KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, October 13, 2017

MALALAMIKO YA PEPSI YAMEKATALIWA



Malalamiko ya Pepsi dhidi ya Madini kuwa timu hiyo ilimtumia mchezaji Shabani Imamu kwenye mechi yao ya Ligi Daraja la Pili (SDL) iliyochezwa Septemba 30 mwaka huu Uwanja wa  Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini wakati akiwa na adhabu ya kutumikia kadi nyekundu yamekataliwa.

Kamati imebaini kuwa mchezaji huyo alishatumikia adhabu ya kukosa mechi moja wakati wa mchezo wa SDL kati ya Madini na JKT Oljoro uliochezwa Februari 6 mwaka huu.

Mchezaji huyo alioneshwa kadi ya pili ya njano msimu uliopita kwenye mechi kati ya Madini na AFC iliyofanyika Januari 31 mwaka huu, na kukosa mechi moja iliyofuata kati ya Madini na JKT Oljoro ya Februari 6 mwaka huu, hivyo kuwa halali kwenye mechi ya Pepsi na Madini iliyochezwa Septemba 30 mwaka huu.

Kocha Msaidizi wa Area C United, Omarooh Omari amesimamishwa kukaa kwenye benchi la timu yake wakati akisubiri suala lake la kumpiga kiwiko mchezaji wa Nyanza FC kusikilizwa na Kamati ya Nidhamu ya TFF.


Alimpiga kiwiko mchezaji wa Nyanza, Rajab Adam alipokuwa akikimbilia mpira uliopita karibu yake. Pia dakika ya 78 alianzisha tena vurugu na Mwamuzi kumtoa kwenye benchi la ufundi lakini aligoma kutoka hadi alipotolewa na askari polisi.


Alifanya vitendo hivyo vya utovu mkubwa wa nidhamu wakati wa mechi kati ya Ligi Daraja la Pili kati ya timu yake na Nyanza iliyochezwa Oktoba 1 mwaka huu kwenye Uwanja wa Nyerere uliopo Mbulu mkoani Manyara.

Uamuzi wa kumsimamisha umefanywa kwa kutumia Kanuni ya 9(5) ya Ligi Daraja la Pili.



KUSIMAMISHWA MCHEZAJI JOHN BARAKA WA AREA C



Kamati ya Bodi ya Ligi ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi katika kikao chake kilichopita ilipitia taarifa na matukio mbalimbali ya Ligi Kuu ya Vodacom, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili msimu wa 2017/2018 zinazoendelea hivi sasa.



Katika taarifa hizo imebainika kuwa mchezaji wako John Baraka jezi namba 2 alioneshwa kadi nyekundu baada ya mchezo kumalizika kwa kumpiga ngumi mwamuzi ngumi ya mgongoni.



Alifanya kitendo hicho kwenye mechi namba 1 ya Kundi D la Ligi Daraja la Pili kati ya timu yako na Nyanza FC iliyofanyika Oktoba 1 mwaka huu kwenye Uwanja wa Nyerere uliopo Mbulu mkoani Pwani.



Kwa vile suala lake ni la kinidhamu, na kwa kutumia Kanuni ya 9(5) ya Ligi Daraja la Kwanza, Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi imemsimamisha kucheza mechi za SDL hadi suala lake litakaposikilizwa na Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).



Mchezaji wako atafahamishwa siku ambayo kikao cha Kamati ya Nidhamu kitafanyika kusikiliza shauri dhidi yake ambapo pia atapata fursa ya kuwasilisha utetezi wake kama upo.



ONYO KALI KWA MKAMBA RANGERS


Kamati ya Bodi ya Ligi ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi katika kikao chake kilichopita ilipitia taarifa na matukio mbalimbali ya Ligi Kuu ya Vodacom, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili msimu wa 2017/2018 zinazoendelea hivi sasa.


Katika taarifa hizo imebainika kuwa timu yako haikuhudhuria katika kikao cha maandalizi (pre match meeting), na pia ilichelewa kufika uwanjani wakati wa mechi namba 3 ya Kundi C dhidi ya Boma FC iliyochezwa Septemba 30 mwaka huu Uwanja wa Mwakangale uliopo Kyela mkoani Mbeya.


Kitendo hicho ni ukiukaji wa Kanuni ya 14(2a) na Kanuni ya 14(9) za Ligi Daraja la Pili. Kwa vile ni kosa la kwanza kwa timu yako msimu huu, Kamati imeipa klabu yako Onyo Kali kwa kuamini kuwa kosa hilo la kikanuni halitajitokeza tena. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(3) na 14 (48) za Ligi Daraja la Pili.


Unakumbushwa kuwa Ligi Daraja la Pili inaendeshwa kwa kuzingatia Kanuni husika, na ni matarajio yangu kuwa ukiwa mtendaji mkuu wa klabu utakuwa mstari wa mbele kuhakikisha kanuni hizo zinafuatwa kikamilifu.



ONYO KALI KWA KLABU YA REHA



Kamati ya Bodi ya Ligi ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi katika kikao chake kilichopita ilipitia taarifa na matukio mbalimbali ya Ligi Kuu ya Vodacom, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili msimu wa 2017/2018 zinazoendelea hivi sasa.



Katika taarifa hizo imebainika kuwa timu yako iliwakilishwa na viongozi watatu tu katika kikao cha maandalizi (pre match meeting) wakati wa mechi namba 3 ya Kundi A dhidi ya Namungo FC iliyochezwa Septemba 30 mwaka huu Uwanja wa Ilulu mjini Lindi.



Kitendo hicho ni ukiukaji wa Kanuni ya 14(2b) ya Ligi Daraja la Pili. Kwa vile ni kosa la kwanza kwa timu yako msimu huu, Kamati imeipa klabu yako Onyo Kali kwa kuamini kuwa kosa hilo la kikanuni halitajitokeza tena. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(3) ya Ligi Daraja la Pili.



Unakumbushwa kuwa Ligi Daraja la Pili inaendeshwa kwa kuzingatia Kanuni husika, na ni matarajio yangu kuwa ukiwa mtendaji mkuu wa klabu yako utakuwa mstari wa mbele kuhakikisha kanuni hizo zinafuatwa kikamilifu.



ONYO KALI BULYANHULU FOOTBALL CLUB


Kamati ya Bodi ya Ligi ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi katika kikao chake kilichopita ilipitia taarifa na matukio mbalimbali ya Ligi Kuu ya Vodacom, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili msimu wa 2017/2018 zinazoendelea hivi sasa.


Katika taarifa hizo imebainika kuwa timu yako haikuhudhuria katika kikao cha maandalizi (pre match meeting) wakati wa mechi namba 3 ya Kundi D dhidi ya Milambo FC iliyochezwa Oktoba 1 mwaka huu Uwanja wa Mwadui Complex mkoani Shinyanga.


Kitendo hicho ni ukiukaji wa Kanuni ya 14(2a) ya Ligi Daraja la Pili. Kwa vile ni kosa la kwanza kwa timu yako msimu huu, Kamati imeipa klabu yako Onyo Kali kwa kuamini kuwa kosa hilo la kikanuni halitajitokeza tena. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(3) ya Ligi Daraja la Pili.


Unakumbushwa kuwa Ligi Daraja la Pili inaendeshwa kwa kuzingatia Kanuni husika, na ni matarajio yangu kuwa ukiwa mtendaji mkuu wa klabu utakuwa mstari wa mbele kuhakikisha kanuni hizo zinafuatwa kikamilifu.

No comments:

Post a Comment