa JAROWE ambapo wana malengo mengi sana kwenye Industry ya Filamu BONGO.. kwasasa hivi wamekuja na filamu yao mpya kabisa inayoitwa THE DIARY kama cover yake inavyoonekana hapo juu.. UNAIONAJE COVER...!!???



Vijana wa Uganda kutua nchini kesho

The Cobs

Vijana Stars



TIMU ya soka ya Taifa ya Uganda ya vijana wa chini ya miaka 23, The Cobs inatarajiwa kuwasili nchini kesho jioni.
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura alisema jana kuwa, timu hiyo itawasili uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere saa 10.30 jioni kwa ndege ya Uganda Air.
Wambura alisema msafara wa timu hiyo utaongozwa na Ofisa wa Shirikisho la Vyama vya Soka vya Uganda (FUFA), Sam Lwere.
Kwa mujibu wa Wambura, wachezaji na viongozi wa timu hiyo wamepangiwa kukaa kwenye hoteli ya Durban, iliyopo barabara ya Uhuru, Dar es Salaam.
The Cobs inatarajiwa kurudiana na timu ya Taifa ya vijana wa umri huo ya Tanzania, Vijana Stars, Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika pambano la marudiano la michuano ya Michezo ya Afrika.
Katika mechi ya awali, iliyochezwa wiki mbili zilizopita mjini Kampala, The Cobs iliichapa Vijana Stars mabao 2-1.
Ili Vijana Stars isonge mbele katika michuano hiyo, italazimika kuishinda The Cobs bao 1-0.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 1,000 kwa viti vya kijani, bluu na rangi ya chungwa. Kwa upande wa VIP C na B, kiingilio kitakuwa sh. 5,000 na sh. 10,000 kwa VIP A. Tiketi kwa ajili ya mchezo huo zinatarajiwa kuanza kuuzwa keshokatika vituo vya Premier Betting (Kariakoo- mtaa wa Sukuma, Buguruni Sokoni, Manzese Midizini, JM Mall na Tandale kwa Mtogole), Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Steers (mtaa wa Ohio na Samora), Big Bon Msimbazi (Kariakoo) na Uwanja wa Uhuru.

Friday, April 8, 2011

Bongo Fleva yamnogesha Dully Sykes

SIKU chache baada ya kudondosha ngoma mpya inayokwenda kwa jina la ‘Bongo Fleva’, msanii Dully Sykes ameamua kushusha kigongo kingine cha ‘Remix’ ya wimbo huo. Akizungumza na Burudani mjini Dar es Salaam juzi, Dully alisema ameamua kufanya hivyo kutokana na wimbo huo kupokelewa vizuri na mashabiki wake. “Nashukuru kuona kwamba mashabiki wangu wameupokea vizuri wimbo huu ndio sababu nimepata mzuka wa kufanya remix yake,”alisema msanii huyo machachari. Amewataja wasanii alioshirikiana nao kurekodi ‘remix’ hiyo kuwa ni pamoja na Profesa Jay, Lady JayDee na Mwana Falsafa. Alisema ameamua kuwapa shavu wasanii hao katika kibao hicho kwa sababu ya uzito wao na heshima yao katika muziki wa kizazi kipya. “Nimewapa heshima hiyo wasanii hawa kwa sababu wamekaa kwenye game kwa muda mrefu sana,”alisema Dully, ambaye kabla ya kibao hicho, alitamba kwa wimbo wake wa ‘Shekide’. Amewataka mashabiki wake kukaa mkao wa kula kukisubiri kibao hicho kwa sababu kitakuwa moto wa kuotea mbali kuliko kile cha awali. Dully, ambaye ni mtoto wa mkongwe wa muziki nchini, Ebby Sykes alianza kupata umaarufu mwanzoni mwa miaka ya 2000 alipoibuka na albamu yake ya kwanza ya ‘Historia ya Kweli’. Kabla ya albamu hiyo, msanii hiyo alitamba kwa vibao vyake vya ‘Julieta’, ‘Salome’, ‘Leah’. Mwaka 2003 aliibuka na albamu ya ‘Handsome’ kabla ya kushusha albamu ya ‘Hunifahamu’ mwaka 2005. Mwaka 2004, Dully alishinda tuzo ya albamu bora ya hip hop kupitia albamu ya ‘Handsome’ na kibao chake cha ‘Dhahabu’ kilishinda tuzo ya wimbo bora wa kushirikisha wasanii wengine. Aliimba wimbo huo kwa kuwashirikisha Joslin na Mr. Blue. Msanii huyo pia aling’ara mwaka 2008 baada ya kibao chake cha ‘Baby Candy’ kushinda tuzo ya wimbo bora wa reggae. Baadaye aling’ara kwa vibao vya ‘Nyambizi’ na ‘Kuche Kuche’.

JULIO: Kuitoa Cameroon inawezekana


TIMU ya soka ya taifa ya vijana wa chini ya miaka 23 ya Tanzania, Vijana Stars, mwishoni mwa wiki iliyopita ilichapwa mabao 2-1 na Cameroon katika mechi ya awali ya raundi ya kwanza ya michuano ya kuwania kufuzu kucheza Michezo ya Olimpiki ya mwaka 2013. Katika makala hii, Kocha Mkuu wa timu hiyo, Jamhuri Kihwelu anaelezea nafasi ya timu hiyo katika mechi ya marudiano, itakayochezwa keshokutwa mjini Dar es Salaam.

SWALI: Unadhani ni kitu gani kilichosababisha timu yako ifungwe katika mechi yenu ya awali iliyochezwa nchini Cameroon?

JIBU: Kikosi changu kilicheza vizuri, ingawa kulitokea tatizo dogo ambalo lilisababisha kufungwa. Kwa jumla nawapongeza wachezaji wangu kwa kuonyesha uwezo mkubwa katika mchezo huo. Wapinzani wetu sio wabaya. Ni timu nzuri na inaundwa na wachezaji wengi wanaocheza soka ya kulipwa Ulaya na ndio walioisaidia kwa kiasi kikubwa katika mechi hiyo. Hata hivyo, nafasi ya kusonga mbele kwetu bado ni kubwa. Bado vijana wangu wana ari kubwa ya kushinda mechi ya marudiano. Ili hilo liwezekane, nimeamua kubadili mfumo wa mazoezi. Nimeamua kuwapeleka gym wachezaji wangu kwa lengo la kuwaongezea nguvu za mwili na stamina ili waweze kukabiliana vyema na wapinzani wetu, ambao wanacheza mpira wa kutumia nguvu zaidi kuliko akili. Mbali na mazoezi hayo, nimekuwa nikiwapa pia mafunzo ya darasani ili kuhakikisha wanauelewa vyema mfumo ninaowafundisha wa kulinda na kushambulia.

SWALI: Unadhani mafunzo hayo yatawawezesha vijana wako kushinda mchezo wa Jumamosi? JIBU: Mimi pamoja na benchi langu la ufundi tuna imani kubwa kwamba vijana wanayaelewa na kuyazingatia vyema mafunzo tunayowapatia na wana uwezo wa kuishinda Cameroon. Kama nilivyosema awali, Cameroon hawatishi sana kama tulivyokuwa tukiwafikiria. Lazima tuwafunge katika mechi ya Jumamosi. Hilo lipo wazi kwa sababu tunajivunia kwamba tutakuwa tukicheza kwenye uwanja wetu wa nyumbani.

SWALI: Huoni kama kuna tatizo kwenye kikosi chako kutokana na baadhi ya wachezaji muda mwingi kuwa katika timu zao, kama Mbwana Samatta na wengineo wanaocheza ligi kuu?

JIBU: Kuchelewa kujiunga kambini kwa baadhi ya wachezaji kunaweza kukasababisha kuwepo kwa baadhi ya mapungufu katika mfumo wa uchezaji, lakini bado hilo sio tatizo kubwa sana. Kwa vile wanaelewana wanapokuwa uwanjani, nadhani hakutakuwa na matatizo makubwa.

SWALI: Je, umekuwa ukipata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) katika maandalizi ya mchezo huo?

JIBU: Kwa kweli nawashukuru sana viongozi wa TFF kwa vile wamekuwa karibu sana na sisi katika maandalizi ya kuhakikisha timu yetu inaifunga Cameroon. Pia napenda kuwapongeza viongozi wa serikali kutokana na kutuunga mkono na mara kadhaa wamekuwa wanakuja kuangalia jinsi tunavyoendelea na maandalizi ya kuiua Cameroon.

SWALI: Una ujumbe gani kwa mashabiki wa soka hapa nchini kuhusu mchezo wa Jumamosi ama unatoa ahadi gani?

JIBU: Nawaomba mashabiki wa soka, bila kujali itikadi zao, wafike kwa wingi kwenye uwanja wa Taifa na kuwashangilia kwa nguvu zote wachezaji wetu ili tuweze kushinda mchezo huo. Ieleweke kuwa, ushirikiano wa mashabiki ni jambo muhimu katika kupata ushindi. Wachezaji wanayo sehemu yao, lakini sehemu nyingine muhimu ya ushindi hutokana na mashabiki. Tunahitaji bao moja pekee ili kusonga mbele na hilo linawezekana.

SWALI: Timu yako imeweka kambi wapi na kuna matatizo yoyote yaliyojitokeza kambini hadi sasa?

JIBU: Tumeweka kambi Mbamba Beach na namshukuru Mungu kwamba hadi sasa hakuna tatizo lolote lililojitokeza. Kambi ipo katika mazingira mazuri na wachezaji wanaifurahia. Deni tulilonalo kwa watanzania ni kushinda mechi hiyo muhimu.

SWALI: Kutakuwepo na mabadiliko yoyote kwenye kikosi chako kitakachocheza Jumamosi na kile kilichocheza Cameroon?

JIBU: Sidhani kama kutakuwepo na mabadiliko makubwa. Hiyo inategemea na hali za wachezaji zitakavyokuwa. Bado ninaendelea na mazoezi ya kuangalia nani atakuwa fiti zaidi kwa ajili ya mchezo huo. Upangaji wa timu pia utategemea na mfumo tunaotumia. Ni mapema mno kutaja kikosi kitakachocheza mechi hiyo kwa sasa.

Manji arejesha logo Yanga

MFADHILI Mkuu wa klabu ya Yanga, Yusuf Manji ameamua kurejesha mali mbalimbali za klabu hiyo na kuamua kutojihusisha na jambo lolote, ikiwa ni pamoja na usajili wa wachezaji wapya. Mali zilizorejeshwa na Manji kwa klabu hiyo ni pamoja na logo ya Yanga na gazeti la Yanga Imara, lililokuwa likimilikiwa na klabu hiyo. Habari za uhakika zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa, Manji amefikia uamuzi huo baada ya kuona hali si shwari ndani ya klabu hiyo. Kwa mujibu wa habari hizo, Manji amemueleza Katibu Mkuu wa muda wa klabu hiyo, Celestine Mwesingwa kwamba ameamua kufanya hivyo kwa sababu hafurahishwi na mgogoro ulipo sasa Yanga. Logo ya Yanga ilisajiliwa na uongozi wa zamani uliokuwa chini ya Iman Madega, ambapo Manji aliingia nao mkataba na kukubaliana kuilipa klabu hiyo sh. milioni 12.5 kila mwezi. Kufuatia mkataba huo, mtu yoyote aliyekuwa akitaka kutengeneza kitu chochote chenye nembo ya Yanga, alipaswa kuwasiliana na Manji ili klabu hiyo iweze kunufaika kimapato. Uamuzi huo wa Manji umewaweka kwenye wakati mgumu viongozi wa Yanga, akiwemo Mwesingwa, ambaye ameshauriwa na mfadhili huyo afunge ofisi anayoitumia ndani ya jengo la klabu hiyo. Tayari ofisi ya katibu mkuu huyo wa Yanga imeshafungwa na kuna habari kuwa, Manji amepanga kuwalipa madai yao wachezaji wote wa klabu hiyo na watendaji wengine mwishoni mwa mwezi huu. “Manji hafurahishwi na hali ilivyo sasa ndani ya Yanga, hasa mvutano uliozuka baina ya Mwenyekiti Lloyd Nchunga na makamu wake,David Mosha, ambaye alitangaza kujiuzulu,” kilisema chanzo cha habari. Mbali na kutofurahishwa na mvutano huo, chanzo hicho kilisema Manji amekerwa kuona Yanga imeshindwa kupata mafanikio katika ligi ya msimu huu na michuano ya kimataifa, ambapo ilitolewa raundi ya kwanza. Kubwaga manyanga kwa Manji kumempa hofu kubwa Nchunga kuhusu usajili wa wachezaji wapya kwa ajili ya msimu ujao wa ligi. Manji ndiye aliyekuwa akigharamia usajili wa wachezaji na kuwalipa mishahara. Kuna habari kuwa, baadhi ya wachezaji nyota wa Yanga wameweka msimamo wa kufungasha virago msimu ujao kutokana na kutokuwa na uhakika wa ajira yao kufuatia Manji kubwaga manyanga. Mbali na kufadhiliwa na Manji, Yanga pia imeingia mkataba na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), ambayo hulipa sehemu ndogo ya mishahara ya wachezaji. Juhudi za kumpata Manji jana zilishindikana kutokana na kila mara simu yake ya mkononi ilipopigwa, kupokewa na msaidizi wake, ambaye alidai kuwa, bosi wake huyo alikuwa kwenye kikao. Habari zaidi zimeeleza kuwa, uongozi wa klabu hiyo upo mbioni kumwangukia aliyekuwa makamu mwenyekiti Mosha ili kumshawishi arejee madarakani kwa lengo la kuokoa jahazi la usajili wa wachezaji msimu ujao.

Vijana Stars yaikamia Cameroon

TIMU ya soka ya taifa ya vijana wa chini ya miaka 23, Vijana Stars imetamba kuwa, itatoa kipigo kwa Cameroon katika mechi yao ya marudiano. Vijana Stars na Cameroon zitarudiana kesho katika mechi ya michuano ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Olimpiki za mwaka 2013, itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Akizungumza mjini Dar es Salaam juzi, mshambuliaji Mbwana Samatta alisema wamepania kuitoa nishai Cameroon na kutoa onyo kwa timu zingine zinazoshiriki michuano hiyo. Samatta alisema wamefanya mazoezi ya kutosha kwa ajili ya kujiandaa kwa mechi hiyo na kuongeza kuwa, wana uhakika mkubwa wa kuibuka na ushindi. "Hatutishiki na Cameroon kwa sababu ni timu ya kawaida tu. Uwezo wa kuishinda na kusonga mbele tunao kwa sababu wachezaji wote wana ari kubwa,"alisema. Katika mechi ya awali, iliyochezwa wiki mbili zilizopita mjini Yaounde, Cameroon iliichapa Vijana Stars mabao 2-1. Ili isonge mbele, Vijana Stars inahitaji ushindi wa bao 1-0. Wakati huo huo, mjumbe wa heshima wa Shirikisho la Soka la Afrika (CAF), Said Hamad El-Maamry anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika pambano kati ya Vijana Stars na Cameroon. Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, El-Maamry amethibitisha kuhudhuria pambano hilo.

OBREN AREJEA BONGO KIAINA!

KIPA wa zamani wa Yanga, Obren Curkovic akiwa ameketi kwenye jukwaa la Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam pamoja na baadhi ya mashabiki wakati wa mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara kati ya Azam na Polisi, iliyochezwa juzi. Kuna habari kuwa, Obren huenda akasajiliwa na Azam katika msimu ujao wa ligi kuu.

Thursday, April 7, 2011

Polisi kumwaga ajira kwa mastaa

UONGOZI wa timu ya soka ya Polisi Dodoma umepanga kumwaga ajira ya kudumu kwa wachezaji nyota ili kujenga kikosi imara msimu ujao. Katibu Mkuu wa timu hiyo, Leonard Kijangwa alisema mjini Dar es Salaam juzi kuwa, kwa sasa wanasubiri ligi kuu ya Tanzania Bara imalizike kabla ya kuanza kutoa ajira hizo. Kijangwa alisema baada ya kumalizika kwa ligi hiyo, watakutana na viongozi wa benchi la ufundi kwa ajili ya kufanya tathimini ya ushiriki wa timu yao na pia kupitia mapendekezo ya Kocha John Simkoko. "Tumepanga kukutana mara ligi itakapomalizika,lengo letu ni kufanya usajili wa nguvu, lakini kwa kufuata mapendekezo na ushauri wa kocha wetu Simkoko,"alisema Kijangwa. Alisema wamejipanga vyema kusajili mchezaji yeyote, ambaye atapendekezwa na viongozi wa benhci la ufundi ili kuhakikisha wanakuwa na timu bora, ambayo msimu ujao itatoa ushindani mkali katika ligi kuu. Kijangwa alisema wamechoka kuiona timu hiyo ikiendelea kufanya vibaya katika ligi, hivyo dhamira yao kubwa ni kuwa na timu kali na yenye uwezo wa kutwaa ubingwa. "Nawaomba wachezaji wote wenye nia ya kucheza mpira, waondoke katika timu kubwa na kuja Polisi Dodoma ili waweze kupatiwa fomu za usajili na ajira ya kudumu kwani hata kama uwezo wao kisoka utaisha, wataendelea kuwepo katika ajira,"alisema Kijangwa. Habari zaidi zimeeleza kuwa timu hiyo imepanga kufanya mazungumzo na mshambuliaji wa Simba, Mbwana Samata na mastaa wengine ili kuwashawishi waweze kujiunga nao na timu hiyo na kupewa ajira.