KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, May 23, 2013

WASAUZI KUZIHUKUMU STARS, MOROCCO


SHIRIKISHO la Soka la Kimataifa (FIFA), limemteua mwamuzi Fraser Daniel Bennett kutoka Afrika Kusini kuchezesha mchezo kati ya timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' na Morocco.

Mchezo huo wa marudiano wa kuwania kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia za 2014, utafanyika Juni 8 mwaka huu Jijini Marrakech, Morocco.

Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura, alisema jana kuwa, Bennett atasaidiwa na Thusi Zakhele Siwela wa Afrika Kusini na Marwa Range kutoka Kenya.

Alisema mwamuzi wa akiba katika mechi hiyo, itakayochezwa kuanzia saa 2.30 usiku atakuwa Lwandile Mfiki wa Afrika Kusini.

Alisema Kamishna wa mechi hiyo ni Robert Mangollo-M’voulou wa Gabon wakati mtathimini wa waamuzi atakuwa Charles Masembe kutoka Uganda.

Stars ipo kundi C na timu za Ivory Coast, Morocco na Gambia, ikiwa inashika nafasi ya pili kwa kuwa na pointi sita, nyuma ya Ivory Coast inayoongoza kwa kuwa na pointi saba.

No comments:

Post a Comment