KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, July 1, 2016

KAMATI YA MAADILIN YA TFF KUMWEKA KIKAANGONI JERRY MURO WA YANGA KESHO



Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)  inatarajiwa kuwa na kikao chake Jumamosi Julai 2, 2016 kwenye ukumbi wa ofisi za TFF zilizoko kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, makutano ya barabara za Shaurimoyo na Uhuru, Ilala jijini Dar es Salaam.

Viongozi watatu kutoka wanachama wa TFF wanahitajika kufika kwenye kikao hicho kinachotarajiwa kuanza saa 4.30 asubuhi.

Viongozi hao ni Jerry Muro - Msemaji wa Young Africans S.C
Nassib Mabrouk - Katibu wa MZFA na Msimamizi msaidizi wa kituo cha Mwanza
Mbasha Matutu - Mjumbe wa mkutano mkuu Mkoa wa Shinyanga.

No comments:

Post a Comment