KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, May 1, 2013

NAKAAYA AKIRI KUWA MJA MZITO



MSANII machachari wa muziki wa kizazi kipya nchini, Nakaaya Sumari amekiri kuwa na uja uzito na kusema kuwa, anatarajia kujifungua wakati wowote.

Hata hivyo, Nakaaya hakuwa tayari kutaja umri wa uja uzito alionao na baba wa mtoto, anayetarajia kujifungua.

"Uja uzito nilionao ni wa mtu mtakatifu, siyo mtu anayejulikana," alisema Nakaaya alipozungumza na kituo kimoja cha redio mjini Dar es Salaam wiki hii.

Wakati huo huo, Nakaaya amerekodi wimbo wake mpya unaojulikana kwa jina la Utu uzima dawa.

Nakaaya alisema amerekodi wimbo huo katika studio za Fish Crub chini ya usimamizi wa Prodyuza Dunga.

Alisema tayari kibao hicho kimeshaanza kupigwa katika vituo mbalimbali vya redio nchini na kupokewa vizuri na mashabiki wa muziki.

Nakaaya alianza kujipatia umaarufu mkubwa baada ya kuibuka na kibao chake kinachokwenda kwa jina la Mr. Politician. Alirekodi kibao hicho miaka mitatu iliyopita.

Baada ya kupata mafanikio makubwa kutokana na kibao hicho, Nakaaya aliamua kujitosa kwenye ulingo wa siasa kwa kujiunga na CHADEMA kabla ya kurejea CCM.

No comments:

Post a Comment