KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, April 18, 2012

Sunzo out Simba, Okwi chini ya ulinzi

Felix Sunzu

Emmanuel Okwi


UONGOZI wa klabu ya Simba umesema mshambuliaji Felix Sunzu ni mgonjwa na hataweza kucheza mechi zilizosalia za michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara.
Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, Sunzu anasumbuliwa na maumivu ya tumbo na hali yake si nzuri.
Kamwaga alisema kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa huo, Sunzu hakuweza kucheza mechi ya ligi dhidi ya Ruvu Shooting mwishoni mwa wiki iliyopita na alitarajiwa kukosa mechi nyingine dhidi ya JKT Ruvu jana.
Hata hivyo, Kamwaga alisema tayari mshambuliaji huyo kutoka Zambia ameshaanza kupatiwa matibabu na iwapo atapata nafuu haraka, anaweza kucheza mechi hizo.
Baada ya kucheza na JKT Ruvu jana, Simba inakabiliwa na mechi zingine mbili kabla ya kuhitimisha ligi hiyo kwa kupambana na Moro United na Yanga.
Mbali na mechi hizo za ligi, Simba pia inakabiliwa na mechi mbili za raundi ya tatu ya michuano ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Al-Ahly Shandy ya Sudan. Mechi ya awali itachezwa Aprili 29 mjini Dar es Salaam na ya marudiano wiki mbili baadaye nchini Sudan. Katika hatua nyingine, Kamwaga amewataka waamuzi wa ligi kuu kumlinda mshambuliaji Emmanuel Okwi wa Simba kutokana na kukamiwa na timu pinzani.
Kamwaga alisema Okwi amekuwa akichezewa vibaya katika kila mechi kutokana na kiwango chake kuwa juu na kusababisha aumie mara kwa mara.
Akitoa mfano, alisema katika mechi kati ya Simba na Ruvu Shooting, mchezaji huyo alichezewa rafu mara 17, lakini mwamuzi alitoa kadi moja ya njano.
"Kwa kweli Okwi yupo kwenye wakati mgumu kwa sababu wakati mwingine inaonekana wazi kuwa, wachezaji wa timu pinzani wanataka kumvunja, hivyo amekuwa akicheza kwa woga na tahadhari kubwa,”alisema.

No comments:

Post a Comment