KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, April 2, 2012

LEILA RASHID WA JAHAZI AIBUKA MWIMBAJI BORA WA TAARAB

Leila Rashid

Khadija Omar Kopa



MWIMBAJI Leila Rashid wa kikundi cha Jahazi ameibuka mshindi katika shindano la kumsaka mwimbaji bora wa muziki wa taarab.

Shindano hilo lililodumu kwa mwezi mmoja, liliendeshwa na blogu ya Liwazozito, inayomilikiwa na mwandishi wa habari, Rashid Zahor.

Katika shindano hilo, wasomaji wa blogu hii walitakiwa kuwapigia kura waimbaji saba walioshindanishwa kwa lengo la kumpata mshindi.

Leila aliibuka mshindi baada ya kupata kura saba kati ya kura 14 zilizopigwa na wasomaji kutoka nchi mbalimbali duniani, ikiwemo Marekani, Uingereza na Canada. Kura hizo ni sawa na asilimia 31 ya kura zilizopigwa.

Nafasi ya pili ilinyakuliwa na Khadija Kopa wa TOT, Sabah Salum wa East African Melody na Khadija Yussuf wa Jahazi waliopata kura nne kila mmoja, ambazo ni sawa na asilimia 18 ya kura zilizopigwa.

Mwimbaji mwenye makeke Isha Ramadhani 'Mashauzi' alishika nafasi ya tatu baada ya kuambulia kura mbili, ambazo ni sawa na asilimia tisa wakati Zuhura Shaaban wa Zanzibar Stars alishika nafasi ya nne kwa kupata kura moja, ambayo ni sawa na asilimia nne. Zena Khamis wa File Stars hakupata kura.

No comments:

Post a Comment