KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, April 16, 2017

SIMBA YAKWAA KISIKI KWA TOTO AFRICAN


MATUMAINI ya Simba kutwaa taji la ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara, jana yaliota mbawa baada ya kulazimishwa kutoka suluhu na Toto African katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza.

Sare hiyo imeifanya Simba iendelee kuongoza ligi ikiwa na pointi 62 baada ya kucheza mechi 26, ikifuatiwa na Yanga yenye pointi 56 huku ikiwa na mechi mbili za viporo mkononi.

Iwapo Yanga itashinda mechi hizo mbili, itafikisha pointi 62, sawa na Simba, hivyo kufanya ushindani wa kuwania ubingwa kuamuliwa kwa idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa.

Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Jacob Adongo wa Mara, timu zote mbili zilishambuliana kwa zamu muda wote wa dakika 90, lakini hakuna iliyoweza kupata bao.

No comments:

Post a Comment