KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, April 9, 2012

KANUMBA KUZIKWA KESHO

Mazishi ya msanii nguli wa filamu nchini, Steven Kanumba yamepangwa kufanyika kesho kwenye makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa kamati ya mazishi ya msanii huyo, Jacob Steven JB alisema jana kuwa, mwili wa marehemu Kanumba utaagwa kwenye viwanja vya Leaders, Kinondoni kuanzia saa nne mbalimbali.
JB alisema shughuli ya kuuaga mwili wa msanii huyo inatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, wasanii, mashabiki na ndugu wa marehemu.
Kwa mujibu wa JB, mazishi yamepangwa kufanyika saa 10 jioni kwenye makaburi ya Kinondoni.
JB alisema shughuli ya kuuaga mwili wa Kanumba itakwenda sambamba na misa mbalimbali za kumuombea dua.

No comments:

Post a Comment