KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, May 10, 2013

SERIKALI YAINGILIA KATI SAKATA LA JAYDEE NA RUGE



SERIKALI imeamua kuingilia kati sakata la mwanamuziki nyota nchini, Judith Wambura 'LadyJaydee' na uongozi wa kituo cha redio cha Clouds FM cha mjini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla alisema jana kuwa, wanatarajia kuzikutanisha pande hizo mbili ili kupata suluhu na mgogoro uliojitokeza kati yao.
Makalla alisema lengo la kuzikutanisha pande hizo mbili ni kutaka kupata ukweli wa nini kilichotokea na kusababisha kuzuka kwa mgogoro huo.
Naibu Waziri alisema malumbano yanayoendelea kati ya JayDee na viongozi waandamizi wa Clouds FM, hayana tija na yanaweza kuukuza zaidi mgogoro huo na kusababisha chuki na visasi.
Makalla alisema yuko tayari kukutana na JayDee na uongozi wa Clouds FM wakati wowote ili kumaliza tofauti zilizojitokeza kati yao.
"Nawasihi sana ndugu zangu hawa, jambo hili halipendezi kwa jamii, hivyo tunapaswa kukaa na kulimaliza kwa njia ya mazungumzo,"alisema Makalla.
Alisema anaamini mzozo uliozuka kati ya pande hizo utamalizika kwa kuwa serikali haifurahii kuona wasanii na viongozi wa wasanii wakilumbana hadharani.
Sakata kati ya JayDee na uongozi wa Clouds FM lilizuka Mei Mosi mwaka huu baada ya JayDee kuandika kwenye mtandao wake akimtaka Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga wa Clouds FM wasihudhurie mazishi yake.
Katika taarifa yake hiyo, JayDee aliwataja viongozi hao wawili kuwa wamekuwa mstari wa mbele kutaka kummaliza kimuziki, ikiwa ni pamoja na kuidhoofisha bendi yake ya Machozi kwa kuwalaghai wanamuziki wake.
Siku chache baadaye, Ruge alijibu tuhuma hizo za JayDee kwa madai kuwa, zinaonyesha wazi jinsi mwanamuziki huyo anavyotapatapa.

No comments:

Post a Comment