KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, May 1, 2013

REHEMA TAJIRI ALIA NA MAMA MKWE

BAADA ya ukimya wa muda mrefu, mwanamuziki Rehema Tajiri ameibuka na kibao kipya kinachokwenda kwa jina la Msikilize mama.

Rehema amerekodi kibao hicho kwa kutumia miondoko ya zouk, akimshirikisha msanii chipukizi wa muziki wa kizazi kipya, Dogo Sama.

Akizungumza mjini Dar es Salaam wiki hii, Rehema alisema amerekodi kibao hicho katika studio za Suresh zilizopo Temeke, Dar es Salaam.

Rehema alisema katika kibao hicho, amezungumzia masuala ya mapenzi kati yake na mpenzi wake, lakini kikwazo kikubwa kipo kwa mkwe wake.

"Nimesimulia jinsi mimi na mpenzi wangu tunavyopendana, lakini mkwe wangu (mama wa mpenzi wake) hanipendi, anataka niachane na mwanawe,"alisema.

Kwa mujibu wa Rehema, tayari wimbo huo umeshaanza kupigwa katika vituo mbalimbali vya redio nchini na kuwavutia mashabiki wengi.

Hata hivyo, kutokana na ushauri alioupata kutoka kwa baadhi ya wataalam wa muziki, Rehema alisema anatarajia kuufanyia marekebisho kidogo wimbo huo.

"Baadhi ya wataalamu waliousikia wimbo huo, wamenishauri niurekodi upya kwa kutumia vyombo vya muziki badala ya kutumia ala za studio. Wanasema kwa hadhi yangu, sipaswi kurekodi muziki wa kompyuta,"alisema.

Rehema amewataka mashabiki wake wakae mkao wa kula kwa vile amejipanga upya kuhakikisha anateka tena soko la muziki nchini.

Alisema ukimya wake wa muda mrefu ulitokana na kutingwa na matatizo ya kifamilia na pia kujipanga upya.

No comments:

Post a Comment