KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, April 23, 2017

YANGA YAZIFUATA SIMBA, AZAM NUSU FAINALI KOMBE LA FA



Mabingwa wa tetezi wa Kombe la Shirikisho, Yanga wametinga hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Tanzania Prisons.

Mchezo huo wa robo fainali ulifanyika jana, katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, ambapo Yanga sasa inaungana na mahasimu wao Simba, Azam na Mbao FC katika hatua inayofuata ya nusu fainali.

Yanga ilipata magoli yake kupitia kwa Amissi Tambwe aliyefunga dakika ya 16 ya mchezo, Obrey Chirwa aliyefunga bao la pili dakika ya 41. Yanga ilikwenda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 2-0.

Simon Msuva aliifungia Yanga bao la tatu dakika ya 46 na kuihakikishia ushindi. Mechi hiyo haikuwa na mvuto kutokana na kunyesha kwa mvua kubwa.

Prisons nusura wapate bao la kufutia machozi baada ya kupata penalti dakika ya 54, lakini mpigaji Victor Hangaya aligongesha mwamba.

Ratiba ya mechi za nusu fainali inatarajiwa kupangwa leo na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

No comments:

Post a Comment