KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, April 2, 2017

YANGA YAIENGUA SIMBA KILELENI MWA LIGI KUU


BAO lililofungwa na mashambuliaji Obrey Chirwa katika kipindi cha pili, jana liliiwezesha Yanga kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Azam katika mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara, iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ushindi huo uliiwezesha Yanga kuiengua Simba kileleni mwa ligi hiyo, baada ya kufikisha pointi 56. Simba inashika nafasi ya pili kwa kuwa na pointi 55.

Hata hivyo, Simba inaweza kurejea kileleni mwa ligi hiyo leo, iwapo itaishinda Kagera Sugar, katika mechi nyingine ya ligi hiyo itakayochezwa kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

No comments:

Post a Comment