KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, April 23, 2017

DK MWAKYEMBA AKUTANA NA KUTETA NA VIONGOZI WA SIMBA





Picha na Kitengo cha Mawasiliano WHUSM Dodoma.

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt Harrison Mwakyembe amekutana na na uongozi wa klabu ya Simba ukiongozwa na Rais wake Bw. Evans Aveva kwenye Ofisi zake Mjini Dodoma.

Uongozi wa Simba umeitikia wito wa Mhe. Mwakyembe wa kukutana naye na kujadili masuala mbalimbali ya mpira wa Miguu zikiwemo fursa na changamoto katika mabadiliko na maedneleo ya uendeshaji wa timu.

Aidha  Mhe. Mwakyembe  amepokea maoni ya Uongozi wa samba na kusahauri kuendelea kutoa ushirikiano na wadau wa mpira wa miguu nchini.

Kikao hicho pia kilihudhuriwa  na Katibu Mkuu Wizara husika prof Elisante Ole Gabriel, Mkurugenzi wa Michezo Yusufu Omary, Katibu Mkuu wa BMT Mohamed Kiganja, na Msajili wa Vilabu na Vyama nchini.

No comments:

Post a Comment