KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, November 12, 2017

TFF YAENDESHA MAFUNZO VYUONI SOKA YA UFUKWENI


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litatoa mafunzo ya soka la ufukweni (Beach Soccer) kwa vyuo mbalimbali hapa nchini vilivyothibitisha kushiriki Ligi Maalumu ya soka la Ufukweni itakayoanza Novemba 18, 2017.

Kwa upande wa mafunzo ni kwamba yatafanyia siku tano kabla ya kuanza kwa ligi hiyo ambako itakuwa ni Novemba 13, mwaka hu. TFF imepanga kutoa mafunzo hayo kwa vyuo hivyo ili wauelewe zaidi mchezo huo pamoja na sheria zake.

Tumepeleka mchezo huo kwenye vyuo ili kutoa hamasa ya soka la ufukweni kuenea zaidi na kuweka hazina ya wachezaji wa timu ya taifa.

Mpaka sasa vyuo 14 tayari vimethibitisha kimaandishi kushiriki kwenye mafunzo hayo.

Vyuo vilivyothibitisha kushiriki ni Chuo cha Ardhi, Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Chuo Cha Ufundi (DIT), Chuo cha Usafirishaji (NIT), Chuo cha Elimu ya Tiba cha Kahiruki, Chuo cha Elimu ya Biashara cha Lisbon, Chuo cha Silva , Chuo UAUT, TIA, El-Maktoum collage Engineering, Magogoni, Chuo cha uandishi wa habari DSJ na TSJ.

Mafunzo hayo yatatanguliwa na tukio la kukutana na viongozi wa vyuo shiriki hapo Novemba 10, 2017.

Wakati huo huo kozi ya waamuzi wa Soka la Soka la Ufukweni imeanza leo Novemba 7, 2017 katika Makao Makuu ya TFF Karume, Dar es Salaam ambayo yanatarajiwa kumalizika Novemba 12, 2017.

TFF YASIMAMISHA MCHEZO WA FORODHANI v AMBASSODOR

Wakati mchezo wa TFF ikisimamisha mchezo wa Azam Sports Federation Cup kati ya Forodhani FC ya Mara na Ambassodor ya Kahama, Mchezo wa Bulyanhulu na Area C, sasa utafanyika kesho Jumatano Novemba 8, mwaka huu kwenye Uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga.

Mchezo kati ya Forodhani FC ya Mara na Ambassodor ya Kahama, umesimamishwa kusubiri uamuzi wa Kamati ya Mashindano baada ya Baruti ambayo imelete malalamiko kuhusu nafasi yake.

Mbali ya mchezo kati ya Bulyanhulu na Area C, mechi nyingine za kesho Jumatano, Novemba 8 zitakuwa ni kati ya Cosmopolitan na Abajalo kwenye Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani wakati makumba Rangers watacheza na Green Warriors kwenye Uwanja wa Bandari, Dar es Salaam.

AFC ya Arusha itaikaribisha Nyanza FC kwenye Uwanja wa Ushirika; Boma Fc na African Sports watacheza kwenye Uwanja wa Ushirika; huku Motochini ikicheza na Ihefu wakati Stand Misuna watacheza na Madini ilihali Burkina FC itaialika Mbinga United kadhalika Mkamba Rangers itacheza na Makambako FC kwenye Uwanja wa Sabasaba.

No comments:

Post a Comment