KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, October 29, 2017

SIMBA, YANGA ZASHINDWA KUTAMBIANA


Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania mzunguko wa nane imeendelea tena kwa mchezo mmoja uliowakutanisha watani wa Jadi nchini Simba na Yanga ambapo timu hizo zimetoshana nguvu ya kugawana alama moja moja baada ya kufungana goli 1-1 kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.

Wakicheza kwa kujiamini vijana wa Lwandamina walionekana kutengeneza nafasi nyingi za kufunga kuliko vinara wa Ligi Simba huku timu zote zikicheza kwa kuogopana hali ambayo ilipelekea timu hizo kwenda mapumziko zikiwa hazijafungana.

Kipindi cha pili timu zote zilifanya mabadiliko mbalimbali hata hivyo hayakuweza kuwa na manufaa kwa pande zote kwani Yanga waliingia wakiwa na hofu ya kukosa baadhi ya nyota wake muhimu ambao wapo katika majeruhi Thabani Kamusoko,Donald Ngoma na Amis Tambwe.

Simba walikuwa wa kwanza kuapata goli kupitia kwa winga matata Shiza Ramadhani Kichuya dakika ya 57 baada ya krosi ya Emanuel Okwi kupanguliwa na golikipa wa Yanga na uzembe wa Papy Kabamba Tshishimbi ulioweza kumuacha Kichuya aliyemtungua Youthe Rostand.

Baada ya kuingia kwa goli hilo Yanga walijipanga na kuendeleza mashambulizi kwa Simba na dakika ya 60 wachezaji Ajibu na Mwashiuya waligogeana na kutoa pasi kwa Mshambuliaji matata ambaye alikuwa mwiba kwa wekundu wa Msimbazi,Obrey Chirwa na kuisawazishia Yanga.

Hadi mwamuzi wa Kimataifa Heri Sasii anapuliza kipyenga cha mwisho Yanga na Simba wamegawana pointi moja moja na kwa matokeo hayo Simba wanarudi katika nafasi yao ya kwanza kwa kufikisha pointi 16 sawa na Yanga na Azam huku yeye akiwa na uwiano mzuri wa magoli ya kufungwa na kufunga.

No comments:

Post a Comment