KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, October 2, 2017

TANZANITE YAPIGWA 6-0 NA NIGERIA


TIMU ya soka ya Taifa ya Wanawake ya vijana wa chini ya umri wa miaka 17, Tanzanite, imetupwa nje ya michuano ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia baada ya kupigwa mweleka wa mabao 6-0 na Nigeria.

Katika mechi hiyo iliyochezwa jana kwenye Uwanja wa Azam Complex, Nigeria ilikwenda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 4-0.

Kipigo hicho kimeifanya Tanzanite itolewe nje ya michuano hiyo kwa jumla ya mabao 9-0. Katika mechi ya awali iliyochezwa wiki mbili zilizopita mjini Lagos, Tanzanite ilichapwa mabao 3-0.

No comments:

Post a Comment