KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, January 27, 2018

AZAM, YANGA KUPIGWA SAA 10 CHAMAZI



Mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2017/2018 kati ya Azam FC na Young Africans utachezwa saa 10 jioni Azam Complex Chamazi.

Mchezo huo namba 115 utachezwa Jumamosi Januari 27, 2018.

Viingilio kwenye mchezo huo ni shilingi elfu kumi(10,000) kwa Jukwaa Kuu na shilingi elfu saba (7,000) kwa majukwaa ya kawaida.

Waamuzi wa mchezo huo wote ni kutoka Dar es Salaam ambapo muamuzi wa kati ni Israel Nkongo akisaidiwa na mwamuzi msaidizi namba moja Josephat Bulali na mwamuzi msaidizi namba mbili Soud Lila, mwamuzi wa akiba Elly Sasii wakati Kamishna wa mchezo huo ni Omar Abdulkadir.

MCHEZO WA MWADUI VS NJOMBE MJI WASOGEZWA

Mchezo namba 114 kati ya Mwadui FC ya Shinyanga na Njombe Mji ya Njombe uliokuwa ufanyike Ijumaa Januari 26, 2018 imesogezwa kwa siku moja kupisha mazishi ya aliyekuwa kocha msaidizi wa Mwadui Jumanne Ntambi.

Mchezo huo sasa utachezwa Jumamosi, Januari 27, 2018.

Kocha huyo msaidizi wa Mwadui alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu kabla ya kufikwa na mauti.

CAF YATAJA WAAMUZI WATAKAOCHEZESHA MECHI YA YANGA NA SAINT LOUIS FC LIGI YA MABINGWA

Shirikisho la Mpira wa miguu Barani Africa CAF limetaja waamuzi watakaochezesha mchezo wa kwanza na mchezo wa pili wa Ligi ya mabingwa Africa kati ya Yanga ya Tanzania dhidi ya Saint Louis FC ya Seychelles.

Mchezo wa kwanza utachezwa Februari 10, 2018 uwanja wa Taifa na utachezeshwa na waamuzi kutoka Ethiopia na Kamishna wa mchezo akitokea nchini Namibia.

Mwamuzi wa kati atakuwa Belay Tadesse Asserese akisaidiwa na mwamuzi msaidizi namba moja Tigle Gizaw Belachew na mwamuzi msaidizi namba mbili Kinfe Yilma Kinfe wakati mwamuzi wa akiba atakuwa Amanuel Heleselass Worku na Kamishna Frans Vatileni Mbidi.

Mechi ya pili itakayochezwa Seychelles kati ya Februari 20 na 21,2018 itachezeshwa na waamuzi kutoka Madagascar na kamishna atatoka Mauritius.

Mwamuzi wa kati atakuwa Andofetra Avombitana Rakotojaona akisaidiwa na mwamuzi msaidizi namba moja Lionel Hasinjarasoa Andrianantenaina na mwamuzi msaidizi namba mbili Pierre Jean Eric Andrivoavonjy na mwamuzi wa akiba Hamada el Moussa Nampiandraza,kamishna wa mchezo huo Ahmad Nazeer Hossen Bowud.

WAAMUZI WA SUDAN KUSINI KUCHEZESHA SIMBA VS GENDARMERIE TNALE KOMBE LA SHIRIKISHO AFRICA

Waamuzi kutoka Sudan Kusini wameteuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Africa CAF kuchezesha mchezo wa kombe la Shirikisho kati ya Simba ya Tanzania na Gendarmerie Tnale ya Djobouti itakayochezwa Februari 21,2018 Uwanja wa Taifa.

Mwamuzi wa kati atakuwa Alier Michael James akisaidiwa na mwamuzi msaidizi namba moja Abdallah Suleiman Gassim ,mwamuzi msaidizi namba mbili Gasim Madir Dehiya wakati mwamuzi wa akiba akiwa ni Kalisto Gumesi Simon Samson na Kamishna wa mchezo huo kutoka Botswana ni Mmonwagotlhe Edwin Senai.

Mchezo wa marudiano utakaochezwa Djibouti kati ya Februari 20 na 21,2018 wenyewe utachezeshwa na waamuzi kutoka Burundi na Kamishna wa mchezo atatokea nchini Rwanda.

Mwamuzi wa kati ni Eric Manirakiza akisaidiwa na mwamuzi msaidizi namba moja Pascal Ndimunzigo,mwamuzi msaidizi namba mbili Willy Habimana,mwamuzi wa akiba Pacifique Ndabihawenimana na kamishna Gaspard Kayijuka.

WATANZANIA TISA KUCHEZESHA NA KUSIMAMIA LIGI YAMABINGWA NA KOMBE LA SHIRIKISHO AFRICA

 Waamuzi nane kutoka Tanzania wameteuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Africa CAF kuchezesha mechi za Ligi ya Mabingwa Africa na Kombe la Shirikisho.

Waamuzi wanne wameteuliwa kuchezesha mchezo wa Ligi ya mabingwa kati ya Lydia Ludic Burundi Academic ya Burundi na Rayon Sports ya Rwanda.

Mwamuzi Mfaume Ali Nassoro atakuwa mwamuzi wa kati akisaidiwa na mwamuzi msaidizi namba moja Frank John Komba wakati mwamuzi msaidizi namba mbili atakuwa Soud Idd Lila na mwamuzi wa akiba Israel Omusingi Njunwa Mujuni huku kamishna wa mechi hiyo akitokea nchini Zimbabwe Gladmore Muzambi.

Mchezo huo utachezwa kati ya Februari 20 na 21, 2018 nchini Burundi.

Waamuzi wengine wanne wa Tanzania watachezesha mchezo wa Kombe la Shirikisho kati ya Masters Security Services FC ya Malawi dhidi ya Atletico Petroleos de Luanda ya Angola nutakaochezwa kati ya Febriari 20 na 21,2018 nchini Malawi.

Elly Ally Sasii atakuwa mwamuzi wa katikati kwenye mchezo huo akisaidiwa na Mwamuzi msaidizi namba moja Salim Mkono Mohamed na mwamuzi msaidizi namba mbili Ferdinand Chacha na mwamuzi wa akiba Alphonce Mwandembwa Emmanuel wakati kamishna wa mchezo huo atatokea Ethiopia Luleseged Gegashaw Asfaw.

Wakati huo huo Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Africa CAF limemteua Makamu wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF Ndugu Michael Richard Wambura kuwa Kamishna wa mchezo wa Ligi ya Mabingwa Barani Africa kati ya Bidvest Wits ya Africa Kusini na Pamplemousses SC ya Mauritius utakaochezwa Februari 10, 2018 kwenye uwanja wa Johannesburg-Bidvest.

Wambura atasimamia mchezo huo utakaochezeshwa na waamuzi kutokea Seychelles.

Mwamuzi wa kati Nelson Emile Fred akisaidiwa na Hensley Danny Petrousse na James Fedrick Emile wakati mwamuzi wa akiba atakuwa Allister Barra

Huu unakuwa ni muendelezo kwa CAF kuteua viongozi mbalimbali wa Tanzania kuwa makamishna wa mechi zinazoandaliwa na Shirikisho hilo.

Tayari Rais wa TFF Ndugu Wallace Karia licha ya kuteuliwa kuwa mmoja wa wajumbe wa kamati ya maandalizi ya fainali za Africa kwa wachezaji wanaocheza ndani CHAN pia ameteuliwa mara mbili kuwa Kamishna wa mechi ya ufunguzi ya CHAN wenyeji Morocco walipocheza dhidi ya Mauritania Februari 13, 2018 na mchezo mwingine uliowakutanisha Namibia na Zambia uliochezwa Februari 22, 2018

Aidha mjumbe mwingine wa kamati ya utendaji Ahmed Iddi Mgoyi naye ameteuliwa na CAF kuwa kamishna wa mchezo wa Kombe la Shirikisho kati ya AFC Leopards ya Kenya dhidi ya Fosa Juniors ya Madagascar mchezo utakaochezwa kati ya Februari 9,10 na 11,2018 nchini Kenya.