KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, November 12, 2017

35 WATEULIWA KUUNDA KILIMANJARO WARRIORS


Benchi la Ufundi la timu za taifa za vijana, limeita wachezaji 35 kwa ajili ya kambi yenye lengo la mchujo kutafuta kikosi imara cha timu ya taifa ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 23 maarufu kwa jina la Kilimanjaro Warriors.

Kocha Msaidizi wa timu hizo, Oscar Mirambo alitangaza majina hayo leo Novemba 03, mwaka huu huku amesema: “Tunataka vijana wasiozidi 25 kwenye kikosi. Tutawapata kwenye kambi hii ya siku 10 inayoanza tarehe 5, mwezi huu wa 11.”

Kocha Msaidizi wa timu hizo, Oscar Mirambo alitangaza majina hayo leo Novemba 03, mwaka huu huku akisema: “Tunataka vijana wasiozidi 25 kwenye kikosi. Tutawapata kwenye kambi hii ya siku 10 inayoanza tarehe 5, mwezi huu wa 11.”

Wachezaji aliowaita ni makipa Metacha Mnata (Azam FC), Joseph Ilunda (JKT Ruvu), Liza Mwafwea (Tanzania Prisons).

Wengine ni Cleotas Sospter (Yanga); Idrissa Mohammed, Bakari Kijuji (Yanga), Joseph Prosper (Azam), Masoud Abdallah (Azam), William (Ruvu Shooting), Yussuph Mhilu (Yanga), Adam Salamba (Stand United), Omary Mponda (Ndanda) na Stanley Angeso (Stand United).

Pia wamo Eliud Ambokire (Mbeya City), Emmanuel Kakuti (Mbeya City), Medson Mwakatunde (Mbeya City), Daruweshi Shaliboko (Ashanti Unted), Abbas Kapombe (Azam/Ndanda), Ismail Aidan (Mtibwa Sugar), Salum Kihimbwa (Mtibwa Sugar), Hassan Mganga (Mtibwa Sugar) na Award Salum (Njombe Mji).

Wengine Awesu Ally (Mwadui), Salum Chuku (Singida United), Yahya Zayd (Azam), Emmanuel Martin (Yanga), Geofrey Mwashiuya (Yanga), Ayoub Masoud (Ndanda), Baraka Majogoro (Ndanda), Mohammed Habib (Miembeni), Yussuf Mlipili (Simba), Agathon Mapunda (Njombe Mji), Faisal Abdallah (JKU) na Yussuph Kagoma (Singida United).

No comments:

Post a Comment