KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, April 4, 2012

Afande Sele akana kuwa na bifu na Chidi Benzi

MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Selemani Msindi ‘Afande Sele’ amesema hana ugomvi na kiongozi wa kundi la La Familia, Chidi Benzi.
Afande Sele alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, kilichotokea kati yake na Chidi Benzi ni mambo ya kawaida katika jamii, lakini alisisitiza kuwa bado wao ni marafiki.
Msanii huyo alielezea msimamo wake huo baada ya kutokea hali ya kutokuelewana kati yao, kufuatia Afande Sele kumponda msanii Ditto wa Watu Pori aliyejiunga na La Familia.
Afande Sele alikaririwa na kituo cha Radio cha East Africa akisema kuwa, uamuzi wa Ditto kujiunga na La Familia ni sawa na mchezaji wa Manchester United kujiunga na Bolton.
“Malumbano yanayoendelea kati yetu si mazuri, ni mambo ya kupita,sina bifu naye. Nipo tayari kurekodi naye wakati wowote na yeye anajua hilo, alishaniambia kitambo. Nasubiri wimbo wake hata kesho ili tufanye kitu kilicho bora zaidi,”alisema Afande Sele.

No comments:

Post a Comment