KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, April 5, 2012

KASEJA: Hatutishiki na vitimbi vyao




NAHODHA wa Simba, Juma Kaseja, amesema vitimbi wanavyofanyiwa na wenyeji
havitawafanya wapunguze ari ya kushinda pambano lao dhidi ya Setif kesho.
Akizungumza na tovuti ya Simba, Kaseja alisema wametazama kwa makini matukio
mbalimbali yanayofanywa na wenyeji wao na wamebaini yako mambo ambayo lengo
lake ni kuwaondoa mchezoni.
“Hebu fikiria, watu wanataka kutusafirisha kwa basi kwa masaa sita wakati wanajua
kanuni ni masaa mawili tu. Halafu, badala ya kutusafirisha hadi mji wa Setif
tulipocheza, wao wametupeleka kwanza mji mwingine na halafu wakatusafirisha kwa
basi kuja Setif. Hizi ni mbinu zao lakini tunazijua,” alisema.
Kaseja alikuwa miongoni mwa wachezaji wa Simba walioitoa Zamalek ya Misri katika
michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika miaka kumi iliyopita na anasema hakuna cha
ajabu iwapo timu yake itaitoa Setif.
“Katika uzoefu wangu wa soka, timu pekee ya kiarabu ambayo ilitutendea vema
ilikuwa ni Harass Al Hadoud ya Misri miaka miwili iliyopita. Lakini hawa walikuwa wema
kwa sababu walikuwa wametufunga katika mechi ya kwanza na hivyo hawakuwa na
wasiwasi.
“Ukiona Waarabu wanakufanyia vitimbi ujue wana wasiwasi na wewe. Kama hawana
hofu, watakupa kila unachohitaji. Nashukuru kwamba tuna wachezaji wazoefu wa
kutosha wanaoweza kupambana na lolote,” alisema.

Wakati huo huo, Simba kesho inashuka kwenye Uwanja wa Mei 8, 1945, jijini Setif, Algeria; uwanja ambao una historia ya kipekee nchini humu.
Tarehe 8, Mei mwaka 1945, majeshi ya Ufaransa iliyokuwa ikiikalia kimabavu Algeria
yaliua wananchi kati ya 6,000 hadi 45,000 wa Setif katika mapambano yaliyofanyika
mjini humo.
Uwanja huo wenye uwezo wa kubeba watu 30,000 ulibadilishwa jina wakati huo na
kupewa jina hilo la tarehe –kwa kifaransa Stade Mai 8 1945, kwa heshima ya watu
waliopoteza maisha siku hiyo.
Mauaji hayo ndiyo yaliyosababisha timu ya Setif kubadili rangi ya jezi zake kutoka
nyeupe na kijani na kuwa nyeusi na kijani –nyeusi ikiwa na maana ya kuomboleza
maelfu hayo ya watu waliouawa siku hiyo.

No comments:

Post a Comment