KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, April 23, 2017

SIMBA KUVAANA NA AZAM; YANGA NA MBAO FC KOMBE LA SHIRIKISHO


SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), leo limetangaza ratiba ya mechi za nusu fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho, maarufu kama Azam Sports Federation Cup.

Kwa mujibu wa ratiba hiyo, iliyopangwa na kutangazwa leo, mabingwa watetezi Yanga wamepangwa kumenyana na Mbao FC, katika mechi itakayopigwa Aprili 30, mwaka huu, kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Ratiba hiyo inayonyesha kuwa, mabingwa wa mwaka juzi, Azam watacheza mechi hiyo kwa kuumana na wakongwe Simba. Mechi hiyo itapigwa Aprili 29, mwaka huu, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment