KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, December 29, 2012

KESI YA LULU YASAJILIWA RASMI MAHAKAMA KUU



JALADA la kesi ya kuua bila kukusudia la msanii nyota wa filamu nchini, Elizabeth Michael 'Lulu' tayari limetua Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na kesi yake imesajiliwa.

Lulu anakabiliwa na mashtaka ya kumuua bila kukusudia, aliyekuwa msanii maarufu wa fani hiyo nchini, Steven Kanumba kinyume cha kifungu cha 195 cha Kanuni za Adhabu.

Awali, kesi hiyo ilifunguliwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa ajili ya kukamilisha hatua za awali ukiwamo upeelelezi, huku akikabiliwa na shtaka la mauaji ya kukusudia kinyume cha kifungu cha 196.

Hata hivyo, baada ya kukamilika kwa upelelezi, Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), alimbadilishia mashtaka na kuwa ya kuua bila kukusudia.

Desemba 21, 2012, Lulu alisomewa maelezo ya kesi, yakiwemo ya mashahidi watakaotoa ushahidi dhidi yake na maelezo yake aliyoyatoa polisi, kisha Mahakama ya Kisutu ilifunga rasmi kesi hiyo na kutamka rasmi kuihamishia Mahakama Kuu, ambako ndiko itakakosikilizwa.

Habari zilizopatikana Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam jana zilisema kuwa, tayari kesi hiyo imeshapokelewa mahakamani hapo na kupewa usajili wa shauri la jinai namba 125 mwaka 2012.

Hata hivyo, habari hizo zilisema kuwa kwa sasa kesi hiyo inasubiri kupangiwa Jaji atakayeisikiliza baada ya taratibu zote za kimahakama kukamilika, kwa tarehe itakayopangwa na msajili kulingana na ratiba ya vikao vya mahakama hiyo.

Lulu anadaiwa kumuua Kanumba bila kukusudia, Aprili 7, 2012, nyumbani kwake Sinza Vatican, Dar es Salaam. Wakati akisoma maelekezo ya kesi hiyo, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Shadrack Kimaro alidai kuwa, upande wa mashtaka utawaita jumla ya mashahidi tisa.

Wakili Kimaro pia alidai kuwa, upande wa mashtaka utawasilisha mahakamani vielelezo kadhaa vitakavyotumika kama sehemu ya ushahidi katika kesi hiyo, ikiwamo ramani ya eneo la tukio kwenye chumba alimofia Kanumba, ripoti ya uchunguzi wa kifo na maelezo ya onyo la Lulu.

Wakili Kimaro alidai kuwa, Aprili 7, 2012, Lulu alitoa maelezo ya onyo, kuhusiana na tuhuma zinazomkabili, katika kituo cha polisi cha Oysterbay, yaliyochukuliwa na askari wa kituo hicho, mpelelezi Sajenti Renatus.

Kwa mujibu wa maelezo hayo ya onyo, Lulu alizaliwa mwaka 1994 na alimaliza kidato cha nne katika shule ya sekondari Midway na kwamba baada ya hapo, aliendelea na shughuli za sanaa kuanzia mwaka 2000.

GAZETI LA MWANANCHI DES 29, 2012

Friday, December 28, 2012

YANGA YATANGAZA WANAOKWENDA UTURUKI J'PILI


Kikosi cha Young Africans Sports Club, mabingwa mara mbili mfululizo wa michuano ya klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati, al maarufu (Kagame Cup )timu ya Young Africans inatarajia kuondoka alfajiri ya Jumapili kwenda Uturuki ambako itaweka kambi ya mazoezi kwa muda wa wiki mbili.

Akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu ya Yanga mitaa ya Twiga/Jangwani, Afisa Habari wa klabu ya Yanga Baraka Kizuguto amesema timu itaondoka alfajiri ya Jumapili kwa shirika la ndege la Turkish Airline, ambapo itakuwa na msafara wa watu 34, wachezaji 27 na viongozi 7.

Timu itaondoka majira ya saa 10:30 alfajiri na itafika katika mji wa Instabul majira ya saa 5 kasoro dakika 10, kisha baadae majira ya saa 9 alasiri itaondoka kwenda katika mji wa Antalya uliopo kusini mwa nchi ya Uturuki ambapo itafika saa 10 na hapo ndipo haswa itakapokuwa kambi ya timu alisema 'Kizuguto'

Kizuguto amesema timu itafikia katika hotel ya Sueno Beach iliyopo pembezoni mwa bahari ya Meditreanian, na itakua ikifanya mazoezi katika viwanja vikubwa viwili vilivyopo katika hotel hiyo na kiwanja kidogo cha nyasi bandia.

Majina ya watakosafiri keshokutwa alfajri ni:

Walinda Mlango: Ally Mustafa 'Barthez', Said Mohamed na Yusuph Abdul

Walinzi wa Pemebeni: Juma Abdul, Shadrack Nsajigwa, Godfrey Taita, Stephano Mwasika na Oscar Joshua

Walinzi wa kati: Mbuyu Twite, Nadir Haroub, Ladisalus Mbogo na Kelvin Yondani

Viungo: Athumani Idd, Frank Domayo, Haruna Niyonzima, Kabange Twite, Nurdin Bakari na Omega Seme

Viungo wa Pembeni: Saimon Msuva, Rehani Kibingu, Nizar Khalfani na David Luhende

Washambuliaji: Didier Kavumbagu, Said Bahanunzi, Jerson Tegete, George Banda na Hamis Kiiza

Viongozi watakaoambatana na timu hiyo ni
Kocha Mkuu: Ernest Brandts,
Kocha msaidizi: Fred Felix Minziro,
Kocha wa makipa: Razaki Siwa,
Daktari wa timu: Dr.Suphian Juma,
Meneja wa timu: Hafidh Saleh,
Afisa wa Habari : Baraka Kizuguto
Kiongozi mkuu wa msafara: Mohamed Nyenge ambae ni mjumbe wa kamati ya utendaji wa klabu ya Yanga

WHITNEY HOUSTON ALIUAWA NA GENGE LA WAUZA UNGA




Medical examiner ruled she accidentally drowned in a hotel bathtub
She had taken cocktail of cocaine, marijuana and prescription drugs
Paul Huebl believes troubled star was targeted by 'high powered' dealers
Says they sent thugs to collect $1.5million debt she owed for drugs
He claims marks on her body look like defensive wounds

Whitney Houston was murdered by drug dealers and a new surveillance video proves it, a Hollywood private investigator is claiming

Paul Huebl says he has turned over evidence to the FBI that shows the 48-year-old singer was killed over a drug debt in February.

The medical examiner ruled that she drowned in her bathtub at the Beverly Hilton hotel after taking a cocktail of cocaine, marijuana and several legal drugs.

The National Enquirer is reporting that Huebl believes the troubled star was targeted by several 'high powered drug dealers who sent thugs to collect a huge debt she owed for drugs.'

She owed $1.5million to dealers, according to some reports.

However, Huebl told MailOnline that he doesn't know for certain that Houston was killed - only that evidence he collected could point in that direction.

He says that the star received a delivery of cocaine to her room the day before her death and could be heard saying, 'I'm tired of this sh*t.'

He says the Houston had previously been subjected to harassment by dealers trying to collect on her debt.

Huebl says he obtained surveillance video that shows two unknown men who repeatedly went to the Beverly Hilton and integrated themselves into Houston's entourage.

The private investigator claims these are the men who may have slipped into Houston's hotel room and killed her.

He also disagrees with the Los Angeles County Coroner's ruling that the star's death was 'accidental.'

'Whitney’s body shows classic defense wounds that would have occurred while she was battling for her life,' he said.

However, Huebl conceded that the marks on her hands and fingernails could have been obtained in some other ways and that they were only 'suspected' defensive wounds.

The private investigator said he also has evidence that Houston's hotel room was ransacked, showing further hints of a violent struggle.

Huebl says he gave his evidence to the Chicago field office of the FBI in the hopes that the agency will open a criminal investigation.

'I think that if you put all these things together, they do kind of spell homicide, with a big red capital "H,"' he told MailOnline.

The FBI did not immediately respond to requests for comment. A message left with Beverley Hills police was not immediately returned.

Heubl, a former Chicago police officer who became an actor after he retired, says he conducted the investigation after being hired by a client who did not believe the official reports on Houston's death.

He believes Beverley Hills police did not fully investigate Houston's death because they did not want to bring the negative attention to Beverly Hills or to the Beverly Hilton.

Huebl would not say who hired him.

PUFFY DIDDY ALA MARAHA NA WANAWE KWENYE YATCH



He says there is only one Diddy man.

But there were plenty of Diddy children as the popular rapper enjoyed a festive break in the Caribbean on Boxing Day.

The family man looked like he was having a great time as he took three of his brood onto his luxurious yacht in St Barts.

The 43-year-old looked full of festive cheer as he marched the youngsters towards the luxury vessel, which is named Oasis.

And the rapper, real name Sean Combs, managed to look effortlessly stylish in a navy T-shirt, baggy trousers, black socks and flip-flops.

To top off his look, and to look even more intelligent than usual, he also wore a trendy pair of tinted spectacles.

Earlier the hip-hop favourite, who previously went by the moniker of Puff Daddy, was spotted indulging himself by sipping champagne and shopping for jewellery.

He chatted with Madonna's manager Guy Oseary as he marched past a crowd of awe-struck holidaymakers.

But he effortlessly switched modes from Diddy to daddy, with the father-of-five looking delighted to be leaving the celebrity rat race behind so he could spend time with his children.

Loving Diddy is known to have a weakness for indulging his youngsters, even buying his 18-year-old son Justin a $360,000 car for his birthday.

However he said he is proud of the way he raises his brood, who he fathered with three different women.

He said: 'I’m very proud about the upbringing, and God has blessed me with three of the most beautiful women to raise my kids.

'And I am – and one day if it’s right, I will get married, but I think it’s more about me being honest with myself, and me loving my children and me being there for my children.'

KLABU ZA LIGI KUU ZAITISHIA NYAU TRA




Klabu 14 ambazo timu zao zinashiriki Ligi Kuu ya Vodacom zimesema hazitacheza hatua ya pili ya Ligi hiyo inayotarajiwa kuanza Januari 26 mwakani hadi zitakaporejeshewa fedha zao zilizochukuliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutoka kwenye moja ya akaunti za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Novemba 23 mwaka huu, TRA kwa uwezo ilionao kisheria iliielekeza benki ya NMB kuilipa fedha hizo (sh. 157,407,968) kutoka kwenye moja ya akaunti za TFF ikiwa ni Kodi ya Lipa Kama Unavyopata (PAYE) kutoka kwenye mishahara ya waliokuwa makocha wa timu za Taifa.

Serikali ndiyo inayolipa mishahara ya makocha hao moja kwa moja kwenye akaunti zao, lakini ilikuwa haikati PAYE kutoka kwenye mishahara hiyo, hivyo malimbikizo kufikia sh. 157,407,968.

TFF bado inaendelea na mazungumzo na pande husika (Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa upande mmoja na TRA kwa upande mwingine) ili fedha hizo zirejeshwe kwani zilitolewa na mdhamini wa Ligi Kuu (kampuni ya Vodacom) kwa ajili ya maandalizi ya timu hizo tayari kwa mzunguko wa pili wa Ligi hiyo.

OFISA WA CAF KUTUA MWAKANI KUKAGUA VIWANJA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) litamtuma nchini ofisa wake Abbas Sendyowa kukagua viwanja na hoteli ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa utaratibu wa klabu kupata leseni zitakazoziwezesha kushiriki michuano inayoandaliwa na Shirikisho hilo.

Ofisa huyo kutoka Uganda atawasili nchini Januari 7 mwakani ambapo anatarajiwa kukamilisha kazi hiyo Januari 14 mwakani na baadaye kupeleka ripoti yake CAF.

Utekelezaji wa kazi yake nchini utahusisha mwakilishi kutoka TFF, mwakilishi kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, mameneja wa viwanja husika na Ofisa Usalama wa TFF.

NAZARIUS KILUNGEJA AONDOLEWA UCHAGUZI RUREFA
Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imekubaliana na uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Rukwa (RUREFA) kumuondoa Nazarius Kilungeja kugombea uenyekiti katika uchaguzi wa chama hicho.

Kutokana na uamuzi huo, Kamati ya Uchaguzi ya TFF imeiagiza Kamati ya Uchaguzi ya RUREFA kuendelea na mchakato wa uchaguzi huo kama ilivyopangwa awali.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

IBF YAMPONGEZA CHEKA KWA KUMDUNDA MMALAWI


Shirikisho la Ngumi la Kimataifa (IBF) limepongeza bingwa mpya wa uzito wa Super Middle katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki yaa Kati, Mtanzania Francis Cheka.

Katika barua yake aliyomtumia Francis Cheka ya tarehe 28/12/2012 Mwenyekiti wa kamati ya Ubingwa wa IBF/USBA Lindsey Tucker alisema "Tunachukua fursa hii kukutakia maisha na mafanikio mazuri kama bingwa wa IBF na kumhimiza kuishi kama bingwa".

Cheka atatakiwa kutetea taji lake katika kipindi cha miezi sita kufikia mwezi wa 6 mwakani dhidi ya mpinzani ambaye ana rekodi ya mapambano yasiyopungua 15 na mengi awe ameyashinda hususan mapambano mawili ya mwisho.

Aidha IBF inampongeza bondia Chiotcha Chimwemwe kutoka Malawi kwa ushupavu wake na ushindani mzuri katika pambano hilo lililofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid katika jiji la Arusha tarehe 26 Desemba, 2012.

Wakati huo huo, bondia kutoka Jamhuri ya watu wa Malawi Chiotcha Chimwemwe alionja machungu ya Mtanzania Francis Cheka katika mpambano wao uliopewa jina na “Vita vya Ziwa Nyasa” tarehe 26 Desemba 2012 siku ya Boxing Day jijini Arusha.

Ulikuwa ni mpambano wa mwaka ambao bondia Francis Cheka nusura aupoteze katika raundi ya pili wakati konde zito la kushoto la kapteni Usu kutoka katika jeshi la jamhuri ya watu wa Malawi, Chiotcha lilipompeleka chini na kuinuka kwa msaaada wa kamba za ulingo.

Konde hilo zito lilifungua mpasuko mkubwa katika paji la Cheka na hivyo kuleta wasiwasi kwa mashabiki zaidi ya elfu 10 waliofurika katika uwanja wa Sheikh Amri Abed kumshughudia Cheka akipambana kiume kwelikweli.

Raundi ya kwanza mpaka ya nne Chiotcha alikuwa anamiliki mpambano huo na makonde mazito ya mkono wake wa kushoto kwani anatumia staili ya South Paw inayomlazimu kutanguliza mbele mguu wa kulia.

Ni katika raundi ya sita ambako Cheka aliweza kubadilisha mwelekeo wa mpambano kwa kuanza kumwadhibu Chiotcha na makonde mazito ya kombinasheni yaliyomfanya Mmalawi huyo kumkumbatia bila mafanikio Mtanzania huyo asiyepigika.

Cheka aliwanyanyua mashabiki waliojaa uwanjani wakiongozwa na Mstahiki Meya wa jiji la Arusha, Mh. Gaudence Lyimo alipompiga bila huruma Chiotcha na kumlazimu refarii wa kimataifa wa mpambano huo Nemes Kavishe wa Tanzania kumwonya kutomshika Cheka kama vile anapigana mieleka.,

Juhudi za Chiotcha kujisalimisha kwa kumkumbatia Cheka hazikuzaa matunda kwani aliendelea kupewa mkong’oto na mwana huyo wa Kitanzania aliyejizolea sifa kemkem kwa kuwapiga wapinzani wake.

Mashabiki wengi walinyanyuka katika viti vyao katika raundi ya 12 ya lala salama wakati Cheka alipodhihirisha kweli ni bondia asiyepigika kwa kumpiga makonde mazito kichwani Chiotcha na kumfanya apepesuke kila mara.

Katika mchezo huo ulioandaliwa na kampuni ya Green Hills (T) Investment ya jijini Dar-Es-Salaam inayomilikiwa na bingwa wa zamani wa taifa Andrew George, mabondia wa mapambano ya utanguliizi walikuwa wa ngumi za ridhaa kutoka katika jiji la Arusha.

Mpambano huo ulisimamiwa na Rais wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati, Mtanzania Onesmo Ngowi akisaidiwa na Kamishna wa TPBC kutoka Jiji la Arusha bw. Roman Chuwa.

Refarii alikuwa Nemes Kavishe kutoka Tanzania wakati majaji walikuwa: Daudi Chikwanje kutoka Malawi, Boniface Wambura kutoka Tanzania na Galous Ligongo kutoka Tanzania.

Imetolewa na
Uongozi, TPBC

Thursday, December 27, 2012

RIDHIWANI MGENI RASMI MKUTANO MKUU WA TASWA




MAANDALIZI ya Mkutano Mkuu wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) yanaenda vizuri na wajumbe wanatarajiwa kufika Bagamoyo Ijumaa Desemba 28, 2012 mchana kwenye hoteli ya Kiromo View Resort watakapolala na kufanyia mkutano.

Ijumaa hiyo washiriki watatembelea maeneo mbalimbali ya kihistoria Bagamoyo na jioni kutakuwa na mechi ya kirafiki kati ya timu ya soka ya TASWA FC na Bagamoyo Veterani itakayofanyika Uwanja wa Mwanakalenge na usiku wajumbe watakuwa na chakula cha pamoja na kubadilishana mawazo kuhusiana na masuala mbalimbali yahusiyo michezo na taaluma ya habari.

Mkutano Mkuu utafunguliwa Jumamosi Desemba 29, saa tatu asubuhi na mgeni rasmi atakuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kusaidia timu za Taifa za Vijana, Ridhiwani Kikwete.TASWA imechukua jukumu la kumualika kutokana na kuwa mdau mkubwa na rafiki wa chama chetu.

Mkutano utafungwa jioni ya siku hiyo na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Assah Mwambene ambaye hiyo pia itakuwa nafasi nzuri kwake kuweza kuzungumza na wana habari kuhusiana na masuala mbalimbali ya kitaaluma.

Katika mkutano huo wanachama wa TASWA watapata fursa ya kupokea na kujadili Ripoti ya Utendaji ya chama, Mapato na Matumizi, maendeleo ya chama na masuala mbalimbali yanayohusu waandishi wa habari za michezo na maendeleo ya michezo kwa ujumla

Pia kutakuwa na semina maalum itakayoendeshwa kwa washiriki wa mkutano huo, ili wawe na uelewa kuhusiana na ajenda ya kuinua kipato kwa wanachama ambayo nayo itajadiliwa kwenye mkutano huo.

Kamati ya Utendaji ya TASWA imekubaliana iwasaidie wanachama wake waweze kujitegemea kwa kuanzisha Chama cha Akiba na Mikopo (SACCO’S), lakini imeamua kwanza iwaite wataalamu wa vyama vya ushirika watoe elimu juu ya jambo hilo na kukishakuwa na uelewa wa kutosha suala hilo litakuwa kama ajenda kamili ya kuanzisha chama hicho kwenye mkutano wetu.
Ahsante.
Amir Mhando
Katibu Mkuu TASWA

MTEMVU AMPIGA JEKI DOGO ASLAY DOLA 1,200



MBUNGE wa jimbo la Temeke kwa tiketi ya CCM, Abbas Mtevu amempatia msanii Dogo Asley wa kundi la TMK Wanaume Family, dola 1,200 kwa ajili ya safari yake ya kwenda Ivory Coast.

Aslay amekabidhiwa kiasi hicho cha fedha na msaidizi wa mbunge huyo katika hafla iliyofanyika ofisini kwake, Temeke, Dar es Salaam.

Msaidizi huyo wa mbunge alisema bosi wake ameamua kumpatia Aslay kiasi hicho che fedha ili kutimiza ahadi aliyoitoa wakati wa mkutano mkuu wa CCM uliofanyika Novemba mwaka huu mjini Dodoma.

Akipokea fedha hizo, Aslay alimshukuru mbunge huyo kwa kutimiza ahadi yake na kuwataka watanzania wamwombee dua ili aweze kufanya vizuri katika tuzo.

Sherehe za utoaji tuzo za Kora kwa wanamuziki bora barani Afrika, zimepangwa kufanyika keshokutwa mjini Abidjan, Ivory Coast.

Aslay ameteuliwa kuwania tuzo ya msanii mpya anayechipukia kupitia wimbo wake wa Niwe Nawe. Aslay anapambana na wasanii kutoka nchi nyingine kama Uganda, Burkina Faso, Zambia, Nigeria na Afrique Du Sud.

Mbali na Dogo Aslay, wasanii wengine kutoka Tanzania walioteuliwa kuwania tuzo hizo ni Lady Jay Dee, Saida Karoli na Ali Kiba.

OBAFEMI MARTINS ALA KRISMAS NA WATOTO YATIMA, AWAZAWADIA VICHANGA NAIRA MILIONI 10




Super Eagles striker, Obafemi Martins took it upon himself to spend his Christmas celebration with some orphanage homes and hospitals in Lagos. The Levante point-man, who is currently on a break from his Spainish football club activities, visited the Maternity Island Hospital, the SOS Village in Isolo and some hospitals in Lagos.

Obagoal, as he is also called, embarked on this gesture on behalf of his foundation which gave gifts items and cash donations to the visited hospitals and orphanages. Sources close to Obagoal told Nigeriafilms.com that over N10million was splashed on hospital bills of babies born on Christmas day in Lagos which also included cash donations to their mothers.

SIMBA YAPIGA MARUFUKU MKUTANO ULIOITISHWA NA WANACHAMA DESEMBA 30



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

HERI ya Krismas na Mwaka mpya kwenu nyote.

Uongozi wa klabu ya Simba leo unapenda kutoa taarifa zifuatazo kwenu.

1. Mkutano wa Wanachama uliopangwa kufanyika Desemba 30 mwaka huu.
UONGOZI umepata taarifa kuwa kuna kundi la wanalojiita wanachama wa Simba waliopanga kufanya mkutano wa wanachama siku ya tarehe 30 Desemba mwaka huu (Jumapili hii) kwa lengo la kujadili mambo ya klabu.

Mkutano huo, kwa mujibu wa Katiba ya Simba ni batili. Ubatili huo unatokana na ukweli kwamba wale walioutisha mkutano huo hawana Locus Standi (nguvu au mamlaka) ya kufanya hivyo. Katiba ya Simba iko wazi kuwa mtu anayeitisha mkutano wa wanachama ni MWENYEKITI wa klabu pekee na si vinginevyo.

Mkutano huo wa wanachama haujaitishwa na Mwenyekiti wa klabu na hivyo hauna uhalali wowote wa kisheria.

Uchunguzi uliofanywa na klabu umebaini kwamba zaidi ya nusu ya walioitisha mkutano huo pia si wanachama halali wa Simba. Wengine hawajawahi kulipa ada zao za uanachama katika kipindi cha hadi miaka 10 iliyopita !

Matendo yanayofanywa na kundi hili yanaashiria watu wanaotaka tu kuleta vurugu klabuni. Kundi hili linafanya hivi wakati Rais Jakaya Kikwete ametoka kutoa kauli kuhusiana na namna vurugu zinavyosababisha kushuka kwa michezo hapa nchini.

Kundi hili linaandaa vurugu katika kipindi ambacho uongozi upo katika mikakati kabambe ya kuiboresha timu ikiwamo kuipeleka nje ya nchi kufanya mazoezi, jambo ambalo halijawahi kufanyika katika kipindi cha miaka 20 iliyopita.

Linaandaa vurugu katika kipindi ambacho Simba ndiyo bingwa mtetezi wa Ligi Kuu ya Tanzania na ikiwa imeongoza ligi katika msimu huu kuanzia mechi ya kwanza hadi ya 11 katika mechi 13 za kwanza.

Klabu inaomba wapenzi na wanachama wake kukaa mbali na kundi hili la waleta vurugu. Huu ni wakati ambapo tunatakiwa kuwa pamoja kwa vile klabu inatakiwa kutetea ubingwa wake na pia kuliwakilisha taifa katika michuano ya kimataifa mapema mwakani.

Huu ni wakati wa wanachama, wapenzi na uongozi kuwa kitu kimoja. Uongozi uko tayari kukosolewa wakati wowote ule lakini haukubaliani na waleta vurugu.

Uongozi unapenda kusisitiza lifuatalo, Mkutano wa Desemba 30 ni batili na wale wote wenye mapenzi mema na klabu wanatakiwa kukaa mbali nao na kutojihusisha kwa chochote na wanaopanga vurugu.

2. Safari ya Oman
MWENYEKITI wa Simba, Mhe; Ismail Aden Rage, amerejea Dar es Salaam akitokea Falme za Kiarabu alikoenda kuandaa ziara ya timu ya Simba kwenda kufanya maandalizi ya Ligi Kuu ya michuano ya kimataifa.

Taarifa kamili kuhusu ziara hiyo atazitoa wakati wowote kuanzia kesho.

3. Mazoezi
WACHEZAJI wa Simba wataendelea na mazoezi kesho Alhamisi Desemba 27 katika Uwanja wa Sigara, Chang’ombe jijini Dar es Salaam.

Timu haikufanya mazoezi katika siku mbili za Desemba 25 na 26 mwaka huu ili kutoa nafasi kwa wachezaji na benchi la ufundi kupumzika na familia zao kwenye sherehe za Krismasi na Mwaka Mpya.

Simba iko mazoezi kwa takribani wiki tatu nne –wiki mbili za kwanza ikijifua katika gym, wiki iliyopita wakifanya mazoezi ya ufukweni na wiki hii ndiyo wameanza ya uwanjani.

Mpaka sasa hakuna mchezaji yeyote majeruhi na mazoezi yanaendelea vizuri kabisa. Wachezaji waliokuwa na timu ya taifa wataanza mazoezi mara baada ya mapumziko ya sikuu za Krismasi na Boxing Day.

4. Zawadi ya Kombe la Uhai
KUFUATIA kupewa zawadi ya mshindi wa tatu katika mashindano ya Kombe la Uhai yaliyomalizika hivi karibuni, uongozi wa Simba umeamua kuwapa wachezaji wake fedha zote (Sh laki tano) za zawadi kwa mshindi wa nafasi hiyo wagawane.

Hatua hii ya uongozi ina lengo la kuwafanya wachezaji walioshiriki mashindano hayo wajitume zaidi katika mashindano mengine ambayo watahitajika kuitumikia klabu ya Simba.

5. Heri ya Krismas na Mwaka Mpya
UONGOZI wa Simba unawatakia wapenzi na wanachama wake sherehe njema za Sikukuu za Krismas na Mwaka Mpya.

Imetolewa na
Ezekiel Kamwaga
Ofisa Habari
Simba SC

YANGA YAPIGWA KIMOJA NA TUSKER



WENYEJI Yanga jana walipigwa mweleka wa bao 1-0 na mabingwa wa soka wa Kenya, Tusker katika mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mechi hiyo ilikuwa ya kuwaaga mashabiki kwa Yanga, ambayo keshokutwa inatarajiwa kukwaa pipa kwenda Uturuki kwa ajili ya maandalizi ya mechi za mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Tanzania Bara.

Bao pekee na la ushindi la Tusker lilifungwa na mshambuliaji Ismail Dunga kwa njia ya penalti dakika ya 44 baada ya kiungo, Nurdin Bakari wa Yanga kumuangusha Khalid Aucho ndani ya eneo la hatari.

Katika mechi hiyo iliyohudhuriwa na mashabiki wachache, Yanga ilicheza vizuri vipindi vyote viwili na kufanya mabadiliko kadhaa ya wachezaji, lakini ilishindwa kutengeneza nafasi za kufunga mabao.



WATANZANIA MBWANA MATUMLA NA MADA MAUGO WATOA VICHAPO KWA WAPINZANI WAO


Bondia Mbwana Matumla (Tanzania) akitangazwa mshindi baada ya kumpa kichapo bondia David Charanga (Kenya).
Mada Maugo (kushoto) akimshushia kichapo bondia Yiga Juma (Uganda) wakati wa mpambano wao.

Bondia Mbwana Matumla (kulia) akitupiana makonde na bondia David Charanga kutoka Kenya.

Bondia David Charanga kutoka Kenya (kulia) akienda chini baada ya kupokea konde kutoka kwa Mbwana Matumla.
David Charanga kutoka Kenya (kulia) akimkabili bondia Mbwana Matumla wakati wa mpambano wao jana.
  Mabondia wa Tanzania juzi waling'ara katika mapambano yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Dar Live Mbagala Zakhem. Bondia maarufu nchini, Mada Maugo alimchapa Yiga Juma kutoka Uganda raundi ya kwanza kwa ‘Knock Out’. Katika hali iliyoonesha kuwa siku ya vichapo kwa wageni, pambano lingine ambalo bondia Mbwana Matumla alipambana na bondia kutoka Kenya, David Charanga lililokuwa la raundi nane, Matumla aliibuka kidedea katika raundi zote nane na kumfanya aibuke na ushindi wa kishindo.
(PICHA NA ISSA MNALLY NA RICHARD BUKOS / GPL)

MULTICHOICE TANZANIA YASAIDIA WATOTO YATIMA


Public Relations Manager of MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi (right) posing with children of Al-Madina Orphanage in Tandale where DStv made a donation of foodstuff worth 1,000,000Tshs. On the left is Kulthum Juma, Matron in Charge of the orphanage and Rehema Zeno, DStv staff.


Monday, December 24, 2012

AZAM BINGWA KOMBE LA UHAI




 Mwenyekiti mstaafu wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Kanali mstaafu Idd Kipingu akimkabidhi nahodha wa timu ya Azam FC, Abdul Mgaya kombe la Ubingwa wa  michuano ya Uhai Cup 2012 baada ya timu hiyo kuifunga Coastal Union ya Tanga kwa penalti 3-1 katika mchezo wa fainali ya vijana chini ya miaka 20 uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam. Katikati ni Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodgar Tenga. (Picha zote na Habari Msetoto Blog)

TIMU ya soka ya vijana wa chini ya umri wa miaka 20 ya Azam imefanikiwa kutwaa ubingwa wa michuano ya Kombe la Uhai baada ya kuishinda Coastal Union kwa penalti 3-1.

Mshindi wa pambano hilo ilibidi apatikane kwa njia ya matuta baada ya timu hizo kumaliza dakika 120 zikiwa sare ya mabao 2-2.

Katika michuano hiyo, Bakari Shime wa Coastal Union ametwaa tuzo ya kocha bora, Mansur A. Mansur wa Coastal Union kipa bora, Ramadhan wa Simba aliyefunga mabao sita, ameibuka mfungaji bora, Ruvu Shooting timu yenye nidhamu, Joseph Kimwaga wa Azam mchezaji bora na Isiaka Mwalile refa bora.

MTIGINJOLA KUONGOZA KAMATI YA RUFANI YA TFF

Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imemteua Idd Mtiginjola kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF iliyoundwa kutokana na marekebisho ya Katiba yaliyofanyika hivi karibuni.

Mtiginjola ambaye ni Wakili wa kujitegemea ataongoza kamati hiyo yenye wajumbe watano ambayo sasa itakuwa chombo cha mwisho kusikiliza rufani zinazotokana na uchaguzi wa TFF, na wanachama wa TFF ambao hawatakubaliana na uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF.
Kabla ya uteuzi huo, Mtiginjola alikuwa mjumbe wa Kamati ya Nidhamu ya TFF inayoongozwa na Kamishna wa Polisi (CP) mstaafu Alfred Tibaigana. Nafasi yake katika kamati hiyo na ile ya mjumbe mwingine Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Shabani Semlangwa aliyefariki dunia Julai mwaka huu zitajazwa hivi karibuni.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF ambayo vinara wake (Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti) wanatakiwa kitaaluma kuwa wanasheria ni Francis Kabwe. Kabwe ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Wajumbe wengine walioteuliwa na Kamati ya Utendaji ya TFF katika kikao chake cha jana (Desemba 23 mwaka huu) ni Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), Mohamed Mpinga ambaye pia kitaaluma ni Mwanasheria.
Wengine ni mshambuliaji wa zamani wa timu ya Reli Morogoro, Profesa Madundo Mtambo ambaye kwa sasa ni Mkufunzi katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) kilichopo mjini Morogoro, na mdau wa soka Murtaza Mangungu ambaye pia ni Mbunge wa Kilwa Kaskazini.

STARS, CHIPOLOPOLO ZAINGIZA MIL 109/-



Pambano la kirafiki la kimataifa kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Zambia (Chipolopolo) lililochezwa juzi (Desemba 22 mwaka huu) limeingiza sh. 109,197,000.

Fedha hizo zimepatikana kutokana na watazamaji 17,383 waliokata tiketi kushuhudia mechi kwa kiingilio cha sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.

Mgawanyo wa mapato hayo ulikuwa kama ifuatavyo; asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ni sh. 16,657,169.49, maandalizi ya mchezo sh. 55,339,510, tiketi sh. 5,803,900, ulinzi na usafi kwa Uwanja wa Taifa sh. 2,350,000, Wachina (technical support) sh. 2,000,000, umeme sh. 300,000 na maandalizi ya uwanja (pitch marking) sh. 400,000.

Nyingine ni bonasi kwa Taifa Stars sh. 13,826,313, asilimia 20 ya gharama za mchezo sh. 2,504,022, asilimia 10 ya uwanja sh. 1,252,011, asilimia 5 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) sh. 626,005 na asilimia 65 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 8,138,070.

Mapato ya mechi nyingine za Taifa Stars ilizocheza nyumbani mwaka huu yalikuwa Taifa Stars vs Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo-DRC (Leopards) iliyofanyika Februari 23 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam sh. 32,229,000. Taifa Stars vs Msumbiji (Mambas) iliyochezwa Februari 29 mwaka huu sh. 64,714,000.

Taifa Stars vs Malawi (The Flames) iliyochezwa Mei 26 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam iliingiza sh. 40,980,000. Taifa Stars vs Gambia (The Scorpions) iliyochezwa Juni 10 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam zilipatikana sh. 124,038,000 na Taifa Stars vs Kenya (Harambee Stars) iliyofanyika Novemba 14 mwaka huu Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza iliingiza sh. milioni 45.

TWFA YAWATUZA TENGA, FURAHA



Chama cha Mpira wa Miguu Wanawake Tanzania (TWFA) kimetoa tuzo kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga na Meneja wa timu ya Taifa (Twiga Stars), Furaha Francis kutokana na mchango wao katika kuendeleza mchezo huo.

Tuzo hizo zilitolewa katika Mkutano wa Uchaguzi wa TWFA uliofanyika Desemba 19 mwaka huu mjini Morogoro kutokana na mchango wao katika kuendeleza mpira wa miguu kwa wanawake nchini.

“Ni dhahiri kazi ya kuendeleza soka ya wanawake ni wajibu wa Shirikisho (TFF), lakini Rais wa TFF alitoa kipaumbele zaidi na alijitoa kuhakikisha misingi imara ya kuendeleza soka ya wanawake inawekwa,” alisema Mwenyekiti wa TWFA, Lina Kessy.

Pia Mkutano huo ulitambua na kumpa tuzo Furaha Francis ambaye amekuwa Meneja wa Twiga Stars kwa miaka minane mfululizo. Licha ya kuwa Meneja wa Twiga Stars, ametumia muda wake na kujitoa katika kuendeleza mpira wa miguu kwa wanawake.

TWFA itaendelea kutumia michango yao katika mpira wa miguu kwa wanawake nchini.

TFF YAIPONGEZA TAREFA, YATOA POLE KIFO CHA MUSA RICO



Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa pongezi kwa uongozi mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Tabora (TAREFA) uliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika jana (Desemba 22 mwaka huu).

Ushindi waliopata viongozi waliochaguliwa kuongoza chama hicho unaonesha jinsi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa TAREFA walivyo na imani kubwa kwao katika kusimamia mchezo huo mkoani Tabora.

TFF inaahidi kuendeleza ushirikiano wake kwa Kamati ya Utendaji ya TAREFA chini ya uenyekiti wa Yusuf Kitumbo aliyeshinda kwa kura 16 dhidi ya nane za Musa Ntimizi, na Paul Werema ambaye hakupata kura.

Uongozi huo mpya una changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni kuhakikisha unaendesha shughuli za mpira wa miguu mkoani Tabora kwa kuzingatia katiba ya TAREFA pamoja na vyombo vya mpira wa miguu vilivyo juu yake.

Pia tunatoa pongezi kwa Kamati ya Uchaguzi ya TAREFA na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kuhakikisha uchaguzi huo unaendeshwa kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF.

Viongozi waliochaguliwa katika uchaguzi huo ni Yusuf Kitumbo (Mwenyekiti), Fate Remtulla (Katibu), Dick Mlimuka (Mjumbe wa Mkutano Mkuu TFF), Razak Irumba (Mwakilishi wa Klabu TFF) na wajumbe wa Kamati ya Utendaji ambao ni Eric Kabepele na Mwalimu Sizya.

Wakati huo huo, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha mchezaji wa zamani wa timu ya Coastal Union, Musa Rico kilichotokea jana (Desemba 22 mwaka huu) jijini Tanga.


Msiba huo ni mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kwani kwa nyakati tofauti akiwa mchezaji Rico, na baadaye kocha alitoa mchango mkubwa kwa timu mbalimbali alizochezea na kufundisha ikiwemo Coastal Union, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.

TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu Rico, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Tanga (TRFA) na klabu ya Coastal Union na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.

Maziko yanatarajiwa kufanyika leo (Desemba 23 mwaka huu) mkoani Tanga. Mungu aiweke roho ya marehemu Rico mahali pema peponi. Amina

SIMBA YASHIKA NAFASI YA TATU KOMBE LA UHAI

Simba imetwaa nafasi ya tatu katika michuano ya Kombe la Uhai inayoshirikisha timu zenye umri chini ya miaka 20 za klabu za Ligi Kuu ya Vodacom baada ya kuitandika Mtibwa Sugar ya Morogoro mabao 3-0.

Hadi mapumziko katika mechi hiyo iliyochezwa leo asubuhi (Desemba 23 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam, Simba ilikuwa mbele kwa bao 1-0.

Mabao yote ya washindi katika mechi hiyo yalifungwa na Ramadhan Mkipalamoto. Mfungaji alifunga bao la kwanza dakika ya 43 wakati mengine alipachika dakika za 57 na 70. Kwa kunyakua nafasi ya tatu, Simba imeondoka na kitita cha sh. 500,000.

Mechi ya fainali ya michuano hiyo kati ya Azam ya Dar es Salaam na Coastal Union ya Tanga itachezwa leo (Desemba 23 mwaka huu) saa 10 jioni kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume.

Mbali ya kombe, bingwa wa michuano hiyo inayodhaminiwa na kampuni ya Said Salim Bakhresa kupitia maji Uhai atapata sh. milioni 1.5 wakati makamu bingwa atazawadiwa sh. milioni moja.

Timu iliyoonesha zaidi mchezo wa kiungwana (fair play) itapata sh. 400,000, mchezaji bora wa mashindano sh. 350,000, mfungaji bora sh. 300,000 na kipa bora sh. 300,000. Naye kocha bora katika mashindano hayo atazawadiwa sh. 300,000 kama itakavyokuwa kwa refa bora.

Saturday, December 22, 2012

LULU HAJAACHIWA KWA DHAMANA, UONGO MTUPU



Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu Dar es salaam jana Desemba 21 2012 imefunga jalada la kesi ya kuua bila kukusudia inayomkabili mwigizaji Elizabeth Michael maarufu kama Lulu tayari kwa kulipeleka Mahakama kuu ya Tanzania ili hiyo kesi ianze kusikilizwa.
Kabla ya kusomwa kwa maelezo ya kesi hiyo ambapo Lulu hakutakiwa kujibu chochote kutokana na Mahakama ya Kisutu kutokuwa na mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo, Hakimu wa Mahakama ya Kisutu Augustina Mmbando amemtaka wakili wa serikali kutaja idadi ya mashahidi watakaotoa ushahidi wao wakati kesi hiyo itakapoanza kusikilizwa.
Wakisoma kwa awamu maelezo ya mashahidi wa kesi hiyo, mawakili wa serikali kwenye hiyo kesi wamesema wanao mashahidi tisa wanaotarajiwa kuwatumia kwenye kesi na kuongeza kwamba shahidi namba moja ni Seth Bosco mdogo wa Marehemu Kanumba waliekua wakiishi pamoja.
Kwenye maelezo yaliyosomwa na Seth mahakamani, imeelezwa kwamba siku ya tukio Kanumba alimtaka asitoke ili watoke pamoja baadae lakini ilipofika saa tano usiku alisikia vurugu chumbani kwa Kanumba ambako alikua na mpenzi wake ambae ni Lulu na baada ya muda Seth aligundua kulikua na ugomvi unaendelea na mlango ulikua umefungwa.
Maelezo hayo yameendelea kwamba baada ya muda Lulu alitoka chumbani kwa Kanumba na kumtaarifu Seth kwamba Kanumba ameanguka ambapo Seth alipoingia chumbani alikuta Kanumba kaegemea ukuta pembezoni mwa mlango huku povu likimtoka mdomoni na kuamua kumlaza chini kabla ya kuomba msaada.
Mashahidi wengine wanaotarajiwa kutoa ushahidi wao wakati kesi itakapoanza kusikilizwa ni Sophia Kassim ambae ni mmiliki wa nyumba aliyokua anaishi Kanumba, madaktari watatu, Polisi watatu, afisa uhamiaji
ambae ni shemeji wake Kanumba na Moris Sekwao ambae ni kijana aliempakia Lulu kwenye gari lake muda mfupi kabla ya kukamatwa.
Baada ya kusomwa kwa maelezo ya mashahidi wote, wakili wa serikali amesoma maelezo ya Lulu na kuamplfy kwamba mwigizaji huyu alianza uhusiano wa kimapenzi na Kanumba january 2012 ambapo walikua na kutoelewana katika baadhi ya nyakati hasa pale mmoja anapompigia simu mwenzake na haipokelewi kwa wakati.
Baada ya maelezo yote kutolewa na kukamilika, Hakimu wa mahakama ya hakimu mkazi Kisutu Augustina Mmbando amezishukuru pande zote na kumtaka Lulu atoe maelezo ya nyongeza kama anayo ambapo Lulu alisema hana maelezo yoyote ya kuongezea.
Hakimu Mmbando amemtaka Lulu kuendelea kubaki rumande mpaka tarehe ya kesi yake itakapotajwa na Mahakama kuu ya Tanzania.
Hakuna ukweli wowote wa taarifa zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii kwamba Lulu ameachiwa kwa dhamana.
TAARIFA HII NI KWA HISANI YA BLOGU YA MILLARDAYO

MTANZANIA ATWAA TAJI LA MISS EAST AFRICA 2012


Mratibu wa shindano la Miss East Africa 2012, Renna Callist akitangaza matokeo ya washindi wa shindano la Miss East Africa 2012 lililofanyika jana kwenye ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaaam.
Mrembo wa Afrika Mashariki 2012 (Tanzania),Jocelyne Maro (katikati) akiwa na mshindi wa pili (Uganda),Ayisha Nagudi pamoja na Mshindi wa tatu (Burundi),Ariella Kwizera mara baada ya kupatikana kwa washindi hao katika Shindano lililofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City,Jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo.

Mrembo wa Afrika Mashariki 2012 (Tanzania),Jocelyne Maro akiwa na washindi wenzake alioingia nao hatua ya tano bora katika Shindano hilo lililofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City,Jijini Dar es Salaam usiku wa
kuamkia leo.

Mrembo wa Afrika Mashariki 2012 (Tanzania),Jocelyne Maro akipungia mkono mashabiki wake mara baada ya kutangazwa mshindi wa Shindano hilo lililofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City,Jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo.

TAIFA STARS YAIGALAGAZA CHIPOLOPOLO, NGASA AWAPA RAHA MASHABIKI, SURE BOY 'MAN OF THE MATCH'



TIMU ya soka ya Taifa, Taifa Stars jioni hii imewachapa mabingwa wa Afrika, Zambia bao 1-0 katika mechi ya kirafiki ya kimataifa ya soka iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Shujaa wa Taifa Stars katika mechi hiyo alikuwa mshambuliaji Mrisho Ngasa aliyefunga bao hilo la pekee na la ushindi katika kipindi cha kwanza.
Ngasa alifunga bao hilo kwa shuti kali akiwa pembeni ya uwanja, ambalo liligonga mwamba wa juu wa goli na kutinga wavuni.
Katika mechi hiyo, mchezaji aliyeng'ara kwa upande wa Taifa Stars alikuwa kiungo Salum Abubakar 'Sure Boy', ambaye aliumiliki vyema mpira na kucheza atakavyo, hali iliyosababisha wakati mwingine Wazambia waogope kumfuata kwa hofu ya kuaibika.
Mbali na Sure Boy, kiungo mwingine Frank Domayo naye alicheza vyema nafasi ya kiungo mshambuliaji, akishirikiana vyema na Mwinyi Kazimoto na Ngasa, ambao walikuwa mwiba kwa mabeki wa Zambia.
Amri Kiemba alilazimika kucheza mechi hiyo akiwa majeruhi, lakini aliweza kuelewana vyema na wenzake japokuwa hakuwa na kasi iliyozoeleka. Taifa Stars ilikwenda mapumziko ikiwa mbele kwa bao 1-0.
Zambia ilikianza kipindi cha pili kwa kufanya mabadiliko ya wachezaji watano kwa mpigo kabla ya kuongeza wengine wawili kadri dakika zilivyokuwa zikiyoyoma. Walipotaka kuingiza wachezaji wengine wawili, mwamuzi Kirwa kutoka Kenya aliwakatalia.
Katika kipindi hicho cha pili, Taifa Stars ilimpumzisha Khamis Mcha na kumwingiza Simon Msuva kabla ya baadaye kuwatoa Ngasa na beki Kevin Yondan na kuwaingiza Amir Maftah na Nadir Haroub Cannavaro.
Wakizungumza na blogu ya liwazozito wakati wa mchezo huo, baadhi ya mashabiki walimpongeza kocha Kim Poulsen kwa uamuzi wake wa kuwachezesha wachezaji vijana wengi na wasiokuwa na majina.
Mshambuliaji Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu, ambao wamekuwa wakidengua kuja kuichezea Taifa Stars, walijikuta wakiwa kwenye wakati mgumu baada ya kuzomewa na mashabiki.
Juma Kaseja, Erasto Nyoni, Shomari Kapombe, Kevin Yondan, Aggrey Morris, Salum Abubakar, Amri Kiemba, Frank Domayo, Mrisho Ngasa/Amir Maftah, Mwinyi Kazimoto, Khamis Mcha/ Simon Msuva.

AZAM, COASTAL UNION KUCHEZA FAINALI KOMBE LA UHAI


Azam ya Dar es Salaam na Coastal Union ya Tanga ndizo zitakazoumana kwenye fainali ya michuano ya Kombe la Uhai 2012 itakayochezwa kesho jioni (Desemba 23 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam.
Timu hizo zimepata fursa hiyo baada ya kushinda mechi zao za nusu fainali ya michuano hiyo inayoshirikisha timu za vijana wenye umri chini ya miaka 20 za klabu za Ligi Kuu ya Vodacom. Michuano hiyo inayodhaminiwa na kampuni ya Said Salim Bakhresa kupitia maji Uhai.
Azam ndiyo iliyokuwa ya kwanza kupata tiketi ya fainali baada ya kuitoa Mtibwa Sugar ya Morogoro kwa mikwaju ya penalti 3-2. Matokeo ya dakika 90 yalikuwa bao 1-1. Nayo Coastal Union iliivua ubingwa Simba kwa kuifunga mabao 2-1.
Mechi ya fainali itaanza saa 10 kamili jioni, na itatanguliwa na ile ya kutafuta mshindi wa tatu kati ya Mtibwa Sugar na Simba ambayo itachezwa saa 2 kamili asubuhi kwenye uwanja huo huo.
Mbali ya kombe, bingwa wa michuano hiyo atapata sh. milioni 1.5, makamu bingwa sh. milioni 1 wakati mshindi wa tatu atajinyakulia sh. 500,000.
Timu iliyoonesha zaidi mchezo wa kiungwana (fair play) itapata sh. 400,000, mchezaji bora wa mashindano sh. 350,000, mfungaji bora sh. 300,000 na kipa bora sh. 300,000.
Naye kocha bora katika mashindano hayo atazawadiwa sh. 300,000 kama itakavyokuwa kwa refa bora.

WASANII WAMTEMBELEA JK IKULU


Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wasanii waliomtembelea Ikulu, Dar es Salaam
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa Chama cha Muziki wa Dansi nchini, Addo Mwasongole
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na mwanamuziki nyota wa zamani wa bendi ya Mlimani Park, Cosmas Thobias Chidumume
Rais Jakaya Kikwete akiteta jambo na mwanamuziki nyota wa Injili, Flora Mbasha na mumewe.
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na kiongozi wa bendi ya Bantu Group na mpiga gita la solo mahiri nchini, Hamza Kalala 'Komandoo'
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na mwanamuziki mkongwe mwenye asili ya DRC, Kikumbi Mwanza Mpango Mwema Kikii
Rais Jakaya Kikwete akionekana kufurahia jambo na msanii wa muziki wa kizazi kipya, Khamis Mwinjuma 'Mwana FA'
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na msanii wa muziki wa kizazi kipya, Khamis Mwinjuma 'Mwana FA'
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na mwanamuziki Abdul Salvador
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na mwimbaji mkongwe wa taarab nchini, Shakila Saidi, ambaye anaimbia kundi la  JKT
RAIS Jakaya Kikwete akisalimiana na mwanamuziki mkongwe, Waziri Ally wa bendi ya The Kilimanjaro 'Wana Njenje'
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Serikali imeanza kutoa Nishani kwa wasanii kwa vile inatambua umuhimu wao katika jamii.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete amewaeleza wawakilishi wa sanaa mbalimbali nchini waliofika Ikulu leo asubuhi kutoa shukrani kwa Mheshimiwa Rais kwa kuwatambua na kuwapa heshima kubwa ya Tuzo na Nishani wasanii katika siku ya sherehe za Uhuru za tarehe 9 Disemba, Ikulu, Dar-Es-Salaam.
“Tumetoa Nishani kwa vile wasanii wanatoa mchango mkubwa, tumeanza kutoa nishani mwaka huu na tutaendelea kutoa miaka ijayo kwani kwa kuitambua sanaa, mnawapa moyo wasanii kuendelea kujituma na kuwa wabunifu zaidi” Rais amesema na kuongeza, “Tumeingiza Nishani ya Wasanii na Watafiti maana nao wanafanya kazi kubwa sana ya kutafiti mazao na mbegu mbalimbali ambazo zinaongeza tija katika kilimo nchini”.
Katika kumbukumbu ya kusherehekea miaka 51 ya Uhuru wa Tanzania bara mwaka huu, Rais Kikwete alitunuku nishani kwa makundi mbalimbali ya watu waliotoa mchango mkubwa katika jamii na waliotumikia taifa kwa uadilifu.
Rais alitoa Nishani ya Sanaa na Michezo kwa mara ya kwanza kwa wasanii nchini ambapo Bi. Fatma Baraka Khamis (Bi Kidude) kupitia Baraza la Sanaa Zanzibar, Kiongozi wa Muziki wa Dansi ya Msondo Ngoma Muhidin Maalim Gurumo, Kiongozi wa Zamani wa Bendi ya Dar Intrenational Marehemu Marijan Rajab walipata tuzo hiyo.
Wengine ni Msanii wa maigizo na filamu nchini Marehemu Fundi Said (Mzee Kipara) na Mwanariadha mkongwe John Steven Akwari.
Rais amewataka wasanii kushirikiana na serikali lakini pia wawe mstari wa mbele katika kupigania haki zao na sio kusubiri serikali tu iwafanyie hivyo.
Wasanii hao wamefika Ikulu wakiongozwa na Bw. Ruge Mutahaba wa Clouds Media Group.
Wengine ni Addo Mwasongwe, Rais wa Shirikisho la Muziki na Mwenyekiti wa Chama cha Muziki wa Injili, Bw. Juma Ubao Mwenyekiti wa Chama cha Muziki Tanzania (CHAMUDATA), aliyewakilishwa na Hamza Kalala.
Bibi Shakila Said, Mkongwe wa Muziki wa Taarab Nchini, Bi Carola Kinasha Msanii wa Muziki , Mzee King Kiki msanii wa Muziki wa Dansi Mwana FA, msanii wa Kizazi Kipya na Bw. Waziri Ally , msanii wa Muziki.
Wawakilishi hao pia wamemshukuru Rais kwa msaada wa hali na mali anaotoa kwa wasanii mbalimbali wanapopata matatizo ambao hivi sasa wapo katika hatua mbalimbali za matibabu ya afya zao hapa nchini na nchi za Nje.
“Haya mengine ninayafanya tukama wajibu wa kibinadamu kwa vile nina nafasi ya kufanya hivyo na pale tunapokua na uwezo tunasaidia kama binadamu wenzetu” Rais Amesema.
Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi Habari wa Rais, Msaidizi,
Ikulu - DSM
21 Desemba, 2012