KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, April 15, 2017

MAJALIWA YA YANGA KOMBE LA SHIRIKISHO MIKONONI MWA MC ALGER



INAWEZEKANA ukawa mwisho wa safari ya Yanga katika michuano ya Afrika mwaka huu, au ukawa ni mwendelezo wa kufuzu kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho.

Jibu hilo litapatikana leo wakati mabingwa hao wa Tanzania Bara, waliotolewa katika michuano ya ligi ya mabingwa Afrika, watakaporudiana na MC Alger ya Algeria mjini Algiers.

Mechi hiyo ni ya marudiano kati ya timu hizo. Katika mechi ya awali, iliyochezwa wiki iliyopita mjini Dar es Salaam, Yanga iliibuka na ushindi wa bao 1-0.

Ili iweze kusonga mbele, Yanga inahitaji kushinda mechi hiyo au kupata sare ya aina yoyote wakati wapinzani wao watalazimika kushinda kwa mabao 2-0.

Kwa mujibu wa ratiba, mechi hiyo imepangwa kuanza saa mbili usiku kwa saa za Afrika Mashariki, lakini bado haijafahamika iwapo utaonyeshwa moja kwa moja na televisheni za hapa nchini.

Katika mechi hiyo, Yanga itamkosa mshambuliaji wake wa kulipwa, Obrey Chirwa kutoka Zambia, ambaye hakusafiri na timu hiyo kwenda Algeria, kwa kile kinachodaiwa kuwa ameweka mgomo baridi kutokana na kutolipwa mishahara kwa miezi mitatu.

Pengine tegemeo kubwa kwa timu hiyo litakuwa kwa washambuliaji wake nyota, Amissi Tambwe na Mzimbabwe, Donald Ngoma, waliokuwa majeruhi kwa muda mrefu.

No comments:

Post a Comment