KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, April 18, 2012

AT awashukuru mashabiki wake

SIKU chache baada ya wimbo wake wa ‘Kifuku mtu’ kushinda tuzo za muziki za Kilimanjaro, msanii AT amesema alistahili kupata tuzo hiyo kutokana na wimbo wake kukubalika kwa mashabiki.
AT alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, wimbo wake huo umekuwa ukipigwa mara kwa mara na vituo vya redio na televisheni nchini kutokana na mvuto wake.
Kibao hicho cha AT, kilichopigwa katika miondoko ya mduara, kimeshinda tuzo ya wimbo bora wenye vionjo vya kiasili.
“Namshukuru sana Mungu kwa kuniwezesha kushinda tuzo hii na hii ni kutokana na wimbo wangu kukubalika na mashabiki,”alisema.
AT alisema msanii anapotaka kukubalika kwa mashabiki, anapaswa kuwa karibu nao badala ya kujitenga na kuwa mbali mbali nao.
Msanii huyo pia alitoa mwito kwa wasanii kutunga nyimbo zenye mvuto na zinazogusa jamii badala ya kutunga zaidi nyimbo za mapenzi.
“Nawashukuru mashabiki wote walionipigia kura na pia vituo vya redio na televisheni kwa kupiga nyimbo zangu mara kwa mara,”alisema.
Hii ni mara ya tatu kwa AT kushiriki kwenye tuzo hizo. Alishiriki kwa mara ya kwanza mwaka juzi kupitia kibao chake cha Nipigie alichomshirikisha Stara Thomas na mwaka jana kupitia kibao cha Mama ntilie, alichomshirikisha Ray C.

No comments:

Post a Comment