KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, April 9, 2017

YANGA YAPATA USHINDI MWEMBAMBA KWA WAALGERIA


BAO lililofungwa na kiungo Thabani Kamusoko jana liliiwezesha Yanga kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya MC  Alger ya Algeria katika mechi ya awali ya hatua ya mtoano ya michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.

Kamusoko alifunga bao hilo dakika ya 61 kwa shuti kali baada ya gonga safi kati yake, Haruna Niyonzima na Simon Msuva.

Kutokana na ushindi huo, Yanga sasa inahitaji sare ya aina yoyote timu hizo zitakaporudiana wiki ijayo mjini Algiers.

Hata hivyo, baadhi ya wachambuzi wa soka wameilaumu Yanga kwa kushindwa kuondoka uwanjani na ushindi mkubwa wa mabao kwa vile wapinzani wao walicheza kwa kasi ndogo huku wakionekana dhahiri kutafuta sare.

Katika mechi hiyo iliyohudhuriwa na mashabiki wachache, Yanga ilipata nafasi nzuri kadhaa za kufunga mabao, lakini zilipotezwa na washambuliaji wake, Obrey Chirwa, Deus Kaseka na Msuva kutokana na kukosa umakini kila walipolikaribia lango la wapinzani wao.

No comments:

Post a Comment