KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, April 5, 2012

MILOVAN: Hali ya hewa haiwezi kutuathiri





KOCHA Mkuu wa Simba, Milovan Cirkovic, amesema hali ya hewa ya mji wa Setif
ambayo ni baridi kali inaweza kuwa faida kwa timu yake na si hasara.
Akizungumza na tovuti ya Simba, Milovan alisema hali ya hewa ya baridi huwafanya
wachezaji wasichoke mapema tofauti na joto ambalo huchosha.
Kuna baridi za aina mbili. Kuna baridi inayotokana na hali ya hewa ya mahali na kuna
baridi inayotokana na eneo kuwa kwenye miinuko (altitude). Zote ni baridi lakini zina
tofauti.
“Ile ya miinuko huwafanya wachezaji washindwe kupumua vizuri na huwa na athari
mbaya sana. Tuliliona hili kwenye mechi ya Kiyovu lakini hapa Setif hakuna miinuko
sana kama Rwanda na hivyo wachezaji wanaweza kucheza vizuri,” alisema.
Alisema jambo la muhimu kwa timu yake ni kutoathiriwa na sauti za washangiliaji wa
Setif wala kughadhabika kirahisi wanapochokozwa na wapinzani wao.
“Mechi yetu na Setif ni ngumu sana. Kila timu ina nafasi ya kufanya vizuri ingawa sisi
tuna faida kutokana na ushindi tulioupata nyumbani. Ni jukumu letu kuhakikisha
tunaulinda ushindi wetu,” alisema.

No comments:

Post a Comment