KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, May 30, 2013

FALCAO AWA MCHEZAJI GHALI MONACO



PARIS, Ufaransa
MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Atletico Madrid ya Hispania, Radamel Falcao, amekuwa mchezaji ghali wa klabu ya Monaco ya Ufaransa baada ya kununuliwa kwa bei mbaya.

Falcao alifuzu vipimo vya afya juzi na sasa ataichezea timu hiyo katika michuano ya Ligi Kuu ya Ufaransa msimu ujao akiwa na nyota wengine kama Zlatan Ibramovic, anayecheza Paris Saint Germain.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Colombia ametua Monaco kwa ada ya uhamisho wa pauni milioni 51 (sh. bilioni 110).

Monaco imezipiku klabu za Chelsea na Manchester United, ambazo zilikuwa zikimuwinda mchezaji huyo kwa udi na uvumba.

Falcao anatarajiwa kutia saini mkataba wa miaka minne au mitano wa kuichezea Monaco na atachuana na Ibrahimovic katika kuwania kiatu cha dhahabu.

"Sijui niwashukuru vipi mashabiki wa Atletico Madrid, sikutegemea kupata mafanikio haya. Siwezi kuwasahau, asanteni," alisema Falcao.

Mchezaji huyo alisema kuwa anaondoka Atletico Madrid akiwa na mafanikio makubwa kwa kuipa mataji matatu katika miaka miwili aliyokuwa akicheza soka Hispania.

Monaco inayonolewa na Claudio Ranieri, pia imewasajili nyota wengine kadhaa wakiwemo Joao Moutinho na James Rodriguez wa FC Porto ya Ureno na kumuongezea mkataba wa mwaka mmoja beki nguli duniani, Ricardo Carvalho.

No comments:

Post a Comment