Sunday, June 3, 2012

AZAM YAANIKA SILAHA ZAKE ZA MSIMU WA 2012/2013

Kikosi kamili cha Azam FC kwa ajili ya msimu ujao wa ligi wa 2012/2013 ni kama ifuatavyo:

Magolikipa ni Mwadini Ally, Deo Munishi 'Dida' Aishi Salum na Jackson Wandwi.

Mabeki wa pembeni kulia ni Ibrahim Shikanda na Erasto Nyoni na kushoto ni
Waziri Salum na Samih Haji Nuhu.

Mabeki wa kati ni Luckson Kakolaki, Said Moradi, Joseph Owino na Aggrey
Morris.

Viungo ni Kipre Bolou, Abdulhalim Humud, Himid Mao, Salum Abubakar,
Abdi Kassim Sadala, Ramadhani Selemani Chombo, Abdulghani Ghulam,
Ibrahim Rajab Jeba, Jabir Aziz Stima na Ibrahim Joel Mwaipopo.

Washambuliaji wa pembeni ni Kipre Tchetche, Mrisho Ngasa, Zahoro Pazi,
Khamis Mcha na George Odhiambo 'Blackberry'.

Washambuliaji wa kati ni Gaudence Mwaikimba na mchezaji bora wa Azam FC,

John Raphael Bocco
"Adebayor"

FLOYD MAYWEATHER AANZA KUTUMIKIA KIFUNGO CHA MIEZI MITATU

Bondia Floyd Mayweather leo ameanza kifungo cha miezi 3 jela
alichohukumiwa mwezi Desemba mwaka jana kutokana na kuvunja sheria kwa
kufanya ugomvi. Wakati akielekea Jela Mayweather alisindikizwa na rafiki yake
kipenzi mwanamuziki 50 Cent.


Mayweather akitiwa pingu na polisi kuelekea kwenye karandinga.

"Nenda dogo nitakumiss kaka yako" 50 Cent na Mayweather.

Hiki ndio chumba atakachokaa Mayweather kwa miezi 3

Hizi ndio sare zake kwa kipindi chote atakachokaa jela.

Buya atwaa taji la Miss Manyara 2012

Mshindi wa taji la Redds Miss Manyara 2012, Buya Ernesi (katikati) akiwa na mshindi wa pili Dalina Sikawa (kushoto) na mshindi wa tatu, Lucy Stephano mara baada ya kutangazwa kwa matokeo ya mshindi wa taji hilo usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa CCM mjini
Babati.

Lightness ndiye Miss Dodoma 2012

Mshindi wa taji la Redd's Miss Dodoma 2012, Lightness Michael (katikati)
akiwa katika picha ya pamoja na mshindi wa pili, Berinda Mdogo (kulia) na
mshindi wa tatu Nulsa Magambo mara baada ya kumalizika kwa shindano hilo

usiku wa kuamkia leo.

Taifa Stars yachapwa 2-0 na Ivory Coast

Mshambuliaji Didier Drogba wa Ivory Coast akijiandaa kutuliza mpira huku akiwa amezongwa na beki Kevin Yondan wa Taifa Stars.

Mshambuliaji Mbwana Samatta wa Taifa Stars akiruka hewani kupiga mpira kwa kichwa sambamba na beki wa Ivory Coast.

Moja ya kosa kosa zilizotokea kwenye lango la Ivory Coast wakati timu hiyo ilipomenyana na Taifa Stars jana.

Shaaban Nditi (kushoto) wa Taifa Stars akijaribu kumshibiti Solomon Kalou wa Ivory Coast.

TIMU ya soka ya Taifa,Taifa Stars jana ilipigwa mweleka wa mabao 2-0 na Ivory Coast katika mechi ya michuano ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia za 2014.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye uwanja wa Felix Houphouet-Boigny mjini Abidjan, Ivory Coast ilijipatia mabao hayo mawili, moja katika kila kipindi.

Bao la kwanza lilifungwa na Salomon Kalou katika kipindi cha kwanza kabla ya Didier Drogba kuongeza la pili katika kipindi cha pili.

Taifa Stars ililazimika kumaliza mchezo huo ikiwa na wachezaji 10 baada ya beki wake, Aggrey Morris kutolewa nje kwa kadi nyekundu na mwamuzi Slim Jedidi kutoka Tunisia kwa kosa la kucheza rafu mbaya.

Katika mechi hiyo, Kocha Kim Poulsen wa Taifa Stars alilazimika kufanya mabadiliko ya wachezaji wawili kutoka katika kikosi alichokichezesha katika mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya Malawi iliyochezwa Mei 26 mwaka huu.

Kim aliamua kumchezesha Amir Maftah katika nafasi ya beki wa kushoto badala ya Waziri Salum na pia alimchezesha Mrisho Ngasa katika nafasi ya mshambuliaji wa kati badala ya Haruna Moshi, ambaye hakwenda Ivory Coast kutokana na kuwa majeruhi.

Friday, June 1, 2012

Taifa Stars ikiwa mazoezini Abidjan



Wachezaji wa timu ya Soka ya Taifa, Taifa Stars wakijifua kwenye Uwanja wa kituo cha michezo mjini Abidjan juzi kwa ajili ya kujiandaa na mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Ivory Coast inayotarajiwa kufayika kesho kwenye uwanja wa Felix Houphouet-Boigny.(Picha kwa hisani ya Bongostaz)

Mrembo wa Nyamagana kupatikana leo

Cecy

Brenda

Amina

Aisha

Shindano la kumsaka mrembo wa kitongoji cha Nyamagana, atakayeshiriki katika shindano la kumsaka mrembo wa Mwanza anatarajiwa kujulikana leo usiku.

Shindano hilo linalotarajiwa kuwashirikisha warembo kadhaa wa kitongoji hicho, limepangwa kufanyika kwenye ukumbi wa Gold Crest.

Shindano hilo limeandaliwa na Kampuni ya Stoppers Entertainment ya Mwanza na kutakuwepo na burudani mbalimbali kutoka kwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya, akiwemo Linah na Hafsa Kazinja.

Mshereheshaji mkuu wa shindano hilo atakuwa msanii maarufu wa kundi la Orijino Komedi, Emmanuel Mgaya almaarufu zaidi kwa jina la Masanja Mkandamizaji.