KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, June 23, 2011

Sista P aburuzwa kortini

MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Happy Thadfi 'Sister P' amepandishwa kizimbani kujibu shitaka la kujeruhi kwa kutumia chupa.
Happy (26), mkazi wa Mwananyamala kwa Kopa, Dar es Salaam, alipandishwa kizimbani jana katika Mahakama ya Mwanzo Kinondoni.
Mbele ya Hakimu wa Mahakama hiyo, Hanifa Mwingira, karani wa mahakama, Shani Idi alidai kuwa, mshitakiwa alitenda kosa hilo Juni 21, mwaka huu, saa 3.00 usiku, maeneo ya Mwananyamala.
Shani, alidai kuwa, msanii huyo alimpiga kwa chupa Jackson Tenga kichwani na kumsababishia majeraha katika sehemu mbalimbali za mwili wake.
Mshtakiwa alikana shitaka hilo na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na kuomba upangiwe tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo.
Hakimu Hanifa alisema haki ya dhamana kwa mshitakiwa ipo wazi na kumtaka awe na wadhamini wawili wanaotambulika kisheria.
Kesi hiyo iliahirishwa hadi Julai 7 mwaka huu, itakapotajwa tena na mshitakiwa yuko nje kwa dhamana.
Happy, ambaye ni maarufu zaidi kwa jina la Sista P, aliwahi kutamba kimuziki kutokana na vibao vyake mbalimbali, kikiwemo ‘Wanachonga sana juu yangu’. Kwa sasa, msanii huyo anatamba kwa kibao cha ‘Nani mkali’, alichomshirikisha Ney wa Mitego.
Akizungumza akiwa nje ya mahakama, Happy ambaye alionekana kuchoka na kuwa kama mtu aliyeshikwa na usingizi alisema, alikuwa kimya kwa muda mrefu kwa vile yupo kwenye maandalizi ya kurekodi wimbo mpya.
Msanii huyo mwenye makeke aliutaja wimbo wake mpya kuwa ni ‘Wapotezee’, ambao amemshirikisha Dully Sykes.
Baadhi ya watu waliokuwepo mahakamani hapo walionekana kumshangaa msanii huyo kutokana na mabadiliko makubwa aliyokuwa nayo, hasa mwili wake kupungua.

RATIBA YA LIGI KUU ENGLAND

Jumamosi, Agosti 13, 2011
Blackburn Rovers vs Wolverhampton
Fulham vs Aston Villa
Liverpool vs Sunderland
Manchester City vs Swansea City
Newcastle United vs Arsenal
Queens Park Rangers vs Bolton
Stoke City vs Chelsea
Tottenham vs- Everton
West Bromwich vs Manchester United
Wigan Athletic vs Norwich City
Jumamosi, Agosti 20, 2011
Arsenal vs Liverpool
Aston Villa vs Blackburn Rovers
Bolton vs Manchester City
Chelsea vs West Bromwich
Everton vs Queens Park Rangers
Manchester United vs Tottenham Hotspur
Norwich City vs Stoke City
Sunderland vs Newcastle United
Swansea City vs Wigan Athletic
Wolverhampton vs Fulham
Jumamosi, Agosti 27, 2011
Aston Villa vs Wolverhampton
Blackburn Rovers vs Everton
Chelsea vs Norwich City
Liverpool vs Bolton Wanderers
Manchester United vs Arsenal
Newcastle United vs Fulham
Swansea City vs Sunderland
Tottenham vs Manchester City
West Bromwich vs Stoke City
Wigan Athletic vs Queens Park Rangers
Jumamosi, Septemba 10, 2011
Arsenal vs Swansea City
Bolton Wanderers vs Manchester United
Everton vs Aston Villa
Fulham vs Blackburn Rovers
Manchester City vs Wigan Athletic
Norwich City vs West Bromwich
Queens Park Rangers vs Newcastle United
Stoke City vs Liverpool
Sunderland vs Chelsea
Wolverhampton vs Tottenham
Jumamosi, Septemba 17, 2011
Aston Villa vs Newcastle United
Blackburn Rovers vs Arsenal
Bolton Wanderers vs Norwich City
Everton vs Wigan Athletic
Fulham vs Manchester City
Manchester United vs Chelsea
Sunderland vs Stoke City
Swansea City vs West Bromwich
Tottenham vs Liverpool
Wolverhampton vs Queens Park Rangers
Jumamosi, Septemba 24, 2011
Arsenal vs Bolton Wanderers
Chelsea vs Swansea City
Liverpool vs Wolverhampton
Manchester City vs Everton
Newcastle United vs Blackburn Rovers
Norwich City vs Sunderland
Queens Park Rangers vs Aston Villa
Stoke City vs Manchester United
West Bromwich vs Fulham
Wigan Athletic vs Tottenham
Jumamosi, Oktoba Mosi, 2011
Aston Villa vs Wigan Athletic
Blackburn Rovers vs Manchester City
Bolton Wanderers vs Chelsea
Everton vs Liverpool
Fulham vs Queens Park Rangers
Manchester United vs Norwich City
Sunderland vs West Bromwich
Swansea City vs Stoke City
Tottenham Hotspur vs Arsenal
Wolverhampton vs Newcastle United
Jumamosi, Oktoba 15, 2011
Arsenal vs Sunderland
Chelsea vs Everton
Liverpool vs Manchester United
Manchester City vs Aston Villa
Newcastle United vs Tottenham
Norwich City vs Swansea City
Queens Park Rangers vs Blackburn Rovers
Stoke City - Fulham
West Bromwich vs Wolverhampton
Wigan Athletic vs Bolton Wanderers
Jumamosi, Oktoba 22, 2011
Arsenal vs Stoke City
Aston Villa vs West Bromwich Albion
Blackburn Rovers vs Tottenham Hotspur
Bolton Wanderers vs Sunderland
Fulham vs Everton
Liverpool vs Norwich City
Manchester United vs Manchester City
Newcastle United vs Wigan Athletic
Queens Park Rangers vs Chelsea
Wolverhampton vs Swansea City
Jumamosi, Oktoba 29, 2011
Chelsea vs Arsenal
Everton vs Manchester United
Manchester City vs Wolverhampton
Norwich City vs Blackburn Rovers
Stoke City vs Newcastle United
Sunderland vs Aston Villa
Swansea City vs Bolton Wanderers
Tottenham vs Queens Park Rangers
West Bromwich vs Liverpool
Wigan Athletic vs Fulham
Jumamosi, Novemba 5, 2011
Arsenal vs West Bromwich
Aston Villa vs Norwich City
Blackburn Rovers vs Chelsea
Bolton Wanderers vs Stoke City
Fulham vs Tottenham
Liverpool vs Swansea City
Manchester United vs Sunderland
Newcastle United vs Everton
Queens Park Rangers vs Manchester City
Wolverhampton vs Wigan Athletic
Jumamosi, Novemba 19, 2011
Chelsea vs Liverpool
Everton vs Wolverhampton
Manchester City vs Newcastle United
Norwich City vs Arsenal
Stoke City vs Queens Park Rangers
Sunderland vs Fulham
Swansea City vs Manchester United
Tottenham vs Aston Villa
West Bromwich vs Bolton Wanderers
Wigan Athletic vs Blackburn Rovers
Jumamosi, Novemba 26, 2011
Arsenal vs Fulham
Bolton Wanderers vs Everton
Chelsea vs Wolverhampton
Liverpool vs Manchester City
Manchester United vs Newcastle United
Norwich City vs Queens Park Rangers
Stoke City vs Blackburn Rovers
Sunderland vs Wigan Athletic
Swansea City vs Aston Villa
West Bromwich vs Tottenham Hotspur
Jumamosi, Desemba 3, 2011
Aston Villa vs Manchester United
Blackburn Rovers vs Swansea City
Everton vs Stoke City
Fulham vs Liverpool
Manchester City vs Norwich City
Newcastle United vs Chelsea
Queens Park Rangers vs West Bromwich
Tottenham vs Bolton Wanderers
Wigan Athletic vs Arsenal
Wolverhampton vs Sunderland
Jumamosi, Desemba 10, 2011
Arsenal vs Everton
Bolton Wanderers vs Aston Villa
Chelsea vs Manchester City
Liverpool vs Queens Park Rangers
Manchester United vs Wolverhampton
Norwich City vs Newcastle United
Stoke City vs Tottenham
Sunderland vs Blackburn Rovers
Swansea City vs Fulham
West Bromwich vs Wigan Athletic
Jumamosi, Desemba 17, 2011
Aston Villa vs Liverpool
Blackburn Rovers vs West Bromwich
Everton vs Norwich City
Fulham vs Bolton Wanderers
Manchester City vs Arsenal
Newcastle United vs Swansea City
Queens Park Rangers vs Manchester United
Tottenham vs Sunderland
Wigan Athletic vs Chelsea
Wolverhampton vs Stoke City
Jumanne, Desemba 20, 2011
Queens Park Rangers vs Sunderland
Tottenham Hotspur vs Chelsea
Wigan Athletic vs Liverpool
Wolverhampton vs Norwich City
Jumatano, Desemba 21, 2011
Aston Villa vs Arsenal
Blackburn Rovers vs Bolton Wanderers
Everton vs Swansea City
Fulham vs Manchester United
Manchester City vs Stoke City
Newcastle United vs West Bromwich
Jumatatu, Desemba 26, 2011
Arsenal vs Wolverhampton
Bolton Wanderers vs Newcastle United
Chelsea vs Fulham
Liverpool vs Blackburn Rovers
Manchester United vs Wigan Athletic
Norwich City vs Tottenham
Stoke City vs Aston Villa
Sunderland vs Everton
Swansea City vs Queens Park Rangers
West Bromwich vs Manchester City
Jumamosi, Desemba 31, 2011
Arsenal vs Queens Park Rangers
Bolton Wanderers vs Wolverhampton
Chelsea vs Aston Villa
Liverpool vs Newcastle United
Manchester United vs Blackburn Rovers
Norwich City vs Fulham
Stoke City vs Wigan Athletic
Sunderland vs Manchester City
Swansea City vs Tottenham
West Bromwich vs Everton
Jumatatu, Januari 2, 2012
Aston Villa vs Swansea City
Blackburn Rovers vs Stoke City
Everton vs Bolton Wanderers
Fulham vs Arsenal
Manchester City vs Liverpool
Newcastle United vs Manchester United
Queens Park Rangers vs Norwich City
Tottenham vs West Bromwich
Wigan Athletic vs Sunderland
Wolverhampton vs Chelsea
Jumamosi, Januari 14, 2012
Aston Villa vs Everton
Blackburn Rovers vs Fulham
Chelsea vs Sunderland
Liverpool vs Stoke City
Manchester United vs Bolton Wanderers
Newcastle United vs Queens Park Rangers
Swansea City - Arsenal
Tottenham vs Wolverhampton
West Bromwich Albion vs Norwich City
Wigan Athletic vs Manchester City
Jumamosi, Januari 21, 2012
Arsenal vs Manchester United
Bolton Wanderers vs Liverpool
Everton vs Blackburn Rovers
Fulham vs Newcastle United
Manchester City vs Tottenham
Norwich City vs Chelsea
Queens Park Rangers vs Wigan Athletic
Stoke City vs West Bromwich
Sunderland vs Swansea City
Wolverhampton vs Aston Villa
Jumanne, Januari 31, 2012
Bolton Wanderers vs Arsenal
Manchester United vs Stoke City
Sunderland vs Norwich City
Swansea City vs Chelsea
Tottenham vs Wigan Athletic
Wolverhampton vs Liverpool
Jumatano, Februari Mosi, 2012
Aston Villa vs Queens Park Rangers
Blackburn Rovers vs Newcastle United
Everton vs Manchester City
Fulham vs West Bromwich
Jumamosi, Februari 4, 2012
Arsenal vs Blackburn Rovers
Chelsea vs Manchester United
Liverpool vs Tottenham
Manchester City vs Fulham
Newcastle United vs Aston Villa
Norwich City vs Bolton Wanderers
Queens Park Rangers vs Wolverhampton
Stoke City vs Sunderland
West Bromwich Albion vs Swansea City
Wigan Athletic vs Everton
Jumamosi, Februari 11, 2012
Aston Villa vs Manchester City
Blackburn Rovers vs Queens Park Rangers
Bolton Wanderers vs Wigan Athletic
Everton vs Chelsea
Fulham vs Stoke City
Manchester United vs Liverpool
Sunderland vs Arsenal
Swansea City vs Norwich City
Tottenham vs Newcastle United
Wolverhampton vs West Bromwich
Jumamosi, Februari 25, 2012
Arsenal vs Tottenham Hotspur
Chelsea vs Bolton Wanderers
Liverpool vs Everton
Manchester City vs Blackburn Rovers
Newcastle United vs Wolverhampton
Norwich City vs Manchester United
Queens Park Rangers vs Fulham
Stoke City vs Swansea City
West Bromwich vs Sunderland
Wigan Athletic vs Aston Villa
Jumamosi, Machi 3, 2012
Blackburn Rovers vs Aston Villa
Fulham vs Wolverhampton
Liverpool vs Arsenal
Manchester City vs Bolton Wanderers
Newcastle United vs Sunderland
Queens Park Rangers vs Everton
Stoke City vs Norwich City
Tottenham vs Manchester United
West Bromwich Albion vs Chelsea
Wigan Athletic vs Swansea City
Jumamosi, Machi 10, 2012
Arsenal vs Newcastle United
Aston Villa vs Fulham
Bolton Wanderers vs Queens Park Rangers
Chelsea vs Stoke City
Everton vs Tottenham
Manchester United vs West Bromwich
Norwich City vs Wigan Athletic
Sunderland vs Liverpool
Swansea City vs Manchester City
Wolverhampton vs Blackburn Rovers
Jumamosi, Machi 17, 2012
Aston Villa vs Bolton Wanderers
Blackburn Rovers vs Sunderland
Everton vs Arsenal
Fulham vs Swansea City
Manchester City vs Chelsea
Newcastle United vs Norwich City
Queens Park Rangers vs Liverpool
Tottenham vs Stoke City
Wigan Athletic vs West Bromwich
Wolverhampton vs Manchester United
Jumamosi, Machi 24, 2012
Arsenal vs Aston Villa
Bolton Wanderers vs Blackburn Rovers
Chelsea vs Tottenham
Liverpool vs Wigan Athletic
Manchester United vs Fulham
Norwich City vs Wolverhampton
Stoke City vs Manchester City
Sunderland vs Queens Park Rangers
Swansea City vs Everton
West Bromwich vs Newcastle United
Jumamosi, Machi 31, 2012
Aston Villa vs Chelsea
Blackburn Rovers vs Manchester United
Everton vs West Bromwich
Fulham vs Norwich City
Manchester City vs Sunderland
Newcastle United vs Liverpool
Queens Park Rangers vs Arsenal
Tottenham vs Swansea City
Wigan Athletic vs Stoke City
Wolverhampton vs Bolton Wanderers
Jumamosi, Aprili 7, 2012
Arsenal vs Manchester City
Bolton Wanderers vs Fulham
Chelsea vs Wigan Athletic
Liverpool vs Aston Villa
Manchester United vs Queens Park Rangers
Norwich City vs Everton
Stoke City vs Wolverhampton
Sunderland vs Tottenham
Swansea City vs Newcastle United
West Bromwich vs Blackburn Rovers
Jumatatu, Aprili 9, 2012
Aston Villa vs Stoke City
Blackburn Rovers vs Liverpool
Everton vs Sunderland
Fulham vs Chelsea
Manchester City vs West Bromwich
Newcastle United vs Bolton Wanderers
Queens Park Rangers vs Swansea City
Tottenham vs Norwich City
Wigan Athletic vs Manchester United
Wolverhampton vs Arsenal
Jumamosi, Aprili 14, 2012
Arsenal vs Wigan Athletic
Bolton Wanderers vs Tottenham
Chelsea vs Newcastle United
Liverpool vs Fulham
Manchester United vs Aston Villa
Norwich City vs Manchester City
Stoke City vs Everton
Sunderland vs Wolverhampton
Swansea City vs Blackburn Rovers
West Bromwich vs Queens Park Rangers
Jumamosi, Aprili 21, 2012
Arsenal vs Chelsea
Aston Villa vs Sunderland
Blackburn Rovers vs Norwich City
Bolton Wanderers vs Swansea City
Fulham vs Wigan Athletic
Liverpool vs West Bromwich
Manchester United vs Everton
Newcastle United vs Stoke City
Queens Park Rangers vs Tottenham
Wolverhampton vs Manchester City
Jumamosi, Aprili 28, 2012
Chelsea vs Queens Park Rangers
Everton vs Fulham
Manchester City vs Manchester United
Norwich City vs Liverpool
Stoke City vs Arsenal
Sunderland vs Bolton Wanderers
Swansea City vs Wolverhampton
Tottenham Hotspur vs Blackburn Rovers
West Bromwich vs Aston Villa
Wigan Athletic vs Newcastle United
Jumamosi, Mei 5, 2012
Arsenal vs Norwich City
Aston Villa vs Tottenham
Blackburn Rovers vs Wigan Athletic
Bolton Wanderers vs West Bromwich
Fulham vs Sunderland
Liverpool vs Chelsea
Manchester United vs Swansea City
Newcastle United vs Manchester City
Queens Park Rangers vs Stoke City
Wolverhampton vs Everton
Jumapili, Mei 13 2012
Chelsea vs Blackburn Rovers
Everton vs Newcastle United
Manchester City vs Queens Park Rangers
Norwich City vs Aston Villa
Stoke City vs Bolton Wanderers
Sunderland vs Manchester United
Swansea City vs Liverpool
Tottenham vs Fulham
West Bromwich vs Arsenal
Wigan Athletic vs Wolverhampton

Isha Mashauzi avunja ukimya



MWIMBAJI nyota wa muziki wa taarab nchini, Isha Ramadhani ‘Mashauzi’ ameamua kuvunjika ukimya kwa kusema bado ni mwimbaji halali wa kundi la Jahazi.
Isha ameelezea msimamo wake huo baada ya kuwepo na uvumi kwamba, ameamua kujiengua Jahazi na kuunda kundi lake akishirikiana na mama yake mzazi, Rukia.
Akizungumza kwa njia ya simu jana, Isha alisema bado hajafikiria kuhama katika kundi la Jahazi, linaloongozwa na Mzee Yussuf.
"Sio kweli, sijahama Jahazi, mimi bado ni mwimbaji halali wa kundi hilo na wala sijafikiria kabisa kuhama kwa sasa,”alisema mwimbaji huyo mwenye makeke.
“Isipokuwa baadhi ya siku huwa najumuika na wasanii mbalimbali kwa ajili ya kufanya maonyesho. Nadhani ndiyo sababu baadhi ya watu wakiniona, wanadai nimehama kwenye kundi langu," aliongeza.
Isha alikiri kuwa, ni kweli hakusafiri na kundi hilo hivi karibuni katika ziara yake ya mikoani kutokana na matatizo binafsi ya kifamilia na kwamba aliomba ruhusa kwa uongozi.
Akizungumzia matarajio yake ya baadaye, Isha alisema amepania kuwa msanii wa kimataifa wa muziki huo na kuongeza kuwa, amejipanga vyema kukamilisha ndoto hiyo.

Shiboli, Jabu, Shamte wauzwa kwa mkopo

Na Gule Mandago, DSJ
KLABU ya Simba imetangaza kuwatema wachezaji wake saba wa zamani, ambao itawauza kwa mkopo kwa klabu zingine katika msimu ujao wa ligi kuu ya Tanzania Bara.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Angetile Osiah alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, Simba iliwasilisha orodha ya wachezaji hao kwa shirikisho hilo juzi.
Aliwataja wachezaji hao kuwa ni Aziz Gila, Meshack Abel, David Naftali, Juma Jabu na Haruna Shamte.
Angetile alisema Simba imeamua kuwauza wachezaji hao kwa mkopo kwa vile bado wana mikataba na klabu hiyo.
Alisema Simba pia imetangaza kuwaacha Rashid Gumbo, Hillary Echessa na Emmanuel Okwi kutokana na mikataba yao kumalizika.Tayari Gumbo ameshasajiliwa na Yanga.
Katibu Mkuu huyowa TFF pia alisema, Simba imewauza wachezaji wake wengine watatu, Mbwana Samatta, Patrick Ochan na Abdulrahim Humud kwa klabu za TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na Azam FC.
Barua ya Simba iliyotumwa TFF imeeleza kuwa, klabu hiyo haitarajii kuwaacha wachezaji wake wengine walioichezea timu hiyo msimu uliopita.
Baadhi ya wachezaji hao ni makipa Juma Kaseja na Ally Mustapha Barthez, Salum Kanoni, Kelvin Yondan, Juma Nyoso, Mohamed Banka, Shija Mkina, Mussa Hassan ‘Mgosi’ na Nico Nyagawa.
Wakati huo huo, viongozi wa klabu ya Simba wameanza kufanya mazungumzo na uongozi wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa ajili ya kumuombea ruhusa ya usajili kiungo, Mwinyi Kazimoto. Mbali na Kazimoto, Simba pia imeanza kufuatilia uhamisho wa wachezaji Salum Machaku na Obadia Mungusa kwa klabu ya Mtibwa Sugar ya Morogoro.
Simba pia huenda ikamrejesha kundini, mshambuliaji wake wa zamani, Ulimboka Mwakingwe, ambaye aliuzwa kwa mkopo kwa timu ya Majimaji ya Songea.
Kuna habari pia kuwa, Simba inafanya mipango ya kuwasajili wachezaji wawili kutoka nchi za Nigeria na Ghana. Hata hivyo, majina ya wachezaji hao bado hayajawekwa wazi.

LUKA MODRIC ANAVYOIPASUA KICHWA TOTTENHAM


LONDON, England
WAKATI klabu ya Tottenham ya England ikihaha kumbakisha kiungo wake, Luka Modric msimu ujao, mchezaji huyo amesisitiza kuwa, anataka kuondoka na kujiunga na Chelsea.
Modric (25) alielezea msimamo wake huo wiki hii huku klabu ya Chelsea ikiwa inajiandaa kuwasilisha maombo ya kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Croatia kwa mara ya pili.
Kiungo huyo alisema anataka kujiunga na Chelsea kwa vile moja ya malengo yake makubwa ni kushinda taji la ligi kuu ya England na mengineyo.
Akihojiwa na gazeti la Daily Mail la Uingereza akiwa mapumzikoni, mchezaji huyo alisema: “Nataka kuondoka Tottenham kama rafiki. Nimefurahia kuwepo kwangu hapa, lakini sasa ni wakati mwafaka kwangu kutafuta klabu nyingine.”
“Nilikuwa na makubaliano na mwenyekiti. Wakati nilipotia saini mkataba wangu mpya, alisema kwamba, kama klabu nyingine itatokea na kutaka kunisajili, wataifikiria ofa yao,”aliongeza.
Awali, Chelsea iliwasilisha maombi kwa Tottenham ya kutaka kumsajili kiungo huyo kwa pauni milioni 22 za Uingereza, lakini yalikataliwa. Kwa sasa, klabu hiyo inajiandaa kuongeza dau lingine na kufika pauni milioni 30.
Mbali na dau hilo, Chelsea inataka kumsajili Modric kwa kubadilishana na kiungo wake, Michael Essien.
“Chelsea ni klabu kubwa na mmiliki wake ni mtu mwenye mvuto. Wanao wachezaji wazuri na malengo yao ni kupigania mataji na kutwaa ubingwa wa ligi ya Ulaya.
“Nataka kubaki London. Nafurahia kuwepo hapa kama ilivyo kwa familia yangu. Naupenda mji huu,”alisema kiungo huyo.
Kauli ya Modric kwamba anapenda kubaki London, imezivutia klabu za Manchester United na Manchester City, lakini hazijasema lolote ama kuwasilisha maombi ya kumsajili.
“Sitaki kuwa na mabishano na Tottenham,”alisema Modric. “Mashabiki wamekuwa wazuri sana kwangu na nimeufurahia muda wote niliochezea klabu hii, lakini ni kwa sababu ya soka, wachezaji wanahama kutoka klabu moja hadi nyingine. Imewahi kutokea hivyo kwa Tottenham huko nyuma. Ni jambo la kawaida kwa mchezaji kuwa na ndoto ya kuchezea klabu kubwa.”
Modric anatarajiwa kuzungumza na Mwenyekiti wa Tottenham, Daniel Levy kuhusu mipango ya uhamisho, lakini alisisitiza kuwa, uamuzi wake wa kuhama hauhusiani na masuala ya pesa.
“Kama atakuja mtu klabuni na ofa ni nzuri kwangu na wanaikubali, bila shaka nitahama. Ni jambo zuri kwa malengo yangu ya baadaye. Nahitaji kuchezea klabu inayotwaa mataji na kucheza katika ligi ya mabingwa wa Ulaya,”alisema.
“Hii haihusu mambo ya pesa, inahusu malengo. Wakati nilipokuja England, nilikuwa na ndoto ya kutwaa mataji. Hivyo ndivyo ilivyo hadi sasa,”alisema.
“Tottenham ni klabu kubwa, ikiwa na wachezaji wazuri na kocha mzuri, lakini nataka kupigania ubingwa. Siku zote Tottenham itakuwa na nafasi moyoni mwangu. Uzoefu wangu katika ligi ya mabingwa umeniacha niwe na kiu ya mafanikio makubwa zaidi,” aliongeza kiungo huyo.
Alipoulizwa nini kitafuata kutokana na msimamo wake huo, Modric alisema: “Nahitaji kuzungumza na mwenyekiti. Siwezi kumuuliza kuhusu uhamisho, hapana. Natumaini wanaweza kufikia makubaliano. Nipo mapumziko, lakini nahitaji kuzungumza na kuona kama naweza kupata suluhisho.”
Wakati huo huo, Mwenyekiti wa Tottenham, Daniel Levy amesisitiza msimamo wake wa awali kuwa, kiungo Luka Modric hatauzwa kwa gharama yoyote.
Levy alisema wiki hii kuwa, klabu yake haijajiandaa kumuuza kiungo huyo kwa Chelsea ama klabu nyingine yoyote.
“Tumeeleza wazi msimamo wetu kuhusu jambo hilo kwa kuiandikia Chelsea,”alisema Levy. “Walikataa kuutambua msimamo wetu huo na kutangaza ofa yao hadharani.”
Tottenham imeelezea msimamo wake huo baada ya Modric kulieleza gazeti la Daily Mail kwamba anataka kuhama. Hata hivyo, Modric hajawasilisha maombi binafsi ya kutaka kuhama.
Levy alisema kwa sasa, Tottenham inajenga timu imara kwa ajili ya baadaye ili iweze kucheza kwa kiwango cha juu na kusisitiza kuwa, hakuna mchezaji yeyote mingoni mwa wachezaji nyota atakayeuzwa msimu huu.
Msimamo huo wa Tottenham imekuja siku chache baada ya Kocha Mkuu wa timu hiyo, Harry Redknapp kukaririwa akisema kuwa, ofa iliyotolewa na Chelsea kwa kiungo huyo haikubaliki.
Redknapp alisema wapo wachezaji wanaoweza kuuzwa kwa kiwango hicho cha pesa, lakini si kwa mchezaji kama Modric, ambaye alikiri wazi kwamba pengo lake haliwezi kuzibika.
Alisema iwapo Tottenham inataka kupata maendeleo zaidi, haipaswi kumuuza Modric kwa vile ni miongoni mwa wachezaji muhimu katika klabu hiyo.
Kocha huyo alisema wanapaswa kufanya kila wanaloweza kumshawishi kiungo huyo abaki White Hart Lane.
Beki wa kulia wa Tottenham, ambaye pia anachezea timu ya taifa ya vijana wa chini ya miaka 21 ya England, Kyle Walker alisema litakuwa pigo kubwa kwa klabu hiyo iwapo Modric atauzwa.
“Huwa ni vigumu kumpokonya mpira wakati wa mazoezi, ni mzuri kucheza naye, mzuri kutoa pasi na ni mchezaji wa aina yake,”alisema Kyle.
Modric, ambaye alijiunga na Tottenham mwaka 2008 akitokea Dinamo Zagreb ya Croatia, ameifungia timu hiyo mabao 12 katika mechi 120. Usajili wake uliigharimu Tottenham pauni milioni 16.6.
Katika msimu wake wa pili ndani ya klabu hiyo, alikuwa mmoja wa wachezaji waliochangia kuiwezesha timu hiyo kufuzu kucheza ligi ya mabingwa wa Ulaya kwa mara ya kwanza.
Mwaka jana, Modric alitia saini mkataba mpya wa kuichezea timu hiyo kwa miaka sita.
Hata hivyo, akihojiwa na gazeti la Jutarnji List la Croatia mwezi uliopita, Modric alisema iwapo itakuja ofa nzuri kwake na Tottenham, uwezekano wa kuhama ni mkubwa.
WASIFU WA LUKA MODRIC
Alizaliwa Septemba 9, 1985

Anacheza nafasi ya kiungo

Ni mchezaji wa Tottenham

Mechi yake ya kwanza ilikuwa dhidi ya Norwich City 2008

Ameifungia timu hiyo mabao 12

Ameichezea mechi 120

Klabu alizochezea awali ni Dinamo Zagreb, Zrinjski Mostar (mkopo), Inter Zapresic (mkopo)

Fabregas, Nasri waitega Arsenal


LONDON, England
WACHEZAJI Samir Nasri na Cesc Fabregas wa klabu ya Arsenal ya England wameendelea kumuumiza kichwa kocha mkuu wa timu hiyo, Arsene Wenger baada ya kushindwa kuweka wazi kuhusu mustakabali wao.
Wakati Fabregas amekuwa akiwindwa vikali na klabu yake ya zamani ya Barcelona ya Hispania, Nasri anaonekana kumtega Wenger baada ya kugoma kutia saini mkataba mpya.
Nasri alisema wiki hii kuwa, hawezi kutia saini mkataba mpya hadi atakapoona klabu hiyo itatumia kiasi gani cha pesa kwa ajili ya kusajili wachezaji wapya msimu ujao.
Gazeti la Times la Uingereza liliripoti kuwa, Nasri amesema atakuwa tayari kutia saini mkataba mpya iwapo atahakikishiwa kuwa, kikosi cha Arsenal kitaimarika zaidi msimu ujao.
Kiungo huyo aliweka wazi kuwa, iwapo atapata ofa nzuri kutoka katika klabu zingine, atakuwa tayari kuondoka Arsenal kwa vile lengo lake ni kutwaa mataji mengi.
Nasri alisema hadi sasa hana hakika iwapo atatia saini mkataba mpya katika klabu hiyo yenye maskani yake kwenye uwanja wa Emirates.
Kuna habari kuwa, Nasri amekuwa akiwindwa na klabu ya Manchester United, lakini Kocha Wenger hataki kumuuza licha ya kubakisha mwaka mmoja kwenye mkataba wake.
Hivi karibuni, beki Patrice Evra wa Manchester United alimtaka mchezaji huyo ajiunge na klabu hiyo kama anataka kutwaa mataji mengi katika kipindi chote atakachocheza soka England.
Uamuzi wa Nasri kukataa kutia saini mkataba mpya na Arsenal umezusha hisia kuwa, huenda kiungo huyo wa kimataifa wa Ufaransa anataka kuhama.
Akihojiwa na kituo cha radio cha TF1’s Telefoot cha Ufaransa hivi karibuni, Nasri alisema atakuwa tayari kujiunga na Manchester United iwapo klabu hiyo itamuhitaji.
“Nataka kwenda Manchester United? Tusubiri tuone kama itakuwa kweli,”alisema Nasri.
Mchezaji huyo alisema kwa sasa hawezi kutoa uamuzi wowote mpaka Ufaransa itakapocheza na timu za Ukraine na Poland katika mechi za kuwania kufuzu fainali za Ulaya za mwaka 2012.
“Sielewi iwapo nitatia saini mkataba mpya. Mazungumzo bado yanaendelea. Kwa sasa, sifikirii kuhusu hili. Tutalizungumza baada ya mechi dhidi ya Poland,”alisema.
Imeelezwa kuwa, Kocha Sir Alex Ferguson wa Manchester United anahaha kusaka kiungo mpya, kufuatia kustaafu kwa Paul Scholes wakati Wenger hayupo tayari kuona mchezaji wake anahamia kwa mahasimu wao.
Gazeti la Daily Mail la Uingereza lilimkariri Wenger hivi karibuni akisema: “Kitu kimoja cha uhakika, hatuwezi kumuuza kwa Manchester United.”
Wenger alielezea msimamo wake huo baada ya kuulizwa kuhusu mustakabali wa Nasri.
Mbali na kumnyemelea Nasri, kuna habari kuwa Ferguson pia anamuwinda kiungo Wesley Sneijder wa klabu ya Inter Milan ya Italia.
Kiungo huyo wa kimataifa wa Uholanzi pia anawindwa na klabu ya Manchester City, ambayo imetenga pauni milioni 30 za Uingereza kwa ajili ya kumsajili.
Wakala wa Nasri, Alain Migliaccio alikaririwa hivi karibuni akisema kuwa, mazungumzo kati yake na Arsenal kuhusu mkataba mpya wa mchezaji huyo hayajavunjika.
“Kabla ya kuzisikiliza timu zingine, tunahitaji na tunataka kuzungumza na Arsenal,”alisema wakala huyo.
Wakati huo huo, Wenger amesema hawezi kumuuza Fabregas kwa klabu ya Barcelona, licha ya klabu hiyo kuwasilisha ofa yenye dau kubwa.
Wenger ameelezea msimamo huo baada ya Barcelona kuwasilisha tena maombi ya kumsajili Fabregas kwa klabu ya Arsenal.
Kwa upande wake, Fabregas amesema anafurahia kuwepo Arsenal na kusisitiza kuwa, hawezi kuiumiza klabu hiyo.
“Siwezi kujitokeza mbele na kusema nataka kujiunga na Barcelona. Baada ya miaka minane Arsenal, siwezi kuiumiza klabu. Hiyo siyo desturi yangu,”alisema.
“Nina furaha kubwa kuwepo hapa. Mimi ni mchezaji wa Arsenal kwa sasa. Zilizobaki ni tetesi. Wenger anafahamu nini ninachokitaka nay eye ni bosi, anaamua,”aliongeza.
Barcelona imekuwa ikihaha kumsajili mchezaji huyo tangu msimu uliopita na hivi karibuni iliweka wazi kuwa, itamuuza mshambuliaji wake David Villa kwa Chelsea ili ipate pesa za kumsajili Fabregas.
Mabingwa hao wa ligi ya Ulaya pia wana matumaini ya kumsajili winga Alexis Sanchez kutoka Udinese ya Italia na mshambuliaji Giuseppe Rossi kutoka Villarreal ili kukiimarisha zaidi kikosi chao.
Hata hivyo, bajeti ya Barcelona ya kusajili wachezaji wapya ni pauni milioni 40, hivyo inataka iongeze fedha zingine kwa kumuuza Villa.
Villa (29), ambaye alijiunga na Barcelona msimu uliopita, akitokea Valencia, huenda akauzwa Chelsea, ambayo inahaha kusaka mshambuliaji mpya.
Awali, Chelsea ilikuwa ikitaka kumsajili Neymar kutoka Brazil, lakini mshambuliaji huyo aliamua kujiunga na Real Madrid. Kwa sasa, lengo kubwa la Chelsea ni kumnasa Villa, ambaye ana uzoefu wa kucheza pamoja na Fernando Torres.
Gazeti la Daily Mail lilimkariri Kocha Pep Guardiola wa Barcelona akisema kuwa, angependa kumbakisha Villa, hasa baada ya kuwa na msimu mzuri, lakini atakuwa tayari kumuuza kwa lengo la kukiimarisha zaidi kikosi chake.

MICHELLE JENG: NAPENDA KUSAIDIA WATOTO WENYE MATATIZO




Ni mshindi wa taji la Miss Africa Scandinavia 2010

Anasomesha watoto yatima wawili hapa Bongo

Aliwahi kupanda Mlima Kilimanjaro hadi kileleni

MSHINDI wa taji la ‘Miss Africa Scandinavia 2010’, Michelle Jeng amesema atalitumia taji hilo kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu hapa nchini.
Akihojiwa katika kipindi cha Jambo cha kituo cha televisheni cha TBC 1 mwishoni mwa wiki iliyopita, Michelle alisema siku zote yeye ni mtu anayependa kusaidia watu wenye matatizo.
Michelle (19), ambaye alishinda taji hilo mwishoni mwa mwaka jana nchini Sweden, alisema tayari ameshaanza kutoa misaada mbalimbali kwa watoto walioathirika katika milipuko ya mabomu iliyotokea kwenye kambi ya jeshi iliyopo Gongo la Mboto mjini Dar es Salaam.
Mrembo huyo alisema, alikabidhi misaada hiyo wiki iliyopita kwa Kaimu Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Mecky Sadiki.
Michelle ni mzaliwa wa Sweden. Mama yake ni mtanzania wakati baba yake ni raia wa Gambia.
Kwa mujibu wa Michelle, alikusanya vitu alivyomkabidhi mkuu huyo wa mkoa kutoka kwa watanzania mbalimbali wanaoishi na kufanyakazi nchini Sweden.
Mbali na misaada huyo, Michelle pia amejitolea kuwasomesha watoto wawili, ambao ni yatima. Alianza kuwasomesha watoto hao tangu akiwa shule ya sekondari mwaka 2005.
Alisema kwa sasa, mmoja wa watoto hao anasoma kidato cha pili katika shule moja ya sekondari mkoani Dodoma na mwingine yupo darasa la tatu katika shule moja ya msingi mjini Arusha.
Michelle, ambaye amekuwa akija nchini mara kwa mara, alisema aliwaona watoto hao mwaka huo wakati yeye na mama yake walipokuja nchini na kumtembelea mmoja wa marafiki zake.
“Unajua kusaidia kwa kutoa tu haitoshi, ni vizuri ukimsaidia mtu kwa ajili ya maisha yake ya baadaye, hasa kwa kumpatia elimu,”alisema mrembo huyo, ambaye aliwahi kupanda Mlima Kilimanjaro mwaka jana na kufanikiwa kufika hadi kileleni.
Mrembo huyo alisema amekuwa akiwalipia pesa za ada watoto hao kutokana na malipo ya kazi za muda, ambazo amekuwa akizifanya kila mwisho wa wiki. Alisema wanafunzi nchini Sweden wanaruhusiwa kufanyakazi mwisho wa wiki.
Alisema pesa zingine zinatokana na posho, ambayo amekuwa akiipata kutoka kwa serikali ya Sweden na zingine zinatokana na mikopo, ambayo amekuwa akichukua kwa ajili ya kujiendeleza.
Kwa mujibu wa Michelle, kila mtoto anayezaliwa Sweden, analipwa posho kwa ajili ya kumsaidia kielimu. Alisema lengo lake ni kuona watoto hao wawili wanafika chuo kikuu.
Alisema uamuzi wake wa kuwasaidia watoto hao umetokana na tofauti ya kimaisha aliyoiona kati ya watoto wanaoishi Sweden na wale wanaoishi katika nchi za Kiafrika.
Mrembo huyo, anayejiandaa kuingia chuo kikuu alisema, anapenda kusomea udaktari kwa vile lengo lake kubwa katika siku zijazo ni kutoa huduma ya afya, hasa kwa watoto.
“Kwa sasa nimemaliza kidato cha sita, najiandaa kuingia chuo kikuu mwakani. Nataka nitakaporudi Afrika, niwe daktari ili niwasaidie watoto na nchi yangu. Afya ni kitu muhimu. Kila mtu anayo haki ya kupatiwa matibabu,”alisema.
Michelle alishinda taji la Miss Africa Scandinavia baada ya kuwabwaga warembo wengine 20 kutoka nchi mbalimbali za Afrika. Washiriki wengine walitoka nchi za Tanzania, Togo, Cameroon, Kenya, Uganda, Sierra Leone na Gambia.
Mrembo huyo anaamini kuwa, alishinda taji hilo kutokana na kujiamini kwake, kujikubali jinsi alivyo, kutokuwa na makuu na pia kupenda kusaidia wengine.
Alisema kwa kawaida, uzuri wa mtu upo ndani yake kwa vile haujionyeshi wazi. Alisema cha msingi ni kuwafikiria na kuwasaidia watu wengine wenye matatizo.
Michelle alisema mama yake alimsaidia kwa kumpa moyo wakati wote wa maandalizi, ikiwa ni pamoja na kumtafutia nguo za Kitanzania, ambazo alizivaa wakati wa shindano hilo.
Akizungumzia hilo, mama wa mrembo huyo, anayejulikana kwa jina la Nuru alisema: “ Kila anachotaka kukifanya, huwa nampa moyo. Katika maisha ni vizuri kujaribu, usishindwe kujaribu.”
Michelle, ambaye atatimiza umri wa miaka 20 ifikapo Novemba mwaka huu alisema, hajui lolote kuhusu mashindano ya kumsaka mrembo wa Tanzania zaidi ya kusoma habari zake kupitia kwenye tovuti mbalimbali.
“Sijawahi kuyashuhudia mashindano haya wala kukutana na waliowahi kushinda taji hili. Napenda kufahamu mengi kuhusu shindano hili,”alisema.
Mrembo huyo alisema, japokuwa washindi wa taji hilo hawakuwahi kufanya vizuri katika shindano la dunia, wamekuwa wakiitangaza vyema nchi yao kimataifa. Alisema kushinda ni matokeo.
Ametoa mwito kwa wasichana wa Tanzania wanaojihusisha na fani ya urembo, waitumie vyema kujinufaisha katika maisha yao badala ya kuichukulia kuwa ya kihuni.
“Si jambo zuri kwa mrembo wa Tanzania kujikweza, wasipende kujiremba kupita kiasi, waringie rangi zao za asili. Mrembo anatakiwa kuwa mtu wa kusaidia watu wenye matatizo, awe na busara na hekima,”alisema.
Michelle alisema binafsi anaichukulia fani ya urembo kama burudani kwa vile hatarajii kujihusisha nayo kwa maisha yake yote. Alisema kwake, anachokipa kipaumbele zaidi ni masomo, hasa kuwa daktari.

NITAIFUMUA TENA YANGA-TIMBE


SWALI: Kocha Sam Timbe, umerejea hivi karibuni kutoka mapumzikoni Uganda na tayari umeanza kuinoa Yanga kwa ajili ya msimu ujao. Mikakati yako ni ipi?
JIBU: Namshukuru Mungu nimepumzika vizuri hasa baada ya kuiwezesha Yanga kuibuka na ubingwa msimu uliopita. Ninachoweza kusema ni kwamba, kwa sasa nipo kwenye kipindi kigumu sana.
Unajua kuunda kikosi cha ushindi, inabidi utulie na kushirikiana na viongozi wa klabu pamoja na benchi la ufundi kuhakikisha mnakuwa na timu imara. Mkiweza kufanya hivyo, ndipo moyo unaweza kutulia.
Msimu ujao sisi tutakuwa tunawakilisha nchi kwenye michuano ya klabu bingwa Afrika, hivyo nikifanya usajili mbovu, lazima nitakuwa na kikosi bomu.
Nimeanza utaratibu wa kupima uwezo wa wachezaji wangu katika mazoezi na mechi tulizocheza hadi sasa kabla ya kuidhinisha rasmi usajili wao kwa ajili ya msimu ujao.
Nimewaangalia baadhi ya wachezaji wanaoitwa nyota kwenye mazoezi na mechi tulizocheza na kugundua kwamba, bado kuna wachezaji, ambao wanatakiwa kufanyakazi ya ziada ili waweze kufikia viwango ninavyovihitaji.
SWALI: Ni kipi hasa ulichokigundua kwa wachezaji hao hadi sasa na ni akina nani?
JIBU: Zipo kasoro kadhaa kwa baadhi ya wachezaji. Unajua mchezaji anapohama kutoka timu moja kwenda nyingine, atakumbana na wakati mgumu kwa vile atakutana na watu, ambao hajawazoea. Hivyo nitalazimika kufanya marekebisho kadhaa katika dosari nilizozibaini.
Tayari nimeshawaona baadhi ya wachezaji, ambao nimebaini kuwa uwezo wao ni mdogo. Nitakachokifanya ni kuwaongezea makali. Kama watashindwa kwenda na kasi ninayoihitaji, itabidi tuachane nao.
Kama unavyofahamu, kikosi changu kitashiriki michuano ya klabu bingwa. Huko tutakutana na timu bora kutoka kila nchi. Hivyo lazima nijenge timu imara na yenye kuweza kutoa ushindani. Hatutaki tushiriki michuano hiyo kama wasindikizaji.
Nawapongeza viongozi wa Yanga, hasa kamati ya usajili kwa kuweza kuyafanyiakazi mapendekezo niliyoyatoa kuhusu usajili wa wachezaji wapya. Kazi waliyoifanya kwa kweli ni nzuri sana na imefanywa kwa umakini mkubwa.
SWALI:Umesema kwamba bado hujaamua kikosi chako cha kwanza kitakavyokuwa. Una maana kwamba wapo baadhi ya wachezaji ambao utalazimika kuwaacha baada ya kusajiliwa na kamati?
JIBU: Ukweni ni kwamba bado Yanga hatujatangaza rasmi kikosi chetu cha msimu ujao. Lakini napenda nikueleze kwamba, mabadiliko lazima yatakuwepo.
Kuna baadhi ya wachezaji wa nje wanaweza kuongezwa. Nimepata taarifa kwamba baadhi ya klabu, ikiwemo Yanga, zimeomba idadi ya wachezaji wa kigeni iongezwe.
Idadi ya sasa ya wachezaji watano wa kigeni kutoka nje kwa kweli ni ndogo sana. Inabidi kocha awe makini kwa vile unaweza kusajili wachezaji wenye uwezo mdogo ikawa matatizo.
SWALI: Yanga imeruhusiwa kushiriki katika michuano ya mwaka huu ya Kombe la Kagame. Umejiandaa vipi na kikosi chako?
JIBU: Nimejiandaa vizuri na kupitia michuano hiyo natarajia nitaweza kupata kikosi cha kwanza kwa ajili ya michuano ya ligi kuu msimu ujao na ile ya klabu bingwa Afrika.
Pamoja na malengo hayo, nimeshaangalia uwezo wa wachezaji waliopo katika kikosi changu kupitia mazoezi na mchezo wetu wa kirafiki dhidi ya kombaini ya Ilala na nitaendelea kufanyakazi hiyo huko Arusha, ambako tunatarajia kucheza na Gor Mahia.
Jambo la msingi ni kwamba nimepanga kuitumia michuano hiyo kutafuta kikosi cha kwanza cha ligi kuu na michuano ya kimataifa.
SWALI: Umeuonaje mfumo wa uendeshaji wa michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara?
JIBU: Binafsi nauona mfumo siyo mbaya, lakini yapo matatizo madogo madogo, likiwemo ratiba kuingiliana na michuano ya kimataifa, jambo ambalo linasababisha baadhi ya wachezaji kushindwa kuzitumikia klabu zao vizuri, hasa inapotokea wameitwa kwenye timu ya taifa.
Tatizo lingine nililolibaini ni kwamba, baadhi ya waamuzi wanashindwa kuzitafsiri vyema sheria 17 za soka na kusababisha wakati mwingine kuwepo na malalamiko kutoka kwa baadhi ya timu.
SWALI:Je, umepata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa viongozi wa klabu ya Yanga katika zoezi hili la usajili?


JIBU: Kwa kweli nawashukuru sana viongozi wa Yanga, hadi sasa tunakwenda vizuri, hakuna matatizo na hii ndiyo siri ya mafanikio ya kutwaa ubingwa msimu uliopita.

BABU NJENJE AANGUA KILIO

Babu Njenje akiwa na mwimbaji mkongwe wa taarab, Shakila Saidi




Atimiza umri wa miaka 64 sanjari na Shakila Saidi

Walizaliwa tarehe moja, mwezi mmoja na mwaka mmoja

Shakila alinyonyeshwa na mama yake Babu Njenje


ILIKUWA kama sinema ama filamu ya mauzauza. Hakuna aliyeamini nini kiliandaliwa ama kingetokea nini. Lakini ndivyo ilivyokuwa.
Mwanamuziki mkongwe wa bendi ya muziki wa dansi ya The Kilimanjaro ‘Njenje’, Mabrouk Hamisi wiki iliyopita alijikuta akitokwa machozi bila kutarajia baada ya kituo cha radio cha Clouds kuandaa kitu, ambacho kilimstaajabisha kama sio kumwacha hoi.
Siku hiyo, mtangazaji wa kipindi cha Leo Tena cha Clouds, Dina Marios alimwalika studio mwanamuziki huyo maarufu kwa jina la Babu Njenje kwa kile alichomweleza kuwa ni kurekodi naye kipindi. Babu Njenje alifika studio za Clouds akiwa na wanamuziki wenzake, akijua ni mahojiano ya kawaida. Kumbe kulikuwa na mpango maalumu wa kumshangaza. Siku hiyo ilikuwa ni siku ya kuzaliwa kwake. Alitimiza umri wa miaka 65.
Ilichokifanya Clouds ni kumshangaza mwanamuziki huyo. Kituo hicho kilianza kupiga nyimbo mbalimbali za Kilimanjaro kisha Babu Njenje akapigiwa wimbo wa kumpongeza wa ‘Happy birthday to you’.
Baada ya wimbo huo, Clouds ikamuunganisha Babu Njenje kwa njia ya simu na familia yake iliyokuwa mjini London, Uingereza bila yeye kutarajia.
Familia yote ya Babu Njenje ipo nje ya nchi. Mkewe anaishi Marekani pamoja na mtoto wake wa kwanza wa kiume, Feisal. Mtoto wake wa kike, Lulu anaishi Uingereza. Babu Njenje anao wajukuu wanne.
Katika mazungumzo hayo, familia ya Babu Njenje ilimtakia kila la heri katika siku hiyo muhimu kwake
Babu Njenje alilia sana na akasema hajawahi kushangazwa na kitu chochote katika maisha yake yote, siku hiyo ilikuwa kiboko. Mara zote alipokuwa akizungumza na familia yake, alijitahidi kujizuia kulia, lakini ilikuwa vigumu.
Babu Njenje na mkewe wote wamezaliwa tarehe na mwezi mmoja. Siku hiyo hiyo, mkewe naye alikuwa akitimiza miaka 60. Bila kujua kwamba Clouds ilishafanya mawasiliano na mkewe kwa njia ya simu, kwake kumsikia ilikuwa ni kama miujiza. Hakuamini.
Dina anasema alikaa na mwanamuziki Waziri Ally wa The Kilimanjaro na kuamua kupanga tukio hilo dogo kwa vile si jambo zuri kumuenzi mwanamuziki baada ya kufa.
Babu Njenje amekuwa na bendi ya The Kilimanjaro kwa miaka zaidi ya 38. Awali, bendi hiyo ilikuwa ikijulikana kwa jina la The Revolution kabla ya kubadili jina na kuitwa The Kilimanjaro. Lakini kwa sasa ni maarufu zaidi kwa jina la Njenje kutokana na wimbo uliobeba jina hilo.
Siku hiyo hiyo, Clouds pia ilikuwa imemwalika mkongwe wa muziki wa taarab nchini, Shakila Said. Wakongwe hao wawili, kila mmoja hakuna aliyetarajia iwapo wangekutana ndani ya studio ya kituo hicho.
Lengo la Clouds kuwakutanisha wakongwe hao ni kwa sababu wana historia inayofanana na tena yenye mvuto.
Babu Njenje na Shakila walizaliwa siku moja, tarehe moja, mwezi mmoja na mwaka mmoja. Mitaa waliyokuwa wakiishi ilikaribiana. Kutoka kwa Babu Njenje kwenda kwa Shakila ni umbali wa nyumba nne.
Babu Njenje alizaliwa asubuhi na Shakila alizaliwa jioni. Mama yake Shakila hakuwa na maziwa ya kutosha kumnyonyesha, hivyo ikabidi apelekwe kwa mama yake Babu Njenje kunyonya.
Wasanii hawa wawili wamekuwa pamoja, wamecheza pamoja na walianza kusoma madrasa pamoja. Siku hiyo kila mmoja alikuwa anatimiza umri wa miaka 65.
Haikuwahi kutokea hata mara moja kwa wakongwe hao kusherekea siku zao za kuzaliwa pamoja. Hiyo ilikuwa mara ya kwanza. Hongera Clouds.
Ilibidi Shakila apewe nafasi ya kuimba nyimbo zake mbalimbali za zamani. Kiukweli sauti yake bado ni maridhawa, licha ya umri wake mkubwa. Ni sauti adhimu. Mola aendelee kumpa afya njema.
Wote wawili bado wanatesa katika anga la muziki. Shakila ni mwimbaji mwalikwa katika kikundi cha sanaa za maonyesho cha Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).
Mbali ya sherehe hiyo ndogo, bendi ya The Kilimanjaro nayo ilimwandalia tafrija ndogo Babu Njenje kwa lengo la kumuenzi. Sherehe hiyo ilifanyika kwenye ukumbi wa Salender Bridge.
Siku hiyo, Lulu aliwasili ukumbini ghafla bila Babu Njenje kuwa na taarifa. Alikuwa ametokea Uingereza. Walikuwa hawajakutana kwa miaka mingi. Yalikuwa maajabu makubwa kwa Babu Njenje kumuona Lulu ukumbini siku hiyo.
Lulu alipewa kipaza sauti na kuanza kuimba wimbo wa Happy birthday. Aliimba wimbo huo huku akiwa anaelekea stejini, ambako baba yake alikuwa amesimama, akiwa hajui hili wala lile.
Babu Njenje alionekana kushangaa. Hakuwa anaelewa nini kinatokea. Walipokaribiana, wakakumbatiana kwa furaha ya ajabu. Hivyo ndivyo ilivyokuwa sherehe ya Babu Njenje kutimiza miaka 65.

WASHIRIKI WA MISS MORO 2011



WASHIRIKI wa shindano la kuwania taji la Miss Morogoro wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kutambulishwa kwa waandishi wa habari kwenye hoteli ya Masuka iliyopo mjini Morogoro. Shindano hilo limepangwa kufanyika Julai Mosi mwaka huu kwenye ukumbi wa hoteli ya Morogoro. (Picha na Latifah Ganzel).

SERENA AMWAGA CHOZI


LONDON, England
MCHEZA tennis nyota duniani, Serena William wa Marekani juzi aliangua kilio baada ya kumbwaga Aravane Rezai wa Ufaransa katika mechi ya michuano ya tennis ya Wimbledon.
Katika mechi hiyo, iliyokuwa na ushindani mkali, Serena alimbwaga Aravane kwa seti 2-1 na kufanikiwa kusonga raundi ya pili.
Akihojiwa na waandishi wa habari baada ya mchezo huo, Serena alisema alishindwa kujizuia kutokwa na machozi kutokana na kushinda mchezo huo.
Serena alisema kutokana na kuumia mguu na kushindwa kushiriki michuano yoyote kwa mwaka mmoja, hakuwa na matarajio ya kurejea katika kiwango chake cha kawaida.
Binti huyo wa Kimarekani aliendelea kutokwa na machozi hata alipokuwa akiondoka kwenye viwanja vya Arena, ambako michuano hiyo inafanyika.
Serena alionekana mara kwa mara akipunga mkono mwa mashabiki wake huku akipangusa uso kufuta machozi yaliyokuwa yakimtoka.
“Kwa kawaida, huwa silii. Sielewi kwa nini imenitokea hivi,”alisema Serena.
“Imekuwa vigumu, kamwe sikuamini iwapo ningerejea uwanjani. Ulikuwa mwaka mgumu kwangi na sikutarajia iwapo ningecheza tena ama kufanya chochote. Nilitaka kushinda mechi angalau moja tu katika michuano hii ya Wimbledon,”aliongeza.

VILLAS-BOAS ATUA RASMI CHELSEA


LONDON, England
HATIMAYE klabu ya Chelsea ya England imetangaza rasmi kumnyakua Kocha Andre Villas-Boas baada ya kukamilisha malipo ya kuvunja mkataba wake.
Chelsea imemnyakua kocha huyo mwenye umri mdogo kuliko makocha wa ligi kuu ya England, kutoka klabu ya FC Porto ya Ureno.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Chelsea jana ilieleza kuwa, klabu hiyo imeilipa FC Porto kitita cha pauni milioni 13.2 za Uingereza (sh. bilioni 29) kwa ajili ya kuvunja mkataba wake.
Kwa mujibu wa taarifa hayo, malipo hayo yalifanyika juzi usiku, ikiwa ni siku chache baada ya kuripotiwa kuwa, kocha huyo amewasilisha maombi ya kuvunja mkataba wake na FC Porto.
Kwa sasa, Villas-Boas yupo mapumzikoni, lakini huenda akaungana na baadhi ya maofisa wa Chelsea kwa ajili ya kukamilisha taratibu za uhamisho wake.
Habari kutoka ndani ya Chelsea zimeeleza kuwa, kocha huyo huenda akatambulishwa rasmi kwa waandishi wa habari mwezi ujao baada ya kuongoza mazoezi ya timu hiyo kwa siku chache.
Porto ilimtangaza rasmi kocha msaidizi wa timu hiyo, Vitor Pereira kuchukua nafasi ya Villas-Boas na pia kutoa taarifa kwa soko la hisa kwamba mkataba wa kocha huyo wa zamani umesitishwa.
Villas-Boas, ambaye alikuwa kufanyakazi Chelsea, akiwa msaidizi wa kocha wa zamani, Jose Mourinho, anatarajiwa kusajili wachezaji wawili wapya kutoka FC Porto. Wachezaji hao ni Falcao na Joao Moutinho.
Mbali na kusajili nyota hao wa FC Porto, kocha huyo pia anatarajiwa kuwasili London akiwa na wasaidizi wake wawili, akiwemo kocha wa viungo, Jose Maria Rocha na Daniel Souza.
Rais wa FC Porto, Jorge Nuno Pinto da Costa ametangaza rasmi thamani za wachezaji hao wawili kuwa ni pauni milioni 26.5 kwa Falcao na pauni milioni 35.5 kwa Moutinho.

YAYA TOURE AONGOZA KWA UTAJIRI AFRIKA


LONDON, England
KIUNGO wa klabu ya Manchester City ya England, Yaya Toure anaongoza kundi la wachezaji wa Afrika wanaovuna fedha nyingi kutokana na kucheza soka.
Toure amechukua nafasi hiyo baada ya kuwapiku washambuliaji, Samuel Eto'o wa Cameroon, Didier Drogba wa Ivory Coast na Michael Essien wa Ghana.
Kiungo huyo wa kimataifa wa Ivory Coast, pia anaongoza orodha ya wachezaji wanaolipwa fedha nyingi wanaocheza soka barani Ulaya.
Toure anakadiriwa kuwa na dola milioni 13.3 za Marekani (sh. bilioni 21.3). Katika orodha hiyo, kaka wa kiungo huyo, Kolo Toure, anayecheza pia Man City, anashika nafasi ya nne akiwa na dola milioni 10.3 (sh. bilioni 16.4).
Katika orodha ya majina manane ya wachezaji tajiri yaliyotangazwa jana, ni wachezaji wawili pekee wanaocheza soka nje ya England. Wachezaji hao ni Frederic Kanoute kutoka Mali, anayechezea klabu ya Sevilla ya Hispania na Mcameroon, Eto'o wa Inter Milan.
John Mikel Obi wa Chelsea, aliyewahi kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa Afrika mwaka 2005, ametajwa kushika nafasi ya tano.
Jambo la kufurahisha zaidi ni kwamba klabu za Chelsea na Manchester City zimetoa wachezaji watatu kila moja kwenye orodha hiyo.
Orodha hiyo ni kama ifuatavyo:
1) Yaya Toure (Manchester City na Ivory Coast)

- dola milioni 13.3 (sh. bilioni 21.3)
2) Samuel Eto’o (Inter na Cameroon)

- dola milioni 12 (sh. bilioni 19.2)
3) Emmanuel Adebayor (Togo na Manchester City)

- dola milioni 12 (sh. bilioni 19.2)
4) Kolo Toure (Manchester City na Ivory Coast)

- dola milioni 10.3 (sh. bilioni 16.4)
5) Frederic Kanoute (Sevilla na Mali)

- dola milioni 8.6 (sh. bilioni 13.8)
6) Didier Drogba (Chelsea na Ivory Coast)

- dola milioni 8 (sh. bilioni 12.8)
7) John Mikel Obi (Chelsea na Nigeria)

- dola milioni 5.8 (sh. bilioni 9.3)
8) Michael Essien (Chelsea na Ghana)

- dola milioni 5.5 (sh. bilioni 8.8)

Tuesday, June 21, 2011

NAOMBA KURA ZENU



Ndugu wasomaji wa blogu hii ya liwazozito, napenda kuwafahamisha kuwa, blogu yangu imechaguliwa kuwania tuzo ya blogu bora Tanzania. Awali ya yote nawashukuru wale wote waliopendekeza blogu hii iingie kwenye tuzo hiyo kupitia kipengele cha Sports na Entertainment. Pili naomba kura zenu ili blogu hii iweze kuibuka na ushindi katika tuzo hizo.

Asante kwa ushirikiano wenu.

Wednesday, June 15, 2011

Cannavaro azua balaa Yanga


WAKATI kikosi cha timu ya soka ya Yanga kikiwa kimeshaanza mazoezi rasmi kwa ajili ya michuano ijayo ya ligi kuu ya Tanzania Bara, beki Nadir Haroub 'Canavaro' amegoma kuanza mazoezi.
Habari za uhakika zilizopatikana jana kutoka ndani ya Yanga zimeeleza kuwa, Canavaro amegoma kuanza mazoezi kutokana na kutokamilishiwa malipo yake ya mkataba mpya na ule wa zamani.
Kwa mujibu wa habari hizo, Canavaro ameapa kutohudhuria mazoezi hadi atakapokamilishiwa malipo yake. Hata hivyo, haikuweza kujulikana mara moja kiasi cha pesa, ambacho mchezaji huyo anaidai Yanga.
Uchunguzi wa Burudani umebaini kuwa, kwa sasa Canavaro yupo nyumbani kwao visiwani Zanzibar, ambako alikwenda kwa mapumziko baada ya kurejea nchini kutoka Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Kuna habari kuwa, Canavaro hakumaliziwa malipo yake ya mkataba wa zamani na pia hajalipwa pesa zote za mkataba wake mpya.
Mmoja wa wachezaji, aliye karibu na Canavaro, ambaye hakupenda jina lake litajwe gazetini, alithibitisha jana kuhusu uamuzi wa mchezaji huyo kugomea mazoezi hadi atakapokamilishiwa malipo yake.
Mbali na nyota huyo, kuna habari pia kuwa, wachezaji wengine kadhaa wa Yanga nao wamepanga kugomea mazoezi iwapo hawatamaliziwa pesa zao za mikataba mipya.
Wachezaji hao wamepanga kuendesha mgomo huo kabla ya kuanza kwa michuano ya Kombe la Kagame, iliyopangwa kuanza Juni 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Hii itakuwa mara ya pili kwa wachezaji wa Yanga kupanga kugoma kwa lengo la kushinikiza walipwe malipo yao. Waliwahi kufanya hivyo mwanzoni mwa mwaka huu kabla ya ligi kuu ya msimu uliopita kumalizika.
Mgomo huo ulisababisha mfadhili mkuu wa klabu hiyo, Yusuph Manji kuitisha mikataba yao ili kujua madeni yote ya wachezaji, ambapo ilibainika kuwa, wachezaji wengi walisajiliwa kwa malipo kiduchu.
Hata hivyo, viongozi wa Yanga hawakuwa tayari kuzungumzia suala la Canavaro, lakini mmoja wa viongozi hao alisema, anachotambua ni kwamba beki huyo alitakiwa kuripoti mazoezi na wenzake Jumatatu iliyopita.
Wachezaji wa Yanga walianza mazoezi wakiwa chini ya kocha msaidizi wa timu hiyo, Fred Felix Minziro. Mazoezi hayo yanafanyika kwenye uwanja wa Kaunda, Dar es Salaam.
Wakati huo huo, Yanga inatarajiwa kushuka dimbani Jumamosi kucheza na kombaini ya Dar es Salaam katika mechi ya kirafiki itakayopigwa kwenye uwanja wa Kaunda.

MNAONAJE MKIJIUNGA NA SIMBA




Kocha Mkuu wa Simba, Moses Basena akizungumza na kiungo, Nkanu Mbiyakanga (juu) na beki Feugang Takudjo (chini) wa Motema Pembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo mara baada ya pambano kati ya timu hizo lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Simba ilishinda bao 1-0. (Picha na Emmanuel Ndege).



Sikinde sasa hakuna kulala


BENDI ya muziki wa dansi ya Extra Bongo na kikundi cha muziki wa kiasili cha Segele, vitatoa burudani katika onyesho la uzinduzi wa vyombo vipya vya Mlimani Park Orchestra.
Katibu wa Mlimani Park ‘Sikinde’, Hamisi Milambo alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, onyesho hilo limepangwa kufanyika Juni 25 mwaka huu.
Milambo alisema tayari Extra Bongo, inayoongozwa na Ally Choki pamoja na Segele, zimeshathibitisha kuisindikiza Sikinde katika onyesho hilo litakalofanyika kwenye ukumbi wa DDC Kariakoo, Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Milambo, vyombo hivyo vyenye thamani ya sh. milioni 45,vimetolewa na Kampuni ya Vinywaji ya Konyagi, ambayo ni wadhamini wakuu wa Sikinde.
“Kwa sasa, Konyagi ndio wadhamini wakuu wa Sikinde na wameamua kutupatia vyombo hivyo kwa lengo la kuuboresha zaidi muziki wetu,”alisema.
Katibu huyo wa Sikinde alisema, wamepanga kuvionyesha vyombo hivyo kwa waandishi wa habari Juni 21 katika mkutano utakaofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani Park, uliopo Mwenge, Dar es Salaam.
Mbali na kuzindua vyombo vipya, Milambo alisema watalitumia onyesho hilo kumtambulisha rasmi mwimbaji wao mpya,Athumani Kambi, aliyejiunga na bendi hiyo hivi karibuni akitokea Vijana Jazz.
Vilevile alisema watalitumia onyesho hilo kuzitambulisha nyimbo zao nne mpya. Alizitaja nyimbo hizo kuwa ni Jinamizi la talaka, Mihangaiko ya kazi, Deni nitalipa na Kinyonga.
“Tumeamua kumtambulisha rasmi Athumani Kambi siku hiyo kwa sababu ndiye atakayekuwa mrithi wa Hassan Bitchuka kwa vile ana uwezo wa kuimba nyimbo zote za zamani za mwimbaji huyo na ndiye atakayemkabidhi kipaza sauti,”alisema.
Milambo amewataka mashabiki wa Sikinde kujitokeza kwa wingi katika onyesho hilo kwa sababu wataibuka kivingine, wakiwa na mambo mpya. Alisisitiza kuwa,wanamuziki wa Sikinde hivi sasa wameamua hakuna kulala.

CHIOMA: Sijawahi kukumbwa na kashfa

LAGOS, Nigeria

MCHEZA filamu Chioma Chukwuka wa Nollywood amesema anamshukuru Mungu kwa kumuepusha na kashfa na matukio ya kufedhehesha kama yanayowakuta wasanii wengine maarufu nchini humo.
Chioma, ambaye hivi karibuni alifunga ndoa na mpenzi wake wa siku nyingi, Franklin Akpotu alisema wiki hii kuwa, licha ya kuwepo kwenye fani hiyo kwa miaka tisa, hajawahi kukumbwa na kashfa yoyote.
Mcheza filamu huyo alisema, amekuwa akijitahidi kwa kadri ya uwezo wake kujiepusha na matukio ya kashfa kwa lengo la kulinda hadhi yake na familia yake.
Chioma, ambaye pia ni mwanamuziki wa Injili, hivi karibuni aliibuka na albamu yake mpya ya muziki huyo, ambayo kwa sasa ipo sokoni na inafanya vizuri.
Mwigizaji huyo alisema anayafurahia maisha yake ya ndoa na kusisitiza kuwa, hayajaathiri kazi zake kwa sababu yeye na mumewe wanapendana na kuelewana.
“Ndoa ni uhusiano mzuri kati ya wawili wapendanao. Ni kitu ambacho huwezi kukiota, unatakiwa kukielewa vyema,”alisema.
Chioma alisema siku ya kwanza alipokutana na mumewe huyo, kila mmoja alitokea kumpenda mwenzake na hivyo ndivyo uhusiano wao ulivyoanza na kufikia hatua ya kufunga ndoa.
Mwanamama huyo mwenye watoto wawili alisema, hana sehemu maalumu katika mwili wake, inayowavutia zaidi wanaume kwa sababu anaamini yeye ni mrembo kuanzia kichwani hadi unyayoni.

Sina haraka ya kuolewa-Nwokoye



LAGOS, Nigeria
QUEEN Nwokoye, mcheza filamu wa Nollywood asiye na makuu amesema, hana papara ya kuolewa kwa sasa na kwamba atafunga ndoa pale atakapoona wakati wa kufanya hivyo umewadia.
Mcheza filamu huyo asiye na makeke alisema wiki hii kuwa, ndoa si kitu cha kuharakishwa kwa vile ni jambo linalopaswa kufanywa kwa umakini mkubwa.
“Sipendi kuolewa na baadae kuachika. Wazazi wangu wameoana miaka mingi na hadi sasa bado wanaishi pamoja na wanapendana,”alisema.
Hata hivyo, mwanadada huyo mwenye umbo la kuvutia hakuwa tayari kumtaja rafiki yake wa kiume kwa madai kuwa, hadi sasa anaishi peke yake.
“Kwa sasa, naishi peke yangu. Nipo makini, naishi peke yangu, lakini sitafuti mwanaume,”alisema.
Alipoulizwa iwapo amewahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwigizaji yeyote wa kiume wa Nollywood, Nwokoye alisema hajawahi kufanya hivyo.
Alisema wapo waigizaji wengi wa kiume wenye mvuto Nollywood, lakini si jambo zuri kuwa na uhusiano wa aina hiyo na mtu mnayefanyakazi pamoja.
Nwokoye alisema alianza kujitosa kwenye fani hiyo mwaka 2004 baada ya kumaliza shule. Alisema kamwe katika maisha yake hakuwahi kutarajia kuwa mwigizaji.
“Wakati wote nilipokuwa sule, kamwe sikufikiria kuwa mwigizaji. Lakini baada ya kumaliza shule na kukosa kazi, nilianza kufikiria mwelekeo huo,”alisema.
“Nilianza kutazama sinema. Hiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kukaa chini na kutazama filamu ya Kinigeria. Nilianza kuvutiwa. Nilianza kwenda kufanya majaribio na hatimaye kupata nafasi,”aliongeza.
Nwokoye alisema anashukuru Mungu kwamba wazazi wake walimuunga mkono kuhusu uamuzi wake huo na mama yake alimweleza wazi kuwa, yeye ni mtu mzima anajua zuri na baya.

Jim Iyke azushiwa kifo


LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu machachari wa Nigeria, Jim Iyke ameibuka na kukanusha uvumi uliokuwa umezagaa kwamba amefariki katika ajali ya gari iliyotokea hivi karibuni katika barabara ya Benin mjini Lagos.
Katika taarifa yake aliyoituma kwa vyombo vya habari, Iyke alisema amestushwa na taarifa hizo kwa sababu hazikuwa za kweli na kwamba yeye ni mzima wa afya njema.
Mbali na kuvumishiwa kifo, baadhi ya vyombo vya habari hivi karibuni viliripoti kuwa, Iyke ametekwa nyara na watu wasiojulikana na hajulikani mahali alipo.
“Hizi ni habari za uzushi mtupu. Mnaweza kuelewa ni kwa kiasi gani mama na familia yangu walipatwa na mshtuko kusikia taarifa hizi?” Alisema na kuhoji mwigizaji huyo.
“Familia yangu nzima ilichanganyikiwa kutokana na taarifa hizi za uzushi na hii si mara ya kwanza, nilizipuuza taarifa za awali, lakini kwa hizi za wakati huu siwezi kukaa kimya,”aliongeza.
Taarifa hiyo aliyoitoa Juni 6 mwaka huu ilieleza kuwa, anachukiwa na baadhi ya waandishi wa habari, wamiliki wa blogu na baadhi ya waigizaji wenzake ndio sababu amekuwa akizushiwa mambo ya uongo mara kwa mara.
Iyke alisema kuna wakati aliwahi kuzushiwa kwamba anajihusisha na utumiaji na biashara ya dawa za kulevya na haelewi taarifa hizi huwa zinatoka wapi na kwa nani.
“Mimi ni mlengwa mkuu wa taarifa hizi za uzushi, ambazo zimekuwa zikiwaathiri kwa kiasi kikubwa familia yangu na watu wanaonipenda,”alisema.
“Wamekuwa wakipanga kuniangamiza na kuniangusha, lakini wanashindwa kuelewa kwamba mimi si nyota. Siwezi kuangushwa na watu wenye malengo mabaya juu yangu. Mimi ni zao la madhehebu ya Jehovah. Nang’ara kama jua. Mungu atawalaani wote wanaonitakia mabaya,”aliongeza.

Genevieve aibuka mwanamke mwenye mvuto

LAGOS, Nigeria
MWIGIZAJI nyota wa kike wa Nollywood, Genevieve Nnaji ameibuka mshindi katika kinyang’anyiro cha kuwania taji la mwanamke mwenye mvuto nchini Nigeria kwa mwezi Juni.
Genevieve alinyakua taji hilo kupitia mtandao wa NFC, ambao uliendesha upigaji kura kwa njia ya maoni kutoka kwa wasomaji mbalimbali.
Mwanadada huyo mwenye sura na umbo lenye mvuto, aliongoza baada ya kupata kura 225 na kumwaga mwigizaji mwingine nyota nchini humo, Omotola Jalade aliyepata kura 190.
Wanawake wengine waliofanya vizuri katika shindano hilo ni Mercy Johnson, aliyepata kura 175, Tonto Dikeh, aliyepata kura 100 na Omoni Oboli, aliyepata kura 70.
Genevieve ni mmoja wa waigizaji wanaolipwa fedha nyingi nchini Nigeria, akiwa anamiliki nyumba ya kifahari, magari ya starehe na jarida la mitindo na maisha.
Mwanadada huyo mantashau pia ni mwanamuziki na ameingia mikataba na kampuni mbalimbali za Nigeria kwa lengo la kutangaza bidhaa zao.
Alizaliwa Mei 3, 1979. Alianza kujihusisha na fani ya uigizaji mwaka 1998 kupitia filamu ya Most Wanted kabla ya kushinda tuzo ya mwigizaji bora wa Afrika mwaka 2005.
Mwanadada huyo, ambaye amebatizwa jina la Julia Roberts wa Afrika, alizaliwa Mbaise katika Jimbo la Imo na kukulia mjini Lagos. Ni mtoto wa nne kati ya watoto wanane wa familia yake.
Alianza uigizaji filamu akiwa mwigizaji mtoto katika tamthilia ya Ripples akiwa na umri wa miaka minane. Miongoni mwa filamu zilizompatia umaarufu ni pamoja na Last Party, Mark of the Beast na Ijele. Hadi sasa ameshacheza filamu zaidi ya 80.
Mwaka 2004 aliingia mkataba na Kampuni ya EKB Records ya Ghana kwa ajili ya kurekodi albamu yake ya muziki, inayojulikana kwa jina la One Logo logo line, ambayo imepigwa katika miondoko ya R&B na Hip hop.

Siimbi nyimbo za kihuni-Temba

MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Amani Temba amesema muziki anaoupiga si wa kihuni na kwamba umelenga kufundisha maadili mema kwa jamii.
Temba alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, nyimbo zake ndizo zinazoongoza kwa kutoa mafunzo yenye mwelekeo wa kuielimisha jamii.
Kiongozi huyo wa kundi la TMK Wanaume Family, alielezea msimamo wake huo baada ya kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa wadau wa muziki huo kwamba, nyimbo zake nyingi zinapotosha jamii.
“Si kwamba najitetea, lakini kiukweli ni kwamba muziki wangu sio wa kihuni kama watu wanavyosema, unaongoza kwa kurekebisha jamii, huwezi kuamini,”alisema msanii huyo.
Temba ni mmoja wa wasanii wanaong’ara katika kundi la TMK, ambapo amekuwa akipenda kurekodi nyimbo zake binafsi kwa kushirikiana na Chege Chigunda.
Msanii huyo aliyezaliwa mwaka 1980, ambaye pia ni mchezaji mzuri wa mpira wa kikapu, amewahi pia kurekodi na wasanii wengine nyota kama vile Ray C, Dully Sykes na wengineo.
Kabla ya kujiunga na TMK, Temba alikuwa mmoja wa wasanii waliokuwa wakiunda kundi la Manduli Mobb pamoja na Juma Nature. Moja ya nyimbo zilizolipatia umaarufu kundi hilo ni ‘Maskini jeuri’ waliyoirekodi mwaka 2000.
Baadaye kundi hilo liligawanyika na kila msanii akaamua kufanyakazi kivyake. Wimbo wa kwanza wa Temba baada ya kujiengua katika kundi hilo unajulikana kwa jina la ‘Nakumindi’, aliourekodi mwishoni mwa 2001.
Msanii huyo baadaye alijiunga na kundi la TMK, ambapo aliibuka na kibao chake kilichompatia umaarufu, kinachokwenda kwa jina la ‘Nampenda yeye’. Alirekodi kibao hicho kwa kushirikiana na Dully Sykes.

BHOKE: Hakuna ninachokijutia



MWAKILISHI wa Tanzania katika shindano la mwaka huu la Big Brother Amplified, Bhoke amesema hana anachokijutia kutokana na aliyoyafanya ndani ya jumba la Big Brother.
Bhoke alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, alifurahia kuwa mmoja wa washiriki wa shindano hilo na pia kuwemo ndani ya jumba la Big Brother.
Mshiriki huyo wa Tanzania, alielezea msimamo wake huo, siku chache baada ya kutolewa katika shindano hilo.
Bhoke alitolewa sanjari na mshindi kutoka Uganda, Ernest. Inadaiwa kuwa, washiriki hao wawili walikuwa na uhusiano wa kimapenzi na walifanya ngono ndani ya jumba hilo.
Baadhi ya magazeti ya Tanzania na Uganda hivi karibuni yalichapisha picha zilizowaonyesha washiriki hao wawili wakifanya ngono huku wakiwa wamejifunika shuka.
“Sijutii chochote, kwa kweli nilifurahia kuwemo ndani ya nyumba na yote niliyoyafanya, niliyafanya kama mimi, hivyo hakuna chochote, ambacho naweza nikakijutia,”alisema.
Imedaiwa kuwa, Bhoke na Ernest walipigiwa kura nyingi za kutoka ndani ya jumbe hilo kutokana na kitendo chao hicho. Pia imedaiwa kuwa, washiriki wengi wa kike walikuwa wakimchukia Ernest.
Bhoke alikuwa miongoni mwa wawakilishi wawili wa Tanzania katika shindano hilo mwaka huu. Mwingine alikuwa Lotus, ambaye alikuwa wa tatu kutolewa baada ya kudaiwa alimpiga mshiriki kutoka Afrika Kusini, Luclay.
Washiriki wengine waliotolewa kwenye shindano hilo hadi sasa ni Michael (Msumbiji), Confidence (Ghana), Jossy (Namibia) na Nkuli (Afrika Kusini).
Waliopigiwa kura ya kutoka mwishoni mwa wiki hii ni Nic (Kenya), Luclay (Afrika Kusini), Kim (Zambia), Karen (Nigeria) na Danny (Ethiopia).

SAMATTA: Lazima niwapangue mastaa wa TP Mazembe


SWALI: Hongera kwa kufanikiwa kuingia mkataba wa kuichezea timu ya TP Mazembe. Je, unaweza kueleza nini siri ya mafanikio hayo?
JIBU: Asante, nashukuru sana. Siri kubwa ya mafanikio yangu ni kuwa na msimamo na kuzingatia mafunzo ya makocha, ambao wamekuwa wakinifundisha na mimi kufanyiakazi .
Mbali na hilo, malengo yangu kwa sasa ni kuonyesha uwezo zaidi wa kucheza soka ndani ya timu hiyo ili hatimaye siku zijazo niweze kwenda kucheza soka ya kulipwa barani Ulaya.
Hilo jambo lipo kwenye mawazo yangu siku nyingi, hasa ninapowaona wachezaji kama Nizar Khalfan, Henry Joseph na Danny Mrwanda wanavyopata maendeleo katika klabu zao kupitia mchezo wa soka.
Lakini napenda kuweka wazi kuwa, safari yangu ya mafanikio ndio kwanza imeanza, hivyo nitahakikisha nachuana vikali na mastaa wa TP Mazembe ili niweze kupata namba katika kikosi cha kwanza.
Hata hivyo, najua wazi kwamba itanibidi nifanyekazi ya ziada ili kuhakikisha lengo la kuwapiku wakali hao linatimia. Nitalazimika kuonyesha uwezo wangu ili niweze kupata ulaji huko ulaya. Sioni sababu ya kushindwa kufanya hivyo.
Lakini napenda kueleza wazi kuwa, tangu nimeanza kucheza soka katika timu za mtaani, Amani nimekuwa nikifanya jitihada kubwa kujiendeleza. Pia nimewahi kuchezea timu za Mbagala Market ,TMK United na African Lyon kabla ya kutua Simba.
SWALI: Baada ya kujiunga na TP Mazembe, umegundua tofauti gani kati ya soka la hapa Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo?
JIBU: Tofauti ipo, lakini sio kubwa. Lakini lazima nikiri kwamba, wenzetu wamejipanga katika kila idara kwenye klabu na kila moja inafanyakazi yake bila ya kuwepo ubabaishaji.
Ukiangalia viongozi wa klabu hiyo, utaona kuwa wanafanyakazi kwa ushirikiano mkubwa na kuwajali zaidi wachezaji ili kuhakikisha wanakuwa fiti na malengo yao yanatimia.
Mbali na hayo, karibu wachezaji wote kila mmoja anatambua kwamba yupo pale kwa ajili ya kucheza soka na kuipa mafanikio klabu hiyo, hivyo wanajali kufanya mazoezi kwa muda mwingi ili kuhakikisha wanakuwa fiti.
Vilevile klabu imeweza kujitosheleza kwa vifaa vya mazoezi kama vile gym na vinginevyo. Vifaa vyote hivyo vimepewa umuhimu kwa lengo la kuwaweka wachezaji fiti.
Binafsi nimepata morari kubwa ya kucheza soka kutokana na hali niliyoikuta TP Mazembe. Nimekuwa nikijituma sana kwenye mazoezi ili niweze kuwa fiti na kupangwa kwenye kikosi cha kwanza.
SWALI:Una maoni gani kuhusu timu ya taifa ya vijana wa chini ya miaka 23, ambayo inatarajiwa kucheza na Nigeria mwishoni mwa wiki hii?
JIBU: Nina imani kubwa na kikosi cha timu hiyo kwani kipo fiti kutokana na mazoezi, ambayo tumekuwa tukipewa na kocha wetu Jamhuri Kihwelu.
Matumaini yetu makubwa ni kwamba tutashinda mechi hiyo kutokana na wachezaji wote kuwa na morari kubwa, hasa ikizingatiwa kuwepo kwa changamoto ya zawadi, ambayo tumepewa hivi karibuni na mfanyabiashara Azim Dewji.
Vilevile napenda kulipongeza Shirikisho la Soka Tanzania (TFF)kwa kuipa matunzo mazuri timu hiyo kama ilivyo kwa timu ya taifa ya wakubwa, Taifa Stars.
SWALI: Unaahidi nini kuhusu mchezo huo wa marudiano, ambao ni muhimu kwa timu ya vijana kushinda?
JIBU: Nawaomba Watanzania wote kila mmoja kivyake, watuombee dua ili tuweze kushinda mchezo huo muhimu na kusonga mbele katika michuano ya kusaka kushiriki Michezo ya Olimpiki ya mwaka 2012 kule Uingereza.
SWALI: Wewe ni mtoto wa ngapi katika familia yenu na katika ukoo wenu kuna mtu yeyote ambaye amewahi kucheza soka?
JIBU: Mimi ni mtoto wa mwisho katika familia ya mzee Ally Samatta, ambaye amejaliwa kupata watoto sita.
Baba yangu aliwahi kucheza soka katika timu ya Pamba ya mkoani Mbeya na watoto wote sita waliweza kufuata nyayo za baba yetu.
Lakini mimi na kaka yangu, Mohamed ambaye yupo African Lyon bado tunaendelea kucheza soka. Mimi nilizaliwa mwaka 1992 katika hospitali ya Bombo mkoani Tanga. Nimesoma shule ya msingi Mbeya kabla ya baba kuacha kazi ya upolisi na kuamua kurudi jijini Dar es Salaam na familia yake.
Nilimaliza masomo ya shule ya awali mwaka 2003 kule Mbagala Rangitatu na kujiunga na shule ya sekondari ya Thaqhalain. Nilimaliza elimu ya sekondari mwaka 2008 na muda wote huo nilikuwa nikicheza soka baada ya masomo.
SWALI: Una maoni gani, ambayo ungependa kuyatoa kwa viongozi wa serikali kuhusu maendeleo ya michezo hapa nchini?
JIBU: Kwanza kabisa napenda kuipongeza serikali, inayoongozwa na Rais Jakaya Kikwete kwa kurejesha michezo katika shule za msingi na sekondari.
Najua wachezaji wengi wapo katika shule mbalimbali, lakini hawapati nafasi ya kuonekana. Ni jambo zuri kuona kuwa, Chuo cha Michezo kilichopo Malya mkoani Mwanza kimeanza kutoa mafunzo ya michezo kwa walimu wa shule za sekondari. Jambo la msingi ni kwa chuo hicho kupatiwa wakufunzi wazuri zaidi.
Iwapo chuo hicho kitapewa kipaumbele, nina hakika katika siku zijazo tutakuwa na wanamichezo wazuri pamoja na makocha wazuri wa michezo mbalimbali kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.
Pia napenda kuwapa somo wachezaji wenzangu kuwa, tuongeze bidii ya kujituma katika mazoezi ili tuwe fiti na kufanikiwa katika maisha yetu kupitia soka.

Thursday, June 9, 2011

Stephanie Okereke akana kuwa mja mzito


MWANADADA machachari katika fani ya uigizaji filamu Nigeria, Stephanie Okereke amekanusha madai kuwa ana uja uzito.
Stephanie alilieleza gazeti la Encomium wiki hii kuwa, anashangaa kusikia taarifa hizo zimeripotiwa tena kwenye vyombo vya habari kwa mara ya pili wakati si za kweli.
"Mimi nina uja uzito? Hii ni mara ya pili kusikia taarifa hizi. Nashukuru Mungu kwamba uvumi huu ni mzuri kwa sababu yeyote anayeusambaza, ananitakia mema,"alisema mcheza filamu huyo mwenye mvuto.
"Hizi ni taarifa nzuri na nawashukuru wale wote wanaonitakia heri. Lakini nasikitika kuwajulisha kwamba mimi sina uja uzito. Itatokea hivyo hivi karibuni, lakini kwa sasa, wote wanaonitakia mema, wanapaswa kusubiri itokee hivyo,"aliongeza.
Hivi karibuni, Stephanie alivishwa pete ya uchumba na mpenzi wake mpya, Linus Idahosa wa Kampuni ya Delyork.

RMD kumbe bado wamo


MCHEZA filamu mkongwe wa Nollywood, Richard Mofe Damijo kwa mara ya kwanza amepamba ukurasa wa mbele wa jarida jipya la Genevieve na kuzungumzia maisha yake ya kiusanii.
Richard, ambaye ni maarufu zaidi kwa jina la RDM, amepamba ukurasa wa mbele wa gazeti hilo katika toleo la mwezi huu, ambalo tayari lipo mitaani.
RMD alikuwa mmoja wa wacheza filamu maarufu wa Nigeria mwanzoni mwa miaka ya 1980. Ni mwigizaji wa kwanza wa nchi hiyo kulipwa naira milioni moja kwa kucheza nafasi ya mwigizaji mkuu.
Mchezaji filamu huyo, aliyeshinda tuzo nyingi, alianza kujipatia umaarufu mkubwa kupitia tamthilia ya Checkmate, ambayo aliicheza kwa kutumia jina la Segun Kadiri.
Hata hivyo, RMD hakudumu sana kwenye fani hiyo. Aliamua kuitosa na kwenda nje ya nchi kwa masomo zaidi ya chuo kikuu na baada ya kurejea Nigeria, aliteuliwa kuwa kamishna wa masuala ya utamaduni na utalii katika jimbo la Delta.
Alizaliwa Julai 6, 1961 katika kitongoji cha Warri kilichopo Jimbo la Delta. Mwaka 2005 alishinda tuzo ya mwigizaji bora ya Afrika. Alijitosa rasmi kwenye siasa mwaka 2009.
Mcheza filamu huyo pia aliwahi kufanyakazi ya uandishi wa habari katika magazeti ya Concord na Metro.
RDM alifunga ndoa na May Ellen Ezekiel, mwandishi wa habari maarufu wa zamani wa Nigeria, aliyekuwa akifahamika zaidi kwa jina la Mee. Mkewe huyo alifariki dunia mwaka 1996.
Kwa sasa, RMD ameoa tena na ana watoto wanne, wawili alizaa na mkewe wa kwanza na wengine wawili amezaa na mkewe wa sasa.

Omotola adaiwa kuwa mpenzi wa bosi wa Sifax


NYOTA wa kike wa Nollywood, Omotola Jalade ameripotiwa kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na Mkurugenzi wa Kampuni ya Sifax Group, Taiwo Afolabi.
Omotola, ambaye ni mama wa watoto wanne, ameripotiwa kuwa na uhusiano na tajiri huyo kwa miaka minne na kwamba wamekuwa wakikutana kwa siri mno.
Gazeti moja la Nigeria liliripoti wiki iliyopita kuwa, Omotola amekuwa akimtembelea Afolabi ofisini kwake mara kwa mara kwa kisingizio cha kujadili masuala ya kibiashara.
Taarifa kuhusu uhusiano wa Omotola na tajiri huyo, zimevujishwa na rafiki mmoja wa karibu wa Afolabi na ambaye amekuwa akishuhudia mara kwa mara kukutana kwao.
Afolabi, ambaye miaka michache iliyopita alidaiwa kuwa na uhusiano na waigizaji wengine, Stella Damasus na Foluke Daramola, ameripotiwa kuwa hana mkono wa birika.
Mwishoni mwa mwaka jana, tajiri huyo wa jiji la Lagos aliliripotiwa kununua gani tano aina ya Jeep, ambazo alizitoa zawadi ya Krismasi kwa wake zake.
Juhudi za gazeti hilo kuwatafuta Omotola na Afolabi ili wathibitishe madai hayo, hazikuweza kupatikana.
Hata hivyo, hii si mara ya kwanza kwa Omotola kudaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanaume wa nje. Amekuwa akiripotiwa hivyo mara kadhaa, lakini mara zote amekuwa akikanusha.

Wazazi hawakupenda niwe mwigizaji-Monalisa


MSANII mahiri wa filamu wa Nigeria, Monalisa Chinda amesema wazazi wake kamwe hawakupenda ajihusishe na fani hiyo kwa kuiona haina mwelekeo mzuri kimaisha.
Akizungumza na mtandao mmoja wa nchi hiyo wiki hii, Monalisa alisema awali, wazazi wake hawakuifurahia kazi hiyo, lakini baadaye waliizoea na kuiona ya kawaida.
“Baba yangu hakuelewa kwa nini nilitaka niwe msanii kwa maisha yangu yote. Hakuiunga mkono kabisa fani hiyo wakati huo, lakini kwa sasa hana kinyongo, wameikubali na wanaona fahari juu yangu,”alisema.
Monalisa alisema licha ya kuwa na ngozi nyororo, hapendi kuacha wazi sehemu kubwa ya mwili wake wakati anapoigiza kwa sababu hiyo si desturi yake.
Alisema yeye ni mcheza filamu msomi na kwamba kazi yake haina uhusiano na mambo yake binafsi.
“Naweza kuigiza nafasi ya msichana mtukutu kwenye filamu, lakini siwezi kuonyesha sehemu kubwa ya mwili wangu,”alisema.
“Naweza kucheza filamu za mapenzi na kuonyesha vitendo vya kubusiana, lakini sifanyi hivyo kwa hisia. Najaribu kujenga mazingira ya mapenzi bila ya kuwa na hisia halisi kwa sababu hiyo ni kazi, tena ya kisomi,” alisema.
Monalisa alisema kamwe hawezi kuonyesha sehemu ya matiti yake katika filamu na kusisitiza kuwa, Wanigeria ni waafrika na kwamba kuna mambo yanayoweza kufanyika Ulaya, lakini hayapaswi kufanywa katika bara la Afrika.
“Mashabiki wameshaona sehemu ya kifua na mgongo wangu, wameshaona miguu yangu, wanataka nini kingine. Siwezi kuonyesha matiti yangu kwenye skrini kila mtu ayaone,”alisema.

Sindodo yu buheri wa afya

MCHEZA filamu Tayo Odueke, maarufu kwa jina la Sikirat Sindodo,ambaye ilivumishwa kuwa yupo mahututi, ameibuka na hali yake imeelezwa kuwa ni nzuri.
Sindodo alionekana kwa mara ya kwanza Mei 22 mwaka huu katika sherehe ya siku ya kuzaliwa ya rafiki yake, Kemi Korede iliyofanyika katika kitongoji cha Egbeda mjini Lagos.
Kemi alithibitisha kuhusu kuwepo kwa Sindodo katika sherehe hiyo na kuongeza kuwa, mwanamama huyo amesharejea katika hali yake ya kawaida.
“Amerejea kwenye mwonekano wake ule ule mzuri na pengine amezidi kuwa mrembo,”alisema Kemi.
Mbali na kuripotiwa kuwa yupo mahututi, pia iliwahi kuvumishwa mara tatu kwamba Sindodo amefariki, lakini baadaye ikabainika kwamba, habari hizo hazikuwa za kweli.
Hivi karibuni, Sindodo aliripotiwa kuwa amelazwa katika hospitali ya Chuo cha Uuguzi cha Lagos kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa kansa.
Baadaye iliripotiwa kuwa, Sindodo alihamishiwa kwenye hospitali ya kanisa la T.B Joshua Synagogue kabla ya kuelezwa kuwa, alipelekwa nje ya nchi kwa ajili ya kupatiwa matibabu zaidi.
Kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa huo kwa muda mrefu, ilielezwa kuwa afya ya Sindodo ilikuwa mbaya na alipungua uzito kwa kiasi kikubwa.
Katika kipindi chote hicho, hakuna aliyeweza kukutana na mwigizaji huyo zaidi ya familia yake na rafiki zake wa karibu.

D'Banj: Mimi na Genevieve ni marafiki wa kawaida


LAGOS, Nigeria
MWANAMUZIKI nyota wa Nigeria, D’Banj amesema hana uhusiano wa kimapenzi na mcheza filamu, Genevieve Nnaji zaidi ya kuwa marafiki wa kawaida.
D’Banj alisema hayo mwishoni mwa wiki iliyopita wakati akiwa ziarani nchini Malaysia, ambako alifanya maonyesho kadhaa ya muziki.
Kauli hiyo ya D’Banj ilikuja baada ya mmoja wa waandishi wa habari wa nchi hiyo kumtaka aeleze iwapo ni kweli ana uhusiani wa kimapenzi na mcheza filamu huyo nyota wa Nollywood.
Mwanamuziki huyo alisema taarifa zilizoripotiwa hivi karibuni na baadhi ya vyombo vya habari kwamba amemvisha pete ya uchumba Genevieve na kwamba wanatarajia kufunga ndoa Agosti mwaka huu si sahihi.
Alisema anatambua kuhusu kuwepo kwa uvumi huo, lakini alisisitiza kuwa yeye na mcheza filamu huo hawana uhusiano mwingine zaidi ya kuwa marafiki wa kawaida.
“Ni rafiki yangu mkubwa, sielewi uvumi huu unatoka wapi. Lakini siwezi kulalamika kwa sababu Genevieve ni mwanamke mrembo,”alisema.
Mwanamuziki huyo alikiri kuhudhuria sherehe ya kuzaliwa ya Genevieve iliyofanyika hivi karibuni mjini London, Uingereza, lakini alisema alifanya hivyo akiwa mgeni mwalikwa na si mpenzi wake.
Hivi karibuni, wazazi wa D’Banj, prodyuza wake, Don Jazzy na Meneja wake, Sunday Are walisema hawana taarifa ya kuwepo kwa mipango ya harusi ya mwanamuziki huyo na Genevieve.
Wazazi wake hao walisema, kwa mujibu wa taratibu na utamaduni wa kabila lao la Yoruba, iwapo angekuwa na mipango ya kufunga ndoa na mwigizaji huyo, alipaswa kumtambulisha kwao kwanza.
Meneja wake, Are alisema D’Banj na Genevieve ni watu wazima na kwamba wanaweza kufunga ndoa iwapo watataka kufanya hivyo bila ya kuwepo kwa kikwazo chochote.

BASENA: Motema Pembe 'Kushnei'



Na Sophia Wakati, Tanga
KOCHA Mkuu wa Simba, Moses Basena amesema kikosi chake kimeiva na kipo tayari kuikabili DC Motemba Pembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo katika mechi ya mtoano ya michuano ya soka ya Kombe la Shirikisho.
Simba na DC Motema Pembe zinatarajiwa kushuka dimbani Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kabla ya kurudiana wiki mbili zijazo mjini Kinshasa.
Akizungumza mjini hapa juzi, Basena alisema kambi ya timu hiyo inaendelea vizuri na wachezaji wake wote wapo fiti, isipokuwa kipa Juma Kaseja, ambaye bado majeruhi.
Kaseja aliumia taya wakati Simba ilipomenyana na Wydad Casablanca ya Morocco katika mechi ya raundi ya tatu ya michuano ya klabu bingwa Afrika, iliyochezwa wiki iliyopita mjini Cairo, Misri.
Kwa mujibu wa Basena, uongozi uliamua kuweka kambi mjini Tanga kwa vile kuna utulivu na wachezaji wangeweza kuelekeza zaidi akili zao katika mchezo wa Jumapili.
Tangu ilipoanza kambi mjini hapa, Simba imecheza mechi moja ya kirafiki dhidi ya Kombaini ya mkoa wa Tanga na kuibuka na ushindi wa mabao 2-1. Mechi hiyo ilichezwa mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye Uwanja wa Mkwakwani.
Basena alisema japokuwa hatambui vyema uwezo wa wapinzani wao, lakini amejifunza mengi kupitia mechi yao dhidi ya Waydad Casablanca na pia kurekebisha kasoro zilizojitokeza katika mchezo huo.
Wakati huo huo, mshambuliaji Emmanuel Okwi wa Simba amejiunga na kambi ya timu hiyo mjini Tanga kwa ajili ya maandalizi ya mechi yao dhidi ya DC Motema Pembe.
Okwi hakuwepo kambini kwa vile aliitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Uganda, ambacho mwishoni mwa wiki iliyopita, kilicheza mechi ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Afrika za 2012.
Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ alisema jana kuwa, Okwi aliripoti kambini Jumatatu akiwa fiti na mwenye ari kubwa ya kuitumikia timu yake.
Kaburu alisema pia kuwa, kiungo Hillary Echessa naye amejiunga na kambi ya timu hiyo kwa ajili ya maandalizi ya mchezo, sanjari na wachezaji waliokuwemo kwenye kikosi cha timu ya Taifa, Taifa Stars.
Kwa mujibu wa Kaburu, kikosi cha Simba kilirejea mjini Dar es Salaam jana kwa ajili ya maandalizi ya mwisho kabla ya kuivaa Motema Pembe.
Kiongozi huyo wa Simba alisema, kipa Kaseja ameshaanza mazoezi mepesi na anatarajiwa kuwa fiti kabla ya mchezo huo. Kaseja alienguliwa kwenye kikosi cha Taifa Stars kutokana na kuwa majeruhi.
Wakati Simba ikijiandaa kukabiliana na wapinzani wao hao, kuna habari kuwa, timu ya Motema Pembe inatarajiwa kuwasili nchini leo ikiwa na kikosi cha wachezaji 20.
Habari kutoka Congo zimeeleza kuwa, Motema Pembe iliamua kuhamishia kambi yake kutoka Goma hadi Kivu kwa ajili ya kujiandaa na mchezo huo.
Kwa sasa, Motema Pembe inanolewa na Kocha Andy Fulila baada ya kutimuliwa kwa Kocha Mohamed Nashridine Nabi kutokana na kushindwa kuwa na ushirikiano na wasaidizi wake.

Dewji amshukia Poulsen



MFADHILI mkuu wa zamani wa klabu ya Simba, Azim Dewji amesema Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars, Jan Poulsen hana uwezo wa kuipa mafanikio timu hiyo.
Akizungumza na Burudani mjini Dar es Salaam wiki hii, Dewji alisema tangu Poulsen alipoanza kuifundisha timu hiyo mapema mwaka huu, hajaweza kuwa na mfumo unaoeleweka.
Dewji, ambaye kwa sasa anamiliki timu ya Moro United, inayoshiriki ligi kuu ya Tanzania Bara, alisema inawezekana tatizo hilo linatokana na wachezaji kushindwa kumuelewa kocha huyo.
“Mimi hadi sasa nashindwa kuelewa Taifa Stars inatumia mfumo gani. Lakini nilichokigundua ni kwamba, Poulsen ameshindwa kuipa mafanikio timu yetu ya taifa,”alisema mfadhili huyo.
Alisema kufungwa kwa Taifa Stars katika mechi nyingi ilizocheza ikiwa chini ya kocha huyo kutoka Denmark, kumedhihirisha wazi kuwa, uwezo wake wa kufundisha soka ni wa kiwango cha chini.
Alitoa mfano wa vipigo ilivyovipata timu hiyo katika mechi tatu mfululizo dhidi ya Msumbiji, Afrika Kusini na Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Kauli hiyo ya Dewji imekuja siku chache baada ya Taifa Stars kujiweka kwenye mazingira magumu ya kufuzu kwa fainali za Afrika za 2012, kufuatia kuchapwa mabao 2-1 na Jamhuri ya Afrika ya Kati mwishoni mwa wiki iliyopita.
"Kwa kweli mimi nashindwa kuelewa Poulsen anafanya kazi gani katika kikosi cha Taifa Stars kwa sababu tangu alipoanza kuifundisha, imekuwa ikifanya vibaya, tofauti na miaka ya nyuma,"alisema.
Dewji ameishauri Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kufuatilia mwenendo wa timu hiyo na ikiwezekana kuchukua hatua za kuinusuru badala ya kuiacha iendelee kuvurunda. “Haiwezekani timu iendelee kuvurunda, lazima kuna tatizo ndani ya kikosi cha Taifa Stars au benchi la ufundi, hivyo hatua zichukuliwe kuinusuru.

LLYOD NCHUNGA: Nitahakikisha Yanga inajiendesha kibiashara


SWALI: Hongera sana mwenyekiti kwa kuiongoza Yanga kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya Tanzania Bara msimu huu.
JIBU: Asante sana ndugu yangu, nashukuru. Lakini nadhani pongezi hizi zinawastahili zaidi wachezaji, viongozi wenzangu, wanachama pamoja na mashabiki kwa kuiunga mkono timu yao muda wote wa ligi.
SWALI: Nini matarajio yenu katika michuano ijayo ya ligi kuu na ile ya klabu bingwa barani Afrika?
JIBU: Kwanza kabisa tumepanga kufanya usajili kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha tunaendelea kufanya vizuri katika michuano ijayo ya ligi kuu.
Uongozi wangu umeunda kamati mbalimbali kwa ajili ya kusimamia shughuli za klabu. Kamati ya usajili ipo chini ya Salum Rupia na Seif Mohamed.
Kutokana na kamati hiyo kuundwa na watu makini, utaona kuwa, tumeweza kusajili wachezaji kadhaa wazuri kutoka ndani na nje ya nchi. Lengo ni kukiboresha zaidi kikosi chetu si kusajili timu mpya.
Tunatarajia kazi hii itakamilika Juni 22 mwaka huu kabla ya Kocha Sam Timbe kukabidhiwa orodha ya wachezaji waliosajiliwa kwa ajili ya msimu ujao. Wachezaji hao ni wale, ambao yeye mwenyewe aliwapendekeza.
SWALI: Pamoja na maelezo yako mazuri, katika siku za hivi karibuni kumekuwepo na taarifa kwamba, kuna baadhi ya wachezaji mmeshindwa kumalizana nao kutokana na matatizo ya pesa. Je, taarifa hizi ni za kweli?
JIBU: Unajua sisi tunafanyakazi zetu kwa umakini. Kila mtu anapaswa kuhakikisha kwamba ametimiza majukumu yake. Kamati ya usajili ndiyo yenye jukumu la kuhakikisha kuwa, kazi hiyo inakamilika kwa muda uliopangwa na inafanyika kwa ufanisi mkubwa. Hivyo si kweli kwamba tumeshindwa kutimiza kazi hiyo.
Ninachoweza kukuhakikishia ni kwamba kazi hiyo inakwenda vizuri na wapo baadhi ya wadau wa Yanga, ambao wamekuwa wakijitolea kwa hali na mali kuifanikisha. Na hivi karibuni tuliitisha harambee ya wanachama kwa ajili ya kuichangia timu pale hoteli ya Regency na nashukuru kwamba mambo yalikwenda vizuri.
SWALI: Mbona kuna taarifa kwamba wajumbe wengi waliopewa mwaliko hawakufika?
JIBU: Siyo kweli hata kidogo. Napenda nikueleze kwamba watu wanaendelea kuchangia pesa za usajili na kazi hiyo inaendelea bila matatizo. Subiri uone, itakapofika Juni 22, kikosi chetu kitakuwa tayari kimekamilika. Kitakuwa kikosi cha mauaji.
SWALI: Vipi suala la uhamisho wa Haruna Niyonzima kutoka APR ya Rwanda?
JIBU: Taarifa ambazo ninazo hadi sasa kutoka kamati yetu ya usajili zinaeleza kwamba, usajili wa mchezaji huyo unaendelea vizuri na tunasubiri ligi kuu ya Rwanda imalizike ili aje nchini kukamilisha taratibu za kujiunga na Yanga.
Nina imani na kamati yetu kwamba itaweza kufanikisha ujio wa mchezaji huyo kutokana na kuwepo watu makini na wenye uwezo wa kazi hiyo.
SWALI: Unazungumziaje kuhusu taratibu za usajili wa wachezaji watano kutoka nje ya nchi badala ya 10 kama ilivyokuwa msimu uliopita?
JIBU: Kwa kweli hapo bado kuna tatizo kidogo, lakini kwa vile utaratibu umeshapangwa, sina cha kusema kwa sababu sheria ni msumeno.
SWALI: Hivi karibuni tulisikia habari kwamba ulikuwa nchini Ghana kwa ajili ya kusaka wafadhili wa kuisaidia Yanga. Hebu tueleze ukweli wa habari hizo?
JIBU: Ni kweli nilikuwa nchini Ghana na niliweza kupata nafasi ya kuhudhuria tamasha la maendeleo ya soka barani Afrika. Huko nilikutana na baadhi ya viongozi wa taasisi nyingi za soka, ambao nitaendelea kuwasiliana nao ili kupata wadhamini wa kuisaidia klabu yangu.
Baadhi ya viongozi hao wameonyesha nia ya kuisaidia klabu yetu pamoja na soka la Tanzania. Tamasha hilo lilifanyika Mei 26 na 27 mjini Accra na pia lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka Shirikisho la Soka Duniani (FIFA).
Pia walikuwepo watu mashuhuri kama vile Cyril Loisel, aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Kombe la Dunia 2010 kule nchini Afrika Kusini.
Mwingine ni Danny Jordan, wajumbe kutoka Shirikisho la Soka Afrika (CAF) na mashirika yasiyo ya kiserikali, ambayo baadhi ya viongozi wake niliweza kuzungumza nao.
Lakini jambo la kufurahisha ni kwamba, mkurugenzi anayesimamia Ligi ya Bundesliga ya Ujerumani, Jog Daubitzer ameahidi kuwa atafanya juhudi za kuanzisha uhusiano wa karibu kati ya klabu hizi mbili kuitangaaza nchini kwao.
Pia Mkurugenzi wa Masoko wa Super Sport, Gary Rathbone aliniahidi kuwa, watafanya jitihada za kurusha matangazo kuhusu Yanga.Haya yote ni miongoni mwa mambo, ambayo tumepania kuyafanya ndani ya mwaka huu ili Yanga iweze kuepuka kuwa tegemezi.
Chini ya uongozi wangu, tumepania kuhakikisha kuwa, mali za klabu zinatumika ipasavyo ili kuiletea maendeleo Yanga na wanachama wake kwa ujumla.
SWALI: Vipi kuhusu mpango wako wa kuanzisha Saccos ya wanachama ndani ya klabu ya Yanga?
JIBU: Kwa upande wa kiuchumi, naweza kusema kuwa, bado naendelea kutumia elimu yangu ili kujenga uhusiano mzuri na taasisi kubwa ili kuanzisha SACCOS na baadaye benki ya Yanga.
Kazi hii inafanywa na wanachama, ambao wapo kwenye kamati ya uchumi. Hao wana watu wenye kujua mambo hayo kwa undani na mchakato bado unaendelea vizuri.
SWALI: Vipi kuhusu hatima ya adhabu mliyopewa na CECAFA?
JIBU: Mambo yanakwenda vizuri na hakuna wasiwasi kwamba tutamalizana nao ili kuhakikisha Yanga inaendelea kuwa na ushirikiano mzuri na CECAFA.
Tunasubiri taarifa ya kikao kati ya viongozi wa CECAFA na Yanga, ambacho kinatarajiwa kufanyika hivi karibuni. Lengo ni kumaliza tofauti zilizojitokeza kati yetu wakati wa mashindano ya Kombe la Kagame mwaka 2008.