KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, April 23, 2017

HAJI MANARA ATUPWA JELA YA SOKA MWAKA MMOJA, ATOZWA FAINI MILIONI MOJA


 
MKUU wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba, Haji Manara, amefungiwa kujihusisha na soka kwa mwaka mmoja, kutokana na kutoa lugha chafu kwa viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Aidha,  Manara, ambaye alishindwa kuhudhuria kikao cha Kamati ya Nidhamu ya TFF, kilichotoa adhabu hiyo leo, ametozwa faini ya sh. milioni moja baada ya kupatikana na hatia ya makosa matatu.

Manara alishindwa kuhudhuria kikao hicho kwa madai ya kupata dharura, lakini anayo nafasi ya kukata rufani.

Saa kadhaa baada ya Kamati ya Nidhamu ya TFF kutangaza kumfungia Manara, Ofisa Habari wa zamani wa Yanga, ambaye naye alifungiwa mwaka mmoja, Jerry Muro, ametumia ukurasa wake wa instagram kuandika alivyoupokea uamuzi huo.

“Mtuache sasa tupumzike, tuliyofanya kwa taifa hili haswa kwenye mpira nadhani yametosha, swahiba karibu kijiweni @hajismanara.“

No comments:

Post a Comment