KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, May 1, 2013

KOLABO ZAMIMINIKA KWA VANESSA


MSANII chipukizi wa muziki wa kizazi kipya nchini, Vanessa Mdee amesema amekuwa akipokea maombi mengi kutoka kwa wasanii mbalimbali nchini kwa ajili ya kufanya nao kolabo.

Vanessa alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, maombi aliyoyapata hadi sasa ni zaidi ya 10 na yamemfanya ajione msanii aliyepata mafanikio katika kipindi kifupi.

Binti huyo mwenye sura na umbo lenye mvuto alisema, amepokea maombi hayo baada ya kufanya vizuri katika wimbo wake mpya wa Closer.

"Unajua watu wanapenda vitu vipya na vitu tofauti, hivyo namshukuru Mungu nimepata ofa za kutosha na kwangu hayo ni mafanikio makubwa,"alisema.

"Mtu anapotaka kukuweka kwenye korasi ya wimbo wake, ujue amekukubali na anaamini utaufanya wimbo wake uwe na mvuto zaidi, hivyo kwangu hilo ni jambo zuri na la kuvutia,"aliongeza.

Vanessa alisema binafsi amepata mafanikio makubwa kupitia wimbo wake wa Closer kutokana na kusaidiwa na Ommy Dimpoz na Ambwene Yesaya (AY) katika viitikio.

Alisema anamshukuru Mungu kuona kwamba watu wameanza kukitambua kipaji chake na kumkubali kama msanii chipuziki anayekuja juu kimuziki.

No comments:

Post a Comment