KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, April 4, 2012

Kiongozi T-Motto akiti Mzee Yussuf ni kiboko

MKURUGENZI wa kundi la muziki wa taarab la Tanzania Motto,Amini Salmini Amour amekiri kuwa, kundi la Jahazi kwa sasa liko juu na kazi zake zinapendwa na mashabiki wengi.
Amini amesema pia kuwa, nyota ya kiongozi wa kundi hilo, Mzee Yussuf 'Mfalme' inaendelea kung'ara katika medani ya muziki wa taarab na anamuheshimu.
Kiongozi huyo wa Tanzania Motto alisema hayo wiki hii mjini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na Burudani kuhusu maendeleo ya taarab nchini.
“Jahazi ni kundi lililoleta mabadiliko makubwa katika muziki wa taarab hapa nchini na Yussuf ni muimbaji hodari, mbunifu na mwenye kuona mbali, hakuna kundi au mwimbaji anayeweza kumfikia kwa sasa,”alisema.
Amini alisema binafsi anakiri kwamba Yussuf yupo juu kimuziki na kundi lake litaendelea kutamba kwa muda mrefu bila kuwa na mpinzani.
Akizungumzia kundi lake la Tanzania Motto, Amini alisema limeanza kujipanga upya baada ya kuanza kwa kusuasua mwishoni mwa mwaka jana.

No comments:

Post a Comment