KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, December 11, 2017

PAPII KOCHA AANGUA KILIO BAADA YA KUPATA TAARIFA ZA KUACHIWA HURU



MWANAMUZIKI Johnson Nguza (Papii Kocha), jana, aliangua kilio cha furaha, baada ya kupata taarifa za kuachiwa huru kutokana na agizo la Rais Dk. John Magufuli.
Papii na baba yake, Nguza Vicking (Babu Seya), ni miongoni mwa wafungwa walionufaika na msamaha wa Rais Magufuli, alioutangaza jana, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 56 ya uhuru wa Tanzania Bara.
Rais Magufuli alitangaza kutoa msamaha kwa wafungwa 61, waliohukumiwa adhabu ya kifo na kuwaachilia huru Babu Seya na mwanawe, Papii Kocha.
Wanamuziki hao walihukumiwa kifungo cha maisha gerezani na Mahakama Kuu, mwaka 2004, baada ya kupatikana na hatia ya kubaka na kulawiti wasichana 10, wa shule ya Msingi Mashujaa, iliyoko wilayani Kinondoni, Dar es Salaam.
Hukumu hiyo ilizua hisia tofauti miongoni mwa Watanzania huku idadi kubwa ya wananchi wakiamini kuwa, wanamuziki hao hawakuhusika na tukio hilo.
Kufuatia kupewa hukumu hiyo, wanamuziki hao waliamua kukata rufani, lakini Novemba 21, mwaka 2013, Mahakama ya Rufaa ilitupilia mbali ombi lao la kuitaka ifanye marejeo ya uamuzi wake wa awali wa kuwapata na hatia, kama ambavyo hukumu dhidi yao ilivyotolewa.
Mahakama hiyo baada ya kufanya mapitio, ikiwa imeketi chini ya majaji watatu, iliamua warufani hao wawili wana hatia, hivyo waendelee kutumikia adhabu yao.
Akitumia Ibara ya 45 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inayotoa mamlaka kwa Rais kutoa msamaha kwa wafungwa, Rais Dk. Magufuli alitangaza kutoa msamaha kwa Babu Seya na mwanaye, kwenye sherehe za miaka 56 ya uhuru wa Tanzania Bara, zilizofanyika katika Uwanja wa Jamhuri mjini hapa.
“Sisi sote ni binadamu na hata mimi huwa namuomba Mungu anisamehe, ingawa sisi wanadamu ni wagumu kusamehe. Hivyo natangaza msamaha kwa familia ya Nguza Viking, maarufu kama Babu Seya na watoke leo,” alisisitiza Rais Magufuli huku akishangiliwa na umati wa watu waliohudhuria sherehe hizo.
Kuhusu wafungwa 61, waliohukumiwa adhabu ya kifo, Rais Magufuli alitangaza kuwasamehe kutokana na kukaa gerezani kwa miaka mingi.
Alisema baada ya kufanyika uchunguzi, imegundulika wafungwa hao wamejutia makosa yao kwa kiasi kikubwa na wamejirekebisha.
“Yupo mtu alifungwa akiwa na miaka 18. Sasa ana umri wa miaka 60, akiwa gerezani. Mwingine Mganga Matonya mwenye umri wa miaka 87, ambaye amekaa gerezani kwa miaka 44.
“Nitamkabidhi Waziri Mkuu orodha ya wafungwa wote ili ahakikishe utaratibu unafanyika wa kuachiwa huru leo au kesho. Na hii document (nyaraka) naisaini hapa hapa. Lisiongezwe jina lingine au kupunguzwa,” alibainisha.
Alisema wafungwa hao 61, hawakuua watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) wala kuhusika na vitendo vya ujambazi, lakini alisisitiza serikali kuendelea kusimamia sheria kwani uwepo wa ibara hiyo ya kikatiba haina maana sheria haitofuata mkondo.
Rais alitaja idadi ya wafungwa waliosamehewa, kwenye gereza la Uyui (2), Butimba (5), Ukonga (19), Isanga (15), Maweni (11) Kinguwila (5) na gereza la Ruanda wapo wafungwa wanne.
Vilevile, Rais Magufuli alitoa msamaha kwa wafungwa 8,157, ambao kati yao, 1,828 walitakiwa kutoka tangu jana na wengine 6,329, walipunguziwa muda wa kukaa gerezani.
Jijini Dar es Salaam, mwanamuziki Papii alipata taarifa za kuachiwa kwao huru wakati akiwa anashiriki kucheza mechi ya soka ya wafungwa wanaozishabikia Simba na Yanga, kwenye gereza la Ukonga.
Wakati wafungwa wengine wakishiriki katika mechi hiyo, baadhi yao walikuwa wakitazama moja kwa moja matangazo ya maadhimisho ya miaka 56 ya uhuru kupitia kwenye runinga iliyokuwepo ndani ya gereza hilo.
Wakati Rais Magufuli akitangaza kuwaachia huru Nguza na Papii, wafungwa waliokuwa wakifuatilia matangazo hayo walilipuka mayowe ya kushangilia na kukimbilia uwanjani, ambako walianza kumkimbiza Papii na hatimaye kumzingira.
Mmoja wa wanamuziki wakongwe nchini, King Kikii, alisimulia mkasa huo jana, kwa waandishi wa Mzalendo, baada ya kwenda kuwatembelea Babu Seya na Papii kwenye gereza la Ukonga.
Kikii alisema alifika kwenye gereza hilo baada ya kumsikia Rais Magufuli akitangaza msamaha huo kwa Babu Seya na Papii, kupitia kwenye runinga, akiwa nyumbani kwake, Ubungo, Dar es Salaam.
“Kwanza namshukuru sana Rais Magufuli. Uamuzi alioufanya ni wa kihistoria. Nimefurahi sana. Siwezi kusema lolote kwa sasa, isipokuwa  namshukuru Mungu na rais wetu. Mdogo wangu na mwanawe wamekaa gerezani kwa miaka 10 na sasa wako huru,” alisema.
Akisimulia jinsi Babu Seya na Papii walivyopokea taarifa hizo, Kikii alisema Papii ndiye aliyeonekana kuwa na furaha kubwa, kutokana na kuzunguka gereza zima, akiwaaga wenzake kwa furaha.
“Papii anasema alipita kila chumba kuwaaga wenzake huku akiwashukuru kwa ushirikiano wao kwa muda wote waliokuwa pamoja gerezani,” alisema Kikii.
Aliongeza kuwa, kitendo cha wafungwa wenzake kumkimbiza na kumzingira, kilimshtua hivyo alilazimika kuwahoji kulikoni, ndipo wakamjulisha kwamba, yeye na baba yake wameachiwa huru na Rais Magufuli.
“Kuanzia hapo Papii anasema alikuwa kama amepagawa kwa furaha. Mwanzoni aliangua kilio kwa kuwa hakuamini, lakini baadaye alianza kufurahia kwa kuzunguka gereza lote akishangilia na kuwaaga wenzake,”alisema.
Akimzungumzia Babu Seya, alisema baada ya kupokea taarifa hizo, hakuwa na mengi ya kusema zaidi ya kumshukuru Mungu na Rais Magufuli kwa uamuzi wake huo.
“Nguza (Babu Seya) alikuwa akifuatilia matangazo hayo na wenzake gerezani, lakini hakuwa akitarajia kitu kama hicho kutokea. Alichosema ni kwamba, anamshukuru Mungu na Rais Magufuli kwa kuwaonea huruma,”alisema.
Mmoja wa askari wa Magereza, aliyekuwepo kazini kwenye gereza la Ukonga, jana, alisema licha ya Rais Magufuli kutoa agizo hilo, isingewezekana kwa Babu Seya na mwanawe kutolewa siku hiyo kwa kuwa kuna taratibu za kisheria, zinazopaswa kukamilishwa.
“Ni kweli mheshimiwa rais ametoa agizo hilo, lakini kwa jinsi ninavyofahamu, kuna taratibu ambazo lazima zifuatwe kabla ya kuwaachia huru. Inawezekana wakaachiwa kesho (leo),” alisema askari huyo, ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini.
Mapema wakati akitoa takwimu za idadi ya wafungwa waliopo magerezani, Rais Magufuli alisema hadi juzi, kulikuwa na wafungwa 39,000, kati yao wafungwa 37,000, ni wanaume na wanawake ni 2,000.
Dk. Magufuli alieleza kuwa wafungwa waliohukumiwa kunyongwa ni 522, kati yao wanaume 503 na wanawake 19.
Alisema wafungwa waliohukumiwa kifungo cha maisha ni 666, kati yao wanaume 655 na wanawake 11.
“Kwa maana hiyo wafungwa wengi waliopo magerezani ni wanaume, hivyo tuanze kujitambua ni kwanini wanaume wanaongoza kwenye vitendo vya uhalifu,”alisema.

Sunday, November 12, 2017

UWANJA WA TAIFA RUKSA KUTUMIKA NOVEMBA 21


Matengenezo Uwanja Mkuu wa Taifa, Dar es Salaam, umekamilika na Mheshimiwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison George Mwakyembe, ameambiwa kuwa unaweza kuanza kutumika kuanzia Novemba 21, mwaka huu.

Kwa msingi, Waziri Dk. Mwakyembe ametoa maagizo ya kuandaliwa mchezo maalumu wikiendi ya Novemba 24, 25 au 26 kupata mchezo mmoja wa ufunguzi wa uwanja huo wenye uwezo wa kubeba takribani mashabiki walioketi 60,000 kwa wakati mmoja.

Akipokea ripoti hiyo kutoka kwa Alex – Mtaalamu kutoka Uingereza, Mheshimiwa Waziri Dk. Mwakyembe amesema: “Tuna changamoto kwenye matunzo na matengenezo. Sasa ili kukabiliana na changamoto hii, hatuna budi vijana sita waliofundishwa kazi na mtaalamu huyu, wakafanyiwa mpango wa ajira. Vijana hao wavumilie kwa sasa”

Mtaalamu huyo wa Uingereza, amesema kwamba wakati uwanja unatumika, ukarabati wa mara kwa mara utakuwa ukiendelea ili kuifanya hazina hiyo ya taifa kuendelea kuboreka  kwa wakati wote.

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia akizungumzia uboreshaji huo, alisema: “Ni vema wataalamu hao wakatumike pia kwenye viwanja vya mikoani. Huko wataviboresha na kuwafundisha wengine.”

DK. MWAKYEMBE ATEUA KAMATI YA AFCON U17 2019


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison George Mwakyembe leo Jumamosi Novemba 11, amezindua Kamati ya Maandalizi ya Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 (AFCON U17) yakayofanyika Machi, 2019.

“Kama unavyofahamu, Tanzania ilipokea heshima ya kuandaa mashindano ya AFCON 2019 kwa vijana chini ya miaka 17 baada ya mashindano kama hayo kufanyika Libreville, Gabon mwezi Mei, mwaka huu.

“Ili kufanikisha maandalizi ya mashindano hayo ya Afrika nimezindua Kamati ya Maandalizi inayojumuisha viongozi wa Serikali na wadau mbalimbali wa Michezo kwa kuzingatia kanuni za Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).

Kabla ya kuzindua kamati hiyo, Mhe. Waziri Mwakyembe alisema: “2019 tuna mtihani. Mtihani mkubwa. Na lazima tuufaulu. Tuna ugeni mkubwa ambao kamati itakuwa na kazi ya kufanya maandalizi haya kwa kazi ya kujitolea. Walioteuliwa ni watu wote wana rekodi na uzoefu mzuri kwenye masuala ya michezo.”

Uzinduzi wa kamati hiyo ulifanyika Ukumbi wa Watu Maalumu (VIP) katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam ambako Mhe. Waziri Dk. Mwakyembe alikubali kuwa Mwenyekiti wa Kamati huku Makamu Mwenyekiti wake akiwa ni Rais wa Heshima wa TFF, Leodegar Chilla Tenga ilihali Mtendaji Mkuu atakuwa Dk. Henry Tandau.

Wajumbe ni Makamu Rais wa TFF, Michael Wambura na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda; Dk. Damas Ndumbaro ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Rufaa za Leseni za Klabu ya TFF; Dk. Francis Michael wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam – Kitivo cha Sheria; Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Mohammed Enterprises, Mohammed Dewji na Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Said Salim Bakhressa, Abubakar Bakhressa.

Pia wamo Yussuph Singo Omari – Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo; Ahmed Msafiri Mgoyi – Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya TFF; Khalid Abdallah – Mwenyekiti Kamati ya Maendeleo ya Vijana ya TFF kadhalika Dk. Hamis Kigwangalla – Waziri wa Maliasili na Utalii.

Wajumbe wengine ni Nassib Mmbagga – Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke; Dar es Salaam; Angetile Osiah Mhariri Mwandamizi wa Magazeti ya Kampuni ya Mwananchi Communications; Dk. Allain Kijazi – Mkurugenzi Mkuu TANAPA; Dk. Dotto James – Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango; Dk. A. P. Makakala – Kamishna Jenerali Idara ya Uhamiaji; Dk. Fredy Manongi – Mkurugenzi Mkuu Hifadhi ya Ngorongoro.

Wamo pia Lameck Nyambaya – Mjumbe Kamati ya Utendaji ya TFF; Mkurugenzi Mkuu wa PPF, William Erio; Kelvin Twissa – Ofisa Masoko Mkuu Sportpesa; Profesa Lawrence Museru – Mkurugenzi Mkuu Hospitali ya Taifa ya Muhimbili; Injinia Ladislaus Matindi – Mkurugenzi Mtendaji ATCL na Devotha Mdachi – Mkurugenzi Bodi ya Utalii Tanzania.

Pamoja na Wajumbe hao, wengine wanaoingia kwenye kwa nafasi zao katika Kamati hiyo ya maandalizi ni Rais wa TFF na Katibu Mkuu wa TFF

CHIRWA MCHEZAJI BORA WA MWEZI LIGI KUU


Mshambuliaji wa Young Africans ya Dar es Salaam, Obrey Chirwa amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Oktoba wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu wa 2017/2018.

Chirwa raia wa Zambia alitwaa tuzo hiyo baada ya kuwashinda wenzake wawili, beki Erasto Nyoni wa Simba na mshambuliaji Ibrahim Ajibu pia wa Young Africans alioingia nao fainali katika uchambuzi uliofanywa na Kamati ya Tuzo za VPL zinazotolewa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kutokana na mapendekezo kutoka kwa makocha waliopo viwanja mbalimbali ambavyo ligi hiyo inachezwa msimu huu.

Mshambuliaji huyo alitoa mchango mkubwa kwa Young Africans mwezi huo ikipata pointi saba katika michezo mitatu iliyocheza na kupanda katika msimamo wa ligi kutoka nafasi ya sita iliyokuwepo mwezi Septemba hadi ya pili mwishoni mwa Oktoba.

Young Africans iliifunga Kagera Sugar mabao 2-1 Uwanja wa Kaitaba, Bukoba,  ambapo Chirwa alifunga bao moja na kutoa pasi ya mwisho ya bao moja, pia Yanga iliifunga Stand United mabao 4-0 Uwanja wa Kambarage, Shinyanga, ambapo Chirwa alifunga bao moja na kutoa pasi ya mwisho ya bao moja.

Kiwango cha mchezaji huyo kilionekana pia katika mchezo wa watani wa jadi Yanga na Simba uliofanyika Oktoba 28, 2017 Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam na kumalizika kwa sare ya bao 1-1. Bao la Yanga lilifungwa na Chirwa, hivyo kwa mwezi huo alifanikiwa kuwa na kiwango cha juu katika kila mchezo ikiwa ni pamoja na kufunga.

Kwa upande wa Erasto naye alitoa mchango mkubwa kwa Simba uliowezesha timu hiyo kupata pointi nane katika michezo minne iliyocheza, akitoa pasi za mwisho za mabao nne, ambapo Simba ilishinda michezo miwili na kutoka sare miwili, huku Ajibu akitoa mchango mkubwa kwa Yanga ikiwa ni pamoja na kufunga mabao matatu na kutoa pasi ya mwisho ya bao moja.

Wachezaji wengine ambao tayari wameshinda Tuzo ya Mchezaji Bora wa mwezi wa VPL msimu huu ni mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi (Agosti), beki wa Singida United, Shafiq Batambuze (Septemba).

Kampuni ya Vodacom, ambao ndiyo wadhamini wa ligi hiyo ina utaratibu wa kuwazadiwa wachezaji bora wa kila mwezi, huku pia mwisho wa msimu kukiwa na tuzo mbalimbali zinazohusu ligi hiyo, ambapo msimu wa mwaka 2016/2017 kulikuwa tuzo 16 zilitolewa kwa washindi wa kada mbalimbali. Chirwa atazawadiwa Sh milioni moja kwa kuibuka Mchezaji Bora wa Oktoba.

TFF YAENDESHA MAFUNZO VYUONI SOKA YA UFUKWENI


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litatoa mafunzo ya soka la ufukweni (Beach Soccer) kwa vyuo mbalimbali hapa nchini vilivyothibitisha kushiriki Ligi Maalumu ya soka la Ufukweni itakayoanza Novemba 18, 2017.

Kwa upande wa mafunzo ni kwamba yatafanyia siku tano kabla ya kuanza kwa ligi hiyo ambako itakuwa ni Novemba 13, mwaka hu. TFF imepanga kutoa mafunzo hayo kwa vyuo hivyo ili wauelewe zaidi mchezo huo pamoja na sheria zake.

Tumepeleka mchezo huo kwenye vyuo ili kutoa hamasa ya soka la ufukweni kuenea zaidi na kuweka hazina ya wachezaji wa timu ya taifa.

Mpaka sasa vyuo 14 tayari vimethibitisha kimaandishi kushiriki kwenye mafunzo hayo.

Vyuo vilivyothibitisha kushiriki ni Chuo cha Ardhi, Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Chuo Cha Ufundi (DIT), Chuo cha Usafirishaji (NIT), Chuo cha Elimu ya Tiba cha Kahiruki, Chuo cha Elimu ya Biashara cha Lisbon, Chuo cha Silva , Chuo UAUT, TIA, El-Maktoum collage Engineering, Magogoni, Chuo cha uandishi wa habari DSJ na TSJ.

Mafunzo hayo yatatanguliwa na tukio la kukutana na viongozi wa vyuo shiriki hapo Novemba 10, 2017.

Wakati huo huo kozi ya waamuzi wa Soka la Soka la Ufukweni imeanza leo Novemba 7, 2017 katika Makao Makuu ya TFF Karume, Dar es Salaam ambayo yanatarajiwa kumalizika Novemba 12, 2017.

TFF YASIMAMISHA MCHEZO WA FORODHANI v AMBASSODOR

Wakati mchezo wa TFF ikisimamisha mchezo wa Azam Sports Federation Cup kati ya Forodhani FC ya Mara na Ambassodor ya Kahama, Mchezo wa Bulyanhulu na Area C, sasa utafanyika kesho Jumatano Novemba 8, mwaka huu kwenye Uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga.

Mchezo kati ya Forodhani FC ya Mara na Ambassodor ya Kahama, umesimamishwa kusubiri uamuzi wa Kamati ya Mashindano baada ya Baruti ambayo imelete malalamiko kuhusu nafasi yake.

Mbali ya mchezo kati ya Bulyanhulu na Area C, mechi nyingine za kesho Jumatano, Novemba 8 zitakuwa ni kati ya Cosmopolitan na Abajalo kwenye Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani wakati makumba Rangers watacheza na Green Warriors kwenye Uwanja wa Bandari, Dar es Salaam.

AFC ya Arusha itaikaribisha Nyanza FC kwenye Uwanja wa Ushirika; Boma Fc na African Sports watacheza kwenye Uwanja wa Ushirika; huku Motochini ikicheza na Ihefu wakati Stand Misuna watacheza na Madini ilihali Burkina FC itaialika Mbinga United kadhalika Mkamba Rangers itacheza na Makambako FC kwenye Uwanja wa Sabasaba.

35 WATEULIWA KUUNDA KILIMANJARO WARRIORS


Benchi la Ufundi la timu za taifa za vijana, limeita wachezaji 35 kwa ajili ya kambi yenye lengo la mchujo kutafuta kikosi imara cha timu ya taifa ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 23 maarufu kwa jina la Kilimanjaro Warriors.

Kocha Msaidizi wa timu hizo, Oscar Mirambo alitangaza majina hayo leo Novemba 03, mwaka huu huku amesema: “Tunataka vijana wasiozidi 25 kwenye kikosi. Tutawapata kwenye kambi hii ya siku 10 inayoanza tarehe 5, mwezi huu wa 11.”

Kocha Msaidizi wa timu hizo, Oscar Mirambo alitangaza majina hayo leo Novemba 03, mwaka huu huku akisema: “Tunataka vijana wasiozidi 25 kwenye kikosi. Tutawapata kwenye kambi hii ya siku 10 inayoanza tarehe 5, mwezi huu wa 11.”

Wachezaji aliowaita ni makipa Metacha Mnata (Azam FC), Joseph Ilunda (JKT Ruvu), Liza Mwafwea (Tanzania Prisons).

Wengine ni Cleotas Sospter (Yanga); Idrissa Mohammed, Bakari Kijuji (Yanga), Joseph Prosper (Azam), Masoud Abdallah (Azam), William (Ruvu Shooting), Yussuph Mhilu (Yanga), Adam Salamba (Stand United), Omary Mponda (Ndanda) na Stanley Angeso (Stand United).

Pia wamo Eliud Ambokire (Mbeya City), Emmanuel Kakuti (Mbeya City), Medson Mwakatunde (Mbeya City), Daruweshi Shaliboko (Ashanti Unted), Abbas Kapombe (Azam/Ndanda), Ismail Aidan (Mtibwa Sugar), Salum Kihimbwa (Mtibwa Sugar), Hassan Mganga (Mtibwa Sugar) na Award Salum (Njombe Mji).

Wengine Awesu Ally (Mwadui), Salum Chuku (Singida United), Yahya Zayd (Azam), Emmanuel Martin (Yanga), Geofrey Mwashiuya (Yanga), Ayoub Masoud (Ndanda), Baraka Majogoro (Ndanda), Mohammed Habib (Miembeni), Yussuf Mlipili (Simba), Agathon Mapunda (Njombe Mji), Faisal Abdallah (JKU) na Yussuph Kagoma (Singida United).

TFF YATOA UFAFANUZI WA MALIPO MICHUANO YA ASFC


Wakati Michuano ya Kombe la Shirikisho la Azam yaani Azam Sports Federation Cup (ASFC), ikiwa imeanza jana Novemba 02, 2017 na kuendelea leo Ijumaa na kesho Jumamosi, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetoa ufafanuzi wa malipo kwa hatua hii ya awali.

Kwa hatua za awali na hatua ya kwanza, TFF imetoa ufafanuzi kwamba kwa timu mwenyeji inalipwa shilingi lakini saba na elfu hamsini (Sh. 750,000) wakati timu ngeni inayosafiri hadi kituo cha mchezo inalipwa shilingi milioni mbili na lakini tano (Sh 2.5m). Fedha zote hizo, zinalipwa katika akaunti ya kila timu.

Lakini TFF imetoa ufafanuzi kwamba, kwa timu ambazo zinatoka katika kituo kimoja (mkoa mmoja) zote zitalipwa Sh 750,000 kama gharama sawa licha ya moja ya timu itakuwa mgeni na nyingine mwenyeji.

TFF imetoa ufafanuzi huo, baada ya kuibuka mjadala wa dhana ya uenyeji na ugeni licha ya kwamba timu shindani zinatoka kituo kimoja (mkoa mmoja). Timu hizo zielewe kwamba zitalipwa gharama inayofanana katika maandalizi.

Fedha zitaongezeka kwa timu ambayo inasonga mbele baada ya hatua ya awali na hatua ya kwanza.

Katika hatua nyingine, TFF inasubiri taarifa za Kamishna na Mwamuzi kuhusu vurugu zinazodaiwa kutokea huko Simiyu katika mchezo kati ya Usalama na Sahare All Stars uliofanyika Novemba 2, mwaka huu.

TFF imepanga mchezo kati ya Kisarawe United ya Pwani na Silabu ya Mtwara ufanyike kesho Novemba 4, mwkaa huu baada ya kuahirishwa Novemba 2, mwaka huu baada ya wachezaji wake kupata ajali  maeneo ya Mchinga mkoani Lindi wakiwa safarini kwenda Pwani. Mechi inayofanyika leo Novemba 3, mwaka huu kati ya Buseresere ya Geita itayocheza na Isako ya Songwe.

Baada ya mechi hizo,itakuja Raundi ya Kwanza ya ASFC ambayo itachezwa ama Novemba 7, 8 au 9 ambako TFF imepanga kesho kutuma fedha zote za maandalizi ya timu husika ili kusiwe na kisingizio chochote cha kujiandaa.

Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Kidao Wilfred ameagiza Idara ya Fedha na Utawala ya TFF kulipa fedha kwa timu hizo haraka, lakini kwenye akaunti ya timu husika badala ya mwakilishi ye yote au kiongozi.

Timu ambayo haijafungua akaunti watakuta fedha hizo kwenye Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa (FA), lakini TFF ingependa kusisitiza kwa wadau hao kufufua akaunti au kufungua akaunti haraka.

Katika raundi hiyo ya kwanza Mashujaa ya Kigoma itacheza na Mshindi kati ya Buseresere ya Geita na Isako ya Songwe; wakati mechi nyingine zitakuwa Msange ya Tabora itacheza na Milambo pia ya Tabora ilihali Bulyanhulu ya Shinyanga itacheza na Area C ya Dodoma.

Kwa mujibu wa droo, Mji Mkuu FC ya Dodoma imeangukia kwa Nyundo ya Kigoma wakati Baruti FC ya Mara itacheza na Ambassodor ya Kahama, Shinyanga huku Eleven Stars ya Kagera ikipangwa kucheza na Ndovu ya Mwanza.

Changanyikeni ya Dar es Salaam itacheza na Reha FC pia ya Dar es Salaam wakati Mshindi kati ya Kisarawe United na Silabu ya Mtwara atacheza na Kariakoo ya Lindi huku Cosmopolitan ikicheza na Ajabalo wakati Makumba FC itapambana na Green Warriors ya Kinondoni wakati Namungo FC ya Lindi itachuana na Villa Squad ya Dar es Salaam huku Dar City ikicheza na Majimaji Rangers ua Nachingwea.

Michezo mingine ya hatua ya kwanza itakutanisha timu za Shupavu FC ya Morogoro na Sabasaba pia ya mjini humo wakati Motochini FC ya Katavi dhidi ya Ihefu FC ya Mbeya wakati The Mighty Elephant ya itacheza na Makanyagio ya Rukwa.

Timu ya Burkina FC ya Morogoro itacheza na Mbinga United ya Ruvuma wakati Makambako Heroes ya Njombe  itacheza na Mkamba Rangers ya Morogoro wakati Real Moja Moja itapambana na African Wonderers – zote za Iringa. Boma FC ya Mbeya itacheza na African Sports ya Tanga.

Mechi nyingine za hatua hiyo itakuwa ni kati ya Pepsi ya Arusha ambayo itacheza na Kilimanjaro Heroes ya Kilimanjaro; huku Stand Misuna ya Singida itacheza na Madini FC ya Arusha ilihali AFC ya Arusha itacheza na Nyanza ya Manyara wakati New Generation itacheza na Mshindi kati ya Usamala FC na Sahale ya Tanga. Bodaboda FC itacheza na Kitayose ya Kilimanjaro.

Michuano hiyo ambayo Bingwa Mtetezi ni Simba SC ya Dar es Salaam, inashirikisha timu 91 msimu huu kwa mchanganuo wa timu 16 za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL); 24 za Ligi Daraja la Kwanza (FDL); 24 za Ligi Daraja la Pili (SDL) na 27 za Ligi ya Mabingwa wa Mkoa (RCL).

LIGI YA WANAWAKE KUANZA NOVEMBA 26


Ratiba ya Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara inayotarajiwa kuanza Novemba 26, 2017, katika vituo viwili vya majiji ya Dar es Salaam na Arusha, imetangazwa.

Katika ratiba hiyo, Kundi A limepangwa kuwa katika Kituo cha Dar es Salaam ambako timu zake Simba Queens ya jijini Dar es Salaam iliyopanda daraja msimu huu, Mburahati Queens, JKT Queens, Evergreen zote za Dar es Salaam pamoja na timu za Fair Play ya Tanga na mabingwa watetezi – Mlandizi Queens.

Kundi B litakuwa na timu za Alliance ya Mwanza ambayo imepanda kutoka kituo cha Dodoma. Timu nyingine ni Marsh Academy pia ya Mwanza; Panama ya Iringa; Kigoma Sisterz ya Kigoma, Baobab ya Dodoma na Majengo Queens ya Singida.

Fungua dimba kwa Kituo cha Dar es Salaam, mabingwa watetezi wa taji hilo, Mlandizi Queens itacheza na JKT Queens katika mchezo utakaofanyika Uwanja wa Karume, Ilala jijini Dar es Salaam.

Katika kundi hilo la A, mechi nyingine zitakuwa siku inayofuata Novemba 27, mwaka huu kati ya Mburahati Queens na Evergreen saaa 8.00 mchana wakati Fair Play ya Tanga itacheza na Simba Queens saa 10.00 jioni.

Jijini Arusha, Panama ya Iringa itafungua dimba na Alliance Queens ya Mwanza huku siku ya pili Novemba 27, mwaka huu Baobab Queens itacheza na Marsh Academy saa 8.00 mchana wakati saa 10.00 jioni Majengo Queens itapambana na Sisterz ya Kigoma.

Timu hizo zitapambana katika vituo hadi Desemba 12, mwaka huu kabla ya kutoa jumla ya timu nane kwa maana ya nne kutoka kila kundi. Timu hizo nane zitapambana katika hatua ya Nane Bora ya Ligi hiyo kuelekea ubingwa. Ligi inatarajiwa kumalizika Machi 28, mwakani.

TANZANIA BARA YATHIBITISHA KUSHIRIKI CHALENJI ZOTE



Baada ya kupita miaka miwili bila kuchezwa kwa mashindano ya kuwania Kombe la Chalenji kwa nchi za Afrika Mashariki, michuano hiyo imerejea tena msimu huu na Tanzania imethibitisha kushiriki.

Nchi wanachama Tanzania Bara, Zanzibar, Uganda, Kenya, Burundi, Rwanda, Somalia, Sudan, Sudan Kusini, Eritrea na Ethiopia.

Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu  Tanzania (TFF), Kidao Wilfred amethibitisha kikosi cha kwanza cha ‘Taifa Stars’ kushiriki na matarajio ya kufanya vema michuano hiyo itakayofanyika kuanzia Novemba 25, 2017 hadi Desemba 9, mwaka huu.

Kidao amesema kwamba uteuzi wa timu za kwanza kwa kila nchi mwanachama wa Baraza la Mpira wa Miguu la Afrika Mashariki ni makubaliano ya viongozi wa CECAFA waliokutana kwa pamoja huko Sudan, Septemba, mwaka huu.

Kutokana na makubaliano hayo ya kuita timu za kwanza, michuano hiyo itaathiri kidogot ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) kwa kuwa wachezaji wengi wanaounda kikosi hicho, wanatoka timu za VPL.

Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi (TPLB), Boniface Wambura amesema: “Tutakaa kama kamati na kuangalia siku ya Jumatano na Alhamisi baada ya michuano hiyo na kupanga ratiba ya mechi ambazo zitapanguliwa wakati wa michuano ya Chalenji.”

Mbali ya michuano hiyo, Tanzania imethibitisha kushiriki michuano ya Chalenji ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 itakayofanyika Bujumbura nchini Burundi kuanzia Desemba 12, 2017 hadi Desemba 22, mwaka huu.

Kadhalika, Tanzania imethibitisha kushiriki michuano ya Chalenji kwa wanawake ikienda kutetea taji katika michuano itakayofanyika Rwanda mwezi Desemba, mwaka huu. Tarehe rasmi itatajwa baadaye.

CECAFA imeamua kurejesha hadhi yake kwani mara baada ya michuano ya Chalenji ya vijana huko Burundi, mwakani itakuwa ni zamu ya Tanzania ambako michuano hiyo inatarajiwa kuanza Agosti 11, 2018 hadi Agosti 25, mwakani.

Wakati huo huo Kidao amethibitisha Tanzania kuwa wenyeji wa mashindano ya Vijana ya Chalenji ya CECAFA/CAF kwa vijana chini ya miaka 17 mwakani na mashindano hayo yatatumika kama sehemu ya kufanya maandalizi Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 (AFCON – U17).

Michuano ya mwakani ina baraka za Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kwa sababu shirikisho hilo linataka kutumia michuano hiyo ya vijana ya Kanda mbalimbali za Afrika kupata timu saba katika michuano AFCON – U17 ya mwaka 2019.

Kanda hizo ni CECAFA (Afrika Mashariki), COSAFA (Nchi za Kusini mwa Afrika), WAFU – UFOA (Afrika Magharibi); UNAF (Afrika Kaskazini) na UNIFFAC (Afrika ya Kati).

Sunday, October 29, 2017

SIMBA, YANGA ZASHINDWA KUTAMBIANA


Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania mzunguko wa nane imeendelea tena kwa mchezo mmoja uliowakutanisha watani wa Jadi nchini Simba na Yanga ambapo timu hizo zimetoshana nguvu ya kugawana alama moja moja baada ya kufungana goli 1-1 kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.

Wakicheza kwa kujiamini vijana wa Lwandamina walionekana kutengeneza nafasi nyingi za kufunga kuliko vinara wa Ligi Simba huku timu zote zikicheza kwa kuogopana hali ambayo ilipelekea timu hizo kwenda mapumziko zikiwa hazijafungana.

Kipindi cha pili timu zote zilifanya mabadiliko mbalimbali hata hivyo hayakuweza kuwa na manufaa kwa pande zote kwani Yanga waliingia wakiwa na hofu ya kukosa baadhi ya nyota wake muhimu ambao wapo katika majeruhi Thabani Kamusoko,Donald Ngoma na Amis Tambwe.

Simba walikuwa wa kwanza kuapata goli kupitia kwa winga matata Shiza Ramadhani Kichuya dakika ya 57 baada ya krosi ya Emanuel Okwi kupanguliwa na golikipa wa Yanga na uzembe wa Papy Kabamba Tshishimbi ulioweza kumuacha Kichuya aliyemtungua Youthe Rostand.

Baada ya kuingia kwa goli hilo Yanga walijipanga na kuendeleza mashambulizi kwa Simba na dakika ya 60 wachezaji Ajibu na Mwashiuya waligogeana na kutoa pasi kwa Mshambuliaji matata ambaye alikuwa mwiba kwa wekundu wa Msimbazi,Obrey Chirwa na kuisawazishia Yanga.

Hadi mwamuzi wa Kimataifa Heri Sasii anapuliza kipyenga cha mwisho Yanga na Simba wamegawana pointi moja moja na kwa matokeo hayo Simba wanarudi katika nafasi yao ya kwanza kwa kufikisha pointi 16 sawa na Yanga na Azam huku yeye akiwa na uwiano mzuri wa magoli ya kufungwa na kufunga.

Tuesday, October 24, 2017

TAIFA STARS KUJIPIMA UBAVU NA BENIN UGENINI


KOCHA wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Salum Mayanga amewarejesha kikosini kiungo Farid Mussa na mshambuliaji, Elias Maguri kwa ajili ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa mapema mwezi ujao.
Baada ya kucheza nyumbani mfululizo mechi za kirafiki za kimataifa, Taifa Stars sasa itatoka mwezi ujao kwenda Benin kucheza na wenyeji Novemba 11, mwaka huu.
Mayanga ameita kikosi cha wachezaji 24, ambacho kitaingia kambini Novemba 5 mjini Dar es Salaam kabla ya kusafiri Novemba 9 kwenda Benin tayari kwa mchezo huo. 
Elias Maguri (kushoto) akiwa na Nahodha wa zamani wa Taifa Stars, Nadir Haroub 'Cannavaro'
Na ndani yake amewaorodhesha Maguri aliyekuwa anacheza Oman na Farid Mussa anayecheza Tenerife B ya Hispania, ambao wote hakuwaita kwenye mchezo uliopita dhidi ya Malawi, uliomalizika kwa sare ya 1-1 Oktoba 7, Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Kikosi kamili cha Taifa Stars kilichotajwa leo kinaundwa na makipa; Aishi Manula (Simba SC), Peter Manyika (Singida United) na Ramadhani Kabwili, mabeki Boniphace Maganga (Mbao FC), Abdi Banda (Baroka FC/Afruka Kusini), Gardiel Michael (Yanga), Kevin Yondan (Yanga), Nurdin Chona (Prisons), Erasto Nyoni (Simba) na Dickson Job (Mtibwa Sugar).
Viungo ni Himid Mao (Azam FC), Hamisi Abdallah (Sony Sugar/Kenya), Muzamil Yassin (Simba), Raphael Daudi (Yanga), Simon Msuva (Yanga), Shiza Kichuya (Simba), Ibrahim Hajib (Yanga), Mohammed Issa (Mtibwa), Farid Mussa (Tenerife/Hispania) na Abdul Mohammed (Tusker/Kenya) na washambuliaji Mbwana Samatta (KRC Genk/Ubelgiji), Mbaraka Yussuf (Azam FC), Elias Maguri (Huru) na Yohanna Nkomola (Huru). 

KUZIONA SIMBA, YANGA BUKU KUMI, MECHI KUCHEZWA SHAMBA LA BIBI


KIINGILIO cha chini katika mchezo wa mahasimu wa jadi, Simba na Yanga utakaofanyika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam Oktoba 28, kitakuwa ni Sh 10,000.
Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Wilfred Kidau ameiambia Bin Zubeiry Sports – Online leo mjini Dar es Salaam kwamba kiingilio hicho kitahusu majukwaa ya mzunguko ya Uwanja huo, wakati jukwaa kuu watu watalipa Sh. 20,000.
Kidau amesema kwamba utaratibu maalum umewekwa kuhakikisha idadi inayotakiwa ya watu 22,000 ndiyo wanaoingia uwanjani kwa kuhakikisha haziuzwi tiketi zaidi.
Aidha, kiungo huyo wa zamani wa Simba SC, amesema kwamba imelazimika mchezo huo kufanyika Uwanja wa Uhuru kwa sababu Uwanja mkubwa wa Taifa upo kwenye ukarabati.
Kidau pia amesema kwamba Alhamisi wiki hii Kamati mpya ya Uongozi wa Bodi ya Ligi (TPLB) ya TFF itafanya kikao chake cha kwanza mjini Dar es Salaam, kubwa likiwa ni maandalizi ya mchezo huo.
Lakini pia, Kidau amesema kwamba ajenda nyingine katika kikao hicho ni kuteua Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi, na Kamati nyingine mbalimbali.
Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Wilfred Kidau amesema kiingilio cha chini Simba na Yanga ni Sh. 10,000

YANGA YATOA DOZI YA 4G KWA STAND UNITED



YANGA SC wameonyesha wapo tayari kutetea ubingwa, baada ya leo kuwafumua mabao 4-0 wenyeji Stand United kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.
Shujaa wa Yanga  alikuwa mshambuliaji mpya, Ibrahim Hajib Migomba aliyefunga mabao mawili na kuseti moja, lililofunga na Obrey Chirwa wakati bao lingine la wana Jangwani hao limefungwa na kiungo Pius Buswita.
Kwa matokeo hayo, Yanga inafikisha pointi 15 baada ya kucheza mechi saba na kupanda hadi nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu, wakizidiwa kwa wastani wa mabao tu ya kufunga na kufungwa na Simba SC wenye pointi 15 pia sawa na Mtibwa Sugar walio nafasi ya tatu.

Sunday, October 22, 2017

SIMBA YAIPA KISAGO MJI NJOMBE



SIMBA jana iliendelea kuchanja mbuga katika kuwania ubingwa wa ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara baada ya kuicharaza Mji Njombe mabao 4-0.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, mabao ya Simba yalifungwa na Muzamir Yassin, aliyetupia mabao mawili, Emmanuel Okwi na Laudit Mavugo.

Kwa matokeo hayo, Simba bado ipo kileleni mwa ligi hiyo, ikiwa na pointi 15, sawa na Mtibwa Sugar, lakini zinatofautiana kwa mabao ya kufunga na kufungwa.

Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena leo wakati Yanga itakapomenyana na Stand United kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.


Saturday, October 21, 2017

DAKTARI ASEMA ALIMKUTA KANUMBA AKIWA AMESHAKUFA




DAKTARI wa familia ya msanii maarufu wa filamu nchini, marehemu Steven Kanumba, Dkt, Paplas Kagaia, ameileza mahakama Kuu ya Tanzania kanda Dar es Salaam Kanumba alifariki toka nyumbani baada ya kumpima na kukuta mapigo yake ya moyo hayakuwepo.
Dk, Paplas amedai hayo leo Oktoba 20, 2017 huu wakati akitoa ushahidi wake mbele ya Jaji Sam Rumanyika.
Amedai kuwa, baada ya mdogo wa marehemu kumfuata hospitali kwake na kumwambia kuwa Kanumba amefariki, alichukua kipino cha sukari na shindikizo la Damu(pressure) na kwenda moja moja nyumbani kwake Sinza ambako baada ya kufika nyumbani kwake alimpima sukari na kukuta io kawaida lakini alipompima pressure haikuwepo kabisa.

Daktari Huyo mwenye elimu ya stashada ya juu (Advance diploma) aliyejipatia Elimu yake chuo cha uuguzi cha jeshi cha Lugalo amedai kuwa, alikuwa daktari wa familia ya Kanumba kwa zaidi ya miaka mitano na anamiliki Hospitali yake binafsi ya St. Anna iliyopo Manzese jijini Dar es Salaam alikuwa akimtibu Kanumba magonjwa ya kawaida na hakuwahi kugundua tatizo lake lolote.

Mahojiano kati ya Dr Paplas na Wakili wa serikali Batlida Mushi yalikuwa kama ifuatavyo;

Wakili: Ulipata wapi taarifa kama ya kuugua kwa Kanumba?
Shahidi: Nikiwa naudumia wagonjwa kama kawaida nilipigiwa simu na Seth akiniomba niende kumuona Kanumba amedondoka, nikamwambia muda ule ulikuwa ni usiku sana aende kumchukua.

Wakili: kwani nini Seth akupigie wewe simu?
Shahidi: Nilikiwa daktari wa familia yao kwa miaka kama mitano hadi sita.

Wakili: Baada ya kukupigia simu, ulifanya nini?
Shahidi: Nilichukua vifaa vya mashine ya sukari na BP, niliingia chumbani kwake nikifuatana na Seth nilipofika nilikuta Kanumba amelala chini chali, nikampima sukari ilikuwa normal nikampima pressure mapigo ya moyo hayakuwepo kabisa.
Wakili:Baada ya kujua mapigo ya moyo hayapo ulifanya ulichukua hatua gani?
Shahidi: Nilimwambia Sethi Fanya umvalishe nguo wafanye utaratibu wa kumpeleka hospitali kubwa ya Muhimbili akafanyiwe Vipimo.

Wakili: Baada ya hapo ulifanya nini?
Shahidi: Baada ya kumvalisha nguo kwa kisaidiana na kijana mmoja wa jirani na mama mwenye nyumba tulimpeleka Muhimbili kitengo cha emergency.
Wakili: Mlipofika Muhimbili kitengo cha Emergency ulifanya nini?
Shahidi: Nilimuomba Dk tuliyemkuta pale ampime Kanumba na alipompima alisema kuwa ameshafariki.

Wakili: Wakati huo anapimwa mlikuwa mahali gani?
Shahidi: Alimpima pale pale nje hata ndani hatukuingia, alitushauri tufuate taratibu za polisi, alituambia twende Kituo cha polisi cha Slender Bridge tukachukue PF3.

Wakili: Mlipokuwa Polisi nini kiliendelea?
Shahidi: Tulipewa askari ili watusaidie kupeleka maiti Mochuari kisha tukaambiwa twende Kituo Osterbay Polisi tukatoe Maelezo.

Wakili: Unamfahamu Lulu?
Shahidi: Ndiyo
Wakili: Unamfahamuje?
Shahidi: Nimemfahamu kwa kupitia Kanumba.

Wakili: Unamfahamu kama nani?
Shahidi: Alikuwa mpenzi wake Marehemu Kanumba.
Wakili: Je Aprili 7 mwaka 2012 baada ya wewe kwenda Polisi Osterbay ulimuona?
Shahidi: Hapana sikumuona.

Wakili: ulimuonea wapi?
Shahidi: Nilimuona usiku kwenye saa 11 alikuwa Sinza sehemu moja inaitwa Bamaga, baada ya yeye kunipigia simu.

Baada ya kumaliz kutoa ushahidi wake kwa upande wa mashtaka wakili wa utetezi, Peter Kibatala naye alipata nafasi ya kumuhoji shahidi huyo ambapo mahojiano yao yalikuwa hivi;
Wakili Kibatara: Kwa nini ulipofika eneo la tukio ulimpima Sukari?
Shahidi: mtu akianguka ghafla Mara nyingi sukari inaweza kuwa imeshuka
Wakili Kibatala, kabla ya Octoba 7 uliwahi kumfanyia uchunguzi marehemu kuhusu sukari.
Shahidi: Hapana
Wakili: Uliwahi kumfanyia vipimo kama anauvimbe kichwani
Shahidi: hapana.
Wakili: je ulimkuta na jeraha lolote?
Shahidi hapana.
Wakili Kibatara: Ni sahihi kuwa mshtakiwa alikuwa anakupigia simu Mara kwa Mara?
Shahidi: Ni sahihi kweli alikuwa akinipigia hata kabla hajaenda hospitali.

Wakili Kibatara:Ni sahihi kwamba mshtakiwa alikuwa anakupigia simu Mara kwa Mara akifikiria kuwa marehemu alikuwa amezimia tu?
Shahidi; Ndiyo ila alikuwa na hofu kama marehemu amekufa.

Wakili Kibatara: Ni sahihi kuwa mshtakiwa alikuwa anaogopa kuonana na wewe kwa sababu alidhani uko na marehemu na ulikuwa na mtego tu wa kumkamata ili andeleze tabia yake ya wivu uliopindukia?
Shahidi: hapana.
Wakili Kibatala: umesema, mlikutana na mshtakiwa Bamaga, kwa nini mshtakiwa alikubali kuonanana wewe Bamaga?, Ni ushawishi gani ulimwambia hadi akakubali kuja?
Shahidi: alikubali tukutane Bamaga alikuwa hajui kwamba Kanumba ameshafariki, yeye ndio alinipigia simu akasema si umesema Kanumba hajafa nikamwambia ndio akasema tukutane Sinza nikasema tukutane Bamaga.

Naye shahidi wa tatu, mrakibu msaidizi wa Polisi PF 16519 ASP Ester Zefania akitoa ushahidi wake huku akiongozwa na wakili wa Serikali,  Ayoub Abood amedai, Oktoba 7, 2012 akiwa kituoni Osterbay alipewa maelekezo na Mkuu wa upelelezi Wa mkoa Wa Kinondoni Camilius wambura kwenda Sinza kwa Kanumba kufuatilia taarifa alizopata za kifo cha Kanumba.

Amedai aliondoka na askari watatu pamoja na msanii Ray ambaye aliwaongoza hadi kwa Sinza kwa marehemu ambako alikuta watu wengi wengine wakilia kuashiria hali ya msiba mahojiani yake na Wakili Abood yalikuwa hivi;
Wakili: Baada ya kufika hapo nyumbani ulifanya nini?
Shahidi : Nilijitambulisha wa watu waliokuwepo pale kuwa Mimi ni askari kutoka kituo cha polisi cha Osterbay, nikaitiwa mdogo wake Kanumba Seth, ambapo nilipomuuliza nini kilitokea alinielezea kwa kifupi.
Baada ya hapo mimi pamoja na askari 2 pamoja na Ray tulioingia chumbani kwa marehemu kwa ajali ya uchunguzi.

Wakili : Baada ya kuingia humo chumbani ulikuta hali gani? na  mliweza kuona kitu gani katika chumba hicho?
Shahidi:Kitanda kilikuwa kimevurugwa, pembeni yake kulikuwa na stuli juu yake ilikuwa na chupa ya soda aina ya Sprite, glass iliyokuwa na kinywaji nusu na chupa ya whisky ya Jackie Daniel, pia pembeni chini ya tendegu za kitanda kulikuwa na panga na pembeni yake kulionekana michirizi ya mburuzo wenye rangi kama nyeusi isiyokolea.

Wakili: Baada ya hapo nini kilitokea?
Shahidi: Nilimpigia simu kamanda Wambura na kumpatia taarifa ambaye aliniambia angetuma timu ya wapelelezi wa matukio kutoka mkoani na eneo la tukio libaki vilevile.

Wakili: Baada ya kufika wakuu wa upelelezi ulifanya nini?
Shahidi: Nilindoka nikarudi kituoni.

Wakili: Baada ya kufika kituoni ulimkuta nani?
Shahidi; Nilimkuta kamanda Wambura ambaye alinipa (task) jukumu la kumtafuta Lulu apelekwe kituoni hapo kwani kwa taarifa alizokuwa nazo atakuwa anafahamu nini kilimpata Kanumba.

Wakili: Alikupa Huyo Daktari kwa ajili gani?
Shahidi; Alinipa Daktari Paplas ili tusaidiane nae kumpata Lulu kwani ndio alikuwa akiongea naye  Mara nyingi ambapo alimpigia simu na kukubaliana kukutana nae bamaga ndipo waliweza kumkamata.
Wakili Kibatala nae alimhoji mrakibu msaidizi wa Polisi PF 16519 ASP Ester Zefania mahojiano yao yalikuwa hivi;

Wakili Kibatala: Mlipomkamata Lulu mlimpeleka hospitali?
Shahidi; NdioWakili Kibatala: Mlimpeleka Lulu hospitali kutibiwa nini?
Shahidi: sifahamu, sikuingi kwa kwenye chumba cha daktari.Wakili Kibatala: Ni sahihi kwamba sababu ya kupelekwa Lulu kwa daktari kuwa alipigwa na ubapa wa panga mapajani na alikuwa na maumivu
Shahidi; Sifahamu.

Kesi hiyo itaendelea Oktoba 23, 2017( Jumatatu) na shahidi wa nne atatoa ushahidi wake.

LIGI KUU BARA USHINDANI KILA KONA

Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), inatarajiwa kuendelea kesho Ijumaa Oktoba 20, 2017 kwa mchezo mmoja utakaokutanisha timu za Mwadui na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Mwadui mkoani Shinyanga.

Timu hizo zinakutana katika Raundi ya Saba katika duru hili la kwanza la VPL ambalo mbali ya Kampuni ya Simu ya Vodacom - wadhamini wakuu, wadhamini wengine ni Kituo cha Televisheni cha Azam (Azam Tv) na Benki ya KCB ambayo huduma zake za kibenki zinazidi kushamiri nchini.

Wadhamini hao wanachagiza ligi hiyo ambayo itaendelea Jumamosi Oktoba 21 kwa michezo sita  itakayofanyika kwenye viwanja tofauti huku mechi nyingi zikipata fursa ya kuonyeshwa kwenye chaneli mbalimbali za Azam Tv kupitia king’amuzi cha Azam.

Michezo ya Jumamosi itakutanisha timu za Mbao na Azam kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, wakati Lipuli itakuwa mwenyeji wa Majimaji ya Songea kwenye Uwanja wa Samora mjini Iringa ilihali Ruvu Shooting watakuwa wageni wa Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

Jumamosi hiyo hiyo Simba yenye mabadiliko kidogo kwenye benchi la Ufundi, itawaalika Njombe Mji kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam huku Ndanda ikicheza na Singida United kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.

Wakati Jumamosi hiyohiyo tena, Mtibwa Sugar wakicheza na Tanzania Prisons ya Mbeya kwenye Uwanja wa Manungu mkoani Morogoro, Jumapili kutakuwa na mchezo mmoja tu - ambao ni kati ya Stand United na mabingwa watetezi, Young Africans ya Dar es Salaam - mchezo utakaopigwa Uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga.

LIGI DARAJA LA KWANZA KUENDELEA WIKIENDI HII
Raundi ya Sita ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL), itaendelea  kesho Ijumaa Oktoba 20, 2017 kwa mechi za makundi yote matatu.

Katika Kundi ‘A’, Mvuvumwa FC ya Kigoma, watacheza na Mgambo JKT katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Mvuvumwa anatumia Kanuni ya 6 (1) na (2) kuhamishia mechi zake za nyumbani Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam kutoka Uwanja wa Tanganyika, Kigoma.

Mechi nyingine kwenye kundi hilo itafanyika Jumapili Oktoba 22, mwaka huu kwa michezo mitatu.

Mechi hizo ni kati ya  Kiluvya United  na Mshikamano  kwenye Uwanja wa Filbert Bayi, ilihali African Lyon  itacheza na Ashanti United  kwenye Uwanja wa Uhuru wakati Friends Rangers itapambana na JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Azam, Dar es Salaam.

Katika Kundi ‘B’ siku hiyo ya Ijumaa Oktoba 20, mwaka huu Polisi Dar itacheza na Coastal Union ya Tanga kwenye Uwanja wa Azam wakati michezo mingine katika kundi hilo ikichezwa Jumamosi na  Jumapili.

Jumamosi Mbeya Kwanza itacheza na JKT Mlale Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi mkoani Pwani na Jumapili Polisi Tanzania watawakaribisha KMC kwenye Uwanja wake wa nyumbani wa Ushirika Moshi, huku Mawenzi Market ya Morogoro wakiwaalika Mufindi United kwenye Uwanja wa Jamhuri Morogoro.

Katika Kundi ‘C’ kutakuwa na mchezo mmoja siku ya Ijumaa Oktoba 20, 2017 Pamba SC ya Mwanza itacheza na Alliance Schools nayo ya Mwanza kwenye Uwanja wa Nyamagana huko Mwanza na michezo mingine itafanyika Jumamosi na Jumapili.

Michezo ya Jumamosi  itazikutanisha Biashara Mara dhidi ya JKT Oljoro kwenye Uwanja wa Karume Mara,Transit Camp itakuwa mwenyeji wa Dodoma FC kwenye Uwanja wa Kambarage Mjini Shinyanga,wakati mchezo mwingine wa Kundi C, Toto Africans ya Mwanza itacheza  na Rhino Rangers ya Tabora katika mchezo utakaochezwa kwenye Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza.

WANAWAKE 28 WAHITIMU KOZI YA UKOCHA TFF

Makocha 28 wanawake kutoka vyuo mbalimbali vya Maendeleo ya Jamii nchini leo Oktoba 17, 2017 wamehitimu kozi fupi ya ukocha katika kozi iliyoratibiwa kwa pamoja kati ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Taasisi ya Karibu Tanzania (KTO).

Kozi hiyo ya siku mbili ambayo ni ya pili kufanyika kwa makocha hao, iliyofanyika kwenye Uwanja wa Karume - Makao Makuu ya TFF ilikuwa chini ya mkufunzi wa TFF, Raymond Gweba.

Akizungumza kwenye ufungaji wa kozi hiyo Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo, Yusuph Singo amesema Serikali inafahamu kuwa inatakiwa kuwekeza kwenye soka la wanawake kuanzia upande wa vijana na ndio maana inatengeneza mazingira na sera zitakazowezesha mafanikio hayo.

Singo amesema nchi mbalimbali wana maendeleo makubwa katika mpira wa miguu kwa wanawake na sasa wakati wa Tanzania kuwekeza katika upande huo kuanzia kwa watoto na makocha.

Kadhalika, Singo amewataka wahitimu kuchukuwa mafunzo hayo kwa uzito mkubwa kwa sababu mpira wa miguu ya ajira na elimu hiyo itaongeza kitu kikubwa kwao.

Naye, Mwenyekiti wa Chama Mpira wa la Wanawake (TWFA), Amina Karuma amesema lengo la chama chake na TFF kuhakikisha soka linachezwa nchi nzima linaelekea kutimia.

Amewataka wahitimu hao wa kozi hiyo fupi kuvitumia vyeti walivyovipata kuendeleza soka la wanawake na kufanyia kazi yale yote waliyofundishwa.

Pia ameiomba Serikali kuwaunga mkono katika maendeleo ya soka la wanawake.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa ufundi wa TFF Salum Madadi amesema kufundisha watoto kuna changamoto nyingi, lakini makocha hao wamefundishwa maarifa ya jinsi ya kukabiliana nazo.

Amesema maarifa hayo sio makocha wote wanaweza kuyapata lakini wameona umuhimu mkubwa kwa wahitimu hao kuweza kuyapata ili kwenda kuibua vipaji kuanzia chini.

Wahitimu wa kozi hiyo wamepatiwa vyeti vya ushiriki na vifaa vya michezo ikiwemo koni na mipira.

Friday, October 13, 2017

TFF YATAWATOA MAKOCHA KATIKA MABENCHI



Bodi ya Ligi (TPLB) ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, limewapiga marufuku makocha watano wa timu za Ligi Daraja la Kwanza kukaa katika mabenchi ya timu hizo kwa sababu ya kukosa sifa.


Makocha hao ni Mathias Wandiba wa Pamba FC ya Mwanza, Salum Waziri wa JKT Mgambo ya Tanga, Adam Kipatacho wa African Lyon ya Dar es Salaam, Omba Thabit wa Mvuvumwa FC ya Kigoma na Ngelo Manjamba wa Polisi Dar.


Makocha hao wamekuwa kwenye mabenchi ya timu wakifanya kazi kama makocha wakuu katika mechi nne mfululizo za Ligi Daraja la Kwanza msimu wa 2017/2018 inayoendelea hivi sasa.


Kwa mujibu wa kanuni ya 72 (3) (5) ya Ligi Daraja la Kwanza, Kocha Mkuu anatakiwa kuwa na Leseni ya chini kuanzia daraja C ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) wakati Kocha Msaidizi anatakiwa kuwa na  sifa isiyopungua ngazi ya Kati cha Ukocha (Intermediate).


Tayari Idara ya Ufundi ya TFF imefafanua wazi kuwa makocha hao hawana Leseni C ya CAF hivyo hawastahili kukaa kwenye mabenchi ya timu zao kama makocha wakuu.


Vitendo vinavyofanywa na timu husika ni ukiukwaji wa kanuni, na ni matarajio ya TFF kuwa viongozi wa timu hizo watasitisha mara moja kwa makocha hao kukaa kwenye mabenchi ili kuepika adhabu.


TFF tunachukua nafasi hii kuzikumbusha klabu husika  kwamba kuanzia msimu ujao 2018/2019 kuwa sifa ya Kocha Mkuu wa kila timu ya Daraja la Kwanza ni Leseni B ya CAF.


PATASHIKA LIGI VPL, FDL, SDL WIKIENDI HII


Baada ya kupisha wiki ya FIFA kwa mchezo wa kirafiki wa kimataifa ukihusisha Taifa Stars ya Tanzania na Miale ya Moto kutoka Malawi iliyotoshana nguvu ya bao 1-1, uhondo wa mashindano ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili, umerejea.


Kwa upande wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea wikiendi hii ambako kesho Oktoba 13, 2017 kutakuwa na mchezo mmoja tu utakaokutanisha timu za Mbao FC na Mbeya City kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Dar es Salaam.


Timu hizo ziko katika nafasi za katikati katika msimamo wa VPL, lakini ushindani unatarajiwa kuwa kwa timu za Simba SC, Mtibwa FC na Azam ambazo kila moja ina pointi 11 na ziko kileleni kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa tu.


Katika michezo ya Jumamosi Oktoba 14, 2017 Azam FC itakuwa mgeni wa Mwadui FC kwenye Uwanja wa Mwadui wakati Kagera Sugar itawaalika mabingwa watetezi, Young Africans kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.


Ndanda itakuwa nyumbani kucheza na majirani zao Majimaji ya Songea kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara wakati Singida United itasafiri hadi Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi kucheza na wenyeji Ruvu Shooting ya Pwani.


Majirani wengine, Njombe Mji na Lipuli ya Iringa watacheza kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe ilihali michezo mingine ya Ligi hiyo ikifanyika Jumapili Oktoba 15, ambako Simba itakuwa mwenyeji wa Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam wakati Tanzania Prisons itacheza na Stand United kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.


Ligi Daraja la Kwanza (FDL) nayo itaendelea ambako kesho kutakuwa na mchezo kati ya African Lyon na JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Timu hizo ni za Kundi A.


Mechi nyingine kwenye kundi hilo itafanyika Jumamosi ambako Ashanti United itacheza na Mvuvumwa ya Kigoma kwenye Uwanja wa Uhuru ilihali Jumatatu Oktoba 16, Kiluvya itacheza na Friends Rangers kwenye Uwanja wa Uhuru huku Mgambo JKT ikishikamana na Mshikamano kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.


Kundi B kwa mujibu wa ratiba ni kwamba kesho Ijumaa JKT Mlale itacheza na Polisi Dar kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea huku michezo mingine katika kundi hilo ikicheza Jumapili kwa michezo mitatu.


Siku hiyo Mbeya Kwanza itacheza na Mawenzi Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi mkoani Pwani, Coastal na Polisi Tanzania kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga huku Mufindi United itacheza na KMC Uwanja wa Samora mkoani Iringa.


Kundi C litakuwa na mchezo mmoja siku ya Jumamosi  Oktoba 14, 2017 ambako Toto African itakipiga na Pamba kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza na michezo mingine mitatu itafanyika siku ya Jumapili Oktoba 15, mwaka huu.


Michezo ya Jumapili itakuwa ni kati ya Dodoma FC dhidi ya JKT Oljoro ya Arusha kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma; Rhino Rangers itacheza Biashara United wakati mchezo wa Alliance Schools na Transit Camp utachezwa kwenye Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza.


Ligi Daraja la Pili (SDL), Jumapili Oktoba 15, 2017 Kundi A kutakuwa mchezo kati ya Villa Squad na Abajalo FC Uwanja wa Kinesi, Dar es Salaam.


Jumamosi kutakuwa na michezo miwili ya Kundi B ambako African Sports itacheza na Pepsi kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga huku Arusha FC itacheza na Kitayose kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.


Jumapili Oktoba 15, 2017 katika kundi B hilo la B kutakuwa na mchezo mmoja kati ya Madini na Kilimanjaro Heroes kwenye Uwanja wa Nyerere mkoani Arusha.


Kundi C kutakuwa na michezo yote mitatu ya raundi ya tatu ambako Ihefu itacheza na Green Warriors kwenye Uwanja wa Highland; Mkamba Rangers itacheza na The Mighty Elephant kwenye Uwanja wa Mkamba huko Morogoro ilihali Boma FC dhidi ya Burkinafaso zitacheza Uwanja wa Mwakangale, Mbeya.


Kundi D pia kutakuwa na mechi zote tatu Oktoba 14, 2017 ambako Nyanza itacheza na Mashujaa kwenye Uwanja wa Nyerere; Area ‘C’ United itacheza na Milambo Uwanja wa Jamhuri Dodoma wakati JKT Msange itacheza na Bulyanhulu kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.


NI ZAMU YA WAAMUZI DARAJA I NA II


Baada ya mtihani wa utimamu wa mwili kwa waamuzi wenye beji za FIFA na wale wa Daraja la Kwanza kufanyika Agosti, 2017, sasa ni zamu ya waamuzi wa madaraja ya Tatu na Pili.


Waamuzi wa madaraja ya Tatu na Pili kuanzia leo Alhamisi Oktoba 12, 2017 wameanza vipimo kabla ya  mitihani ya utimamu wa mwili katika vituo viwili vya Dar es Salaam na Mwanza. 


Kwa wale watakaopata matokeo mazuri, watapata fursa ya kupandisha madaraja kwa mujibu wa utaratibu.


Zoezi hilo litajumuisha pia wale waamuzi wa Daraja la Kwanza walioshindwa mitihani hiyo mwezi Agosti, mwaka huu. Hivyo nao wanaruhusiwa kwenda kufanya mitihani tena.


Kituo cha Dar es Salaam kitakuwa na waamuzi wa mikoa ya Dar es Salaam yenyewe, Pwani, Morogoro, Tanga, Kilimanjaro, Lindi, Mtwara, Ruvuma, Njombe, Iringa, Mbeya, Rukwa na Songwe.


Kituo cha Mwanza kitakuwa na waamuzi wa mikoa ya Mwanza yenyewe, Mara, Kagera, Simiyu, Geita, Kigoma, Arusha, Shinyanga, Tabora, Dodoma, Singida, Manyara na Katavi.


Waamuzi wote waende kwenye vituo vyao walivyopangiwa kama ilivyoelekezwa Oktoba 12, 2017 - ni siku ya kupima afya kabla ya kuanza kwa mitihani mingine ukiwamo wa utimamu wa mwili hapo kesho.

BEKI SINGIDA UTD MCHEZAJI BORA SEPTEMBA, 2017



Mchezaji wa timu ya Singida United, Shafik Batambuze  amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa mwezi Septemba wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu wa 2017/2018.


Batambuze anayecheza nafasi ya ulinzi wa pembeni, alitwaa tuzo hiyo baada ya kuwashinda wenzake wawili, Ibrahim Ajibu wa Yanga na kiungo Mohammed Issa wa Mtibwa Sugar, alioingia nao fainali katika uchambuzi uliofanywa Dar es Salaam.


Uchambuzi huo kwa mujibu wa utaratibu hufanywa na kikao cha Kamati ya Tuzo ya VPL inayotolewa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kutokana na mapendekezo kutoka kwa makocha waliopo viwanja mbalimbali ambavyo ligi hiyo inachezwa msimu huu.



Mchezaji huyo alitoa mchango mkubwa kwa Singida United kupata pointi 10 katika michezo minne, ambayo timu yake ilicheza kwa mwezi huo, matokeo ambayo yaliiwezesha Singida United kutoka nafasi ya 10 katika msimamo na kupanda hadi nafasi ya nne kwa mwezi huo wa Septemba. Singida United ndiyo timu iliyokusanya alama nyingi kwa mwezi huo ukilinganisha na timu nyingine 15 zinazoshiriki VPL.


Singida United iliifunga Mbao FC mabao 2-1 Uwanja wa Jamhuri Dodoma,  ikaifunga Stand United bao 1-0 Uwanja wa Kambarage, Shinyanga, iliifunga Kagera Sugar Uwanja wa Jamhuri Dodoma na ilitoka sare ya bao 1-1 na Azam FC uwanja huo huo. Michezo yote hiyo Batambuze alicheza dakika zote 90 kwa kila mchezo, ambayo ni sawa na kucheza dakika 360.


Kwa upande wa Ibrahim Ajibu alitoa mchango mkubwa kwa Yanga uliowezesha kupata pointi nane kwa mwezi huo, baada ya kushinda michezo miwili na kutoka sare miwili, ambapo pia Mohammed Issa aliisaidia timu yake kupata pointi nane katika michezo minne iliyocheza mwezi huo, ikishinda miwili na kutoka sare miwili.


Kampuni ya Vodacom, ambao ndiyo wadhamini wa ligi hiyo ina utaratibu wa kuwazawadia wachezaji bora wa kila mwezi, huku pia mwisho wa msimu kukiwa na tuzo mbalimbali zinazohusu ligi hiyo, ambapo msimu wa mwaka 2016/2017 kulikuwa tuzo 16 zilitolewa kwa washindi wa kada mbalimbali. Batambuze atazawadiwa Sh milioni moja kwa kuibuka Mchezaji Bora wa mwezi.

MALALAMIKO YA PEPSI YAMEKATALIWA



Malalamiko ya Pepsi dhidi ya Madini kuwa timu hiyo ilimtumia mchezaji Shabani Imamu kwenye mechi yao ya Ligi Daraja la Pili (SDL) iliyochezwa Septemba 30 mwaka huu Uwanja wa  Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini wakati akiwa na adhabu ya kutumikia kadi nyekundu yamekataliwa.

Kamati imebaini kuwa mchezaji huyo alishatumikia adhabu ya kukosa mechi moja wakati wa mchezo wa SDL kati ya Madini na JKT Oljoro uliochezwa Februari 6 mwaka huu.

Mchezaji huyo alioneshwa kadi ya pili ya njano msimu uliopita kwenye mechi kati ya Madini na AFC iliyofanyika Januari 31 mwaka huu, na kukosa mechi moja iliyofuata kati ya Madini na JKT Oljoro ya Februari 6 mwaka huu, hivyo kuwa halali kwenye mechi ya Pepsi na Madini iliyochezwa Septemba 30 mwaka huu.

Kocha Msaidizi wa Area C United, Omarooh Omari amesimamishwa kukaa kwenye benchi la timu yake wakati akisubiri suala lake la kumpiga kiwiko mchezaji wa Nyanza FC kusikilizwa na Kamati ya Nidhamu ya TFF.


Alimpiga kiwiko mchezaji wa Nyanza, Rajab Adam alipokuwa akikimbilia mpira uliopita karibu yake. Pia dakika ya 78 alianzisha tena vurugu na Mwamuzi kumtoa kwenye benchi la ufundi lakini aligoma kutoka hadi alipotolewa na askari polisi.


Alifanya vitendo hivyo vya utovu mkubwa wa nidhamu wakati wa mechi kati ya Ligi Daraja la Pili kati ya timu yake na Nyanza iliyochezwa Oktoba 1 mwaka huu kwenye Uwanja wa Nyerere uliopo Mbulu mkoani Manyara.

Uamuzi wa kumsimamisha umefanywa kwa kutumia Kanuni ya 9(5) ya Ligi Daraja la Pili.



KUSIMAMISHWA MCHEZAJI JOHN BARAKA WA AREA C



Kamati ya Bodi ya Ligi ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi katika kikao chake kilichopita ilipitia taarifa na matukio mbalimbali ya Ligi Kuu ya Vodacom, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili msimu wa 2017/2018 zinazoendelea hivi sasa.



Katika taarifa hizo imebainika kuwa mchezaji wako John Baraka jezi namba 2 alioneshwa kadi nyekundu baada ya mchezo kumalizika kwa kumpiga ngumi mwamuzi ngumi ya mgongoni.



Alifanya kitendo hicho kwenye mechi namba 1 ya Kundi D la Ligi Daraja la Pili kati ya timu yako na Nyanza FC iliyofanyika Oktoba 1 mwaka huu kwenye Uwanja wa Nyerere uliopo Mbulu mkoani Pwani.



Kwa vile suala lake ni la kinidhamu, na kwa kutumia Kanuni ya 9(5) ya Ligi Daraja la Kwanza, Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi imemsimamisha kucheza mechi za SDL hadi suala lake litakaposikilizwa na Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).



Mchezaji wako atafahamishwa siku ambayo kikao cha Kamati ya Nidhamu kitafanyika kusikiliza shauri dhidi yake ambapo pia atapata fursa ya kuwasilisha utetezi wake kama upo.



ONYO KALI KWA MKAMBA RANGERS


Kamati ya Bodi ya Ligi ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi katika kikao chake kilichopita ilipitia taarifa na matukio mbalimbali ya Ligi Kuu ya Vodacom, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili msimu wa 2017/2018 zinazoendelea hivi sasa.


Katika taarifa hizo imebainika kuwa timu yako haikuhudhuria katika kikao cha maandalizi (pre match meeting), na pia ilichelewa kufika uwanjani wakati wa mechi namba 3 ya Kundi C dhidi ya Boma FC iliyochezwa Septemba 30 mwaka huu Uwanja wa Mwakangale uliopo Kyela mkoani Mbeya.


Kitendo hicho ni ukiukaji wa Kanuni ya 14(2a) na Kanuni ya 14(9) za Ligi Daraja la Pili. Kwa vile ni kosa la kwanza kwa timu yako msimu huu, Kamati imeipa klabu yako Onyo Kali kwa kuamini kuwa kosa hilo la kikanuni halitajitokeza tena. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(3) na 14 (48) za Ligi Daraja la Pili.


Unakumbushwa kuwa Ligi Daraja la Pili inaendeshwa kwa kuzingatia Kanuni husika, na ni matarajio yangu kuwa ukiwa mtendaji mkuu wa klabu utakuwa mstari wa mbele kuhakikisha kanuni hizo zinafuatwa kikamilifu.



ONYO KALI KWA KLABU YA REHA



Kamati ya Bodi ya Ligi ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi katika kikao chake kilichopita ilipitia taarifa na matukio mbalimbali ya Ligi Kuu ya Vodacom, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili msimu wa 2017/2018 zinazoendelea hivi sasa.



Katika taarifa hizo imebainika kuwa timu yako iliwakilishwa na viongozi watatu tu katika kikao cha maandalizi (pre match meeting) wakati wa mechi namba 3 ya Kundi A dhidi ya Namungo FC iliyochezwa Septemba 30 mwaka huu Uwanja wa Ilulu mjini Lindi.



Kitendo hicho ni ukiukaji wa Kanuni ya 14(2b) ya Ligi Daraja la Pili. Kwa vile ni kosa la kwanza kwa timu yako msimu huu, Kamati imeipa klabu yako Onyo Kali kwa kuamini kuwa kosa hilo la kikanuni halitajitokeza tena. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(3) ya Ligi Daraja la Pili.



Unakumbushwa kuwa Ligi Daraja la Pili inaendeshwa kwa kuzingatia Kanuni husika, na ni matarajio yangu kuwa ukiwa mtendaji mkuu wa klabu yako utakuwa mstari wa mbele kuhakikisha kanuni hizo zinafuatwa kikamilifu.



ONYO KALI BULYANHULU FOOTBALL CLUB


Kamati ya Bodi ya Ligi ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi katika kikao chake kilichopita ilipitia taarifa na matukio mbalimbali ya Ligi Kuu ya Vodacom, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili msimu wa 2017/2018 zinazoendelea hivi sasa.


Katika taarifa hizo imebainika kuwa timu yako haikuhudhuria katika kikao cha maandalizi (pre match meeting) wakati wa mechi namba 3 ya Kundi D dhidi ya Milambo FC iliyochezwa Oktoba 1 mwaka huu Uwanja wa Mwadui Complex mkoani Shinyanga.


Kitendo hicho ni ukiukaji wa Kanuni ya 14(2a) ya Ligi Daraja la Pili. Kwa vile ni kosa la kwanza kwa timu yako msimu huu, Kamati imeipa klabu yako Onyo Kali kwa kuamini kuwa kosa hilo la kikanuni halitajitokeza tena. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(3) ya Ligi Daraja la Pili.


Unakumbushwa kuwa Ligi Daraja la Pili inaendeshwa kwa kuzingatia Kanuni husika, na ni matarajio yangu kuwa ukiwa mtendaji mkuu wa klabu utakuwa mstari wa mbele kuhakikisha kanuni hizo zinafuatwa kikamilifu.

KOCHA TOTO AFRICANS AZUIWA KUKAA BENCHI



Kocha wa Toto Africans, Almasi Moshi amezuiwa kukaa kwenye benchi la timu yake kutokana na kutokidhi matakwa ya Kanuni ya 72(3) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu benchi la ufundi.
 

Kwa mujibu wa Kanuni hiyo, Kocha Mkuu wa timu ya Ligi Daraja la Kwanza anatakiwa kuwa na Leseni ya chini kuanzia Daraja C ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).


Klabu ya Mvuvumwa FC imepigwa faini ya sh 100,000 (laki moja) kwa kuhudhuria kikao cha maandalizi (pre match meeting) ikiwa na maofisa wawili tu badala ya wanne wakati wa mechi namba 5 ya Kundi A la Ligi Daraja la Kwanza dhidi ya Kiluvya United iliyochezwa Septemba 22 mwaka huu katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.


Adhabu dhidi ya klabu hiyo ni kwa mujibu wa Kanuni ya 14(3) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Taratibu za Mchezo, na kitendo chao cha kuwa pungufu kwenye pre match meeting ni kukiuka Kanuni ya 14(2b) ya Ligi Daraja la Kwanza.


Nayo Toto Africans imepigwa faini ya sh 100,000 (laki moja) kwa kuhudhuria kikao cha maandalizi (pre match meeting) ikiwa na maofisa watatu badala ya wanne wakati wa mechi namba 10 ya Kundi C la Ligi Daraja la Kwanza dhidi ya Transit Camp FC iliyochezwa Septemba 29 mwaka huu katika Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza.


Adhabu dhidi ya klabu hiyo ni kwa mujibu wa Kanuni ya 14(3) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Taratibu za Mchezo, na kitendo chao cha kuwa pungufu kwenye pre match meeting ni kukiuka Kanuni ya 14(2b) ya Ligi Daraja la Kwanza.


JKT Oljoro imepigwa faini ya s 100,000 (laki moja) kwa timu hiyo kufika uwanjani ikiwa imechelewa kinyume na Kanuni ya 14(9) ya Ligi Daraja la Kwanza. Ilifanya kosa hilo kwenye mechi namba 5 ya Kundi la Ligi Daraja la Kwanza katika mechi dhidi ya Pamba iliyofanyika Septemba 23 mwaka huu kwenye Uwanja wa Ushirika mjini Moshi.


Mchezaji Hussein Nyamandulu wa Transit Camp amesimamishwa kucheza wakati akisubiri suala lake la kufanya vurugu kwenye benchi la Toto African kusikilizwa na Kamati ya Nidhamu ya TFF.


Nyamandulu aliyekuwa amevaa jezi namba 10 alifanya vurugu hizo baada ya mechi dhidi ya Toto Africans iliyofanyika Septemba 29 mwaka huu kwenye Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza kumalizika. Mchezaji huyo amesimamishwa kwa mujibu wa Kanuni ya 9(5) ya Ligi Daraja la Kwanza.


Timu ya Polisi Dar imepigwa faini ya sh. 100,000 (laki moja) kwa kutohudhuria kikao cha maandalizi (pre match meeting) wakati wa mechi yao namba 7 dhidi ya KMC iliyofanyika Septemba 24 mwaka huu Chamazi Complex, Dar es Salaam.

Kitendo hicho ni kinyume na Kanuni 14(2) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Taratibu za Mchezo, na adhabu dhidi yao imetolewa kwa mujibu wa Kanuni ya 14(3) ya Ligi Daraja la Kwanza.

Kamati ya Bodi ya Ligi ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi katika kikao chake kilichopita ilipitia taarifa mbalimbali za Ligi Kuu ya Vodacom na Ligi Daraja la Kwanza msimu wa 2017/2018 zinazoendelea hivi sasa.

Dodoma FC imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na timu hiyo kuonesha vitendo vinavyoashiria ushirikina kwa kumwaga vitu kwenye mlango wa kuingilia uwanjani, na pia golikipa namba pili aliweka kitu golini.

Timu hiyo ilifanya vitendo hivyo kabla ya mechi ya Ligi Daraja la Kwanza dhidi ya Biashara United Mara iliyochezwa Septemba 23 mwaka huu kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma.Adhabu yao ni kwa mujibu wa Kanuni ya 42(1) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Klabu.

Mwamuzi Youngman Malagila ameondolewa kwenye ratiba ya waamuzi wa Ligi Daraja la Kwanza kutokana na kuchezesha chini ya kiwango mechi kati ya Rhino Rangers FC na JKT Oljoro FC ya Arusha iliyofanyika Septemba 30, 2017 katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.

Uamuzi dhidi ya Mwamuzi huyo umezingatia Kanuni ya 38(5) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Waamuzi. Hivyo, amerejeshwa kwenye Kamati ya Waamuzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa hatua zingine.

Nao waamuzi Steven Patrick (Mwamuzi wa Kati) na Msaidizi wake Adrian Kalisa wameondolewa kuchezesha Ligi Daraja la Kwanza kutokana na kuchezesha chini ya kiwango mechi kati ya Pamba na Biashara United Mara iliyofanyika Oktoba 2, 2017 katika Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza.

Uamuzi dhidi ya Mwamuzi huyo umezingatia Kanuni ya 38(5) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Waamuzi. Alama walizopata waamuzi hao kwenye mechi namba 12 haziwaruhusu kuchezesha Ligi hiyo.