KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, October 22, 2017

SIMBA YAIPA KISAGO MJI NJOMBE



SIMBA jana iliendelea kuchanja mbuga katika kuwania ubingwa wa ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara baada ya kuicharaza Mji Njombe mabao 4-0.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, mabao ya Simba yalifungwa na Muzamir Yassin, aliyetupia mabao mawili, Emmanuel Okwi na Laudit Mavugo.

Kwa matokeo hayo, Simba bado ipo kileleni mwa ligi hiyo, ikiwa na pointi 15, sawa na Mtibwa Sugar, lakini zinatofautiana kwa mabao ya kufunga na kufungwa.

Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena leo wakati Yanga itakapomenyana na Stand United kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.


No comments:

Post a Comment