KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, April 18, 2012

MAFISANGO: NITAENDELEA KUCHEKA NA NYAVU

KIUNGO mahiri wa klabu ya Simba, Patrick Mafisango amesema ataendelea kufunga mabao mengi zaidi katika mechi zao zilizosalia za michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara.
Akizungumza mjini Dar es Salaam wiki hii, Mafisango alisema yeye na wachezaji wenzake wanafurahia mbinu mpya za soka wanazofundishwa na Kocha Milovan Cirkovic.
Mafisango, ambaye ni raia wa Rwanda alisema, ushirikiano uliopo kati ya viongozi na wachezaji wa Simba ni miongoni mwa mambo yaliyochangia timu hiyo kupata mafanikio.
Kiungo huyo ndiye aliyeifungia Simba bao pekee na la ushindi katika mechi yake ya ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Ruvu Shooting iliyochezwa mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
"Lengo letu ni kutwaa ubingwa wa ligi kuu msimu huu na hilo litawezekana kama tutashinda mechi zetu zote zilizosalia na dhamira yangu ni kuendelea kufunga mabao,"alisema.
Mafisango alisema uamuzi wake wa kuja kucheza soka ya kulipwa nchini, umelenga kukuza kipaji chake na pia kuongeza kipato, hivyo hawezi kufanya mzaha katika soka.
Amewashukuru wachezaji wenzake kwa kumpa ushirikiano mkubwa ndani na nje ya uwanja na kuongeza kuwa, mafanikio ya Simba kwa kiasi kikubwa yanachangiwa na mshikamano uliopo miongoni mwao.
Mafisango alisema ana imani Kocha Milovan ataendelea kumwamini na kumpa namba kwenye kikosi chake ili aweze kudhihirisha uwezo wake.

No comments:

Post a Comment