KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, September 29, 2013

SIMBA MATAWI YA JUU




MABAO yaliyofungwa na washambuliaji Hamisi Tambwe na Ramadhani Singano 'Messi' leo yameiwezesha Simba kuzidi kujichimbia kileleni mwa ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya kuichapa JKT Ruvu mabao 2-0.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Simba ilikwenda mapumziko ikiwa mbele kwa bao 1-0.

Tambwe aliifungia Simba bao la kwanza dakika ya 24 kwa njia ya penalti baada ya beki jamal Saidi wa JKT Ruvu kuunawa mpira ndani ya eneo la hatari. Bao hilo lilikuwa la saba kwa Tambwe msimu huu.

Singano aliihakikishia Simba ushindi dakika ya 49 baada ya kuifungia bao la pili baada ya gonga safi kati ya Tambwe na Abdulrahim Humud.

Ushindi huo umeiwezesha Simba kuendelea kuongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 14 baada ya kucheza mechi sita, ikifuatiwa na Kagera Sugar yenye pointi 11.

Simba: Abbel Dhaira, Haruna Shamte, Adeyoum Seif, Kaze Gilbert, Joseph Owino, Abdulhalim Humud, Amri Kiemba/Ramadhani Singano, Said Ndemla, Betram Mombeki/Miraj Madenge, Amisi Tambwe na Haroun Chanongo/Marcel Kaheza.

JKT Ruvu: Shaaban Dihile, Damas Makwaya, Stanley Nkomola, Omar Mtaki, Jamal Said, Nashon Naftali, Alhaj Zege, Emanuel Swita/Richard Msenya, Bakari Kondo/Paul Ndauka, Salum Machaku na Emanuel Pius.

Katika mechi zingine za ligi hiyo zilizochezwa leo, Azam FC imetoka sare ya 1-1 na Prison wakati Ashanti United imetoka sare ya 2-2 na Mtibwa Sugar.

No comments:

Post a Comment