KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, May 23, 2013

WANAHABARI KUKIPIGA NA WABUNGE JUNI MOSI



TIMU za soka na netiboli zinazoundwa na wachezaji kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini, zinatarajiwa kucheza mechi za kirafiki na wabunge Juni Mosi mwaka huu mjini Dodoma.

Timu hizo za vyombo vya habari zimeundwa na baadhi ya wachezaji walioshiriki katika michuano ya kuwania Kombe la NSSF iliyofanyika Machi mwaka huu mjini Dar es Salaam.

Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa NSSF, Juma Kintu alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, mechi hizo mbili zinatarajiwa kuchezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Kintu alisema mechi hizo zimelenga kujenga uhusiano wa kirafiki kati ya wabunge na wafanyakazi wa vyombo vya habari.

Alisema timu hizo mbili za waandishi wa habari zinatarajiwa kuondoka Mei 31 mwaka huu kwenda Dodoma na kurejea Dar es Salaam Juni 2 mwaka huu.

Kintu alisema wachezaji wa timu hizo wanatarajiwa kufanya mazoezi kwa siku tatu kabla ya safari hiyo kwa lengo la kujiweka fiti.

"Uteuzi wa wachezaji timu zote mbili za soka na netiboli umeshafanyika na ulitokana na viwango walivyovionyesha wakati wa michuano ya Kombe la NSSF,"alisema Kintu.

Aliwataja wachezaji 17 walioteuliwa kuunda timu ya soka kuwa ni Mzee Mfaume (NSSF), Mbozi Katala (TBC), Paul Urio (IPP Media), Majuto Omary (Mwananchi), Fred Mweta (BTL), Anwar Mkama (Mlimani TV), Julius Kihampa (Jambo Leo) na Nurdin Msindo (Tumaini Media).

Wengine ni Said Ambua (Uhuru Media), Mohamed Mharizo (New Habari), Mohamed Mkandemba (Free Media), Edward Mbaga (Sahara Media), Saleh Ally (Global Publishers), Mussa Abdalla (Habari Zanzibar), Ridhiwani Ramadhani (Changamoto), Heri Mselem (Redio Kheri) na Mgaya Kingoba (TSN).

Wachezaji walioteuliwa kuunda timu ya netiboli ni Pili Mogela (NSSF), Agnes Mbapu (TBC), Somoye Ng'itu (IPP Media), Imani Makongoro (Mwananchi), Lulu Habibu (BTL), Sophia Turuka (Mlimani TV), Charity James (Jambo Leo).

Wengine ni Monica Kinyemi (Tumaini Media), Sophia Ashery (Uhuru Media), Zuhura Abdulnoor (New Habari), Crecensia Tryphon (Free Media), Immaculata Kiluvya (Sahara Media), Glory Massawe (Global Publishers), Beshuu Abdalla (Habari Zanzibar) na Vicky Godfrey (Changamoto).

No comments:

Post a Comment