KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, April 29, 2017

SIMBA YATINGA FAINALI KOMBE LA SHIRIKISHO, YAICHAPA AZAM 1-0


SIMBA leo imekata tiketi ya kucheza fainali ya michuano ya soka ya Kombe la Azam, maarufu kama Kombe la Shirikisho, baada ya kuichapa Azam bao 1-0.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Simba ilijipatia bao hilo la pekee na la ushindi dakika ya 48 kupitia kwa mshambuliaji Mohamed Ibrahim.

Hata hivyo, Mohamed alishindwa kumaliza mchezo huo baada ya kutolewa nje kwa kadi nyekundu dakika ya 74 kwa kucheza rafu mbaya.

Awali, Azam nayo ilipata pigo baada ya kiungo wake, Salum Abubakar kutolewa nje kwa kadi nyekundu na mwamuzi Mathew Akrama kutoka Mwanza dakika ya 15 kwa kosa la kumkwatua kwa nyuma Ibrahim Ajib wa Simba.

Simba sasa inasubiri mshindi wa pambano lingine la nusu fainali kati ya Yanga na Mbao FC litakalochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza.

No comments:

Post a Comment