KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, April 7, 2012

Kanumba alikuwa mtu wa watu,



KUTOKANA na kifo cha msanii Steven Kanumba, mitandao mbalimbali jana ilifurika wasomaji na wachangiaji wakitaka kujua na kujuzana mambo mbalimbali kuhusu msanii huyo, huku wengine wakifuatilia michango aliyowahi kuitoa enzi za uhai wake.
Ifuatayo ni michango yake michache katika mtandao wa twitter, ambao alipenda kuutumia kuwasiliana na watu mbalimbali wakiwemo wabunge, wanasiasa na watu wa kawaida.
Katika ukurasa wake, mtandao huo unaonyesha kuwa juzi, 'alichati' na mashabiki wake fulani, lakini mwishoni aliishia kuvituhumu vyama vyao (vya wasanii) kwa kutomsaidia mwenzao aitwaye Kajala Masanja, ambaye yupo mahabusu.
Kanumba alisema: "Wakati msanii mwenzetu Kajala yuko jela, eti TAFF na Bongo Movie hawamtambui Kajala wala hawawezi kusaidia lolote, hii roho mbaya inatoka wapi? "
Pia siku tatu zilizopita (kabla ya jana), Kanumba aliandika katika ukurasa huo akiwatuhumu mashabiki wanaopenda kumpingia simu usiku na mwisho wa siku wanakuwa hawana cha kusema zaidi ya kutaka tu kumsalimia.
Kanumba alisema: "Sometym mashabiki mnaboa sana, m2 unapiga cm ucku wa manane ukiulizwa shida? oh nilikuwa nataka kukusalimia? mchana mnakua wp? kdg mara unaringa"
Aidha siku 13 kabla ya jana, aliwatumia ujumbe mashabiki wake kupitia ukurasa huo akiwaonya dhidi ya mtu aliyekuwa akitumia jina lake katika mtandao wa Facebook akitaka atumiwe fedha, ambapo Kanumba aliandika akisema:"TAFADHALI MASHABIKI WANGU WOTE FACEBOOK KUNA MTU ANATUMIA JINA LANGU LA STEVEN KANUMBA KUOMBA PESA,PLZ MSITUME NI MWIZI".
Katika kuonyesha mapenzi yake kwa Kajala, siku 18 zilizopita, Kanumba aliandika katika mtandao huo akiwaomba mashabiki wake wamuombee msanii huyo ambaye yupo mahabusu, alisema: "Everybody plz pray for Kajala, prison is not a gud place to be."
Aidha katika blogu yake ya kanumbathegreat juzi Kanumba aliweka picha ya ndege wakiwa juu ya mbuzi na kuandika maneno yafuatayo:
Look at this pic careful. Mmoja ya vitu tulivyotofautishwa na wanyama na ndege ni akili ya kujua mema na mabaya, tizama hao ndege na huyo mbuzi hawana akili kabisa, lakini wanapendana ndio maana unaona wako pamoja, ila binadamu aliyepewa akili ana roho mbaya sana. Katika mafundisho ya YESU KRISTO alisema neno kuu nawapeni PENDANENI. Hata uwe na uwezo wa kuhamisha milima kama huna upendo ni bure, mpende jirani yako kama unavojipenda, upendo haujivuni, hauhesabu mabaya, hautakabari, hauhusudu.....nk
WAKORINTHO 13, Mungu ana akili sana kutuumba kwa mwili huu wa nyama, laiti kama angetuumba kwa vioo au sightmirror ili uweze kuona mwenzako anakuwazia nini?anakufanyia nini?anapanga nini juu yako? ungekuta ni heri ukaishi msituni na wanyama wakali kuliko kukaa na binadamu. Katika tafiti zangu nimegundua kuna dawa mbalimbali mfano ya kichwa, homa nk, lakini dawa ya chuki na roho mbaya hakuna. Kama hiki kingekuwa kipindi kama kile cha zamani za Sodoma na Gomora au cha Nuhu, ambacho Mungu alikuwa akiadhibu hapo hapo, watu wengi sana wangeumbuka hasa wale wanaojifanya wasafi usoni, lakini rohoni ni tofauti. Mungu atusaidie sana hasa sisi vijana tujue kusimama katika ukweli na uwazi, tuubebe upendo wa dhati toka rohoni huku mdomoni tukitamka amani ya kweli impendezayo Mungu ili watoto wetu waje watuenzi kwa mazuri na dunia ijivunie uwepo wetu.
Wakati wa uzinduzi wa duka la mitindo ya mavazi uliofanyika hivi karibuni, Kanumba aliandika maneno yafuatayo kupitia kwenye blogu yake: TULIOSAPOTI MPAKA KITUO HIKI KUFIKIA HAPA KILIPO SOMA MAJINA HAPO JUU JINA LANGU LIPO HAPO. KUSEMA UKWELI INAPOKUJA MAMBO YA KUSAIDIA JAMII, NAJITAIDI KUTOA NINACHOKUA NACHO MAANA HAPA HUKUMBUKA MANENO YA MWANDISHI ALBERT PINE: "What we do for ourselves dies with us. What we do for others and the world remains and is immortal."
Siku chache zilizopita, Kanumba alionekana kukerwa na taarifa zilizoripotiwa na gazeti moja la udaku zikimkariri kusema maneno, ambayo hakuyasema. Aliandika hivi kwenye blogu yake:TAFADHALI SANA SIJASEMA MANENO HAYO WALA SIJAHOJIWA LOLOTE KUHUSU HUO MTAFUTANO,SASA HIYO NUKUU IMETOKA WAPI??VIJANA WENZANGU EBU TUJIFUNZE KUSIMAMA KTK UKWELI MAANA HATA MUNGU HAPENDEZWI NA UONGO.
MASHABIKI WAMLILIAKatika ukurasa wake facebook, mashabiki na rafiki zake walifurika kutuma salamu zao na hizi ni chache kati ya nyingi zilizoko katika ukurasa huo.
Peris Mamadi Ratemo: "Its hard to take it!May ur soul rest in peace!We av every reason to celebrate u!"
Jane Kati: "REST IN PEACE KANUMBA"
Gayle Gabriel: rest in peace Kanumba Steve, every year I celebrate my daughter's birthday, I will remember u because u share birthday with my daughter"
Fatma Binti Mrisho Watuta: "Hata nimekosa la kusema.. ila kwa Mola tunatoka na marejeo ni kwake pia"
Kudra Makunzo: "R.I.P Kanumba Steve, Tanzanians love u, but God loves u more"
Ezekiel Simon Munge: "R.I.P The great one Steve Kanumba!"
Mary Maganga: "Gone too soon! R.I.P Kanumba,you'll be missed by many."
Joyce Joseph Mollel: "Gone to soon...! RIP Steve Kanumba!"
Johnson Mkubwa Super: Kanumba tunaku miss tungekua na uwezo ungeludi tunakupenda ila mungu amekupenda zaidi yetu sawa uende salama tunajisikia vibaya huku nchini Canada" Nigaze Perfect: "We are and for alway miss you Kanumba, rest in peace my friend."
Sophie Kessy: "R.I.P Stevin Kanumba Nyota ya filamu iliyozimika ghafla tutakukumbuka daima we will miss you Kanumba."
Malikia Hapi Kichuna: "R.I.P ua gone 2 soon"
Katika ukurasa huo, nyota huyo alikuwa na marafiki aliowasajili 3,693 huku kukiwa na picha 619 zinazoonyesha mambo na matukio mbalimbali yanayomhusu.

No comments:

Post a Comment