KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, December 20, 2012

MSAMA PROMOTION YAIPIGA JEKI TASWA


KAMPUNI ya Msama Promotions inayoandaa Tamasha la Pasaka imeahidi kutoa Sh. Milioni 1.5 kwa ajili ya Mkutano Mkuu wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) utakaofanyika Bagamoyo mkoani Pwani wiki ijayo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama ambaye ndiye Mkurugenzi wa kampuni hiyo amesema ushirikiano wake na wanahabari umemsukuma kusaidia kiasi hicho cha fedha.
Msama ameahidi kuendelea kushirikiana na TASWA kadri awezavyo na kwamba mafanikio ya Tamasha la Pasaka yanachangiwa kwa kiasi kikubwa na wanahabari.
“Kampuni yangu ya Msama Promotions kupitia Tamasha la Pasaka tumeamua kuungana na wanahabari katika kufanikisha mkutano wenu, tunaamini uhusiano wetu utaendelea kuwa wa kupigiwa mfano,” ilisema sehemu ya taarifa ya TASWA jana ikimkariri Msama.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa TASWA, Amir Mhando alishukuru kwa udhamini huo na kuomba wengine wenye moyo wajitokeze kuwasaidia kwani bajeti yao ni Sh. Milioni 20. Tayari kampuni ya simu za mkononi ya Zantel imeshatangaza udhamini wa Sh. Milioni sita.
Mhando alisema maandalizi ya Mkutano Mkuu wa TASWA utakaofanyika wiki ijayo Bagamoyo mkoani Pwani yanaendelea vizuri na kwamba zaidi ya wanachama 100 wa TASWA na wadau wengine wa TASWA wamethibitisha kushiriki.
(B) Pongezi
Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), kinatoa pongezi kwa wanachama wake Benny Kisaka na Zena Chande kwa kufanikiwa kuwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Kisaka alishinda wadhida huo wiki iliyopita kupitia uchaguzi wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), wakati Chande alishika Jumatano katika uchaguzi wa Chama cha Mpira wa Miguu Wanawake Tanzania (TWFA).
Tunaamini wajumbe wa Mkutano Mkuu DRFA na wale wa TWFA hawakufanya makosa, wamefanya uamuzi sahihi na wamepata watu sahihi na makini na michango yao itakuwa yenye tija kubwa kwa maendeleo la mpira wa miguu hapa nchini.
Tunawatakia kila la heri wanachama wetu hao katika changamoto mbalimbali watakazokutana nazo kwenye nafasi zao hizo walizopata.
Nawasilisha
Amir Mhando
Katibu Mkuu TASWA
20/12/2012

No comments:

Post a Comment