KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, July 21, 2016

PEPSI YAPANDA DARAJA LA PILI KWA KLABU YA 2016/2017


Shirkisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linapenda kutoa pongezi zake za dhati kwa Klabu ya Pepsi FC ya Arusha kwa kupata nafasi ya kupanda daraja na kuingia Daraja la Pili SDL msimu wa 2016/2017.

Hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 5 kipengere cha (5) ya mashindano ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa RCL msimu wa 2015/2016.

Timu imefanikiwa kupata nafasi ya pili katika msimamo wa ligi ya mabingwa wa Mikoa 2015/2016 kituo cha Singida na kuongoza kati ya timu zilizoshika nafasi ya pili katika vituo vilivyosalia ambavyo ni Njombe, Morogoro na Muleba. TFF inaItakia kila la kheri katika maandalizi ya kushiriki Daraja la Pili msimu wa 2016/2017

No comments:

Post a Comment