KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, July 31, 2016

WADAU WA SANAA WAHAMASISHWA KUDHAMINI MASHINDANO YA UREMBO

Miss Dar Indian Ocean aliyemaliza muda wake, Camilla John (katikati) akimvisha skafu Mshindi wa Mashindano ya Miss Tanzania Indian Ocean 2016 Jackline Kimambo (kushoto) mara baada ya kuibuka mshindi katika mashindano hayo yaliyofanyika 30 Julai, 2016 katika Ukumbi wa MRC Ulioko Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Miss Tanzania Indian Ocean 2016 Jackline Kimambo (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na warembo wenzie ambaye ni Mshindi wa pili na wa tatu mara baada ya kumalizika kwa mashindano hayo yaliyofanyika 30 Julai, 2016 katika Ukumbi wa MRC Ulioko Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkuregenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bw. Francis Songoro (kulia) akimpongeza Miss Tanzania Indian Ocean 2016 Jackline Kimambo kwa kuibuka mshindi wa mashindano hayo baada ya kumalizika kwa mashindano hayo yaliyofanyika 30 Julai, 2016 katika Ukumbi wa MRC Ulioko Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Miss Tanzania Indian Ocean 2016 Jackline Kimambo akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki baada ya kumalizika kwa mashindano hayo yaliyofanyika 30 Julai, 2016 katika Ukumbi wa MRC Ulioko Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Na. Benedict Liwenga-WHUSM.

Wadau wanaojishughulisha na masuala ya Sanaa nchini wamehamishwa kujitokeza kwa wingi katika kusaidia maendeleo ya Sanaa kwa kudhamini na kufadhili mashindano ya urembo bila kubagua.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bw. Francis Songoro wakati alipokuwa akiwasilisha hotuba ya Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Anastazia Wambura ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi katika Mashindano ya Miss Tanzania Indian Ocean 2016 yaliyofanyika katika Ukumbi wa MRC uliopo Mikocheni jijini hapa.

Akiwasilisha hotuba hiyo, Songoro amesema kwamba kazi inayofanywa na wadau wa sanaa ni hatua ya utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Utamaduni ambayo inasisitiza jamii na wakuzaji sanaa kuendeleza ubunifu katika kazi za kiutamaduni.

Ameeleza kuwa, Serikali kupitia Wizara yake inathamini na kuunga mkono juhudi zinazofanywa na wadau hao hasa katika kukuza na kuviendeleza vipaji vya vijana nchini, hivyo amewapongeza wadau hao kwa moyo wao wa kujitoa na kuwataka kuendeleza kwa vitendo Sera ya Taifa ya Utamaduni ya mwaka 1997 katika Sura ya 9 kifungu cha 9:5:8 ambacho kinasisitiza na kuhimiza watu binafsi pamoja na Mashirika kuwekeza rasilimali katika sekta ya utamaduni.

‘’Maonyesho haya ni ishara tosha kuwa sanaa ni kazi, ajira, biashara na burudani, hivyo kipekee nawapongeza sana’’, alisema Songoro.

Aliongeza kuwa, Warembo ambao wameshiriki katika mashindano hayo wanautangaza utalii wa ndani na nje ya nchi na kwa kufanya hivyo wanaiwakilisha vyema Tanzania Duniani katika mashindano ya Miss World na pia kukuza uchumi wa nchi.

Aidha, amewataka warembo ambao hawakubahatika kuibuka washindi katika mashindano hayo kutokata tamaa, bali waitumie fursa hiyo hususani ya elimu waliyoipata wakiwa kambini kwa kuisadia jamii inayowazunguka na kuwa wanawake wa mfano wa kuigwa katika kujitambua na kujiamini.

‘’Mtambue kwamba, siyo wote mtakaoibuka washindi na kuendelea mbele katika mashindano haya, niwaombe wale ambao hamtashinda msivunjike moyo, bali mkaitumie elimu mliyoipata na yale ambayo mmejifunza mkiwa kambini kwa kuisaidia jamii inayowazunguka na muwe wanawake wa mfano wa kuigwa’’, alisema Songoro.

Katika mashindano hayo, Mshindi wa Kwanza aliyeibuka na kunyakua taji hilo ni Jackline Kimambo ambaye alipatikana kati ya tano bora  na kuvikwa taji la Miss Tanzania Indian Ocean 2016 na Mshindi wa pili ni Regina Ndimbo huku wengine waliobaki kwenye tano bora wamepata fursa ya kuingia katika mashindano ya Miss Kinondoni.

Shindano hilo lilihusisha jumla ya washiriki wapatao 20 ambapo mmoja kati yao ndiyo aliyeibuka mshindi na lilidhaminiwa na wadau mbalimbali wakiwemo Mikocheni Resort Centre, Mlimani TV, Channel Ten, Darling, Helmic, Tanzania Breast Cancer Foundation, Magic FM, Jozi Lounge, Kiss Printers pamoja na NTS.

Saturday, July 30, 2016

MSIWE WACHOYO WA ELIMU – WALLACE KARIA


Makamu Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF), Wallace Karia amewaagiza waamuzi wenye Beji kutoka Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kadhalika waamuzi waandamizi waliohitimu kozi leo Julai 29, 2016 kutokuwa wachoyo wa kutoa elimu waliyopata kwa wenzao wa madaraja ya kwanza, pili na tatu.

Karia aliyefunga kozi hiyo na kugawa vyeti kutoka FIFA kwa wahitimu 48, alisema hayo jana kwenye Ukumbi wa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati wa hafla ya kufunga kozi hiyo iliyochukua takribani siku tano ambako sehemu ya mafunzo hayo ilikuwa ni kusoma baadhi ya marekebisho kwa msimu wa 2016/17.

“Tuna matagemeo makubwa kutoka kwenu, lakini nasema mfikirie kusaidia wenzenu ili kama si kumaliza matatizo kwenye soka basi yapungue, nasisitiza msiwe wachoyo, fundisheni wengine na muwape hamasa,” alisema Karia kwa niaba ya Rais Jamal Malinzi ambaye kwa sababu za majukumu, hakudhuria hafla hiyo.

Karia ambaye aliishukuru FIFA kuendelea kutoa kozi nyingi nchini, alisema kwamba tayari Tanzania imefaidika kwa kozi za makocha na makamishna, lakini akaagiza Idara ya Ufundi ya TFF chini ya Kocha Mkongwe, Salum Madadi kutoa mafunzo hayo kwa viongozi wa klabu na waandishi wa habari ambao ni sehemu kubwa ya familia ya mpira wa miguu.

Alisema kwamba umahiri wa makocha utakuwa chachu ya mafanikio ya soka la Tanzania kwa kutoa waamuzi bora watakaokuwa wakipata nafasi kubwa ya kuchezesha michezo mbalimbali ya mpira wa miguu.

“Mkifanya vibaya kwenye mashindano, mtakuwa mmejiharibia wenyewe na pia kupoteza sifa ya nchi,” alisisitiza.

Kozi za Waamuzi wa Mpira wa Miguu wa Tanzania ilianza Julai 25, 2016 ambako iliendeshwa na wakufunzi Carlos Henrique kutoka Afrika Kusini, Mark Mzengo kutoka Malawi na Felix Tangawarima wa Zimbabwe.

Leo Julai 29, 2016 limeanza darasa la waamuzi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Ligi Daraja la Kwanza ya StarTimes (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL) kwa msimu wa 2016/2017

TFF YAELEZA SABABU YA KUIBUA VIPAJI



Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Mwesigwa Selestine amesema kutimia kwa malengo ya Kampuni ya Simu za mkononi ya Airtel imesukuma kampuni hiyo kuendelea kudhamini mashindano ya soka kwa vijana – wavulana na wasichana.

Selestine alisema hayo kwenye hafla ya kukabidhiana vifaa kwa Airtel kwenda TFF kabla ya kwenda kwa klabu shiriki iliyofanyika Ukumbi wa TFF, Dar es Salaam. Vifaa vilivyotolewa kwa timu jezi kamili ikiwa ni pamoja na jezi za waamuzi, viatu, mipira na vizuia ugoko kutopata madhara.

Alisema sababu hizo ni uhusiano mzuri kati ya TFF na Airtel inayotoa bora za mawasiliano kwa miaka sita sasa sambamba na kuendeleza vipaji kwani nusu ya wachezaji wa timu ya taifa ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17, wanatoka katika michuano hiyo ya mwaka jana.

Wachezaji hao ni  Ramadhani Awm Kabwili, Nickson Clement Kibabage, Dickson Nickson Job, Ally Hamisi Ng’anzi, Syprian Benedictor Mtesigwa, Mohammed Abdallah Rashid na Muhsin Malima Makame na Katibu Mkuu alisema: “Hawa wamepita Airtel. Tunashukuru Airtel kwa kuingia katika zonal (ukanda) ambao wengi hawapendi kuingia.”

Selestine alisifu Airtel akisema imejitofautisha na taasisi nyingine na kuamua kwenda shambani au jikoni kulima au kupika chakula ambacho leo tunajivunia kuwa na kikosi bora na imara cha Serengeti Boys ambayo wiki ijayo itakuwa na mtihani dhidi ya Afrika Kusini.

Rai wa Karibu Mkuu, Selestine ni kwa viongozi kuratibu vema mashindano ya Aitel msimu huu kwa kufuata kanuni ambazo zilijadiliwa na kupitishwa mara baada ya kuzindua mashindano hayo. “Kama viongozi mmeingia kwenye mashindano haya na hujafuata au hujui kanuni ujue tu umejiandaliwa kushindwa.”

Kadhalika aliwataka wazazi na walezi kuwatia shime wachezaji ili wafanye vema kwenye michuano hii ili siku moja waingie kwenye ajira ya soka wakitokea mashindano ya kuibua vipaji ya Airtel. Pia alitaka wajitokeze kwa wingi kwenye mashindano hayo yatayosimamiwa na kuendeshwa na TFF katika mikoa mbalimbali.

Mikoa ambayo itazindua Mashindano hayo ni pamoja na Mbeya, Mwanza, Morogoro, Ilala, Kinondoni na Temeke kwa upande wa wavulana wakati wasichana mikoa iliyoteuliwa ni Lindi, Zanzibar, Arusha na Ilala, Kinondoni na Temeke.

Thursday, July 28, 2016

SERENGETI BOYS YATUA SALAMA MADAGASCAR

Msafara wa timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’, uliondoka jana alfajiri Dar es Salaam, Tanzania imetua salama jijini Antananarivo, Madagascar kwa ajili kambi ya siku 10 kujiandaa na mchezo dhidi ya Afrika Kusini kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika utakaofanyika Agosti 6, 2016.

Mchezo wa marudiano utafanyika Agosti 21, mwaka huu kwenye Uwanja wa Azam, ulioko Chamazi-Mbagala, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam na kwamba mshindi atakuwa amejiwekea mazingira mazuri ya kuwania nafasi ya kufuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana, zitakazofanyika mwakani huko Madagascar.

Mkuu wa msafara akiwa ni Ayoub Shaibu Nyenzi ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Soka la Vijana, maofisa wengine waliosafiri na timu hiyo ni Kocha Mkuu, Bakari Nyundo Shime maarufu zaidi kwa jina la Mchawi Mweusi, Daktari wa timu hiyo, Shecky Francis Mngazija na Mtunza Vifaa, Andrew Vanance Andrew.

 Pia yumo Juma Kaseja Juma ambaye kwa muda amechukua nafasi ya makocha wasaidizi, Sebastian Nkoma na Muharam Mohammed ‘Shilton’ wanaohudhuria kozi ya makocha ngazi ya juu inayoratibiwa na CAF.

Nyota waliosafiri ni pamoja na makipa, Ramadhani Awm Kabwili, Kelvin Deogratius Kayego na Samwel Edward Brazio wakati mabeki wako Kibwana Ally Shomari, Nickson Clement Kibabage, Israel Patrick Mwenda, Dickson Nickson Job, Ally Hussein Msengi, Issa Abdi Makamba na Enrick Vitalis Nkosi.

Viungo ni Kelvin Nashon Naftal, Ally Hamisi Ng’anzi, Asadi Ali Juma Ali, Syprian Benedictor Mtesigwa, Ibrahim Abdallah Ali, Shaban Zuberi Ada huku washambuliaji wakiwa ni Mohammed Abdallah Rashid, Yohana Oscar Mkomola na Muhsin Malima Makame.

Serengeti Boys inakwenda kucheza na Afrika Kusini baada ya kuwatoa Shelisheli kwa jumla ya mabao 9-0 katika mechi zake mbili za kimataifa. Mshindi wa jumla kati ya Serengeti Boys na Afrika Kusini, atacheza na timu mshindi kati ya Namibia na Congo-Brazaville.

Hivi karibuni Serengeti Boys ilifanya ziara India ambako walishiriki mashindano ya vijana ya Kimataifa yanayotambuliwa na FIFA (AIFF International Youth Tournament 2016) kabla ya kurudi na rekodi ya kupigiwa mfano si tu katika Tanzania na kwa nchi za Afrika Mashariki. Ilishika nafasi ya tutu nyuma ya Korea Kusini na Marekani.

MAAGIZO KWA KLABU ZA LIGI KUU, LIGI DARAJA LA KWANZA

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Mwesigwa Selestine ameziasa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kutimiza masharti ya kupata vibali vya kuishi na kufanya kazi Tanzania kwa Wataalamu wa kigeni wakiwamo makocha, madaktari na wachezaji kabla ya kuingia kandarasi.

Masharti hayo ni vibali vya kufanya kazi nchini, visa ya kuishi nchini, vibali vya kucheza mpira wa miguu nchini, vibali vya kufundisha mpira na vibali vya watalaamu wengine kama madaktari na hayo ni kwa mujibu wa Idara ya Uhamiaji na Serikali, lakini wakati huohuo kwa wachezaji nao kukatiwa leseni ya kucheza kutoka TFF.

“Mchezaji au mtaalamu ye yote anapokuja nchini na kuanza mazoezi na timu yo yote anachukuliwa yuko kazini. Tusingependa watu wapate usumbufu. Kama Katibu Mkuu nimepata taarifa kutoka mamlaka zinazohusika kuwa nifuatiulie kuwa kuwa sisi ndio waratibu soka nchini, natakiwa kufuatilia,” amesema Selestine.

“Vilabu vihakikishe vyeti vya taaluma vinawasilishwa TFF kwa ajili ya ukaguzi kabla ya kutiliana kandarasi na wachezaji au walimu. Inawezekana hawahitajiki. Ni vema wakafanya uratatibu wa kuhakiki,” amesema.

Wakati huohuo, huo huo TFF imeagiza klabu kuendelea na usajili kabla ya Agosti 6, 2016 ambayo itakuwa siku ya mwisho na kwamba hakutakuwa na muda wa kuongezwa kwa klabu ambayo itashindwa kukamilisha usajili kwa wakati.

Wednesday, July 27, 2016

NAY WA MITEGO AFUNGIWA KUJIHUSISHA NA KAZI ZA SANAA KWA MUDA USIOJULIKANA, ATOZWA FAINI YA TSH. MILIONI MOJA


Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limemfungia kwa kipindi kisichojulikana Msanii wa muziki wa kizazi kipya Emmanuel Elibariki maarufu kwa jina la Nay wa Mitego hadi hapo litakapojiridhisha kwamba ametekeleza maagizo yote aliyopewa na Baraza sambamba na yeye kubadilika katika kubuni kazi zenye maadili na zisizo dhalilisha watu wa kada mbalimbali.

Maagizo aliyopewa Msanii Nay ni pamoja na kulipa faini (adhabu) ya kiasi cha Shilingi milioni 1, kufanya marekebisho ya mashairi ya wimbo wake wa ‘Pale Kati’, kufuata sheria, kanuni na taratibu za urasmishaji sekta ya Sanaa kwa maana ya kusajiliwa na BASATA na kuhakikisha wimbo wake umefuata taratibu zote.

Aidha, Msanii Nay ameagizwa kuwaomba radhi watanzania kwa kutoa kazi ya muziki yenye kuvunja maadili na kudhalilisha watu wa kada mbalimbali hususan wanawake.

Maamuzi haya yamefanyika kwa mujibu wa kifungu cha 4(2) cha sheria nambari 23 ya mwaka 1984, ikisomwa pamoja na kifungu cha 30(1)(2) na waraka wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo wa tarehe 16/7/2009 ambayo kwa sasa inafahamika kama Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Adhabu hizi zimetolewa kufuatia BASATA kufanya kikao cha pamoja na Msanii huyu jana siku ya Jumanne tarehe 26/07/2016 kwenye Ukumbi wa Baraza na yeye kukiri makosa na kuahidi kubadilika.

Makosa aliyosomewa na yeye kuyakiri kwa maandishi ni pamoja na;

Kujihusisha na shughuli za Sanaa pasipo kusajiliwa na BASATA.
Kutoa wimbo wa “Pale Kati” na kuupakia katika mitandao ya kijamii bila kuuleta kufanyiwa uhakiki wa maudhui yake.
Maudhui ya wimbo wa ‘Pale Kati’ kwa sehemu kubwa hayafai kwa matumizi ya wazi na ni kinyume cha sheria za nchi na maadili ya mtanzania.

Ikumbukwe kwamba mnamo tarehe 16/07/2016 BASATA lilitoa taarifa kwa umma ya kuufungia wimbo wa Pale Kati kufuatia kubeba maudhui yenye uvunjifu mkubwa wa maadili na kupambwa na picha dhalilishi kwa wanawake.

Aidha, tarehe 12/02/2016 BASATA liliufungia wimbo wa Shika Adabu Yako wa Msanii huyuhuyu kwa makosa yanayofanana na haya. Hivyo adhabu hii imetolewa ili kumpa muda wa kujifunza, kujitathimi na kujirekebisha kama kweli ana nia ya kuendelea kufanya kazi ya muziki

SANAA NI KAZI TUIKUZE, TUILINDE NA KUITHAMINI

Godfrey L. Mngereza
KATIBU MTENDAJI, BASATA

JACQUELINE WOLPER AJIUNGA NA CCM, AOMBA RADHI KWA KUMPIGIA DEBE LOWASSA MWAKA JANA


YANGA YAPIGWA THALATHA NA MEDEAMA YA GHANA


JAHAZI la Yanga limeendelea kuzama katika michuano ya soka ya Kombe la Shirikisho baada ya kuchapwa mabao 3-1 na Medeama ya Ghana.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye uwanja wa Essipong Sports mjini Sekondi-Takoradi, Yanga ilikwenda mapumziko ikiwa imeshafungwa idadi hiyo ya mabao.

Hiyo ni mechi ya nne mfululizo kwa Yanga kushindwa kutoka uwanjani na kishindo katika hatua ya makundi ya michuano hiyo, ikiwa imefungwa mechi tatu na kutoka sare moja.

Mabingwa hao wa soka nchini walianza michuano hiyo kwa kufungwa bao 1-0 na Mo Bejaia nchini Algeria, kabla ya kufungwa bao 1-0 na TP Mazembe na kutoka sare ya 1-1 na Medeama mjini Dar es Salaam.

Katika mechi hiyo, Medeama ilijipatia mabao yake kupitia kwa Daniel Amoah dakika ya saba, aliyemalizia kona ya Enock Atta Agyei.

Bao la pili lilifungwa na Abbas Mohammed, dakika ya 23 kabla ya kuongeza la tatu dakika ya 37.

Yanga ilijipatia bao lake la pekee dakika ya 25 lililofungwa kwa njia ya penalti na Simon Msuva baada ya Obrey Chirwa kuangushwa kwenye eneo lahatari.

Kipa Deo Munishi 'Dida' aliiokoa Yanga isiadhirike zaidi baada ya kuokoa penalti dakika ya 10 iliyopigwa na Malik Akowuah.

SERENGETI BOYS YAENDA KUWEKA KAMBI MADAGASCAR

Dua na sala za Watanzania zielekezwe pia kwa timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’, iliyoondoka leo saa 12.00 Uwanja wa Ndege ya Mwalimu Julius K. Nyerere, Dar es Salaam, Tanzania kwenda Antananarivo, Madagascar kupitia Uwanja wa Ndege wa Ndege ya Oliver Tambo jijini Johannesburg, Afrika Kusini.

Serengeti Boys inayokwenda kuweka kambi huko Antananarivo, Madagascar inatarajiwa kufika huko saa 8.10 mchana. Timu hiyo inajiandaa kucheza na Afrika Kusini katika mchezo wa awali kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika utakaofanyika Agosti 6, 2016.

Mchezo wa marudiano utafanyika Agosti 21, mwaka huu kwenye Uwanja wa Azam, ulioko Chamazi-Mbagala, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. Serengeti ipo kwenye ushindani wa kuwania nafasi ya kufuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana, zitakazofanyika mwakani huko Madagascar.

Wakati mkuu wa msafara akiwa ni Ayoub Shaibu Nyenzi ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Soka la Vijana, maofisa wengine waliosafiri na timu hiyo ni Kocha Mkuu, Bakari Nyundo Shime, Daktari wa timu hiyo, Shecky Francis Mngazija na Mtunza Vifaa, Andrew Vanance Andrew pamoja na Juma Kaseja Juma ambaye kwa muda amechukua nafasi ya makocha wasaidizi, Sebastian Nkoma na Muharam Mohammed ‘Shilton’ wanaohudhuria kozi ya makocha ngazi ya juu inayoratibiwa na CAF.

Nyota waliosafiri ni pamoja na makipa, Ramadhani Awm Kabwili, Kelvin Deogratius Kayego na Samwel Edward Brazio wakati mabeki wako Kibwana Ally Shomari, Nickson Clement Kibabage, Israel Patrick Mwenda, Dickson Nickson Job, Ally Hussein Msengi, Issa Abdi Makamba na Enrick Vitalis Nkosi.

Viungo ni Kelvin Nashon Naftal, Ally Hamisi Ng’anzi, Asadi Ali Juma Ali, Syprian Benedictor Mtesigwa, Ibrahim Abdallah Ali, Shaban Zuberi Ada huku washambuliaji wakiwa ni Mohammed Abdallah Rashid, Yohana Oscar Mkomola na Muhsin Malima Makame.

“Najua mchezo utakuwa mgumu, lakini nakiamini kikosi change. Kiko imara,” amesema Shime, maarufu zaidi kwa jina la Mchawi Mweusi.

Serengeti Boys inakwenda kucheza na Afrika Kusini baada ya kuwatoa Shelisheli kwa jumla ya mabao 9-0 katika mechi zake mbili za kimataifa. Mshindi wa jumla kati ya Serengeti Boys na Afrika Kusini, atacheza na timu mshindi kati ya Namibia na Congo-Brazaville.

Hivi karibuni Serengeti Boys ilifanya ziara India ambako walishiriki mashindano ya vijana ya Kimataifa yanayotambuliwa na FIFA (AIFF International Youth Tournament 2016) kabla ya kurudi na rekodi ya kupigiwa mfano si tu katika Tanzania na kwa nchi za Afrika Mashariki. Ilishika nafasi ya tutu nyuma ya Korea Kusini na Marekani.

SHEIKH SAID BADO MAKAMU MWENYEKITI TPLB

Bwana Said Mohamed bado ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) baada ya kuingia kwenye wadhifa huo katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 2013.

Nafasi hiyo ya Bw. Mohamed ni kwa mujibu wa Kanuni za Uendeshaji za TPLB, na aliipata kupitia uchaguzi huo. Pia Makamu Mwenyekiti huyo ni Mwenyekiti wa klabu ya Azam FC inayoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom.

Bw. Mohamed alikuwa Meneja Mkuu wa Kampuni ya Salim Said Bakhresa ambayo pia inamiliki pia timu ya Azam FC kabla ya kustaafu Mei mwaka huu. Licha ya kustaafu ajira yake ndani ya SSB, lakini Bw. Mohamed bado ni Mwenyekiti wa Azam FC.

Kwa mujibu wa Katiba ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa TPLB pia ni wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho hilo na wanaendelea na majukumu yao kama kawaida.

Uchaguzi ujao wa viongozi wa TPLB ambayo inaongozwa na Mwenyekiti wake Hamad Yahya unatarajiwa kufanyika mwakani.

RAIS WA FIFA, INFANTINO AMSIFU MALINZI

Rais wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Gianni Infantino amemsifu Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kuwa ni miongoni mwa viongozi wa vyama vya soka duniani walioamua kuendesha soka kwa weledi kutokana na kuratibu mafunzo mbalimbali kwa makocha na waamuzi.

Salamu za Infantino zimetolewa na Msimamizi Mkuu wa kozi ya waamuzi nchini, Carlos Henrique kutoka Afrika Kusini akisema, “Infantino ana ripoti zote ya namna mpira wa miguu unavyoendeshwa duniani. Anasifu Tanzania kwa  namna mnavyopiga hatua. Ana ripoti idadi ya makocha walivyokuwa wachache na sasa mna makocha wengine wako kwenye kozi.

“Mbali ya makocha, leo tuko nanyi waamuzi, ni hatua kubwa ambayo Rais Infantino amemsifu Rais wa TFF, Bwana Malinzi,” alisema Henrique.

Henrigue aliyeka waamuzi hao kujikita zaidi kusoma namna sheria 17 za mpira wa miguu zilivyoboreshwa kwa kuondoa zaidi ya maneno 1,000 ili kuja kusimamia vema michezo wa soka huku akiwataka kuwa mahiri wakati wote. Henrique anafanya kazi hiyo kwa kushirikiana na Mark Mzengo kutoka Malawi, Felix Tangawarima wa Zimbabwe na Gladys Onyago kutoka Kenya.

Kozi za Waamuzi wa Mpira wa Miguu wa Tanzania sasa ilianza  jana Julai 25, 2016 kwa waamuzi wenye Beji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kimataifa (FIFA) na waaamuzi waandamizi wanaotarajiwa kuveshwa beji hizo kwa majina yao kupendekezwa FIFA kama watapata matokeo mazuri kwenye kozi inayoendelea.

Kozi ilianza kwa ratiba ya waamuzi wote kuchukuliwa vipimo (physical fitness test) kwa kila mwamuzi chini ya wakufunzi hao kutoka FIFA. Baada ya vipimo, darasa la waamuzi hao litaanza kwa nadharia na vitendo. Darasa hilo litafikia mwisho Julai 29, 2016 kabla ya kuanza darasa la waamuzi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Ligi Daraja la Kwanza ya StarTimes (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL) na makamishna wa michezo kwa msimu wa 2016/2017.

MKWASA AITA NYOTA 24 STARS


Kocha Mkuu timu ya Mpira Tanzania ‘Taifa Stars’, Charles Boniface Mkwasa ameita kikosi cha wachezaji 24 watakaoanza kambi ya awali kuajindaa na mchezo dhidi ya Nigeria utakaofanyika Lagos, Septemba 2, 2016.

Kwa mujibu wa Mkwasa, timu hiyo itaingia kambini Agosti 1, 2016 na itadumu kwa siku tano tu kabla ya kuvunjwa na kuitwa tena mwishoni mwa mwezi Agosti, 2016 kujiandaa na kambi ya mwisho na moja kwa moja itakuwa ni kwa ajili ya safari kwenda Nigeria.

Katika kikosi hicho, Mkwasa hajaita nyota wa kimataifa akiwamo Nahodha, Mbwana Samatta wa FC Genk ya Ubelgiji na Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kwa sababu ya majukumu waliyonayo kwenye klabu zao kwa sasa.

Kadhalika, nyota hao wataungana na wenzao nchini Nigeria kwa kuwa mchezo huo upo kwenye kalenda ya CAF na ni wa mashindano. Mchezo huO ambao ni wa kukamilisha ratiba, Mkwasa amesema utakuwa mgumu kwani Nigeria wamebadili benchi la ufundi hivyo kila timu inaungalia mchezo huu kwa jicho la pekee.

Wachezaji walioitwa ni:


Makipa:
Deogratius Munishi
Aishi Manula
Benny Kakolanya

Mebeki:

Kelvin Yondani
Aggrey Morris
Oscar Joshua
Mohamed Husein ‘Tshabalala’
Juma Abdul
Erasto Nyoni

Viungo:
Himid Mao
Mohamed Ibrahim
Shiza Kichuya
Jonas Mkude
Ibrahim Jeba
Mwinyi Kazimoto
Farid Mussa
Juma Mahadhi
Hassan Kabunda

Washambuliaji:

Simon Msuva
Joseph Mahundi
Jamal Mnyate
Ibrahim Ajib
John Bocco
Jeremia Juma

Thursday, July 21, 2016

PEPSI YAPANDA DARAJA LA PILI KWA KLABU YA 2016/2017


Shirkisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linapenda kutoa pongezi zake za dhati kwa Klabu ya Pepsi FC ya Arusha kwa kupata nafasi ya kupanda daraja na kuingia Daraja la Pili SDL msimu wa 2016/2017.

Hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 5 kipengere cha (5) ya mashindano ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa RCL msimu wa 2015/2016.

Timu imefanikiwa kupata nafasi ya pili katika msimamo wa ligi ya mabingwa wa Mikoa 2015/2016 kituo cha Singida na kuongoza kati ya timu zilizoshika nafasi ya pili katika vituo vilivyosalia ambavyo ni Njombe, Morogoro na Muleba. TFF inaItakia kila la kheri katika maandalizi ya kushiriki Daraja la Pili msimu wa 2016/2017

TFF YACHANGIA MADAWATI 200


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetoa madawati 200 ikiwa ni sehemu ya mapato ya Ngao ya Hisani utakaochezwa Agosti 17, 2016.

TFF inaunga mkono juhudi za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na juhudi za Serikali kwa ujumla katika kuhakikisha vijana wa Kitanzania wanakuwa na mazingira bora ya kupata elimu.

Kadhalika TFF inamshukuru Katibu Mkuu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah kwa juhudi za kuendelezaa mpira wa miguu na kuutumia katika kuliletea Taifa maendeleo.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania litaendelea kushirikiana na Ofisi ya Bunge Sports Club katika kufanikisha mashindano mbalimbali hasa mhezo wa Hisani kati ya Simba Sports Club na Young African (Wabunge) utakaofanyika hapo baadaye kwa mujibu wa ratiba na uratibu wa Bunge.

MALINZI AWAPA DARASA MAKOCHA WA SOKA



Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi, amewataka makocha 20 wanaoshiriki kozi ya ukocha wa leseni A, kwenda kutumia elimu hiyo kusaidia na kuendeleza soka katika nyanja mbalimbali.

Malinzi aliyasema hayo jana Julai 19, 2016 wakati akifungua kozi hiyo ambayo inashirikisha makocha 20 na kufanyika kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

“Ndugu zangu makocha nawasihi mnapohitimu kozi hii msiende kuweka vyeti vyenu ndani bali mkawe chachu ya mafanikio ya soka kwani kwa idadi ya makocha 23 ambao wana leseni A ni makocha saba tu ambao wanafundisha,” alisema Malinzi.

Pia Malinzi alisema ikimaliza kozi hii Tanzania itakuwa na makocha 43 wenye leseni A jambo ambalo ni idadi ndogo ikilinganishwa na Tanzania ambayo ina watanzania milioni 50.

Pia Malinzi alisema kuanzia msimu huu mpya wa ligi makocha watakaoruhusiwa kuwa na timu za ligi kuu ni wale wenye leseni A na kwa daraja la kwanza ni wenye leseni B huku akisema wasaidizi watatakiwa kuwa na leseni C.

Kozi hii itakuwa inafendeshwa na mkufunzi Sunday Kayuni akisaidia na Salum Madadi na itakuwa ya mwezi mmoja lakini ikimalizika wiki mbili itasimama na kuja kumalizika baadaye.

WACHEZAJI WATATU MISUNA FC WAFUNGIWA

Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imewafungia wachezaji watatu, walioshiriki katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL), kituo cha Morogoro 2015/2016.

Kikao cha Kamati ya   TFF kilichokaa Julai 14, 2016 kujadilina kupitia malalamiko na taarifa za waamuzi na Kamisaa za mashindano ya ligi ya mabingwa wa mikoa RCL kituo cha Mororgoro, kimebaini kwamba wachezaji Imani T. Mwanga, Fred John Lazaro na Brown Chalamila walifanya udanganyifu wa majina ili kukamilisha zoezi la usajili.

KUHUSU MCHEZAJI IMANI T. MWANGA

Kamati imepitia taarifa za waamuzi na Kamisaa pamoja na uthibitisho uliopatikana imemkuta na tuhuma za udanganyifu wa jina. Alitumia majina mawili tofauti. Imani Vamwanga ligi daraja la kwanza klabu cha Kurugenzi FC na Emmanuel T. Mwanga klabu cha Stand Misuna.

Kwa mujibu wa kanuni za ligi ya mabingwa wa Mikoa, kanuni ya 39 (1) Kamati imekufungia kucheza mpira ndani na nje ya nchi kwa kipindi cha miezi 12. Adhabu hii inaanza toka tarehe ya kuandi kwa barua yake.

KUHUSU FRED JOHN LAZARO

Kikao cha Kamati ya Mashindano ya TFF kilichokaa Julai 14, 2016 kujadili na kupitia malalamiko na taarifa za waamuzi na Kamisaa za mashindano ya ligi ya mabingwa wa mikoa RCL kituo cha Mororgoro, kimebaini kwamba Fred John Lazaro pamoja na klabu ya Stand Misuna FC walifanya udanganyifu wa majina ili kukamilisha zoezi la usajili.

Kupitia taarifa za waamuzi na Kamisaa pamoja na uthibitisho uliopatikana, imebainika Fred John Lazaro alifanya udanganyifu wa majina hivyo kuchezea klabu mbili tofauti katika msimu mmoja isivyo halali.

Katika klabu ya Stand Misuna FC iliyoshiriki ligi ya mkoa Singida na ligi ya mabingwa wa mikoa kituo cha Morogoro 2015/2016 ulisajiliwa kwa jina la Fred John Lazaro kwa usajili namba 044 ukivaa jezi namba 13, pia katika klabu ya Singida United FC ya Singida iliyoko daraja la pili (SDL) msimu wa 2015/2016 ulisajiliwa kwa jina la Adolf Anthon leseni namba 950725003 ukivaa jezi namba 3, 6 na 8 katika mechi tofauti.

Kwa taarifa hapo juu kamati imebaini kuwa wewe siyo mchezaji halali kuichezea timu ya Stand Misuna FC katika ligi ya mabingwa wa mikoa kwa ni hukucheza ligi ya mkoa Singida, na pia kwa kushirikiana na uongozi wa klabu ya Stand Misuna FC umedanganya majina ili kufanikisha zoezi la usajili kinyume cha kanuni ya 48 kipengere cha (2) na (4).

Hivyo kwa mujibu wa kanuni za ligi ya mabingwa wa Mikoa, kanuniya 31 kipengere cha (11) na kanuni ya 39 kipengere cha (1) wewe Fred John Lazaro jezi namba 13 (mchezaji) unafungiwa kucheza mpira ndani na nje ya nchi kwa kipindi cha miezi kumi na mawili (12).

Adhabu hiyo inaanza mara moja baada ya muhusika kupata barua yake.

KUHUSU BROWN CHALAMILA

Kikao cha Kamati ya Mashindano ya TFF kilichokaa Julai 14, 2016 kujadilina kupitia malalamiko na taarifa za waamuzi na Kamisaa za mashindano ya ligi ya mabingwa wa mikoa RCL kituo cha Mororgoro, kimebaini kwamba Brown Chalamila pamoja na klabu ya Stand Misuna FC walifanya udanganyifu wa majina ili kukamilisha zoezi la usajili.

Kupitia taarifa za waamuzi na Kamisaa pamoja na uthibitisho uliopatikana umekutwa na makosa ya udanganyifu wa majina hivyo kuchezea vilabu viwili tofauti katika msimu mmoja isivyo halali.

Katika klabu ya Stand Misuna FC iliyoshiriki ligi ya mkoa Singida na ligi ya mabingwa wa mikoa kituo cha Morogoro 2015/2016 ulisajiliwa na kucheza kwa jina la Costa Bryan Bosco kwa usajili namba 029 ukivaa jezi namba 03, wakati wewe ni mchezaji halali wa klabu ya Kurugenzi FC ya Mafinga-Iringa iliyoko daraja la kwanza (FDL) msimuwa 2015/2016 leseni namba 921004001 ukivaa jezi namba 03.

Kwa taarifa hapo juu kamatii mebaini kuwa wewe siyo mchezaji halali wa timu ya Stand Misuna FC katika ligi ya mabingwa wa mikoa kwani hukucheza ligi ya mkoa Singida, na pia kwa kushirikia na uongozi wa klabu ya Stand Misuna FC ulidanganya majina ili kufanikisha zoezi la usajili kinyume na kanuni ya 48 kipengele cha (2) na (4) ya ligi ya mabingwa wa mikoa.

Hivyo, kwa mujibu wa kanuni za ligi ya mabingwa wa Mikoa, kanuniya 31 kipengele cha (11) na kanuni ya 39 kipengele cha (1) wewe Brown Chalamila unafungi wa kucheza mpira ndani na nje ya nchi kwa kipindi cha miezi kumi na mawili (12). Adhabu hiyo inaanza mara moja kuanzia tarehe ya barua yake.

NAMUNGO YAPIGWA FAINI, YAPANDA DARAJA



Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imeipiga faini ya Sh. 500,000, Klabu ya Namungo FC ya Lindi kwa kila mechi ambayo mchezaji Imani Vamwanga aliichezea timu hiyo akitumia jina la Emmanuel T. Mwanga katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL), kituo cha Morogoro 2015/2016.

Katika kikao kilichoketi Julai 14, 2016 kujadilina, kupitia, malalamiko na taarifa za waamuzi na Kamisaa za mashindano ya RCL katika kituo cha Morogoro, kamati imebaini kwamba Namungo ilifanya udanganyifu wa jina la mchezaji kwa kumsajili na kumchezesha mchezaji Imani Vamwanga leseni Na. 930909003 ya usajili wa Ligi Daraja la Kwanza FDL msimu wa 2015/2016 klabu ya Kurugenzi Mafinga akitumia jina la Emmanuel T. Mwanga.

Kamati imebaini hayo kupitia taarifa za usajili, ripoti za waamuzi na makamisaa kwa michezo ambayo mchezaji tajwa hapo juu amecheza katika Mashindano ya Ligi ya mkoa wa Lindi na Mashindano ya Ligi ya Daraja la Kwanza FDL msimu wa 2015/16. Namungo inaadhibiwa kwa mujibu wa Kanuni ya 39 (1) inayozungumza adhabu kwa klabu.

Kamati ya Mashindano ya TFF imetoa uamuzi huo kwa Namungo FC kupigwa faini ya Sh. 500,000 kwa kila mechi ambayo mchezaji Imani Vamwanga akitumia jina la Emmanuel T. Mwanga amecheza katika mashindano ya RCL.

Pamoja na faini hiyo kwa kila mchezo ambao Namungo ilimchezesha mcheza huyo, timu hiyo Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imeitangaza Namungo FC kupanda daraja kwenda Ligi Daraja la pili msimu wa 2016/2017 kama ilivyoainishwa kwenye kanuni ya 5 kipengere cha (4).

Kamati imejiridhisha kwa kupitia taarifa za usajili, ripoti za waamuzi na makamisaa kwa michezo ambayo ilikuwa inalalamikiwa imefikia uamuzi huo kwa mujibu wa kanuni za mashindano hayo. Kamati imeipongeza na kukutakia kila la heri katika michezo.

Wednesday, July 20, 2016

SIMBA, YANGA KUVAANA OKTOBA MOSI, 2016


MIAMBA ya soka nchini Yanga na Simba, inatarajiwa kuteremka dimbani Oktoba Mosi, mwaka huu.

Mchezo huo utakuwa wa kwanza kwa mahasimu hao kukukata katika msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara ambao ni mechi namba 49 katika raundi ya 10.

Yanga na Simba, zitavaana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara unatarajiwa kuanza Agosti 20, mwaka huu katika viwanja mbalimbali.

Kufuatia ratiba iliyotolewa jana na Shirikisho la Soka Tanzania TFF, mchezo wa Ngao ya Jamii ambao utazikutanisha Yanga na Azam utachezwa Agosti 17, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Baada ya kufanyika kwa mchezo huo, Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu mpya utakuwa umefunguliwa rasmi.

Baada ya mchezo huo Yanga watafungua dimba na JKT Ruvu Agosti 31, katika mchezo utakaochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Ofi sa Habari wa TFF, Alfred Lucas alisema kwa ujumla Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2016/ 2017 itaanza Agosti 20, Simba wakifungua dimba na Ndanda Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, huku Azam wakiikaribisha African Lyon Uwanja wa Chamazi.

Lucas alisema kuwa ratiba hiyo imekamilika na imeangalia mambombalimbali ikiwemo mechi za kimataifa ili kuepukana na viporo kama ilivyokuwa msimu uliopita.

“Ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao imeshakamilika na tumezingatia mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na mechi za kimataifa ili kuhakikisha tunaepuka viporo,” alisema Lucas.

Mechi zingine za ufunguzi zitakuwa kati ya Kagera Sugar na Mbeya City Uwanja wa Kaitaba, Bukoba, TotoAfricans na Mwadui Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza, Stand United na Mbao FC zitakazomenyana kwenye Uwanja wa Kambarage, Shinyanga.

Mechi zingine zitazikutanisha timu za Mtibwa Sugar na Ruvu Shooting Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro na Majimaji na Prisons Uwanja wa Majimaji Songea.

Saturday, July 16, 2016

TFF YATANGAZA MAJINA YA WANAOWANIA TUZO ZA LIGI KUU


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania limetangaza wanamichezo wote wanaowania tuzo 13 kwenye hafla ya washindi wa Ligi Kuu ya Vodacom kwa msimu wa 2015/2016 itakayofanyika Jumapili (Julai 17 mwaka huu), kwenye hoteli ya Double Tree by Hilton jijini Dar es Salaam.

Aina 13 za tuzo ya Ligi hiyo inayodhaminiwa na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania zitatolewa kwa washindi chini ya uratibu wa Kamati ya Tuzo ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) inayoundwa na waandishi wa habari za michezo, makocha, viongozi (administrators) na wawakilishi kutoka kwa wadhamini (Vodacom na Azam Tv).

Tuzo hizo na kiasi cha fedha wanazopata washindi kwenye mabano ni

Bingwa (sh. 81,345,723)
Makamu bingwa (sh. 40,672,861)
Mshindi wa tatu (sh. 29,052,044)
Mshindi wa nne (sh. 23,241,635)

Timu yenye Nidhamu Bora (sh. 17,228,820)
*Zilizopendekezwa kuwania tuzo hiyo ni:

JKT Ruvu
Mgambo Shooting na
Mtibwa Sugar

Mchezaji Bora wa Ligi (sh. 9,228,820)
Waliopendekezwa (nominees) kuwania tuzo hiyo ni:
Shiza Kichuya (Mtibwa Sugar)
Juma Abdul (Yanga)
Mohamed Hussein (Simba)

Mfungaji bora (sh. 5,742,940)

Kipa Bora (sh. 5,742,940)
Waliopendekezwa (nominees) kuwania tuzo hiyo ni:
Aishi Manula (Azam),
Beno Kakolanya (Tanzania Prisons)
Deogratius Munishi (Yanga)

Mchezaji Bora wa Kigeni (sh. 5,742,940)
Donald Ngoma (Yanga)
Thabani Kamusoko (Yanga)
Vincent Agban (Simba)

Kocha Bora (sh. 8,000,000)
Waliopendekezwa (nominees) kuwania tuzo hiyo ni:
Hans Van Pluijm (Yanga)
Mecky Maxime (Mtibwa Sugar) na
Salum Mayanga (Tanzania Prisons)

Mwamuzi bora (sh. 5,742,940)
Waliopendekezwa (nominees) kuwania tuzo hiyo ni:
Anthony Kayombo
Ngole Mwangole
Rajab Mrope

Mchezaji Bora Chipukizi (sh. 4,000,000
Waliopendekezwa (nominees) kuwania tuzo hiyo ni:
Farid Mussa (Azam)
Mohamed Hussein (Simba)
Mzamiru Yasin (Mtibwa Sugar)
Shiza Kichuya (Mtibwa Sugar)

Goli bora la msimu (sh. 3,000,000)
Kinyang'anyiro cha goli bora ni:
Ibrahim Ajib (magoli mawili ) na
Amisi Tambwe  (goli moja)

TFF SASA YAUTAMBUA UONGOZI MPYA WA STAND UNITED



Katika kikao chake cha 13 Julai, 2016, Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imetoa msimamo kuhusu suala la Stand United kama ifuatavyo:-

Kamati imepitia vielelezo vyote na kujadiliana na wadau wa Stand United na kubaini bayana kwamba Stand United Football Club, ndiyo jina sahihi na halali lililosajiliwa kwa Msajili wa Klabu na Vyama vya Michezo.

Uchaguzi uliofanyika hivi karibuni kwenye Klabu ya Stand United una sifa zote za kuitwa uchaguzi huru na wa haki kwa vile mchakato ulihusisha wanachama halali klabu hiyo.

Wanachama wa Stand United ambao hawakushiriki uchaguzi ikiwa ni pamoja na wale waliokwenda kundi la kampuni wana uhalali wa kuendelea kuwa wanachama wa Stand United.

Viongozi waliochaguliwa katika uchaguzi wa Stand United FC ni halali na ni ruksa kwao kuendesha ofisi na shughuli za Stand United kwa ujumla.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania linatambua daftari la Wanachama wa Stand United lililoboreshwa kwa maelekezo ya TFF.


IMETOLEWA NA DOMINA MADELI –

MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA UCHAGUZI TFF

TFF YAIADHIBU ABAJALO



Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji chini ya Mwenyekiti, Richard Sinamtwa imebaini kasoro kwa Abajalo FC kumtumia mchezaji Laurent E. Mugia hivyo kuamua kumfungia mchezaji huyo kwa kipindi
cha mwaka mmoja kwa mujibu wa kanuni ya 36 (16) toleo la mwaka 2014 la Ligi Daraja la Pili kwa kosa la kuchezea klabu mbili katika msimu mmoja.

Kwa kuwa kanuni za Ligi Daraja la Pili mpaka Ligi Kuu zina upungufu unaofanyiwa mapitio pale kiongozi wa timu anapofanya udanganyifu wa usajili wa mchezaji bila kumshirikisha mchezaji, Kamati sasa
imelazimika kutumia kanuni za Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Ibara ya VII (10) ikinukuu:

“A team which will have committed a fraud on the identity of player or which will have allowed a suspended or non-qualified player to take part in match shall, lose the match and shall be completely eliminated
from the competition as soon as the incriminating fact are clearly established by CAF organizing committee.” Mwisho wa kunukuu.

Kwa maelezo hayo, timu ya Abajalo FC inanyang’anywa pointi sita. Timu za Pamba SC na The Mighty Elephant wanapewa pointi tatu kila timu na magoli matatu.

Kamati inaagiza Sektretarieti kuwachukulia hatua na kuwapeleka katika vyombo vya Serikali viongozi wote wa timu ya Abajalo walioshiriki kubadilisha jina la mchezaji alilotumia akiwa na timu ya  Kagera Sugar ili kufanikisha usajili wao na pia kwa kubadilisha tarehe, mwezi na mwaka wa kuzaliwa za mchezaji ili kufanikisha usajili wao kwa msingi kwamba waligushi.

Uamuzi huu, ni wa mwisho na kwamba kama kuna ambaye hajaridhika, ana nafasi ya kukata rufaa kwenye CAS - Mahakama ya Mashauri ya Soka ya FIFA iliyoko Geneva, Uswisi.

Awali kwa nyakati tofauti, Pamba SC ya Mwanza na The Mighty Elephant ya Songea zilikata rufaa kuilalamikia Abajalo FC kwa kumtumia mchezaji wa Kaliua City ya Tabora, Laurence Mugia kutoka
Kagera Sugar katika michezo ya mtoano wa Ligi Daraja la Pili kwa ajili ya kupanda daraja la kwanzaa huku wakijua kuwa ni kosa kwa mujibu wa kanuni.

MALINZI AWAPONGEZA NDULANE NA KUULI KWA KUTEULIWA KUWA WAKURUGENZI WA WILAYA


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amewapongeza Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa TFF, Wakili Revocatus Kuuli na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Lindi, Francis Ndulane.

Kuuli, Wakili msomi aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Rufani ya Nidhamu ya TFF, ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Igunga mkoani Tabora.

Kadhalika, katika uteuzi huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli amemteua Ndulane ambaye ni Mjumbe Mkutano Mkuu wa TFF kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara mkoani Morogoro.

Katika salamu hizo, Rais Malinzi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli kwa kuwateua viongozi hao wa TFF, akisema kwamba ameonyesha namna alivyo na imani na watendaji hao katika shughuli zao mbalimbali ikiwamo TFF.

WAAMUZI LIGI MBALIMBALI WAANZA KUJIPANGA


Kamati ya Waamuzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, imeandaa kozi mbalimbali ikiwa ni maandalizi ya kwa waamuzi katika michuano ya kimataifa sambamba na Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Ligi Daraja la Kwanza ya StarTimes (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL) kwa msimu wa 2016/2017.

Kozi hiyo MA (Members Associations) itaanza kwa waamuzi wenye Beji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kimataifa (FIFA) ambao kwa sasa wako 18 hapa Tanzania na wengine 12 wa ‘Elite’ ikiwa na maana ya waamuzi wanaotarajiwa kuveshwa Beji za FIFA. Darasa la waamuzi hao litakuwa na waamuzi 30.

Waamuzi hao wenye Beji ya FIFA na wale wanaotarajiwa kuveshwa beji hiyo, wanatakiwa kuripoti Dar es Salaam Julai 23, 2016 ambako kwa mujibu wa ratiba wataanza program ya kozi hiyo kwa kupima kasi ya kukimbia siku inayofuata Julai 24, 2016 wakisimamiwa na wakufunzi kutoka FIFA.

Mara baada ya programu hiyo, kozi itaendelea kwa waamuzi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Ligi Daraja la Kwanza ya StarTimes (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL) na makamishna wa michezo kwa msimu wa 2016/2017 na kwamba wahusika wote watajigharamia gharama zote.

Waamuzi hao wa ligi ya ndani wataripoti na kujisajili Kituo cha Dar es Salaam Julai 29 na siku inayofuata Julai 30, 2016 na Julai 31, 2016 watakuwa na kozi ya kitathmini kasi kwa kukimbia kabla ya Agosti 1 na 2, 2016 kuwa na semina darasani na mitihani wakati Agosti 3, 2016 kutakuwa na semina na mitihani kwa makamishna mbalimbali wa michezo ya mpira wa miguu.

Thursday, July 14, 2016

TFF YASAKA MENEJA MASOKO NA HABARI


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limeongeza muda zaidi kuimarisha idara zake ambako imeongeza muda wa wiki moja kwa Watanzania wenye sifa za Idara ya Masoko na Habari ili kuongoza Idara hiyo.

Awali tarehe ya  mwisho ilikuwa Julai 11, 2016 lakini kwa sasa tarehe ya mwisho itakuwa Julai 19, mwaka huu kwa nafasi ambazo TFF imetangaza ajira.

Lengo hasa ni kuendana na hali halisi ya uendeshaji mpira wa miguu duniani ambako masoko, habari na mahusiano ya Kimataifa yamekuwa funguo za kupata rasilimali kwa ajili ya maendeleo ya mchezo wa mpira wa miguu popote duniani.

Pili ni kuhakikisha rasilimali za kuendesha mpira wa miguu zinatokana na soka na vilevile kuhakikisha wadau wanapata habari sahihi kwa wakati mwafaka.

Kwa nafasi za kazi TFF tembelea tovuti yao www.tff.or.tz au waandikie ili utumiwe tangazo kwa barua pepe tanfootball@tff.or.tz

Mbali ya kuboreshwa kwa Idara hiyo ya Masoko, pia TFF imepania kutoa kipaumbele katika masuala ya waamuzi na wanawake kwa kuanzisha madawati ya kudumu katika Kurugenzi ya Ufundi. Hapo awali madawati ya wanawake na waamuzi yaliendeshwa na watumishi wa kujitolea (Volunteers) au wa muda (Part timers).

Akizungumza na www.tff.or.tz, Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine aliamsha changamoto mbalimbali za soka la wanawake miongoni mwanzo ikiwa ni uibuaji na uendelezaji vipaji, Timu ya Taifa, mafunzo katika taaluma mbalimbali, ligi za wanawake na masoko kwa bidhaaa (products) za soka la wanawake.

Kuhusu waamuzi, Katibu Mkuu alilielezea eneo hili kama lenye changamoto nyingi hasa hasa katika kupata waamuzi wenye viwango vya Kimataifa.

KENYA YAKACHA KUKIPIGA NA SERENGETI BOYS



Timu ya Vijana ya Kenya, imefuta ziara yake ya kwenda Dar es Salaam kwa ajili kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya vijana wa Tanzania wenye umri wa chini ya miaka 17 maarufu kwa jina la Serengeti Boys.

Mchezo huo ulipangwa kufanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Julai 23, 2016.

Kwa mujibu wa barua kutoka kwa Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Kenya (FKF), Robert Muthomi kwenda Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kufuta kwa ziara hiyo kunatokana na nafasi ambayo Kenya imeipata.

Timu ya Taifa ya Vijana ya Kenya imeteuliwa kushiriki michuano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu la COSAFA inayotarajiwa kuanza Julai 22, 2016 hadi Julai 31, 2016 mara baada ya Msumbiji kujitoa kwenye mashindano hayo.

“Tunaomba kukutarifu kuwa timu yetu imetuliwa katika michuano ya vijana ya COSAFA, hivyo ziara yetu Tanzania haitakuwako kama ambavyo sisi wenyewe tuliomba mchezo huo kwenu (TFF) ufanyike Julai 23, 2016,” ilisema sehemu ya barua hiyo iliyosainiwa na Muthomi.

Licha ya kwamba mchezo huo hautakuwako, ratiba ya Serengeti Boys ambayo inapambana kuwania nafasi ya kucheza Kombe la Mataifa Afrika hapo mwakani, imebaki vilevile kwa timu kuingia kambini Jumapili Julai 17, 2016 kwenye Hosteli za TFF zilizoko Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Ilala jijini Dar es Salaam.

Timu hiyo inayonolewa na Bakari Shime itapiga kambi ya wiki moja katika hosteli hizo, kabla ya kwenda Madagascar ambako itapiga kambi ya takribani wiki mbili ikiwa ni ahadi ya Rais wa TFF, Jamal Malinzi ambaye alitoa ofa hiyo baada ya kuwatoa Shelisheli kwa jumla ya mabao 9-0 katika mechi zake mbili za kimataifa.

Serengeti Boys inatarajiwa kucheza na Afrika Kusini kati ya Agosti 5, 6 au 7, 2016 huko Afrika Kusini kabla ya mchezo wa marudiano utakaofanyika saa 9.00 alasiri, Agosti 14, 2016 kwenye  Uwanja wa Azam Complex, ulioko Chamazi, Dar es Salaam.

Mshindi wa jumla katika michezo hiyo, itacheza na timu mshindi kati ya Namibia na Congo-Brazaville.

Wednesday, July 13, 2016

PAMBANO LA TWIGA STARS VS RWANDA LAAHIRISHWA




Shirikisho la Mpira wa Miguu Rwanda (FERWAFA), limeahirisha mchezo wa kirafiki wa kimataifa kati ya timu ya taifa ya wanawake ya Rwanda dhidi ya wageni, Tanzania ‘Twiga Stars’ uliokuwa ufanyike Jumapili Julai 17, 2016.

Mchezo huo uliandaliwa na FERWAFA na Rais Paul Kagame alipendekeza mchezo huo kuwa sehemu ya burudani kwa wakuu mbalimbali wa nchi za Afrika wanaotarajiwa kuwa na mkutano wa viongozi hao kuanzia kesho Julai 14, 2016.
 

Kwa mujibu wa barua ya Rais wa FERWAFA, Nzamwita Vincent ya Julai 12, 2016 kwenda Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), sababu za kuahirisha mchezo huo ni ratiba ya mkutano huo wa 27 wa wakuu nchi.

“Tunasikitika kuwataarifu kuwa ile ratiba ya kuwa na mchezo wa kirafiki kati ya Rwanda na Tanzania, imefutwa. Tunaomba radhi kwa taarifa hii ya ghafla ambayo iko nje ya uwezo wetu inayowafikia huku tukijua kwamba mlikuwa tayari mmeandaa timu kwa ajili ya mchezo,” ilisema sehemu ya barua hiyo.

“Hata hivyo tunaahidi kuendelea kufanya mawasiliano ili kupanga tarehe nyingine ya kufanyika mchezo huo,” ilisisitiza barua.

Taarifa hiyo imekuja wakati tayari Twiga Stars ilikuwa imeanza maandalizi ya kutosha kwa mchezo huo ambao ulianza kuvutia mamia ya mashabiki wa mpira wa miguu wan chi za Afrika Mashariki.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Rwanda (FERWAFA), limeahirisha mchezo wa kirafiki wa kimataifa kati ya timu za wanawake za Tanzania ‘Twiga Stars’ na wenyeji Rwanda uliokuwa ufanyike Jumapili Julai 17, 2016.

Mchezo huo uliandaliwa na FERWAFA na Rais Paul Kagame alipendekeza mchezo huo kuwa sehemu ya burudani kwa wakuu mbalimbali wa nchi za Afrika wanaotarajiwa kuwa na mkutano wa viongozi hao kuanzia kesho Julai 14, 2016.

Kwa mujibu wa barua ya Rais wa FERWAFA, Nzamwita Vincent ya Julai 12, 2016 kwenda kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), sababu za kuahirisha mchezo huo ni kuingiliana kwa ratiba ya mkutano huo wa 27 wa wakuu nchi za Afrika.

“Tunasikitika kuwataarifu kuwa ile ratiba ya kuwa na mchezo wa kirafiki kati ya Rwanda na Tanzania, imefutwa. Tunaomba radhi kwa taarifa hii ya ghafla ambayo iko nje ya uwezo wetu inayowafikia huku tukijua kwamba mlikuwa tayari mmeandaa timu kwa ajili ya mchezo,” ilisema sehemu ya barua hiyo.

“Hata hivyo tunaahidi kuendelea kufanya mawasiliano ili kupanga tarehe nyingine ya kufanyika mchezo huo,” ilisisitiza barua iliyosainiwa na Nzamwita Vincent.

Taarifa hiyo imekuja wakati tayari Twiga Stars ilikuwa imeanza maandalizi ya kutosha kwa mchezo huo ulioanza kuvutia mamia ya mashabiki wa mpira wa miguu wa ncza Afrika Mashariki na kati.

WAPINZANI WA YANGA KUTUA NCHINI KESHO



Wapinzani wengine wa Young Africans, katika michuano ya kuwania Kombe la Shirikisho Barani Afrika, timu ya mpira wa miguu ya Medeama kutoka Ghana, itawasili Dar es Salaam, Tanzania Alhamisi Julai 14, 2016 kwa ndege ya Shirika la Ndege la Kenya (KQ), imefahamika.

Young Africans itaikaribisha Medeama ikiwa ni mchezo wa tatu kuwania taji hilo hatua ya makundi. Mchezo utafanyika saa 10.00 jioni Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Julai 16, mwaka huu.

Huu ni mchezo wa tatu kwa Young Africans katika harakati za kuwania Kombe la shirikisho hatua ya makundi. Michezo miwili ya awali ilikuwa ni dhidi ya Mo Bejaia ya Algeria ambako ilipoteza kwa bao 1-0 kabla ya kupoteza tena dhidi ya TP Mazembe, mechi iliyopigwa jijini Dar es Salaam.

Mchezo wa Jumamosi utachezeshwa na waamuzi kutoka Misri ambao ni Ibrahim Nour El Din atakayekuwa mwamuzi wa kati; akisaidiwa na Ayman Degaish na Samir Gamal Saad wakati mwamuzi wa akiba akiwa ni Mohamed Maarouf Eid Mansour.

Kamishna wa mchezo huo atakuwa Pasipononga Liwewe kutoka Zambia na maofisa wasimamizi ni Mfubusa Bernard ambaye atasimamia utendaji wa waamuzi wakati Mratibu Mkuu wa mchezo huo kutoka CAF atakuwa Ian Peter Keith Mc Leod.

Monday, July 11, 2016

YANGA YALIMWA FAINI YA DOLA 5,000 NA CAF


Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), limeipiga faini ya dola 5,000 Klabu ya Young African kwa kosa la kuchelewesha mchezo baada ya wachezaji wake kumzonga mwamuzi wakati mchezo wa kuwania kuingia hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho dhidi ya GD Sagrada Esperanca uliofanyika Angola Mei 18, 2016.

Uamuzi wa mchezo huo Na. 100 ulifanywa na Kamati ya Nidhamu ya CAF inayoundwa Mwenyekiti Raymond Hack – Raia wa Afrika Kusini na wajumbe Mustapha Samugabo (Burundi) na Gbenga Elegbeleye (Nigeria). Pia alikuwako Amina Kassem kutoka Sekretarieti ya CAF ambaye ni Mtawala katika Kitengo cha Nidhamu.

Katika mkutano huo uliofanyika Cairo, Misri – Makao Mkuu ya CAF, Julai 3, 2016, kamati ilipitia taarifa zote za mchezo na kufikia uamuzi wa kuipiga faini Young Africans.

Taarifa za mchezo zinasema, wachezaji wa Young Africans walionyesha utovu wa nidhamu kwa kumzonga mwamuzi na kumsukuma mara baada ya kutoa adhabu ya penalti kwa wapinzani. Kwa tukio hilo, mchezo huo ulisimama kwa dakika sita. Polisi waliingia uwanjani kudhibiti hali hiyo.

Kwa kosa hilo, Wachezaji wa Young Africans walivunja Ibara ya 82 inayozungumza utaratibu wa mawasiliano. Kwamba chama chochote cha mpira wa miguu, klabu, ofisa au mtu yoyote wakiwamo wachezaji, lazima waheshimu utaratibu za kuvumilia, uadiliufu na uanamichezo.

Kwa mujibu wa Kamati hiyo ya Nidhamu ya CAF, Young Africans ilistahili kutozwa faini ya dola 10.000 za Marekani kwa makosa ambayo si uungwana kwenye soka yaliyoonyeshwa na wachezaji wake.

Lakini kwa kuwa Young Africans haikuonyesha utovu wa nidhamu katika mchezo mingine ya kimataifa iliyofuata dhidi ya MOB ya Algeria na TP Mazembe ya DRC, imepunguziwa adhabu na sasa wametakiwa kulipa dola 5,000 za Marekani kama faini. Faini hiyo haina budi kulipwa mara moja. Na imetakiwa kuendelea kuwa na nidhamu, vinginevyo adhabu hiyo itawarudia.

Tayari Young Africans imepewa namba za akaunti ya CAF inakotakiwa kulipa, lakini pia imepewa fursa ya kukata rufaa kama wataona kuna haja ya kufanya hivyo. Muda wa kukata rufaa ni siku tatu baada ya kupewa taarifa hiyo kwa maandishi.

TFF YAOMBOLEZA KIFO CHA MWANAHABARI ELIZABETH MAYEMBA


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemtumia salamu za rambirambi Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), Juma Pinto kutokana na kifo cha Elizabeth Mayemba - Mwandishi wa Habari za Michezo wa Gazeti la Majira.

Rais Malinzi amesema, amepokea taarifa za kifo cha mwandishi huyo mwandamizi wa habari za michezo nchini kilichotokea Julai 09, 2016 na habari zake kuanza kusambaa majira ya jioni jana kabla ya kuthibitishwa na wanafamilia na uongozi wa TASWA kupitia njia mbalimbali za mawasiliano.

Salamu za rambirambi za Rais wa TFF Malinzi pia zimekwenda kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki na kuwataka kuwa na moyo wa subira wakati huu mgumu wa msiba wa Elizabeth Mayemba.

Elizabeth Mayemba, wakati wa uhai wake alikuwa na mchango mkubwa katika tasnia ya habari za michezo akitoa mawazo yake hivyo ameacha alama ya ucheshi, kujituma na uwajibikaji katika kufanikisha kazi zake katika gazeti la Majira na wakati fulani magazeti ya Kampuni ya New Habari House 2006.

Mwenyezi Mungu aipumzishe roho ya marehemu Elizabeth Mayemba mahala pema peponi.

Bwana alitoa, Bwana alitoa, jina la Bwana lihimidiwe.

Sunday, July 10, 2016

RATIBA LIGI KUU ENGLAND 2016/217


Agosti 13/14, 2016
Arsenal v Liverpool
Bournemouth v Man United
Burnley v Swansea City
Chelsea v West Ham Utd
Crystal Palace v West Bromwich
Everton v Tottenham
Hull City v Leicester City
Manchester City v Sunderland
Middlesbrough v Stoke City
Southampton v Watford
Agosti 20/21, 2016
Leicester City v Arsenal
Liverpool v Burnley
Man United v Southampton
Stoke City v Man City
Sunderland v Middlesbrough
Swansea City v Hull City
Tottenham v Crystal Palace
Watford v Chelsea
West Bromwich v Everton
West Ham United v Bournemouth
Agosti 27/28, 2016
Chelsea v Burnley
Crystal Palace v Bournemouth
Everton v Stoke City
Hull City v Man United
Leicester City v Swansea City
Man City v West Ham
Southampton v Sunderland
Tottenham v Liverpool
Watford v Arsenal
West Bromwich v Middlesbrough
Septemba 10/11, 2016Arsenal v Southampton
Bournemouth v West Bromwich
Burnley v Hull City
Liverpool v Leicester
Man United v Man City
Middlesbrough v Crystal Palace
Stoke City v Tottenham
Sunderland v Everton
Swansea City v Chelsea
West Ham United v Watford
Septemba 17/18, 2016
Chelsea v Liverpool
Crystal Palace v Stoke City
Everton v Middlesbrough
Hull City v Arsenal
Leicester City v Burnley
Man City v Bournemouth
Southampton v Swansea City
Tottenham v Sunderland
Watford v Man United
West Bromwich v West Ham
Septemba 24/25, 2016
Arsenal v Chelsea
Bournemouth v Everton
Burnley v Watford
Liverpool v Hull City
Man United v Leicester City
Middlesbrough v Tottenham
Stoke City v West Bromwich
Sunderland v Crystal Palace
Swansea City v Man City
West Ham v Southampton
Oktoba 1/2, 2016
Burnley v Arsenal
Everton v Crystal Palace
Hull City v Chelsea
Leicester City v Southampton
Man United v Stoke City
Sunderland v West Bromwich
Swansea City v Liverpool
Tottenham v Man City
Watford v Bournemouth
West Ham United v Middlesbrough
Oktoba 15/16, 2016
Arsenal v Swansea City
Bournemouth v Hull City
Chelsea v Leicester City
Crystal Palace v West Ham United
Liverpool v Man United
Man City v Everton
Middlesbrough v Watford
Southampton v Burnley
Stoke City v Sunderland
West Bromwich v Tottenham
Oktoba 22/23, 2016
Arsenal v Middlesbrough
Bournemouth v Tottenham
Burnley v Everton
Chelsea v Man United
Hull City v Stoke City
Leicester City v Crystal Palace
Liverpool v West Bromwich
Man City v Southampton
Swansea City v Watford
West Ham United v Sunderland
Oktoba 29/30, 2016
Crystal Palace v Liverpool
Everton v West Ham United
Man United v Burnley
Middlesbrough v Bournemouth
Southampton v Chelsea
Stoke City v Swansea City
Sunderland v Arsenal
Tottenham v Leicester City
Watford v Hull City
West Bromwich v Manchester City
Novemba 5/6, 2016
Arsenal v Tottenham
Bournemouth v Sunderland
Burnley v Crystal Palace
Chelsea v Everton
Hull City v Southampton
Leicester City v West Bromwich
Liverpool v Watford
Manchester City v Middlesbrough
Swansea City v Manchester United

AZAM YAWAPIGA KIBUTI NYOTA WAKE SITA, WAMO MURAD NA KAVUMBAGU, MAPROO WAWILI WAFELI MAJARIBIO



Mtandao wa azamfc.co.tz umeripoti kwamba, uongozi wa klabu ya Azam FC, umetangaza rasmi kuwatema wachezaji sita kwa awamu ya kwanza huku nyota wawili wakifeli majaribio.

Nyota hao walioachwa ni makipa Ivo Mapunda, Khalid Mahadhi aliyekuwa ametolewa kwa mkopo Mafunzo ya Zanzibar, mabeki Said Morad, Racine Diouf kutoka Senegal pamoja na washambuliaji Didier Kavumbagu (Burundi) na Allan Wanga (Kenya).

Akizungumza na mtandao rasmi wa klabu www.azamfc.co.tz Ofisa Habari wa Azam FC, Jaffar Idd, alisema wachezaji hao wameachwa wakiwa wamepata stahiki zao kwa wale ambao waliokuwa wamebakiwa na mikataba.

Alisema mbali na wachezaji hao, pia wachezaji wawili kati ya wanne waliokuwa kwenye majaribio nao wameachwa rasmi ambao ni beki wa kushoto kutoka Ghana, Nurudeen Yusif aliyetokea Medeama ya huko na kiungo mshambuliaji David Wirikom (Cameroon).

Wawili hao wamepewa majibu ya kufeli majaribio yao leo asubuhi kufuatia Kocha Mkuu Zeben Hernandez, kutoridhishwa na uwezo wao kwa siku nne walizofanya mazoezi na kikosi cha Azam FC.

“Wakati tunajiandaa na msimu mpya kuna wachezaji tuliwaalika kutoka nchi mbalimbali Afrika kwa ajili ya kufanya majaribio, ambao mpaka sasa wapo wanne, tangu tulipoanza mazoezi kwa siku takribani nne mwalimu leo ameamua kuwapunguza wawili na wawili wamebakia.

“Waliofeli majaribio ni David Wirikom kutoka Cameroon na Nurudeen Yusif kutoka Ghana, kocha ameona viwango vyao havitofautiani sana na viwango vya wachezaji wetu hapa nyumbani, kocha ameongea nao leo mara baada ya mazoezi na kuwaambia haoni kama wanaweza kumsaidia kwa sababu anataka kuona mtu wa kimataifa anayekuja awe zaidi ya wachezaji wetu,” alisema.

Wachezaji wanaoendelea kwenye majaribio ni makipa Daniel Yeboah (Ivory Coast) na Juan Jesus Gonzalez (Hispania), ambao wanawania nafasi moja ya usajili katika eneo la golikipa.

Jaffar alimalizia kwa kusema kuwa wanatarajia kuwapokea wachezaji wengine wa kimataifa ndani ya siku mbili au tatu zijazo kwa ajili ya majaribio yote ni katika kuendelea.

TFF YAPANIA KUBORESHA SOKA YA WANAWAKE



Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) limepania kutoa kipaumbele katika masuala ya waamuzi na wanawake kwa kuanzisha madawati ya kudumu katika Kurugenzi ya Ufundi.

Hapo awali madawati ya wanawake na waamuzi yaliendeshwa na watumishi wa kujitolea (Volunteers) au wa muda (Part timers).

Akizungumza na www.tff.or.tz, Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine aliamsha changamoto mbalimbali za soka la wanawake miongoni mwanzo ikiwa ni uibuaji na uendelezaji vipaji, Timu ya Taifa, mafunzo katika taaluma mbalimbali, ligi za wanawake na masoko kwa bidhaaa (products) za soka la wanawake.

Kuhusu waamuzi, Katibu Mkuu alilielezea eneo hili kama lenye changamoto nyingi hasa hasa katika kupata waamuzi na viwango vya Kimataifa.

Wakati huohuo, TFF inatarajia kuimarisha Kurugenzi yake ya masoko ambako sasa ataajiriwa Mkurugenzi wa masoko na habari.

Lengo hasa ni kuendana na hali halisi ya uendeshaji mpira duniani ambako masoko, habari na mahusiano ya Kimataifa yamekuwa funguo za kupata rasilimali kwa ajili ya maendeleo ya mchezo wa soka.

Lengo ni kuhakikisha rasilimali za kuendesha mpirwa a miguu zinatokana na mpira wa miguu na vilevile kuhakikisha wadau wanapata habari sahihi kwa wakati muafaka “ Alisema Mwesigwa Selestine”

Kwa nafasi za kazi katika TFF tembelea tovuti yao www.tff.or.tz au waandikie ili utumiwe tangazo kwa barua pepe tanfootball@tff.or.tz

TUZO ZA LIGI KUU KUTOLEWA JULAI 17



Hafla ya kukabidhi tuzo mbalimbali za washindi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa msimu wa 2015/2016 itafanyika Julai 17 mwaka huu.

Jumla ya tuzo 13 za Ligi hiyo inayodhaminiwa na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania zitatolewa katika hafla hiyo itakayofanyika jijini Dar es Salaam, na kuratibiwa na Kamati ya Tuzo ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Kamati hiyo inaundwa na waandishi wa habari za michezo, makocha, viongozi  (administrators) na wawakilishi kutoka kwa wadhamini (Vodacom na Azam Tv).

Tuzo hizo ni mabingwa, makamu bingwa, mshindi wa tatu, mshindi wa nne, timu yenye nidhamu, mfungaji bora, mchezaji bora wa Ligi, kipa bora, kocha bora, mchezaji bora chipukizi, mchezaji bora wa kigeni, goli bora la msimu na mwamuzi bora.

Waliopendekezwa (nominees) kuwania tuzo ya mchezaji bora wa Ligi ni Shiza Kichuya (Mtibwa Sugar), Juma Abdul (Yanga) na Mohamed Hussein (Simba) wakati kwa upande wa kipa bora ni Aishi Manula (Azam), Beno Kakolanya (Tanzania Prisons) na Deogratius Munishi (Yanga).

Kocha bora wapo Hans Van Pluijm (Yanga), Mecky Maxime (Mtibwa Sugar) na Salum Mayanga (Tanzania Prisons). Waliopendekezwa kuwania tuzo ya mchezaji bora chipukizi ni Farid Mussa (Azam), Mohamed Hussein (Simba), Mzamiru Yasin (Mtibwa Sugar) na Shiza Kichuya (Mtibwa Sugar).

Waliongia kwenye orodha ya tuzo ya mchezaji bora wa kigeni ni Donald Ngoma (Yanga), Thabani Kamusoko (Yanga) na Vincent Agban (Simba). Waamuzi bora katika kinyang'anyiro hicho ni Anthony Kayombo, Ngole Mwangole na Rajab Mrope.

Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu amewapongeza wateule wote waliopendekezwa kuwania tuzo hizo. "Kama wadhamini tuna matumaini makubwa kuwa  msisimko wa ligi hii utazidi kuongezeka katika msimu ujao na kuzidi kuwapatia mashabiki wa soka wanaoifuatilia hapa nchini na nje ya nchi."

Alisema Vodacom itaendelea kudhamini ligi hiyo kubwa ya soka nchini  ili kutekeleza moja ya malengo yao ya kuibua na kuendeleza vipaji vya wachezaji nchini. Pia kuwawezesha wachezaji kujipatia ajira na kuboresha maisha yao kupitia sekta ya michezo bila kusahau kuwapatia burudani wateja wake na Watanzania wote kwa ujumla.

Sunday, July 3, 2016

SERENGETI BOYS YAITANDIKA SHELISHELI MABAO 6-0


Na Alfred Lucas, VICTORIA
TIMU ya taifa ya vijana ya Tanzaia chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys imeshinda mabao 6-0 dhidi ya Shelisheli katika mchezo wa marudiano Raundi ya Kwanza kufuzu Fainali za U17 Afrika mwakani Madagascar jioni ya leo Uwanja wa Stade Linite mjini Victoria.
Kwa matokeo hayo, Serengeti Boys inasonga mbele Raundi ya Pili na hatua ya mwisho ya mchujo kwa ushindi wa jumla wa 9-0 baada ya wiki iliyopita kushinda 3-0 katika wa kwanza Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Serengeti Boys sasa itamenyana na Afrika Kusini, hayo yakiwa ni marudio ya mchezo wa mwaka jana katika hatua hiyo hiyo, ambayo vijana wa Tanzania walitolewa.
Serengeti Boys imesonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 9-0
Mabao ya Serengeti  yamefungwa na Shaaban Zubeiry dakika ya saBa, Mohammed Abdalah dakika ya 49, Hassan Juma mawili dakika ya 47 na 75, Issa Makamba kwa penalti dakika ya 65 na Yohana Nkomola dakika ya 90.

Friday, July 1, 2016

SIMBA YAMTAMBULISHA RASMI KOCHA WAKE MPYA, JOSEPH OMOG KUTOKA CAMEROON

RAIS wa Simba, Evans Aveva akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mkutano huo
KATIBU Mkuu wa Simba, Patrick Kalemela akizungumza
OMOG naye alipata nafasi ya kusema yake ya moyoni wakati wa mkutano huo

KLABU ya Simba jana ilimtambulisha rasmi kocha wake mpya, Joseph Omog kutoka Cameroon.

Omog, ambaye aliwahi kuifundisha Azam msimu uliopita kabla ya mkataba wake kukatishwa, ameingia mkataba wa kuifundisha Simba kwa miaka miwili.

Kocha huyo kutoka Cameroon, anachukua nafasi ya kocha wa zamani wa timu hiyo, Jackson Mayanja kutoka Uganda.

Akizungumza katika mkutano huo, Rais wa Simba, Evans Aveva alisema wameamua kumpa Omog mkataba wa mwaka mmoja kwa ajili ya majaribio. Alisema iwapo atafanya vizuri, wanaweza kumuongezea mkataba mwingine.

Kwa mujibu wa Aveva, kocha huyo amepewa nafasi ya kuchagua wasaidizi wake wa benchi la ufundi na kusisitiza kwamba, uongozi hautamuingilia.

Kwa upande wake, Omog alisema amefurahi kurudi tena Tanzania na kuahidi kufanya kila linalowezekana kuiletea Simba mafanikio.


SERENGETI BOYS KURUDIANA NA SHELISHELI KESHO, KOCHA SHIME ASEMA HATAFANYA MABADILIKO YA KIKOSI CHA KWANZA


Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’, Bakari Nyundo Shime, amesema hatarajii kuwa na mabadiliko makubwa ya kikosi katika mchezo dhidi ya vijana Shelisheli utakaopigwa kesho Jumamosi Julai 2, 2016 kwenye Uwanja wa Stade Linite mjini Victoria.

“Timu haitakuwa na mabadiliko makubwa. Almost kikosi kitakuwa ni kilekile cha Dar es Salaam kwa sababu nitampumzisha Job (Dickson Nickson) tu katika mchezo wa kesho, na nafasi yake atacheza Enrick (Vitalis Nkosi),” amesema Shime leo Julai 1, 2016 kabla ya kwenda kwenye mazoezi ya mwisho yatakayofanyika Uwanja wa Linite.

Shime maarufu kwa jina la Mchawi Mweusi, amesema anauchukulia mchezo huo kwa uzito uleule na kuongeza ana sababu za kiufundi na kimbinu kumpumzisha Job katika mchezo wa marudiano kuwania nafasi ya kufuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana, zitakazofanyika mwakani huko Madagascar.

 Kwa hali halisi ilivyo timu iko vema na ikathibitishwa na Shime mwenyewe akisema: “Kikosi kiko vema kwa maana ya wachezaji wako vizuri na kambi iko vizuri kwa sababu hakuna majeruhi.” Pia Daktari wa timu hiyo, Shecky Francis Mngazija alithibitisha.

“Sioni kama kuna dalili zozote za hujuma na kimbinu tumejipanga vema. Tumefuta matokeo ya Dar na tuko huku tunataka matokeo mapya. Mbinu zangu siku zote ni ushindi wa nyumbani na ugenini,” amesisitiza.

Serengeti Boys ilitua kwenye Kisiwa cha Mahe uliko Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Visiwa vya Shelisheli jana Juni 30, 2016 majira ya saa 11 jioni.

Timu hiyo iliyosafiri kwa ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia ilisafiri salama na wachezaji wote 20 wakiwa na viongozi wanane, walikuwa kwenye hali nzuri na kupokewa vema na wenyeji waliowaandalia usafiri kutoka uwanjani hapo hadi Victoria- Mji Mkuu wa nchi hii na kufikia Hoteli ya Berjaya Beau Vallon Resort iliko Kilometa 25 kutoka uwanja wa ndege.

Leo Julai mosi, itakuwa na mazoezi ya kipindi kimoja tu kwenye uwanja huo kuanzia saa 10.30 jioni (saa 9.30 kwa saa za Tanzania au Afrika Mashariki). Uwanja wa Stad Linite upo kilometa 10 kutoka hotelini.

Shime ana matumaini makubwa kuiondoa Shelisheli katika mbio hizo baada ya kuvuna ushindi mnono wa mabao 3-0 katika mchezo wa kwanza uliofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Jumapili ya Juni 26, 2016.

Na ili iweze kufuzu, Serengeti Boys inahitaji kusimama imara katika matokeo hayo ama kwa kupata sare ya aina yoyote, kushinda au ikitokea kupoteza, basi isifungwe zaidi ya mabao 2-0.

Katika mchezo wa Dar es Salaam waliozifumania nyavu walikuwa Nickson Kibabage, Ibrahim Abdallah na Ally Hussein ambaye alifunga kwa penalti na kila mmoja amepania kufunga kama kocha akiwapa nafasi ya kuanza katika kikosi cha kwanza.

Nyota waliosafiri ni pamoja na makipa, Ramadhani Awm Kabwili na Samwel Edward Brazio wakati mabeki wako Kibwana Ally Shomari, Nickson Clement Kibabage, Israel Patrick Mwenda, Dickson Nickson Job, Ally Hussein Msengi, Issa Abdi Makamba.

Viungo ni Kelvin Nashon Naftal, Ally Hamisi Ng’anzi, Asadi Ali Juma Ali, Syprian Benedictor Mtesigwa, Ibrahim Abdallah Ali, Yassin Muhidini Mohamed, Shaban Zuberi Ada huku washambuliaji wakiwa ni Rashid Mohammed Chambo, Mohammed Abdallah Rashid, Yohana Oscar Mkomola, Muhsin Malima, Makame Vitalis.

Serengeti Boys ambayo inahudumiwa na TFF kwa asilimia 100 ilikuwa kambini tangu Juni 14, 2016 kujiandaa na mechi hizo za kufuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika dhidi ya Shelisheli na Afrika Kusini ambayo itapambana nayo baadaye mwezi ujao.

Katika kuajindaa na mchezo huo, Serengeti Boys ilifanya ziara India ambako walishiriki mashindano ya vijana ya Kimataifa yanayotambuliwa na FIFA (AIFF International Youth Tournament 2016) kabla ya kurudi na rekodi ya kupigiwa mfano si tu katika Tanzania na kwa nchi za Afrika Mashariki. Ilishika nafasi ya tutu nyuma ya Korea Kusini na Marekani.

KAMATI YA MAADILIN YA TFF KUMWEKA KIKAANGONI JERRY MURO WA YANGA KESHO



Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)  inatarajiwa kuwa na kikao chake Jumamosi Julai 2, 2016 kwenye ukumbi wa ofisi za TFF zilizoko kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, makutano ya barabara za Shaurimoyo na Uhuru, Ilala jijini Dar es Salaam.

Viongozi watatu kutoka wanachama wa TFF wanahitajika kufika kwenye kikao hicho kinachotarajiwa kuanza saa 4.30 asubuhi.

Viongozi hao ni Jerry Muro - Msemaji wa Young Africans S.C
Nassib Mabrouk - Katibu wa MZFA na Msimamizi msaidizi wa kituo cha Mwanza
Mbasha Matutu - Mjumbe wa mkutano mkuu Mkoa wa Shinyanga.