KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, July 16, 2016

WAAMUZI LIGI MBALIMBALI WAANZA KUJIPANGA


Kamati ya Waamuzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, imeandaa kozi mbalimbali ikiwa ni maandalizi ya kwa waamuzi katika michuano ya kimataifa sambamba na Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Ligi Daraja la Kwanza ya StarTimes (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL) kwa msimu wa 2016/2017.

Kozi hiyo MA (Members Associations) itaanza kwa waamuzi wenye Beji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kimataifa (FIFA) ambao kwa sasa wako 18 hapa Tanzania na wengine 12 wa ‘Elite’ ikiwa na maana ya waamuzi wanaotarajiwa kuveshwa Beji za FIFA. Darasa la waamuzi hao litakuwa na waamuzi 30.

Waamuzi hao wenye Beji ya FIFA na wale wanaotarajiwa kuveshwa beji hiyo, wanatakiwa kuripoti Dar es Salaam Julai 23, 2016 ambako kwa mujibu wa ratiba wataanza program ya kozi hiyo kwa kupima kasi ya kukimbia siku inayofuata Julai 24, 2016 wakisimamiwa na wakufunzi kutoka FIFA.

Mara baada ya programu hiyo, kozi itaendelea kwa waamuzi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Ligi Daraja la Kwanza ya StarTimes (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL) na makamishna wa michezo kwa msimu wa 2016/2017 na kwamba wahusika wote watajigharamia gharama zote.

Waamuzi hao wa ligi ya ndani wataripoti na kujisajili Kituo cha Dar es Salaam Julai 29 na siku inayofuata Julai 30, 2016 na Julai 31, 2016 watakuwa na kozi ya kitathmini kasi kwa kukimbia kabla ya Agosti 1 na 2, 2016 kuwa na semina darasani na mitihani wakati Agosti 3, 2016 kutakuwa na semina na mitihani kwa makamishna mbalimbali wa michezo ya mpira wa miguu.

No comments:

Post a Comment