KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, May 10, 2013

UCHAGUZI MKUU WA TFF SASA SEPT 29



HATIMAYE uchaguzi mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF)
umepangwa kufanyika Septemba 29 mwaka huu.

Uchaguzi huo utafanyika baada ya mkutano wa dharula wa marekebisho
ya katiba uliopangwa kufanyika Julai 13 mwaka huu.

Akizungumza mjini Dar es Salaam jana, Rais wa TFF, Leodegar Tenga
alisema tarehe hizo zimepangwa na kikao cha dharula cha kamati ya
utendaji ya shirikisho hilo kilichofanyika mjini Dar es Salaam
jana.

Tenga alisema kamati hiyo imepokea maagizo ya Shirikisho la Soka la
Dunia (FIFA) na kupanga utekelezaji wake unaoelekeza cha kufanya na
siyo TFF au mtu mwingine anayeweza kuongeza jambo lingine.

Rais huyo alisema FIFA iliagiza kuundwa kwa kamati ya maadili,
kamati ya rufani ya maadili na kufanya marekebisho ya katiba kabla
ya kutangaza tarehe mpya ya uchaguzi na wagombea waliokuwepo na
wengine wapya waruhusiwe kugombea.

"Tumejitahidi kuhakikisha uchaguzi uwe kabla ya Oktoba 30 mwaka huu
kama FIFA walivyotuagiza, tumefanya kikao cha dharula na kupanga
tarehe za mkutano mkuu wa uchaguzi,"alisema Tenga.

Aliongeza kuwa, kazi kubwa itakuwa ni kutayarisha kanuni hizo kwa
kuwa kamati za maadili lazima ziwe na kanuni zake na kuhakikisha
hakuna mgongano kati ya kanuni za nidhamu na kanuni za maadili.

Alisema kwa mujibu wa ratiba ya utekelezaji, rasimu ya mwanzo ya
kanuni hizo inatakiwa iwe imetoka kufikia Mei 30 na Juni 15 mwaka
huu.

Tenga alisema kamati ya utendaji ya TFF itakutana kwa ajili ya
kupokea mapendekezo hayo na baada ya kuyapitisha, itayapeleka FIFA.

Alisema yaatifa ya mkutano mkuu wa dharula, ambayo kikatiba ni siku
30, itatolewa Juni 12 au 13 na baada ya mkutano mkuu wa dharula wa
marekebisho ya katiba, kamati ya utendaji itakutana kati ya Julai
14 a 15 mwaka huu kuunda kamati ya maadili na kamati ya rufani ya
maadili ili kuruhusu mchakato wa uchaguzi uanze.

Uchaguzi huo umetokana na FIFA kuagiza mchakato wake uanze upya
baada ya kuibuka kwa mgogoro mkubwa kutokana na baadhi ya wagombea
kuenguliwa. Uchaguzi wa awali ulipangwa kufanyika Februari 24 mwaka
huu.

No comments:

Post a Comment