KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, September 30, 2013

BREAKING NEWSSSSS....MPIGA GITA LA BESI JOSEPH WATUGURU AFARIKI



MPIGA gita la besi wa bendi ya muziki wa dansi ya WK Sound, Joseph Watuguru amefariki dunia.
Watuguru alifariki dunia jana asubuhi nyumbani kwake Mabibo mjini Dar es Salaam baada ya
kuugua ugonjwa wa kifua kikuu.

Mmiliki wa bendi hiyo, Wiston Kagusa alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, marehemu Watuguru alianza kuugua ugonjwa huo wiki mbili zilizopita kabla ya kufariki dunia.

Kwa mujibu wa Kagusa, afya ya Watuguru ilianza kudhoofika mwezi uliopita
na baada ya kwenda kufanyiwa uchunguzi katika hospitali ya Amana, iligundulika kwamba alikuwa na kifua kikuu.

Kwa mara ya mwisho, mwanamuziki huyo alipanda jukwaani na bendi hiyo wiki mbili zilizopita katika ukumbi wa Safari ulioko Mbagala, Dar es Salaam.

Kagusa alisema taratibu za mazishi zinatarajiwa kufanyika kesho nyumbani kwa marehemu.
Marehemu Watuguru alianza kujipatia umaarufu miaka ya 1990 alipokuwa katika bendi ya Mchinga Sound, iliyokuwa ikiongozwa na Muumin Mwinjuma.

Alikuwa mmoja wa wapiga gita mahiri la besi nchini, kiasi kwamba Muumin alikuwa akipenda kutaja jina lake katika nyimbo mbalimbali za Mchinga Sound.

Habari zaidi zitafuata baadaye.

No comments:

Post a Comment