KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, April 3, 2017

SIMBA YAPIGWA MWELEKA 2-1 NA KAGERA SUGAR


MATUMAINI ya Simba kutwaa taji la ligi kuu ya Tanzania Bara yameanza kuota mbawa baada ya kupigwa mweleka wa mabao 2-1 na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

Kipigo hicho kimeifanya Simba iendelee kushika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo, ikiwa na pointi 55, nyuma ya mabingwa watetezi Yanga wanaoongoza kwa kuwa na pointi 56.

Washambuliaji wa zamani wa Simba, walioachwa kwa madai ya viwango vyao kushuka, Mbaraka Yussuf na Christopher Edward, ndio waliopeleka kilio Msimbazi baada ya kuifungia Kagera Sugar mabao hayo mawili.

Mbaraka, mchezaji kinda kwenye kikosi cha timu ya Taifa, Taifa  Stars, aliifungia Kagera Sugar bao la kwanza dakika ya 27 kwa shuti kali lililomshinda kipa Daniel Agyei wa Simba. Bao  hilo lilidumu hadi mapumziko.

Christopher, aliiongezea Simba bao la pili dakika ya 50 baada ya gonga safi kati yake na washambuliaji wenzake wa Kagera.

Bao la kujifariji la Simba lilifungwa na Muzamil Yassin dakika ya 65 baada ya kutokea piga nikupige kwenye lango la Kagera.

Simba ilijitahidi kucheza kufa na kupona ili kusawazisha, lakini kikwazo kikubwa kilikuwa kipa wa zamani wa timu hiyo, Juma Kaseja, aliyekaa imara kwenye lango la Kagera.

No comments:

Post a Comment