KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, July 16, 2016

MALINZI AWAPONGEZA NDULANE NA KUULI KWA KUTEULIWA KUWA WAKURUGENZI WA WILAYA


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amewapongeza Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa TFF, Wakili Revocatus Kuuli na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Lindi, Francis Ndulane.

Kuuli, Wakili msomi aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Rufani ya Nidhamu ya TFF, ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Igunga mkoani Tabora.

Kadhalika, katika uteuzi huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli amemteua Ndulane ambaye ni Mjumbe Mkutano Mkuu wa TFF kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara mkoani Morogoro.

Katika salamu hizo, Rais Malinzi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli kwa kuwateua viongozi hao wa TFF, akisema kwamba ameonyesha namna alivyo na imani na watendaji hao katika shughuli zao mbalimbali ikiwamo TFF.

No comments:

Post a Comment